Sunday 10 December 2017

Korea Kaskazini yawekewa vikwazo na Korea Kusini


Korea Kusini imetangaza vikwazo vipya dhidi ya mashirika 20 mengine ya Korea Kaskazini, na watu kadha, ili kujibu jaribio la kombora pamoja na mradi wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Wizara ya fedha ilisema hatua hizo zinalenga kuzuia fedha kugharamia mradi wa silaha, kinyume cha sheria.

Karibu mashirika na watu hao wote, yamo katika sekta za benki na safari za meli, na tayari yamepigwa marufuku na Marekani.

Hatua hiyo inachukuliwa majuma mawili baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya kufyatua kombora ambalo linasemekana linaweza kufika pahala popote pale nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment