Saturday, 16 December 2017

Cervical Cancer Saratani ya Mlango Wa kizazi



Saratani ya mlango wa kizazi
Hii ni njia ya kizazi kati ya uke na mji wa mamba.Ugonjwa huu ukijulikana mapema unweza kutibiwa, wakati wa kufanyiwa uchunguzi wa ubwabwa na fupa nyongo.
Nani yumo hatarini
Wanawake wengine wamo hatarini mwa kupata saratani ya mlango wa kizazi:
Wanawake wasioenda kwa uchunguzi wa kila mwaka wa fupa nyongo na ubwabwa
Wanawake walio na “human papillomavirus” HPV au genital warts
Kuvuta sigara, kuwa na ukimwi,na kutokula vyakula bora huweza kusababisha saratani ya mlango wa kizazi.
Dalili ya saratani ya mlango wa kizazi
Hamna dalili zozote mpaka unaposambaa nje ya mlango wa kizazi.
Hali hii ikitokea waweza kuwa:
Kuvuja damu katikati ya siku za hedhi, unaposhiriki ngono au baada ya hedhi kukatika
Kuvuja damu nyingi zaidi ya kawaida.
Ukiona dalili hizi pata ushauri wa daktari.
Saratani ya Utumbo Mpana na Sehemu za Siri za Nyuma
Saratani ya sehemu za siri za nyuma zipo. Huambukiza sehemu za mmeng’enyo (digestive system) wa chakula. Watu wengi wanaopata ugonjwa huu ni wa umri wa zaidi ya miaka 50.
Matibabu yake yameimarika, lakini ni vyema kugundua mapema.Watu wanahitaji kufahamu madhara, dalili na umuhimu wa kupimwa na madaktari wao.
Walio hatarini kupatwa na saratani ya utumbo mpana:
Ajuza wa miaka 50 na zaidi.
Wanaokula vyakula vya mafuta mengi
Walio na maoteo (ndani ya utumbo mpana )
Wanawake ambao washaugua saratani ya matiti, au mji wa mimba au yai la mwanamke
Aliye wahi kuugua saratani ya utumbo mpana
Aliye na mzazi, jamaa au motto aliye na saratani ya utumbo mpana
Aliye na utumbo mpana wenye kiungulia (donda au uvimbe)
Dalili za saratani ya utumbo mpana ni:
Kuvimbiwa, kusokotwa au kujihisi tumbo limejaa sehemu ya chini
Kuhara, kufunga choo au kujihisi haukamilishi haja kabisa
Damu katika kinyesi
Kinyesi chembamba zaidi
Kupoteza uzito bila ya kufahamu kisababu
Kujihisi mchovu kila wakati
Kutapika
Hizi dalili zinaweza kusababishwa na shida nyingine ambazo si saratani. Muulize daktari wako ili ufahamu
Saratani ya Mapafu
Saratani ya mapafu ndio aina hatari ya magonjwa ya saratani, lakini ndio rahisi kuzuia.Uvutaji wa sigara husababisha asilimia 9% kwa 10% ya kesi za ugonjwa huu.Matibabu ya ugonjwa huu yameimarika lakini bado hakuna tiba.Ili kuimarisha afya yako na walio karibu yako usivute sigara.
Pia hakikisha nyumba yako haina 'radon' gesi hatari isababishayo saratani ya mapafu.
Watu wengine wamo hatarini zaidi ya kupata saratani ya mapafu.
Wanaovuta sigara au kiko, na hata usipo vuta moshi ndani, umo hatarini kupata saratani ya domo. Kukaa karibu na mvutaji sigara au kuishi naye ama kufanya kazi katika mazingira yenye moshi huongeza hatari hasa kwa watoto wasio na namna.
Kiwango kingi cha madini ya radon nyumbani mwako.
Kufanya kazi karibu na asbestos, aseniki, uranium au bidhaa kutokana na mafuta.
Kuwa na kifua kikuu.
Ishara ya saratani ya mapafu ni nini?
Kikohozi kisicho kwisha.
Kuumwa na kifua.
Kukohoa damu
Shida ya kupumua au kukorota upumuapo
Nimonia(kichomi) au mkamba usiyokwisha
Uvimbe shingoni au usoni.
Kupoteza uzito wako bila sababu au kutohisi njaa.
Kujihisi mchovi kila wakati.
Ukiwa na mojawapo ya dalili hizi, hasa ikiwa umo hatarini ya kupata huu ugonjwa, mwone daktari.
Saratani ya Mdomo
Saratani ya mdomo husambaa kinywani kwenye ulimi, ufizi, kidakatonge na koromeo.Watu hawatambui ugonjwa huu upesi.Wanaovuta sigara,kuvuta tumbako au kunywa kunywa pombe wamo hatarini mwa kupata sratani yam domo.Unaweza kusaidiwa ili kuwacha sigara au pombe.Ugonjwa huu unaweza kitibiwa ukiuwahi mapema.
Ishara ya saratani ya Mdomo ni kama zifuatazo;
Uvimbe sehemu yoyote mdomoni, ambao hauponiau kutokuwa na damu kwa urahisi.
Kuhisi uchungu au kufa ganzi mdomoni.
Kuhisi uchungu unapo tafuna, kumeza chakula ulimi unapotumika au taya.
Kubadilika kwa sauti yako.
Kuumwa na sikio.
Koo linalowasha bila kupona.
Ukiwa na ishara hizi mwone daktari haraka sana.

Waziri kalemani awawashia moto watendaji Wa TANESCO kanda ya kusini akataa kupokea taarifa ya meneja Wa REA


Na. Ahmad Mmow. WAZIRI wa nishati, Merdard Kalemani jana aliwajia juu watendaji wa TANESCO kanda ya kusini. Huku akikataa kupokea taarifa ya meneja wa wakala wa umeme vijijini(REA), mkoani Lindi, Jackson Lawuo, nakumtaka naibu mkurugenzi mkuu wa TANESCO amchukulie hatua meneja wa TANESCO mkoa wa Lindi.
Kalemani alifikia uamuzi huo kutokana na kutoridhirishwa na hali ya mambo na utendaji wa shirika hilo katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
Miongoni mwa sababu zilizosababisha akatae kupokea taarifa ya meneja wa wakala wa umeme vijijini ni kuchelewa kuanza kwa utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini katika awamu ya tatu mkoani humu.
Kuhusu meneja wa TANESCO mkoa wa Lindi, Johnson Mwigune, waziri Kalemani amemuagiza naibu mkurugenzi mkuu wa TANESCO amchukulie hatua meneja huyo kutokana na kutoridhirishwa na utendaji wake. Hasa kwakushindwa kutoa taarifa kwa wakati kwa waziri mwenye dhamana ya nishati kuhusu hali ya umeme na kuchelewa kuanza utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijiji awamu ya tatu.
Waziri huyo licha ya kumuagiza naibu mkurugenzi huyo, lakini pia alimtaka meneja huyo ahakikishe anamsimamia mkandarasi wa usambazaji umeme vijijini aharakishe zoezi la usambazaji. Huku akiagiza utekelezaji wa mradi huo uanze ndani ya mwezi huu katika vijiji Vilivyopo kwenye mpango huo.
Waziri Kalemani aliyetoa maagizo hayo jimboni Mtama wilaya ya Lindi ameutaka pia uongozi wa TANESCO kanda ya kusini uhakikishe unarekebisha miundombinu ya umeme ndani ya siku tatu. Ikiwamo nguzo za umeme. Akibainisha kuwa tatizo la nguzo linachangia kukosekana upatikanaji umeme kwa uhakika katika baadhi ya maeneo. Japokuwa mashine zakufua umeme zimetengenezwa.
"Umeme unakatika mara kwa mara licha ya mashine kukarabatiwa nakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 15.8 ambazo zingekidhi mahitaji ya mikoa hii ya Lindi na Mtwara, "alisema Kalemani.
Awali mkuu wa mkoa Lindi, Godfrey Zambi katika taarifa yake kwa waziri huyo alieleza kutoridhishwa na utoaji taarifa sahihi za hali ya upatikanaji umeme mkoani humu. Huku tatizo la umeme likiendelea kuwaathiri wananchi, taasisi za umma nakukwamisha shuguli za maendeleo na kiuchumi mkoani humu.

