Thursday, 2 November 2017

Julio aanza majigambo




KOCHA MKUU WA TIMU YA DODOMA FC YA DODOMA, JAMHURI KIHWELU ‘JULIO’,.

KOCHA Mkuu wa timu ya Dodoma FC ya Dodoma, Jamhuri Kihwelu ‘Julio’, amesema matokeo mazuri ambayo timu yake inapata katika mechi za Ligi Daraja la Kwanza yanatokana na wao kujipanga na si kubebwa kama baadhi ya wadau wanavyosema.

Akizungumza na gazeti hili jana, Julio, alisema kuwa anaamini kikosi chake kina nafasi ya kupanda daraja na kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao kwa sababu wamejipanga kuendelea kupambana ili watimize malengo waliyoyaweka.

Beki na kocha huyo wa zamani wa Simba alisema pia ligi hiyo ni ngumu na ina changamoto mbalimbali huku akiweza wazi kukukutana na ushindani kwenye michezo yote wanayocheza.

“Hakuna mechi rahisi, tunapambana katika kila mechi, hatubebwi, hata ukiangalia matokeo yetu, mechi nyingi tulizoshinda tumecheza ugenini, tutaendelea kupambana tutakaporudi kumalizika michezo ya nyumbani," alisema Julio.

Baada ya juzi kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Toto Africans, Dodoma FC imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa na pointi 18, ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine katika kundi lao ikiwamo Alliance ambayo imekuwa mshindani.

Timu sita kutoka katika Ligi Daraja la Kwanza zitapanda daraja na kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao wa 2017/18

Omog hafukuzwi ng’o: Simba



KAIMU RAIS WA KLABU HIYO, SALIM ABDALLAH "TRY AGAIN.

WAKATI mkataba wa Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, ukiwa umebakiza miezi minne kumalizika na hakuna mazungumzo yoyote ya kusaini mkataba mpya yaliyofanyika, Kaimu Rais wa klabu hiyo, Salim Abdallah "Try Again", ameibuka na kusema kuwa kocha huyo hafukuzwi.

Minong'ono ya kutimuliwa kwa Omog imeendelea kwa kasi baada ya kutua kwa Mrundi Masoud Djuma Irambona, ambaye amerithi mikoba ya Jackson Mayanja aliyeamua kuachia ngazi na kurejea kwao Uganda kumaliza matatizo ya kifamilia.

Akizungumza na Nipashe jana, Salim, alisema kuwa Omog bado ni kocha wa Simba na hakuna kikao chochote ambacho kimefanyika na kufikia uamuzi wa kumtimua kocha huyo raia wa Cameroon.

Salim alisema kuwa mpaka sasa timu yao haijapoteza mchezo wowote kwenye ligi na anawaomba wote ambao wanafikiria Omog ataondoka kwenye klabu hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, kwa sasa waache kuwaombea "mabaya".

"Kuna watu wana ndoto na matarajio ambayo hatuwezi kuwazuia kuyafikiria, hatujafungwa, tunaongoza ligi, ligi ni ngumu msimu huu, sio ya kawaida, timu nne zote zinalingana pointi, haijawahi kutokea," alisema Salim ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kundi la Friend's of Simba.

Hata hivyo, Salim alikataa kuweka wazi kama klabu ina mpango wa kumpa mkataba mpya Omog ambaye aliwahi kuifundisha Azam FC, lakini akikiri kuwa waliwahi kufanya mazungumzo na Kocha Mkuu wa Lipuli FC, Selemani Matola ili kuchukua nafasi ya Mayanja.

"Mkataba ni siri kati ya sisi na kocha, hatuwezi kuweka hadharani, ila tuna mkataba naye mrefu, hatuna mpango wa kumfukuza, pia siwezi kusema kesho kitatokea nini, anaweza yeye akaamua kuachana na sisi na kwenda mahali kwingine," alisema Salim.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa Omog na msaidizi wake wanafanya kazi kwa ushirikiano na tayari wameshaanza kutoa mapendekezo ya kuimarisha kikosi cha timu hiyo kuelekea dirisha dogo la usajili.

"Omog ametupa ubingwa wa FA, tukamaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita, kwa sasa Simba iko vizuri, hakuna migogoro na viongozi tunajenga mifumo imara na sahihi, tunataka kuiendesha klabu kisasa, tunaachana na kufanya mambo kwa mazoea," aliongeza kiongozi huyo.

