Sunday, 10 December 2017

Alberto Msando aikosoa UVCCM




Wakili msomi, Alberto Msando ambaye alijiunga na (CCM) amefunguka na kuwachana vijana wa chama hicho UVCCM baada ya viongozi wake kumdanganya  Dkt. John Pombe Magufuli juu ya idadi wa vijana wao.

Albert Msando aliomba nafasi kwa Rais Magufuli ili aweze kuwasema vijana wa CCM baada ya moja ya taarifa yao kusema wapo vijana wa CCM zaidi ya milioni sita jambo ambalo linapingana na taarifa zao wenyewe.

"Nimeazima taarifa ya utekelezaji na mpango mkakati naona mmesema kwamba UVCCM mpo milioni sita, je ni kweli? Kama vijana mtakuwa mnafanya mambo kama haya tutakuwa na nchi ya hovyo sana na chama cha hovyo sana, mmeandika takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya vijana wenye umri kati ya 14-35 ni asilimia 34 ya watu wote nchini. mara tu baada ya ukurasa wa nane, ukurasa wa tisa mmeandika kundi la vijana ni kubwa takwimu zinaonyesha sasa wamefikia asilimia 65 ya idadi ya watu nchini ina maana hatujijui tupo wangapi? alihoji Msando

Wakili Msomi Msando aliendelea kuonyesha mapungufu hayo ambayo yalikuwa na lengo la kumdanganya Rais John Pombe Magufuli

"Kwenye kitabu hiki mmemwambia Rais Magufuli kuwa vijana wa UVCCM mnafika milioni sita lakini kwenye jedwali la kweli mmeandika idadi ya vijana wa UVCCM kila mkoa 2013/2017 jumla walio hai ni milioni moja laki sita wasio hai ni laki nne sasa kwanini mumdanganye Rais?  Tukafanye kazi na hizi ndiyo takwimu zenu sasa hivi mnamwambia Rais tunakaribia milioni sita mnataka Rais aondoke akiwa na picha ya kuwa mpo zaidi ya milioni sita wakati mpo milioni moja laki tano, jamani hatuendi hivyo tunakata CCM mpya ya vijana wachapa kazi, wanachama wote ambao hawapo hai warudi, tupate wanachama wapya" alisema Msando.

ACT -Wazalendo wasitisha mchakato wa uchaguzi mdogo



Chama cha ACT -Wazalendo kimesitisha mchakato wa uchaguzi mdogo wa majimbo matatu na kata sita kikisubiri uamuzi wa Kamati Kuu.

Kaimu Katibu Mkuu wa ACT -Wazalendo, Dorothy Semu katika taarifa kwa makatibu wa mikoa ya Tanga, Tabora, Ruvuma, Arusha, Iringa, Pwani na Singida amesema kamati ya uongozi ya chama hicho katika kikao cha dharura cha Desemba 8,2017 mjini Dar es Salaam imetoa maelekezo mawili.

Amesema mosi; kwamba viongozi wa mikoa, majimbo na kata zenye uchaguzi wasitishe mchakato wa kushiriki uchaguzi mdogo.

Pili; Dorothy amesema mikoa itapokea maelekezo kuhusu uchaguzi mdogo kutoka ofisi ya katibu mkuu baada ya Kamati Kuu ya ACT -Wazalendo kukutana hivi karibuni.

Amesema kamati ya uongozi ya Taifa imefikia uamuzi huo kutokana na hali iliyotokea wakati wa uchaguzi mdogo wa kata 43 uliofanyika Novemba 26,2017.

Baadhi ya yaliyojitokeza amesema ni pamoja na kubinywa kwa demokrasia na vurugu zilizotokea katika maeneo mbalimbali.

“Hivyo, kamati kuu itafanya tathmini ya uchaguzi mdogo wa kata 43 na kutoa mwelekeo wa chama juu ya uchaguzi wa majimbo matatu na kata sita unaoanza mchakato Desemba 12,2017 na kukamilika Januari 13,2018,” amesema.

Mwananchi:

Hii ndio zawadi ya Manara kwa Papii Kocha baada ya kutoka jela



 Jumamosi ya December 9 2017 ni siku ya furaha kwa watanzania na wapenzi wa muziki wa dansi kwa ujumla, hiyo inatokana na Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kutangaza msamaha kwa wafungwa wakiwemo msanii Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na Mwanae Papii Kocha.

Rais Magufuli ametangaza msamaha kwa Babu Seya na mwanae Papii Kocha akiwa mjini Dodoma katika maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania na muda mchache baada ya taarifa hizo kutoka watu mbalimbali tumeona wakioneshwa kufurahishwa na uamuzi huo wa Rais Maguli.

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa club ya Simba Haji Manara ni moja kati ya watu waliooneshwa kufurahishwa na maamuzi hayo na kaamua kuandika hivi kupitia ukurasa wake wa instagram katika picha ya Papii Kocha akiwa kavaa jezi ya Simba.

