Monday, 22 January 2018

AT: Tuzo zangu za Marekani siwezi kuzipasua


Msanii wa muziki Bongo, AT amesema hawezi kuzipasua tuzo zake alizoshinda nchini Marekani November mwaka jana, 2017.

Muimbaji huyo katika mahojiano na kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm amesema awali alipanga kupasua tuzo zake za Kilimanjaro Music Award (KTMA) zilizokuwa zikitolewa hapa nchini lakini baadaye akagundua kuwa tuzo hizo ni mali ya Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

“Ni baada ya kuomba msaada ili nisaidiwe kwenda Kongo nikafanye kolabo na Koffi Olomide, wakanizungusha sana, ilikuwa hasira tu, ila hizi tuzo zangu za Marekani siwezi kuzipasua,” amesema AT.

November mwaka jana AT alishinda tuzo mbili katika ‘B&K Music & Video Music Awards’, vipengele alivyoshinda ni International Artist na Best Music Video kupitia wimbo wake ‘Sili Feel’.

Kingozi CCM awataka Wananchi Kuwaombea JWTZ Waliopo Kongo


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla ‘Mabodi’ amewasihi wananchi wa Tanzania   kuendelea kuwaombea Dua na visomo mbali mbali Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wanaouawa  wakilinda Amani katika nchini mbali mbali ikiwemo DRC Kongo.

Pia ameliomba Jeshi hilo pamoja na familia za ndugu wa marehemu Askari 10 waliofariki waliofariki siku za hivi karibuni wakilinda Amani Kongo, kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Wito huo ameutoa leo mara baada ya kumalizika shughuli ya kisomo cha Khitma na Dua ya pamoja ya Arubaini ya kuwaombea marehemu hao iliyoandaliwa na Kamati ya Amani Kitaifa Zanzibar huko katika Msikiti wa Noor Muhammad (SAW) kwa Mchina Mwanzo Zanzibar.

Dk.Mabodi ameeleza kwamba Askari hao watakumbukwa daima kwa mchango wao wa kutetea na kulinda maisha ya Waafrika katika Nchi ya Kongo ambapo walikuwa wakiiwakikisha Tanzania kupitia Jeshi la Pamoja la Umoja wa Mataifa lililopo nchini humo kwa ajili ya kulinda Amani.

Aliwambia wananchi kuwa Mashujaa hao hakuna cha kuwalipa kwa sasa kwani wamepoteza uhai wao kutokana na uzalendo uliotukuka hivyo kilichobaki ni kuwaombea Dua wao Mwenyezi Mungu awapumzishe pahala pema peponi Amini na kuziombea familia zao ziendelee kuwa na subra.

Amefafanua kuwa msiba huo mzito ni sehemu ya Askari wa Majeshi mbali mbali ya Ulinzi na Usalama nchini wanaoendelea na kazi zao za kawaida wawe imara Kifkra na Kimwili bila kukata tamaa ili kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa Kituo kikuu cha Amani Barani Afrika na Duniani kwa ujumla.

Akizungumzia matunda ya kulinda misingi ya Amani nchini Dk.Mabodi amesema ni kuwepo kwa maendeleo katika Nyanja mbali mbali za Kiuchumi, Kisiasa na Kijamii.

“Wananchi tulinde tunu ya Amani na Utulivu tuliokuwa nao katika Taifa letu, ili tuweze kuwa Mabalozi wazuri wa kulinda Amani kwa nchi jirani na Mataifa mengine.”, amesisitiza.

“Nawapongeza Kamati ya Amani ya Taifa Zanzibar kwa maandalizi yao mazuri ya kuandaa shughuli ya kuwaombea Dua kubwa kama hii vijana wetu waliouwawa na watu wanaosadikiwa kuwa Waasi huko Nchini Kongo.”, amesema Dk.Mabodi.

Aidha ameeleza kuwa wananchi wanatakiwa kujenga utamaduni wa kuenzi Amani na Utulivu, uliopo nchini kwa lengo la kuepuka machafuko na migogoro isiyokuwa ya lazima nchini.