Kikosi cha Simba kinatarajia kuondoka jijini kesho kuelekea Mbeya kwa ajili ya kuwafuata wenyeji wao Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kupigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Sokoine jijini humo

Nafasi za kazi leo November 2

Basi lagonga kichwa cha tren




Kada Maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Jimbo la Mtera Mkoani Dodoma amewasihi Watanzania kumpuuza Mwanasiasa Lazaro Nyalandu ambaye juzi ametangaza kujivua nyadhifa zake zote katika CCM ikiwemo ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa kile alichodai Serikali kukigandamiza Chama na CCM kupoteza mwelekeo.

Lusinde amesema Bw. Lazaro Nyalandu hakuwahi kunyimwa nafasi yoyote ya kutoa maoni yake ama dukuduku zake ndani ya chama wala bungeni na kwamba uamuzi huo unaashiria kuwa anatafuta kinga ya kutochukuliwa hatua kutokana na tuhuma nzito zinazomkabili.

Kada huyo wa CCM amesema ana wasiwasi ndani ya Serikali wapo watendaji ama viongozi wasio waaminifu ambao watakuwa wamevujisha taarifa za hatua ambazo Serikali inatarajia kuzichukua dhidi kutokana na makosa makubwa aliyoyasababisha alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na alipokuwa Naibu Waziri

Lusinde Amchana Nyalandu



Kada Maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Jimbo la Mtera Mkoani Dodoma amewasihi Watanzania kumpuuza Mwanasiasa Lazaro Nyalandu ambaye juzi ametangaza kujivua nyadhifa zake zote katika CCM ikiwemo ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa kile alichodai Serikali kukigandamiza Chama na CCM kupoteza mwelekeo.

Lusinde amesema Bw. Lazaro Nyalandu hakuwahi kunyimwa nafasi yoyote ya kutoa maoni yake ama dukuduku zake ndani ya chama wala bungeni na kwamba uamuzi huo unaashiria kuwa anatafuta kinga ya kutochukuliwa hatua kutokana na tuhuma nzito zinazomkabili.

Kada huyo wa CCM amesema ana wasiwasi ndani ya Serikali wapo watendaji ama viongozi wasio waaminifu ambao watakuwa wamevujisha taarifa za hatua ambazo Serikali inatarajia kuzichukua dhidi kutokana na makosa makubwa aliyoyasababisha alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na alipokuwa Naibu Waziri

Mwanamuziki huyu afariki Dunia

Mwanamuziki Keith Wilder(65) amefariki dunia. Wider alikuwa akifanya vizuri na bendi yake ya Heatwave  kipindi cha miaka ya 70.

Kupitia bendi yake hiyo wameshafanya hits song kama “Always and Forever,” “Boogie Nights” na “The Groove Line”, chanzo cha kifo chake kimetajwa kuwa ni matatizo ya kiafya.

Taarifa ya kifo cha mkongwe huyo wa burudani imetolewa na binamu yake Billy Jones, ambaye ameeleza kuwa siku ya Jumapili marehemu alikuwa amelala na ndipo kifo kilipomkuta.

Kupitia band yake wameshawahi kushiriki tuzo kubwa duniani za Grammys mara mbili ila hawakuwahi kushinda tuzo hizo.


Ajira za afya zasitishwa



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu 

Dar es Salaam. Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imesitisha ajira mpya za kada ya afya zilizoombwa kwa kipindi cha Agosti mwaka huu.

Taarifa iliyotolewa Oktoba 31 na Tamisemi ikieleza kusitisha ajira hizo kwa walioitwa kazini.

Taarifa hiyo iliwataarifu waajiri na waombaji wote wa nafasi za ajira za kada za afya kuwa imesitisha zoezi hilo kwa muda mfupi ili kukamilisha taratibu za ajira.

“Tafadhali rejeeni tangazo letu lenye Kumb. Na CD. 162/355/01 la tarehe 30 Oktoba, 2017 lililowataarifu waombaji wa kazi wa nafasi mbalimbali za kada za afya walioomba kazi kuanzia 25/07 - 30/08/2017,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imethibitishwa kutolewa na Naibu Katibu Mkuu Tamisemi, Zainabu Chaula ambaye aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli wamesitisha kwa muda kwa sababu za kiufundi na halihusiani na madaktari wa Kenya.