“Nchi imezizima sababu yenu . Mungu ametenda miujiza kupitia kwa Rais wetu..uliitangaza Simba hadi gerezani..ntakuvalisha jezi mpya iliosainiwa na wachezaji wote🙏🙏…ila Wenger bado hajatwaa taji…. kama ulivyomuacha🙇🙇”>>> Haji Manara

Huo ni ujumbe wa Haji manara kupitia ukurasa wake wa instagram, kama utakuwa unakumbuka vizuri Babu Seya na watoto wake watatu akiwemo Papii Kocha walihukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka 2004 baada ya kukutwa na hatia ya kesi ya kubaka na kunajisi watoto 10.

Umoja wa kiarabu waitaka Marekani kufuta uamuzi wake kuhusu Jerusalem



Umoja wa kiarabu katika mkutano wake uliofanyika mjini Cairo umetolea wito Marekani kutupilia mbali uamuzi uliochukuliwa kuhusu jiji la Jerusalem.

Mawaziri wa mambo ya nje katika Umoja wa Kiarabu wametolea wito Marekani kutupilia mbali uamuzi kuhusu Jerusalem , uamuzi ambao unakiuka mikataba ya kimataifa iliyosainiwa kuhusu mji wa Jerusalem.

Umoja wa kiarabu unasema kuwa uamuzi wa Trump ni hatari na una kiuka mikataba ya kimataifa.

Wito umetolewa kwa ulimwengu mzima kukemea uamuzi wa Trump.

Kufuati uamuzi huo, Marekani haina vigezi kuwa mpatanishi katika mzozo baina ya Israel na Palestina.

Marekani yazidi kupata tabu kufuatia suala la mji wa Jerusalem



Ghasia zazuka mbele ya ubalozi wa Marekani baina ya waandamanaji na Polisi katika maandamano mjini Beyruth nchini Lebanon.

Ghasia rimeripotiwa kutokea  mbele ya ubalozi wa Marekani mjini Beyruth  nchini Lebanon.

Maandamano hayo ymaefanyika kwa lengo la kuonesha ghadhabu kufuatia  uamuzi wa Marekani kutangaza kutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Polisi ililazimika kutumia gesi ya kusababisha machozi ili kuwasambaratisha waandamanaji waliokuwa wakielekea  katika ubalozi wa Marekani.

Kiongozi wa mamlaka ya wapalestina akataa kukutana na makamu wa rais wa Marekani



Kiongozi wa mamlaka ya wapalestina Mahmud Abbas hatokukutana na  makamu wa rais wa Marekani Miğke Pence katika ziara yake Mashariki ya Kati.

Mshauri wa nmasula ya kisiasa wa Mahmud Abbas  Bwana Majdi Haldi amesema kuwa uamuzi huo wa kiongozi wa mamlaka ya wapalestina kutokuonana na makamu wa rais wa Marekani umechukuliwa kufuatia uamuzi wa Trump kutangaza kuwa seirikali yake anatambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Mike Pence anatarajiwa kufanya ziara Palestina ili kuzungumzia  mazungumzo ya amani.

Korea Kaskazini yawekewa vikwazo na Korea Kusini


Korea Kusini imetangaza vikwazo vipya dhidi ya mashirika 20 mengine ya Korea Kaskazini, na watu kadha, ili kujibu jaribio la kombora pamoja na mradi wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Wizara ya fedha ilisema hatua hizo zinalenga kuzuia fedha kugharamia mradi wa silaha, kinyume cha sheria.

Karibu mashirika na watu hao wote, yamo katika sekta za benki na safari za meli, na tayari yamepigwa marufuku na Marekani.

Hatua hiyo inachukuliwa majuma mawili baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya kufyatua kombora ambalo linasemekana linaweza kufika pahala popote pale nchini Marekani.

Rais Magufuli aweka saini nyaraka za msamaha kwa wafungwa



Rais John Magufuli ametia saini nyaraka za msamaha alioutoa kwa wafungwa 61 waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa na wawili Nguza Viking (Babu Seya) na Johnson Nguza (Papii Kocha) waliohukumiwa kifungo cha maisha jela.

Rais Magufuli ametia saini nyaraka hizo leo Jumapili Desemba 10,2017 Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Msamaha huo aliutoa jana Jumamosi Desemba 9,2017 katika maadhimisho ya Uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara).

Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kazi nzuri ya kurekebisha tabia za wafungwa.

Taarifa ya Ikulu imesema Rais Magufuli amesisitiza kuwa pamoja na kutolewa msamaha huo, vyombo vya dola viendelee kusimamia sheria.

Amelitaka Jeshi la Magereza kuhakikisha linawatumia wafungwa kuzalisha mali, yakiwemo mazao ya kilimo na kufanya kazi za ujenzi.

“Nimeona nitumie kifungu hiki cha Katiba -Ibara ya 45 (1) ambacho nilipewa na Watanzania, ingawa kilikuwa hakijawahi kutumika, unajua mtu ambaye alihukumiwa kunyongwa halafu baadaye anaachiwa, ni kitu kinashangaza kwa sababu hakijawahi kutokea, lakini nimeona nifanye hivyo kwa ajili ya Watanzania,” amesema.

Rais Magufuli amesema, “Muendelee kusimamia wajibu wenu na kusimamia sheria, mtu anayehukumiwa kufungwa afungwe kweli, na nilishatoa wito kwa magereza, pasiwepo wafungwa wa kukaa tu na kupumzika, wafanye kazi, kufungwa si kustarehe.”

Akizungumzia hilo, Kamishna Jenerali wa Magereza Dk Juma Malewa amemshukuru Rais kwa kutoa msamaha huo wa kihistoria.

Amesema wafungwa na maofisa Magereza wameipongeza hatua hiyo ambayo itasaidia kuwatia moyo wafungwa wanaorekebishwa tabia katika magereza nchini.

Kamishna Jenerali Malewa amesema wafungwa waliopatiwa msamaha wa kuachiwa huru, waliruhusiwa kutoka magerezani tangu jana.

Amesema maofisa Magereza wamewaasa kwenda kuonyesha mfano bora kwenye jamii watakakokwenda kuishi.

Wakati huohuo, Rais Magufuli amelipongeza Jeshi la Magereza kwa kutekeleza agizo lake la kutengeneza viatu kwa ajili ya askari badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi.

Jeshi la Magereza linazalisha jozi 150 za viatu kwa siku katika kiwanda cha Karanga kilichopo Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kwa kushirikiana na mfuko wa hifadhi ya jamii wa PPF, jeshi hilo limeanza kuboresha kiwanda hicho ili kufikia uzalishaji wa jozi 450 kwa siku.

Mwananchi:

Hii ndio sababu itakayompelekea Guardiola kustaafu



Kocha wa Manchester City Pep Guardiola, amesema atastaafu kufundisha soka endapo kitafika kipindi ambacho timu atakayokuwa anaifundisha itashindwa kucheza mfumo wake wa kumiliki mpira yaani (TIKTAKA).

Guardiola ameyasema hayo kwenye mkutano na wanahabari kuelekea mchezo wa leo wa ligi kuu ya EPL dhidi ya mahasimu wao Manchester United. Alipoulizwa atafanya nini endapo aina ya soka analofundisha halitafanya kazi, amejibu, “nitastaafu”.

"Kama hilo litatokea, nitastaafu kwa sababu sitajisikia vizuri kuona mpira hauchezwi vizuri”, ameongeza kocha huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich.

Mtaalam huyo wa ufundi raia wa Hispania amesisitiza kuwa anatamani kuona mpira ukichezwa zaidi kuliko aina nyingine ya mbinu hivyo hawezi kuendelea kufunisha wakati kitu anachokifurahia hakipo tena.

“Tangu mchezo wangu wa kwanza na timu B ya Barcelona nilifundishwa kucheza soka la kuvutia hadi naanza kufundisha soka timu B ya Barcelona nilifundisha ‘TIKTAK’ na nilifanya hivyo na timu ya wakubwa na timu zingine nilizofundisha”, amemaliza Guardiola.

Saturday, 9 December 2017

BREAKING: ''Kuanzia leo Babu Seya aachiwe huru'' - Rais Magufuli

BREAKING: ''Kuanzia leo Babu Seya aachiwe huru'' - Rais Magufuli

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

It’s been quite the year for hip hop. It was finally identified as the most consumed genre in America and made helped break a few records along the way. So it should come as no surprise that hip hop has dominated the top earning spots on Forbes’ highest paid musicians list of 2017. They publication recently released their annual list and some of hip hop & R&B’s most revered artists of this year landed on the top spots.

According to Forbes, Diddy, Beyonce and Drake claim the top three spots while The Weeknd came in at number four. Diddy had his best year so far, income wise, with $130 million before taxes. Much of that credited to his Bad Boy Family Reunion Tour, Ciroc and the estimated $70 million he earned by selling a third of Sean John clothing. As the only other artist to make nine figures this year, Queen Bey came in with $105 million, which they say is due to the Formation World Tour. Although it wrapped up in 2016, it still ended up on her calendar and she made $250 million off it alone. Drake comes in at third with $94 million, largely due to his highly successful “Boy Meets World” Tour.

The Weeknd came $2 million short of Drake in earnings, making $92 million which they say is predominantly due to his Live Nation advance from touring.

Along them, Jay-Z hit number 19 on the list, making $42 million which ties him with Celine Dion.

Overall, it’s been a good year for hip hop and clearly, it’s been getting people paid out here.

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

DOWNLOAD