Balozi alnajem amkabidhi diwani bharwani wa vigwaza vifaa vya mil. 4.5



Na Omary Mngindo, Vigwaza
BALOZI wa Kuwait nchini Tanzania Jasem Alnajem amemkabidhi Diwani wa Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Alhaj Mohsin Bharwani mabeseni 100 yenye thamani ya sh. Mil. 4.5 yatayotumika kwa wajawazito wataofika kujifungulia kwenye Zahanati iliyopo Kijiji cha Vigwaza.
Mabeseni hayo yenye sabuni, poda na vifaa vyote muhimu kwa ajili ya matumizi ya mtoto anayezaliwa ni sehemu ya vifaa ambavyo mpango wake ulizinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Hassani Suluu kwa kushirikiana na Ubalozi huyo wa Kuwait.
Akizungumza na wananchi hao, Balozi Alnajem kwanza alielezea furaha yake ya kufika Vigwaza kukutana na wakazi hao, pia ameangalia madhari ya eneo hilo huku akisema kuwa kufika kwake Vigwaza kumetokana na juhudi za Diwani huyo kumtafuta ofisini kwake kisha kumwelezea changamoto zinazowakabiri wananchi waishio Kijiji cha Vigwaza na Kata hiyo kwa ujumla.
Aliongeza kuwa amefika Vigwaza lengo kusaidia Mama na mtoto na wananchi si kujitangaza na kuwa hatua hiyo imetokana na kuguswa na changamoto alizoelezwa na Diwani wao, pia ataendelea kusaidi sekta ya afya na elimu huku akisisitiza misaada iwafikie walengwa wa mpango huo na kuwa uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Kuwait utaendelezwa kwa maslahi ya nchi na watu wake.
Kwa upande wake akizungumza baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo, Bharwani alianza kwa kumsukuru Balozi kwa msaada huo unaolenga kuwasaidia mama wajawazito wanaojifungulia katika Zahanati hiyo huku akisema utakuwa msaada walengwa wanaofika kwa ajili ya kupata huduma hiyo na kwamba anaimani vitatumika kama malengo yalivyokusudiwa.
"Mabeseni haya mabeseni 100 yatawasaidia wajawazito kabla ya kujifungua na baada ya kujifungua vyote vinagharimu kiasi cha sh. Mil. 4.5, hii ni sehemu ya mpango uliozinduliwa na Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluu kwa kushirikiana na Ubalozi wa Kuwait hapa nchini nasi Vigwaza tumeambulia msaada huu" alisema Bharwani.
Aidha Diwani huyo aliongeza kuwa mbali ya vifaa hivyo pia Balozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu amezindua mpango mwingine unayogusa watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), miguu, mikono pamoja na wasioona ambapo amekabidhi miwani, magongo, baskeli yenye mataili manne pamoja na mafuta kwa wenye ulemavu wa ngozi vyote vikiwa na thamani ya sh. Mil. 13.
"Nilipokutana na Balozi nilimgusia mambo mbalimbali yakiwemo sekta za maji, afya pamoja na elimu ambazo sisi wana-Vigwaza bado tunauhitaji mkubwa wa huduma hizo kutoka kwa wadau, katika kufanikisha hili la leo namshukuru sana ndugu yangu Muna amenipatia ushirikiano mkubwa, asingekuwa yeye nisingeonana na Balozi," alisema Diwani huyo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Thomas Mollel alielezea shukrani zake kwa Balozi huyo kwa kuona umuhimu wa kufika ndani ya wilaya hiyo huku akisema misaada hiyo itatumika kama ilivyokusudiwa huku akiwaomba wataosimamia zoezi hilo kuhakikisha wanalitekeleza kwa walengwa na si vinginevyo.

Friday, 15 December 2017

Yanga na Timu ya Polisi kucheza Jumapili badala ya Jumamosi

Mechi ya kirafiki iliyopangwa kuchezwa kesho Jumamosi kati ya Yanga na Polisi Tanzania itachezwa keshokutwa Jumapili.

Awali, mechi hiyo ilipangwa ichezwe kesho Jumamosi maalumu kwa Yanga kuangalia nyota wake baada ya kufanya mazoezi.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata salehjembe, mechi imehairishwa kuchezwa mechi hiyo iliyopangwa ichezwe Uwanja wa Taifa kutokana na nyasi kufyekwa bila ya viwango ambazo ni fupi zaidi.

Meneja Mkuu wa Yanga, Hafidh Saleh alithibitisha hilo kwa kusema kuwa "Mechi yetu tuliyopanga tucheze kesho Jumamosi itachezwa Jumapili na siyo Jumamosi kama tulivyopanga baada ya kutokea matatizo.

Guardiola aweka rekodi kushinda tuzo ya kocha bora

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ameendelea kuweka rekodi katika ligi kuu ya soka nchini England (EPL) baada ya kushinda tuzo ya kocha bora wa mwezi Novemba.