Naye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Hussein Mwinyi, amewashukru wananchi mbali mbali waliojitokeza katika Khitma hiyo kwa lengo la kuwaombea Dua Marehemu Askari hao.

Amesema licha ya Tanzania kuwapoteza Mashujaa hao bado Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) litaendelea kuwa imara na kulinda mipaka na kushiriki harakati mbali mbali za kulinda amani hata nje ya Tanzani kwa lengo la kudumisha mahusiano mema na nchi nyingine Duniani

Baada ya kuona picha ya mtoto akiomba jezi yake, Samatta afunguka


 Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars anayecheza soka la kulipwa katika club ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta licha ya kuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili lakini ameonesha kuzidi kupendwa na mashabiki wa club yake.

Moja kati ya ujumbe unaosambaa kwa sasa katika mitandao ya kijamii ni pamoja na post ya bango ya shabiki mtoto wa KRC Genk ikiwa imeandikwa “Mbwana Can I have Your Shirt Pendeza” akiwa kamaanisha “Mbwana unaweza kunipa jezi yako? Pendeza”

Baada ya Mbwana Samatta kuona post ya picha ya mtoto huyo akajibu “Ndio naweza kukupa kwa nini ishindikane” hiyo imezidi kudhihirisha mapenzi ya dhati ya mashabiki kwa Mbwana Samatta maana sio kila mchezaji soka huwa anapata nafasi ya kupendwa na mashabiki kwa kiwango hicho.

Wenger atakuwepo George Weah akiapishwa?


Wananchi wa Liberia wanasubiria kwa hamu tukio la kuapishwa kwa Rais mteule George  Weah, ambapo wengi wamekesha katika uwanja wa mpira wa taifa hilo, mahali ambapo leo January 22, 2018 anategemea kuapishwa na kuandika historia mpya kutoka kung’aa kwenye soka hadi kuwa Rais

George Weah, maisha yake ya utoto, yalikuwa katika mazingira duni katika mji mkuu wa Liberia Monrovia, alipata mafanikio makubwa katika  soka na kufanikiwa kuchezea timu kadhaa barani Ulaya ikiwemo Chelsea, Monaco na AC milan.

Ni Muafrika pekee kuwahi kushinda tuzo mchezaji bora wa FIFA na tuzo ya Ballon. Weah aliingia katika siasa baada ya kustaafu soka mwaka 2002 na akawa miongoni mwa Maseneter katika bunge la Liberia.

Aligombea urais mwaka 2005 na alimshinda Johnson Sirleaf wakati wa duru ya kwanza katika uchaguzi huo lakini akashindwa katika duru ya pili ambapo kambi yake ilisusia kushiriki.

Aliyewahi kuwa meneja wa George Weah katika klabu ya Monaco ya ligi kuu ya Ufaransa Arsene Wenger amealikwa na atakuwepo katika tukio la kuapishwa.

Wazazi wanashikiliwa na Polisi kwa kupokea mahali ya Ng'ombe saba


JESHI la Polisi mkoani Geita linawashikilia watu  wawili wakazi wa  Kijiji cha Kasubuya  wilayani Nyang’wale kwa kula njama wakiwa wazazi  kupokea mahari ya ng’ombe saba na kumwozesha  mwanafunzi wa  kidato cha pili.

Binti huyo  aliyekuwa anasoma katika shule ya sekondari Nyijundu, sasa ana ujauzito.

Aliyethibitisha kukamatwa kwa wazazi hao wa pande zote mbili ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Mponjoli Lotson na kuwataja ni baba mzazi wa msichana huyo, Herman Makanika (48) na Maximillian Makila ambaye ni baba mzazi wa mtuhumiwa aliyemuoa mwanafunzi huyo.

Ingawa hakulitaja jina la mtuhumiwa, Kamanda Mpojoli alimpongeza mwalimu wa shule ya sekondari aliyetoa taarifa  za kuwapo kwa tukio hilo na akabainisha  jinsi wazazi wa pande zote mbili walivyoshiriki  kutenda kosa licha ya mtuhumiwa kutoroka.