Hivi karibuni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema kwamba kumekuwa na upungufu wa watumishi wa afya hivyo wapo katika mikakati ya kuhakikisha wanaajiri upya watumishi.

Alisema kwamba wizara yake kupitia kibali cha Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, walitangaza nafasi za kazi 3,152 kwa wahitimu wa kada za afya nchini.

“Wizara ina jukumu la kuwapangia vituo vya kazi waombaji wenye sifa kwa mujibu wa waraka wa maendeleo ya utumishi namba moja wa mwaka 2009 kuhusu muundo wa utumishi ya kada ya chini ya wizara ya afya,” alisema waziri huyo.

Hata hivyo Waziri Ummy alipoulizwa jana kuhusu kusitishwa kwa ajira za kada ya afya katika halmashauri hakujibu chochote na hata alipoulizwa tena idadi kamili na kwa nini ajira hizo zimesitishwa pia hakujibu hadi tunakwenda mitamboni.

Viongozi wawili wa Acacia wajiuzulu



Dar es Salaam. Wakati utekelezaji wa makubalino baina ya Serikali na Barrick ukisubiriwa, Ofisa Mtendaji Mkuu na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya Acacia, wametangaza kujiuzulu kuanzia leo Alhamisi.

Kwenye barua yake, Ofisa Mtendaji Mkuu, Brad Gordon amesema anataka kurudi nyumbani Australia kusimamia masuala ya familia yake wakati Ofisa Mkuu wa Fedha, Andrew Wray akisema amepata fursa nzuri zaidi sehemu nyingine.

“Pamoja na uamuzi huo, wote wataendelea kuhudumu kwenye nafasi hizo wakati wakikabidhi majukumu ya ofisi kwa warithi wao,” imesema taarifa ya Acacia iliyotolewa leo Alhamisi asubuhi.

Kuziba nafasi hizo, Bodi ya Wakurugenzi wa Acacia imemtangaza Peter Geleta kuchukua majukumu ya ofisa mtendaji mkuu baada ya Gordon na Jaco Maritz kusimamia masuala yote ya fedha za kampuni hiyo.

Wote wawili walikuwa watendaji wa Acacia kwa muda mrefu. Geleta alikuwa mkuu wa oganaizesheni wakati Maritz alikuwa meneja mkuu wa idara ya fedha.

“Licha ya majukumu ya uendeshaji, Geleta atahudhuria vikao vya bodi vitakavyofanyika mwishoni mwa mwaka huu badala ya Gordon na kuifanya idadi ya wajumbe kuendele akubaki saba,” imesema taarifa hiyo.

MAGAZETI YA LEO 2/11/2017

Mama yake Dogo Janja azungumzia ndoa ya mwanaye


Mama mzazi wa msanii Dogo Janja Bi. Zaituni Omari, amesema habari za mtoto wake kuoa ni za kweli na yeye kama mzazi alimpa baraka zote, vinginevyo asingeweza kuoa.

Mama yake Dogo Janja ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari na kusema kwamba yeye kama mzazi ameridhika kwani pia ametimiza matakwa ya dini.

“Alishawahi kuniambia kuwa anataka kuoa na mimi nikampa baraka zote, alivyokuwa tayari alinijulisha akaniambia kama kuna uwezekano niende isipokuwa kuna mambo yakaingilia kati, ila kwa vile Madee ni kama baba yake na ninamuamini sana nikawaruhusu waendelee, kila anachofanya hafanyi yeye kama yeye lazima kiko nyuma yangu, sio stori za kiki ni kweli kaoa na hawezi kuoa bila kuwasiliana na familia yake”, amesema mama yake Dogo Janja.

Kuhusu suala la tofauti ya umri kati yake na Irene Uwoya, mama yake Dogo Janja amesema kwamba suala la umri halijalishi sana isipokuwa kikubwa ni maelewano.

“Nimeridhika kwa sababu hata dini yetu ya Kiislam Mtume Mohamad alioa mwanamke mkubwa, kwa hiyo umri haujalishi, kikubwa na maelewano”, amesema Mama yake Dogo Janja.

