Friday 15 December 2017

Beki Yanga awapasha wakosoaji



 

Beki Yanga awapasha wakosoaji

Beki wa Yanga Juma Abdul amesema matokeo mabaya waliyopata kikosi cha Kilimanjaro Stars, Watanzania hatupaswi kulaumiana bali tunatakiwa kujiuliza tulipokosea.

Abdul ambaye amewahi kuitumikia timu hiyo, amesema hakuna sababu ya kuendeleza lawama kwa makocha na watu wengine, ambapo tathmini ya kina inatakiwa kufanyika kujua wapi tulipokosea kama nchi katika soka letu.

Aidha Abdul amesema bado hajafikiria kuitumikia timu ya taifa, lakini ataendelea kujituma ili kusubiri kuitwa kwa mara nyingine na makocha wa timu za taifa.

No comments:

Post a Comment