Alisema wazazi wa pande zote mbili wanahusika ingawa mtuhumiwa (muoaji) anaendelea kusakwa, hivyo wanapaswa kuwajibika kutokana na kufanya makubaliano kwa kutoa mahari ya ng’ombe saba na mzazi wa msichana kuwapokea ng’ombe hao kama mahari.

Aliongeza kuwa baada ya polisi kuarifiwa ilichukua hatua za haraka na watuhumiwa kukamawta na hadi jana walikuwa wanaendelea kushikiliwa huku juhudi za kumsaka mtuhumiwa zikiendelea kuhakikisha anapatikana na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Ronaldo apasuliwa uso



LICHA ya ushindi wa bao 7-1 dhidi ya Derpotivo la Coruna walioupata Real Madrid katika La Liga, mshambuliaji wake, wa Kimataifa Raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo alikutana na dhoruba baada ya kuumia kwa kupasuka usoni.

Ronaldo aliumia kwa kuchanipa sehemu ya usoni baada ya kugongwa wakati akijaribu kufunga.

Alikuwa ameruka kichwa kwa lengo la kufunga lakini akagongana na mchezaji wa Derpotivo. Hata hivyo, Ronaldo alipata huduma nzuri na kilichovutia zaidi ni yeye kutumia simu ya daktari kuangalia kama alikuwa ameumia au la.

Nduda awasihi mashabiki na wapenzi wa Simba SC



Mlinda mlango wa kimataifa wa klabu ya Simba Said Mohamed Nduda amewataka mashabiki na wapenzi wa wekundu wa msimbazi kuwa na subira katika kipindi hiki kwa madai ana matumaini timu yake watachukua ubingwa safari hii.

Nduda ameeleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa 'East Afrika Television' baada ya kuwepo nje ya uwanja kwa kipindi kirefu kutoka na matatizo ya goti aliyoyapata akiwa mazoezini pindi timu yake ilipokuwa ikijiandaa kwa mchezo dhidi ya watani wao jadi.

"Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu hali yako kwa sasa naendelea vizuri na ninafuata maelekezo ya daktari ya kufanya mazoezi kama anavyoniambia, hapa nasubiri tu kauli yake kama ataniruhusu nianze mazoezi uwanjani ili niungane na wenzangu", alisema Said Nduda.

Pamoja na hayo Nduda aliendelea kwa kusema "nahisi mwezi Februari utakaoanza ninaweza nikawa nimerejea uwanjani, napenda kuwaambia mashabiki wa Simba kuwa na subira katika kipindi hichi kwa kuwa nina imani timu yetu itafanya vizuri na kukinyakua kikombe"

Kwa upande mwingine timu ya Simba itarajia kushuka dimbani alasiri ya leo (Jumatatu) kuvaana na Kagera Sugar katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara mzunguko wa 14.

Sunday, 21 January 2018

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Faiza ampa somo Diamond



Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Faiza Ally amempa ushauri msanii wa muziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kuwa kwa sasa ni muda wake wa kula ujana na kuizunguuka dunia na sio muda wa kujipa majukumu mazito ile hali umri wake bado mdogo.

Faiza Ally amesema Diamond bado hajamaliza hata robo ya dunia hivyo ingawaje ana jina kubwa barani Afrika hivyo angefanya kwanza vitu kama hivyo kuizunguuka dunia ikibidi ajiweke kando na mambo ya mahusiano.

“Diamond kijana mdogo sana anahitaji kuhave funny na watoto wenzie na sisi wadada wazima lazima taungalie watu wa kutoka nao, Go baba have a funny enjoy the world ndio useto down,“ameandika Faiza Ally kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumshauri kuwa ikibidi ajiweke mbali na mahusiano.

“Jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano, bado hujaiona dunia hata robo wewe ni star hela ipo there is alot to see nasema with clean heart no hate kwa Zari au kwa yeyote.“ameandika Faiza.

Ushauri huo umekuja ikiwa ni wiki sasa imepita tangu kuenee tetesi kuwa Diamond Platnumz yupo kwenye mahusiano na msichana maarufu kwenye mitandao ya kijamii anayejulikana kwa jina la Tunda.