Ijumaa ya wiki iliyopita kulianza kuonekana kwa picha mtandaoni zinazoonyesha Irene Uwoya na Dogo Janja








Tuesday, 31 October 2017

Haji Manara avutiwa na mbinu za kocha wa Yanga

Ni mara chache sana kusikia kiongozi au hata shaki wa Simba na Yanga kusifia timu pinzani kutokana na utamaduni wa vilabu hivyo ulivyo hata kama watatakiwa kupongeza, leo October 31, 2017 Haji Manara amesema waziwazi kukubali mbinu zilizotumiwa na kocha wa Yanga George Lwandamina kwenye mchezo wa Yanga vs Simba Jumamosi iliyopita.

Manara amesema Lwandamina ni mtu wa mbinu na alifanikiwa katika mbinu zake za kujilinda na kushambulia kwa kushtukiza ambapo  timu hizo zilitoka sare ya kufungana 1-1, Simba walianza kupata goli la kuongoza lakini Yanga wakasawazisha dakika mbili baadaye.

“Yanga walicheza vizuri tena kwa nidhamu, kocha wao ni mtu wa mbinu sana alikuja kupaki ‘basi’ kwa heshimba ya kuiheshimu Simba lakini akazitumia vizuri ‘counter attack’, walicheza vizuri bila shaka kwa sababu walikuja kama underdogs wakatuheshimu, wakapaki basi lao vizuri.”

Manara amewaambia Yanga kwamba, kushangilia kwao matokeo ya sare ya 1-1 yanadhihirisha Simba ni klabu kubwa Tanzania.

“Yanga ni imu kubwa, hamuwezi kwenda kucheza na Simba kamawanyonge lakini baada ya matokeo ya 1-1 wakashangilia na hiyo ndiyo inayonipa tatu. Tuliwazidi umiliki wa mpira 58% kwa 42%. Sisi hatukuridhika kutoka sare na Yanga na hatutaridhika kutoka sare na timu yoyote Tanzania kwa sasa hivi kwa sababu tuna kikosi kizuri.”

Zitto Kabwe ameachiwa huru

Zitto Kabwe ameachiwa huru

Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameachiwa huru kwa dhamana na kutakiwa kuripoti siku ya Jumanne saa tatu asubuhi kwa Mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya jinai (DCI) jijini Dar es Salaam.

Mwanasheria wa Zitto Kabwe amesema kuwa mpaka sasa mteja wake anatuhumiwa kwa makosa mawili tofauti likiwepo kuchapisha taarifa kinyume cha sheria ya mitandao lakini kosa jingine ni kutoa takwimu za uongo kinyume na kifungu cha 37 (5) cha sheria ya takwimu ya mwaka 2015 hivyo mwanasheria anasema Zitto Kabwe amehojiwa na kutoa maelezo yake hivyo wanasubiri kujua kama watakwenda mahakamani.

Kwa upande wake Zitto Kabwe amefunguka na kusema kwa sasa wanasubiri kuona wanapelekwa mahakamani ili waweze kujadiliana huko na kusema kama wao kuna makosa ambayo wanayaona kwake sehemu pekee ambayo wanaweza kwenda kufafanua vizuri ni mahakamani na kudai kuwa kama asingekamatwa angeshangaa kwa kuwa tayari Rais alikuwa ameshatoa agizo.

"Tunasubiri ni lini watatupeleka mahakamani kwa ajili ya kutetea masuala ambayo tumezungumza lakini ya ziada ni kama ambavyo Mwanasheria amezungumza kwa hapa ni makosa mawili ya Sheria ya Takwimu na Sheria ya makosa ya mitandao, wananchama waendelee kuwa watulivu tu kwa sababu kila mtu alitarajia kuwa tutakamatwa kwa kuwa Rais alisema kuwa nikamatwe hivyo tusingekamatwa ningeshangaa, la ziada ni kwamba tusubiri mahakamani itakuaje" alisisitiza Zitto Kabwe
Mbali na hilo kiongozi huyo wa ACT Wazalendo amewataka wanachama pamoja na viongozi wa chama hicho kuendelea na harakati za uchaguzi mdogo wa udiwani na kusema endapo wakishinda katika uchaguzi huo ni kitu ambacho kitakuwa faraja kwao