Mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling akikosa bao la wazi kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya wenyeji, Burnley leo Uwanja wa Turf Moor timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Man City ilitangulia kwa bao la Danilo dakika ya 22 kabla ya Johann Berg Gudmundsson kuisawazishia Burnley dakika ya 82.Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Saturday, 3 February 2018
Man City yaambulia sare mikononi mwa Burnley
Mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling akikosa bao la wazi kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya wenyeji, Burnley leo Uwanja wa Turf Moor timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Man City ilitangulia kwa bao la Danilo dakika ya 22 kabla ya Johann Berg Gudmundsson kuisawazishia Burnley dakika ya 82.New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods
New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods

New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods
Justin Timberlake just delivered his fifth studio album Man Of The Woods and now he doubles down with an official music video for the project’s title-track featuring a cameo by his wife Jessica Biel, directed by Paul Hunter.

New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods
Justin Timberlake just delivered his fifth studio album Man Of The Woods and now he doubles down with an official music video for the project’s title-track featuring a cameo by his wife Jessica Biel, directed by Paul Hunter.
Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download
Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download

Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download
Yanga yajihakikishia ushindi dhidi ya Lipuli leo

KOCHA wa Yanga, George Lwandamina, amesema kama watashindwa kupata ushindi kwenye mchezo wa leo dhidi ya Lipuli ya Iringa watajiweka pabaya katika kuutetea ubingwa wao msimu huu.
Lwandamina, alisema kuwa kwenye mchezo wa leo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, wana kila sababu za kuhakikisha wanapata ushindi ili kuendelea kuifukuzia Simba inayoongoza ligi.
Yanga itaingia kwenye uwanja huo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 18 tangu Lipuli ilishuka daraja mwaka 1999 na kuwafanya mashabiki wa mkoa wa Iringa kushindwa kuziona timu kubwa na kongwe zenye mashabiki wengi, ikiwemo Yanga.
“Ni mchezo mgumu kama ilivyo michezo mingine, tupo ugenini lakini kwa namna mambo yalivyo ni lazima tupambane ili kutoongeza pengo la pointi na wanaoongoza ligi,” alisema Lwandamina.
Yanga imeachwa kwa pointi saba na Simba wenye pointi 35 huku Azam wanaoshika nafasi ya pili wakiachwa kwa pointi tano na vinara hao, kikosi cha Lwandamina kinashika nafasi ya tatu kwa kuwa na pointi 28.
Mchezo wa leo utamshuhudia mshambuliaji Ibrahim Ajibu akirejea uwajani baada ya kuukosa mchezo wa kombe la FA dhidi ya Ihefu, muunganiko wake na Obrey Chirwa unatazamiwa kuwa chachu ya ushindi kwa mabingwa hao watetezi.
Canavaro anena
Kuelekea kwenye mchezo wa leo, nahodha wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Canavaro’, amesema watahakikisha wanapambana mpaka dakika ya mwisho kuhakikisha wanapata ushindi.
“Tulitoka sare kwenye mchezo wetu wa kwanza Dar es Salaam, hiyo inaonyesha Lipuli si timu ya kuibeza, kama wachezaji tutahakikisha tunakuwa makini na kupambana muda wote,” alisema Canavaro.
Naye kocha wa Lipuli, Selemani Matola, aliiambia Nipashe kuwa wamejiandaa vyema kuwakabili mabingwa hao watetezi.
Askari Magereza watiwa mbaroni wakidaiwa kuua
KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA, EDWARD BUKOMBE.
ASKARI 12 wa Jeshi la Magereza wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wanahojiwa na polisi kwa tuhuma za mauaji yaliyochochewa na ugomvi wa mapenzi.
Askari hao wanadaiwa kumshambulia mkazi wa kijiji cha Kerenge wilayani hapa, Aloys Makalla na kusababisha kifo chake mwishoni mwa mwezi uliopita huku wakiwa wamevaa kininja.
Katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, imedaiwa kuwa saa chache kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa amepigana na mmoja wa askari.
Kamanda Bukombe alisema tukio hilo lilitokea Januari 28 na kwamba askari 12 wa Magereza wanahojiwa na polisi katika upepelezi wake.
“Ni kweli tumepata taarifa za tukio hilo la mauaji ya mwanakijiji huyo na askari 12 tunawachunguza kupata ukweli wake, ili kuona kama kuna wanaohusika hatua ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Kamanda Bukombe.
Akihadithia mkasa wa mauaji hayo, mkazi wa kijiji cha Kerenge, Juma Salim, alisema marehemu alikuwa na mzozo wa muda mrefu na askari Magereza mmoja (jina tunalihifadhi) wakituhumiana kuingiliana katika penzi la mmoja wa wanawake kijijini hapo.
"Na siku hiyo (mzozo huo) ulizusha vurugu kubwa," alisema Salim.
Salim alisema katika ugomvi huo kati ya askari na Makalla, Magereza huyo alijeruhiwa na kurudi kwenye makazi yao lakini baada ya muda alirejea kijijini hapo na wenzake wakiwa wamevalia kininja na kuwapiga wenyeji.
Baadaye walimkamata Makalla waliyemtuhumu kumpiga mwenzao na kuondoka naye, alisema Salim.
Naye Jeniffer Leonard, mkazi mwingine wa Kerenge alisema askari hao waliondoka na Makalla kwa madai ya kumpeleka kituo cha polisi lakini walishangaa kupata taarifa za kifo chake baadaye.
HAKUMTAJA JINAAkielezea tukio hilo, Kamanda Bukombe alisema taarifa zinaonyesha kutokea ugomvi baina ya askari ambaye hata hivyo hakumtaja jina wala cheo chake na marehemu huyo, hali iliyosababisha Magereza kujeruhiwa.
Bukombe alisema baada ya kujeruhiwa, askari huyo alikwenda kambini kuchukua wenzake ambapo walirudi kwa mara ya pili na kumkamata marehemu, kumpakia kwenye gari na kuondoka naye kwa madai ya kumpeleka kituo cha polisi.
Kamanda Bukombe alisema taarifa kutoka kwa askari Magereza zinadai wakati wakiwa njiani, marehemu aliruka kutoka kwenye gari hiyo na kuanguka barabarani ambako alifikwa na mauti.
“Tunachunguza upi (ndiyo) ukweli wa marehemu," alisema Kamanda Bukombe. "Kauawa kwa kipigo cha askari hao ama (ni) kifo kinachotokana na kuanguka kwa kuruka kwenye gari."Mambo hayo ndiyo tunayoyachunguza tupate ukweli.”
Alisema matokeo ya uchunguzi huo ndiyo yatakayoamua kama kuna hoja na ukweli kwamba askari wamehusika na kifo cha marehemu na hatua zitachukuliwa, ikiwemo kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote.
Makamu wa Rais aguswa na Cover ya wimbo wa Nandy na Aslay