Waziri Mkuu atoa agizo kwa TAKUKURU

Waziri Mkuu .Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa ameaagiza TAKUKURU kumkamata Meneja wa TBA wilaya ya Butiama mkoani Mara kutokana na uzembe na kutumia fedha za Serikali kinyume na maelekezo.

Waziri Mkuu amefanya maamuzi hayo baada ya Serikali kupeleka fedha zaidi ya milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la halmashauri lakini mpaka sasa fedha ujenzi huo haujaanza na fedha hizo kutumika katika miradi mingine ambayo haijapangwa na Serikali.

"Tumeleta fedha milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la halmshauri lakini mmezipeleka kwenye shughuli nyingine, kwanini hajajenga jengo hili ikiwa fedha zimeshaletwa? Tumeleta fedha milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya, DAS na nyumba ya watumishi lakini mmejenga nyumba moja tu ya DC, nyumba zingine mbona hamjaanza kujenga?

Waziri Mkuu baada ya kukosa majibu yanayoridhisha kutoka kwa viongozi hao ndipo alipoagiza TAKUKURU kumchukua moja ya mtumishi wa halmshauri hiyo na kusema kuwa serikali haiwezi kuwavumilia watumishi na namna hiyo.

"Meneja TBA upo? Umepata fedha toka mwezi wa nne mwaka jana mpaka leo hii 21 Januari 2018 miezi mingapi ishapita? Msingi wa jengo upo? Kamanda wa PCCB hebu ondoka na huyu bwana, mchukue huyu hatuwezi kuchelewesha kazi, tumeleta fedha kujenga jengo la halmashauri watumishi wanahangaika wewe una hela mpaka leo unazo tu. Kwanini tuwe na watumishi wa namna hii? Alihoji Majaliwa.

Kamati ya Bunge yashtushwa na bei nyumba za NSSF



Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wameshtushwa na bei ya kuuza nyumba za mradi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizoko eneo la Dege Kigamboni jijini Dar es Salaam wakisema haziendani ya hadhi na hali ya wananchi walio wengi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, bei za nyumba za Dege ni kati ya Dola za Marekani 110,000 (Sh220 milioni) hadi Dola 250,000 (Sh500 milioni) kulingana na aina ya nyumba.

Wakizungumza jana baada ya kutembelea miradi ya NSSF jijini Dar es Salaam, wabunge hao walitilia shaka uuzwaji wa nyumba hizo huku shirika hilo likikiri kutozitangaza mapema kwa wateja.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka alisema nyumba za mradi wa Dege hazina hadhi ya kuuzwa bei hiyo.

“Ukiangalia nyumba zenyewe zina ‘poor quality’ (kiwango cha chini), hata ukiangalia ‘design’ yake sio nzuri. Vyumba ni vidogo, hivi kweli mtu atashawishika kutoa Sh200 milioni kununua nyumba hiyo?” alihoji Kaboyoka.

Hoja hiyo, iliungwa mkono na Mbunge wa Magomeni Zanzibar, Jamal Kassim akisema hazikujengwa kwa kuwalenga watu wa kipato cha chini.

“Hizi nyumba hazikujengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini, bali wenye kipato cha juu hasa wageni. Hata hivyo, kwa kuwa wameshawekeza fedha lazima mradi ukamilike na nyumba ziuzwe,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu Dodoma, Felister Bura alihoji upatikanaji wa wateja ikiwa watumishi wa umma wanaotegemewa wengi wao wanahamia Dodoma ambako ndiko makao makuu ya nchi.

Akijibu hoja na maswali ya wabunge, Profesa Kahyarara alisema nyumba hizo za Dege zitauzwa kati ya Dola 110,000 hadi Dola 125,000 kwa moja na Dola 195,000 hadi Dola 250,000 kwa nyumba aina ya villa.

Alisema mteja atatakiwa kulipa kwa muda wa miaka sita.

Mbali na mradi wa Dege, NSSF pia iliwaonyesha wajumbe hao wa PAC mradi wa Dungu, ambao Profesa Kahyarara alisema una nyumba 439 na umegharimu jumla ya Sh89.5 bilioni.