Kwa kushinda tuzo hiyo leo, Guardiola sasa ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kuchukua tuzo hiyo mara tatu mfululizo. Mhispania huyo ameshinda katika miezi ya Septemba, Oktoba na Novemba ambayo ameshinda leo.

Pep amechukua tuzo hiyo leo akiwashinda waliokuwa wapinzani wake kwenye kuwania tuzo hiyo Antonio Conte, Sean Dyche, Jurgen Klopp, Jose Mourinho na Arsene Wenger.

Jumatano wiki hii Pep aliweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kushinda michezo 15 mfululuizo kwenye EPL na kuzikaribia rekodi zake mwenyewe ambazo amewahi kuziweka kwenye ligi za La Liga (16) na Bundesliga (19).

Ulega akamata tani 11 za samaki wakiandaliwa kusafirishwa nje

Mwanza. Naibu Waziri wa Uvuvi, Abdalla Ulega, leo Ijumaa amefanya ziara ya kushtukiza katika soko la kimataifa la samaki la Kirumba jijini Mwanza na kukamata tani 11 za samaki waliokuwa wakiandaliwa kusafirishwa nje ya nchi kinyume cha sheria.

Shehena hiyo ya samaki  ambao hawaruhusiwi kuvuliwa kisheria, wanadaiwa kuwa walitaka kusafirishwa kwenda nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) kupitia mpaka wa Rusumo mkoani Kagera.

Pamoja na kukamata samaki hao, naibu waziri huyo pia ameagiza kuondolewa mara moja kutoka sokoni hapo maofisa uvuvi kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waliokuwa na dhamana ya kusimamia ukaguzi katika soko hilo kwa kushindwa kutimiza wajibu.

Iniesta hana tatizo na Neymar kwenda Madrid

KIUNGO mkongwe wa Barcelona, Andres Iniesta amesema hana hofu kuhusu Neymar kujiunga na Real Madrid lakini akakiri kuwa ikitokea hivyo haitampendeza kutokana na uhusiano wa Neymar na mastaa wengine wa Barcelona wakati alipokuwa akiichezea timu hiyo.

Iniesta amecheza na Neymar kwa miaka minne kabla ya mchezaji huyo kuondoka na kuhamia Paris Saint- Germain lakini kumekuwa na taarifa za kuwaniwa kwa ukaribu na Real Madrid.
 “Chochote kinaweza kutokea kwenye soka, kuna mambo ambayo yalionekana ni magumu kutokea na yakatokea, sitashangaa lakini haitapendeza kwa kuwa kwa kuwa ni mchezaji mzuri lakini sina hofu,” alisema Iniesta.

Mwenyekiti wa zamani wa CCM apata dhamana

Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wenzake watano wamefanikiwa kupata dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Ni baada ya Wakili wa Serikali, Shedrack Kimaro kuwasilisha cheti kutoka Kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ambapo kimeipa mamlaka mahakama hiyo ya Kisutu kusikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo, washtakiwa hao walisomewa mashtaka mapya matano mahakamani hapo leo Ijumaa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Katika mashtaka hayo mawili ni ya kusambaza dawa bandia za kufubaza makali ya ukimwi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, uzembe wa kuzuia kosa kutendeka na kusababisha hasara.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa walikana na wapo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wanaominika, kila mdhamini akisaini bondi ya Sh 12 milioni.

Pia washtakiwa hao watoe fedha taslimu Sh 12 milioni ama mali isiyo hamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.
Facebook Tw

Diamond azidi kukimbiza Afrika Mashariki


Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.

Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.
 

Diamond azidi kukimbiza Afrika Mashariki


Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.

Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Kwa sasa wimbo wa ‘Waka’ unaweka rekodi ya kuwa wimbo wa kwanza kutrend namba moja kwa nchi tatu za Afrika Mashariki kwenye mtandao wa YouTube.

Video hiyo mpaka jana usiku ilikuwa ndiyo video inayotazamwa zaidi mtandaoni (Trending) kwa kushika namba moja kwa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania.

Wimbo wa ‘Waka’ awali ulipotoka ulikaa siku mbili kwenye mtandao wa YouTube hapa Tanzania  bila kukaa kwenye namba 1 ya video zinazotrend hapa nchini. Lakini mpaka sasa video ya wimbo huo yenye siku saba mtandaoni ipo namba moja kwenye Trending.

Awali rekodi ya video iliyotrend namba 1 kwa nchi mbili tofauti tofauti ilikuwa ilikuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB , Salome ya Diamond Platnumz na Video ya wimbo wa ‘Seduce Me’ wa Alikiba ambapo video zote wakati zinatoka zilishika namba moja Tanzania na Kenya kwa muda tofauti tofauti.

