
Shehena hiyo ya samaki ambao hawaruhusiwi kuvuliwa kisheria, wanadaiwa kuwa walitaka kusafirishwa kwenda nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) kupitia mpaka wa Rusumo mkoani Kagera.
Pamoja na kukamata samaki hao, naibu waziri huyo pia ameagiza kuondolewa mara moja kutoka sokoni hapo maofisa uvuvi kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waliokuwa na dhamana ya kusimamia ukaguzi katika soko hilo kwa kushindwa kutimiza wajibu.
No comments:
Post a Comment