“Mradi wa nyumba hizo utakamilika Juni mwaka huu na mpaka sasa tumeshatumia Sh50 bilioni,” alisema Profesa Kahyarara.

Kuhusu mradi wa Toangoma wenye nyumba 161, mkurugenzi huyo alisema umetumia gharama ya Sh61 bilioni.

Hata hivyo, Profesa Kahyarara alikiri kutozitangaza nyumba hizo mapema jambo lililozua maswali kwa wabunge kuhusu uhakika wa kuziuza.

Mbali na bei hizo, pia imeelezwa kuwa mvutano wa hisa kati ya NSSF na kampuni ya Azimio ni chanzo mojawapo cha kucheleweshwa kwa mradi wa nyumba zaidi ya 7,000.

Profesa Kahyayara aliiambia kamati hiyo kuwa mradi huo umeshatekelezwa katika awamu mbili na nyumba 3,750 zimeshakamilika kati ya 7,160 za mradi mzima.

Kwa mujibu wa mkataba huo, kampuni ya Azimio iliyotoa ardhi ya hekta 300 inamiliki hisa asilimia 55 huku NSSF iliyowekeza zaidi ya Dola 500 ikimiliki hisa asilimia 45.

Alisema mradi huo ulitarajiwa kukamilika mwisho wa mwaka huu lakini haitawezekana kutokana na dosari za mkataba. Baadhi ya wajumbe wa PAC walihoji sababu ya mkurugenzi wa kampuni ya Azimio kutoonekana kila anapotafutwa.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Kilimanjaro, Shaly Raymond alisema kuchelewa kwa mradi huo kutapandisha gharama kutoka Dola 544 milioni hadi 700 na kuhoji nani atakayelipa, huku pia akihoji sababu za mwekezaji wa Azimio kutokuwapo katika ziara hiyo.

“Angalia hiyo meza kuu, mwekezaji hayupo, wewe mkurugenzi umekuja peke yako, wenzako wako wapi?” alihoji Shaly.

Mbunge Bura alisema kama Azimio hawataki kuonyesha ushirikiano, atafutwe mwekezaji mwingine. “Tulipozungumza na mwekezaji huyu alikubali kupunguza hisa zake kwa sababu amewekeza kidogo. Kama anasumbua, NSSF waangalie namna ya kupata mwekezaji mwingine.”

Akijibu hoja za wabunge, Profesa Kahyarara alikiri kucheleweshwa kwa mradi huku akisema bado wanajadiliana na kampuni ya Azimio.

Alimtetea mwekezaji huyo akisema amekuwa na safari nyingi nje ya nchi na kwamba atakuwepo kwenye kikao cha Januari 26 na mambo yote yatajadiliwa na kutolewa uamuzi.

Kamanda wa trafiki aunga mkono kauli ya Mambosasa



Kamanda wa Kikosi cha Polisi wa Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Muslim ameunga mkono kauli ya kamanda wa jeshi hilo Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kuhusu utendaji kazi wa trafiki.

Haukuishia kuunga mkono tu, Kamanda Muslim amesema askari wa usalama barabarani wanatakiwa kuangalia makosa hatarishi yanayoweza kusababisha kutokea kwa ajali na kuachana na yale yasiyokuwa ya msingi.

Juzi, Kamanda Mambosasa aliwataka askari hususan wa usalama barabarani kutumia busara katika utendaji kazi wao ili kuondoa malalamiko ya uonevu na kuwakandamiza raia na kusisitiza kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda raia na mali zao na kusimamia sheria.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda Muslim alisema askari wote wa kikosi hicho wanaelekezwa kuzingatia makosa hatarishi kwa kuwa kazi kubwa ya kikosi hicho ni kuhakikisha sheria za barabarani zinazingatiwa ili kupunguza ajali zinazogharimu maisha ya watu.

Alisema kuna makosa ambayo hayana athari kulingana na mazingira husika hivyo askari hawana sababu ya kuyapa kipaumbele.