Komando Jide azidi kudata na Spicy


BAADA ya mwanadada ‘lejendari’ kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ kufanya vyema na Ngoma ya Together Remix akiwa na mpenzi wake, Spicy, staa huyo amejipanga kutengeneza naye ngoma tena.




BAADA ya mwanadada ‘lejendari’ kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ kufanya vyema na Ngoma ya Together Remix akiwa na mpenzi wake, Spicy, staa huyo amejipanga kutengeneza naye ngoma tena.

 Akizungumzia stori hiyo, Jay Dee alisema kwamba ameamua kurudi tena na Spicy na ngoma mpya ya Baby baada ya kolabo ya Together Remix kufanya vizuri ambapo anaamini itampeleka mbali zaidi kimuziki kuliko alipo kwa sasa.


“Nimeamua kumganda Spicy kwa sababu ninaamini ni mwanamuziki mzuri na muungano wetu huwa unafanya vizuri, angalia ngoma iliyopita na hii utagundua kwamba tunapokuwa pamoja tunatengeneza kitu kizuri sana,”alisema Spicy.

 Akizungumzia stori hiyo, Jay Dee alisema kwamba ameamua kurudi tena na Spicy na ngoma mpya ya Baby baada ya kolabo ya Together Remix kufanya vizuri ambapo anaamini itampeleka mbali zaidi kimuziki kuliko alipo kwa sasa.

Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza








Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza  tangu awasili wiki hii nchini Singapore kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.

Kiongozi huyo aliyekuwa  madarakani kwa miaka 37 ameonekana akiwa amezungukwa na walinzi wake huku kwa mbele akionekana mwanamke ambaye inaaminika atakuwa mke wake, Grace Mugabe.

Picha za tukio hilo zinamwonyesha akiwa amevalia shati jeupe na suruali nyeusi wakati mtu anayedhaniwa kuwa mke wake akiwa katika vazi jekundu na beki ya mkononi lenye rangi ya zambarau.










Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza  tangu awasili wiki hii nchini Singapore kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.

Kiongozi huyo aliyekuwa  madarakani kwa miaka 37 ameonekana akiwa amezungukwa na walinzi wake huku kwa mbele akionekana mwanamke ambaye inaaminika atakuwa mke wake, Grace Mugabe.

Picha za tukio hilo zinamwonyesha akiwa amevalia shati jeupe na suruali nyeusi wakati mtu anayedhaniwa kuwa mke wake akiwa katika vazi jekundu na beki ya mkononi lenye rangi ya zambarau.

Walinzi wake pia wameonekana kuvalia katika hali ya kawaida ikiwa mashati na suruali. Mara nyingi Mugabe pamoja na walinzi wake wa karibu huonekana wakiwa wamevalia suti isipokuwa wakati alipokuwa akishiriki shughuli za chama au katika sherehe za uhuru.

Canavaro kumbe hana wasiwasi na Simba

Beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema licha ya Simba kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, lakini bado kikosi chao kina nafasi kubwa ya kutetea ubingwa.

Canavaro amesema tofauti ya pointi mbili kati yao na Simba wanaongoza ligi ni kitu kilicho ndani ya uwezo wao kuiweza kuwashusha na sasa wanajipanga vyema kwa hatua hiyo.

Mkongwe huyo alisema mazoezi wanayofanya sasa ni maalum kwa kuhakikisha ligi itakavyoanza wanakuwa tayari ambapo endapo wenzao waliokuwa katika Micchuano ya Kombe la Chalenji watajiunga mapema watakuwa na maandalizi kamili kwa ligi.

Beki Yanga awapasha wakosoaji



 

Beki Yanga awapasha wakosoaji

Beki wa Yanga Juma Abdul amesema matokeo mabaya waliyopata kikosi cha Kilimanjaro Stars, Watanzania hatupaswi kulaumiana bali tunatakiwa kujiuliza tulipokosea.

Abdul ambaye amewahi kuitumikia timu hiyo, amesema hakuna sababu ya kuendeleza lawama kwa makocha na watu wengine, ambapo tathmini ya kina inatakiwa kufanyika kujua wapi tulipokosea kama nchi katika soka letu.

Aidha Abdul amesema bado hajafikiria kuitumikia timu ya taifa, lakini ataendelea kujituma ili kusubiri kuitwa kwa mara nyingine na makocha wa timu za taifa.