“Naungana kabisa na Mambosasa ila mimi nisitumie neno busara labda niseme askari wakamate makosa hatarishi, mnamkamata vipi dereva kwa kosa la taa mchana au wiper mbovu wakati wa jua kali? Hayo yote hayawezi kusababisha ajali kwa nyakati hizo. Hapo ndipo linapokuja suala na mazingira, wiper zinatakiwa kufanya kazi kipindi cha mvua.”

Kuhusu askari wa usalama barabarani kumsimamisha dereva na kuanza kutafuta kosa, Kamanda Muslim alisema ni muhimu kwa madereva kuzingatia sheria si muda wote wanasimamishwa kwa sababu ya makosa.

“Tatizo ni kwamba madereva wenyewe wameshajenga mtazamo hasi, sio kila wakati askari anapokusimamisha lazima uwe na kosa inawezekana anataka kukupa tahadhari huko unakoelekea sio kuzuri hivyo uongeze umakini.

“Ninachosisitiza madereva wafuate sheria, waache kulalamika. Wakizingatia sheria sidhani kama hao askari watakuwa wanawasimamisha ovyo kama wanavyodai,” alisema Kamanda Muslim.

Pia aliungana na Mambosasa kuwataka madereva wasikubali kutoa fedha kwa askari bila kupata risiti zinazotokana na mashine au fomu namba 101 ya polisi inayofahamika kama ‘notification’.

Kadhalika alisema askari wa pikipiki maarufu kama tigo wataendelea kufanya kazi yao ya kuzuia uhalifu unaohusisha makosa ya jinai na usalama barabarani na kusisitiza kuwa hawana mamlaka ya kutoza faini.

Ukusanyaji wa mapato

Kamanda Muslim alionyesha kukerwa na watu wanaohusisha tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na ukusanyaji wa mapato.

Alisema kazi ya kukusanya mapato inafanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tofauti na tozo zinazokusanywa na kikosi hicho kutokana na uvunjifu wa sheria barabarani.

“Nashangaa wanaosema tunakusanya mapato kwani Jeshi la Polisi lina biashara gani? Sisi tunatoza tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na lengo letu ni kuzuia ajali na kuhakikisha usalama unakuwa wa kutosha katika barabara zetu.

“Tozo hizo zipo kwa mujibu wa sheria na anayepaswa kulipa ni yule aliyevunja sheria na inasimama badala ya kifungo kwa hiyo watu wanapaswa kutambua askari wa usalama barabarani hawakusanyi mapato.”

Hali ya usalama barabarani

Kamanda hiyo alisema hali ya usalama barabarani nchini imeimarika na ajali zinaendelea kupungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema hiyo inatokana na askari wa kikosi hicho kuimarisha ukaguzi na usimamizi wa sheria.

“Nikitolea mfano wa leo (jana) yaani ndani ya saa 24, nchi nzima kuna ajali tatu pekee. Hii ni hatua kubwa na siku nyingine hakuna ajali kabisa hayo ni matokeo ya usimamizi wa sheria kazi inayofanywa vizuri kabisa na askari wa kikosi cha usalama barabarani.

“Usimamizi wa sheria umeongezwa maradufu kwenye maeneo ya kuvukia watembea kwa miguu, nimesisitiza lazima dereva asimame aangalie pande zote ndipo apite hata kama hakuna mtu anayevuka. Kwa magari yanayosafiri ukaguzi unafanyika kabla hayajatoka vituoni na madereva tunawapima ulevi, huko njiani askari nao wanajipanga vizuri.”

Kamanda Muslim alisema jitihada zote hizo zinafanyika kuhakikisha ajali zinapungua au kutokomezwa kabisa.

Alisema, “Hatuwezi kuvumilia watu wapoteze maisha sababu ya madereva wazembe, hatutafungua ‘tuition’ barabarani ya kutoa elimu. Kama unataka elimu acha gari lako nyumbani ukija nalo barabarani na ukavunja sheria neno ni moja tu “kamata” na watalipa faini na wale ambao watakuwa wagumu zaidi kuelewa neno lao ni “funga” hawa tutawafungia leseni zao.”