Makamu wa Rais, Bi Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa na wasanii Nandy na Aslay.
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana jioni aliwakaribisha nyumbani kwake wasanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ na Faustina Charles maarufu kama Nandy kwa ajili ya mazungumzo mafupi na chakula cha jioni.
Katika mazungumzo yake na wasanii hao, Bi Samia alieleza kuvutiwa sana na marudio ya kibao cha SUBALKHERI kilichorudiwa na wakali hao wa Bongo Fleva hivi karibuni na kuwapa wosia wa kuendelea kufanya kazi nzuri zaidi na kujiepusha na makundi mabaya.
Esma aweka wazi mahaba yake kwa Wema Sepetu

Esma Abdul ‘Esma Platnumz’
MWANADADA Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ ameonesha mahaba yake kwa staa mkubwa wa filamu Bongo, Wema Sepetu akidai kuwa, amekuwa shosti wake kwa muda mrefu na hivyo hawezi kujitenga naye.
Akipiga stori na gazeti hili, Esma alisema Wema ametoka naye mbali kiasi kwamba leo hii hawezi kumuweka pembeni na kujiweka zaidi kwa wifi wake wa sasa, Zarina Hassan ‘Zari’.
“Jamani Wema hata kidogo siwezi kumuweka pembeni, hata kama aliachana na kaka yangu lakini kwangu bado ana umuhimu. Kama kila anayeachana na kaka basi
niwe naye mbali, nikifa inabidi nikazikwe Uganda au Sauzi maana Bongo sitakuwa na rafiki,” alisema Esma
Kauli ya kocha wa Simba yamwacha mdomo wazi Tambwe

KAULI ya Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma, aliyedai kwamba atafurahi zaidi kama straika wake Emmanuel Okwi atafunga mabao 30 msimu huu, imemshitua mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe.
Tambwe ambaye anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi katika msimu wa 2015/16 akifunga mabao 21, baada ya kusikia kauli hiyo ya Djuma alisema; “Siyo kazi rahisi Okwi kufunga mabao 30.”
Akizungumza na Championi Jumamosi, Tambwe alisema ili Okwi ambaye hivi sasa anaongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 12, aweze kufikisha mabao 30, anatakiwa kufunga katika kila mechi atakayocheza.
“Siyo kazi rahisi kwa Okwi kufunga mabao 30, kwani mzunguko wa pili ligi huwa ni ngumu sana, kila timu hupambana kuhakikisha inafanya vizuri ili kuwania ubingwa, nyingine zinapambana zisishuke daraja.
“Inabidi Okwi apambane kwelikweli na ajitahidi pia kufunga katika viwanja vya mikoani lakini kama ataendelea kutegemea Uwanja wa Uhuru na ule wa Taifa pekee, itakuwa ni vigumu kufikisha mabao hayo,” alisema Tambwe.
Uchebe akana madai ya kuwa Sangoma

Mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ akiwa na mume wake Ashrafu Uchebe.
MUME wa mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ Ashrafu Uchebe amekana kuwa mganga (Sangoma) wa kutumia vitabu na kuweka wazi kuwa kazi yake ni ufundi wa magari.
Maelezo hayo yamekuja kutokana na madai yaliyokuwa yumeenea kwamba, mbali na kufanya mambo mengine lakini pia anatibu kwa kutumia Quran na amekuwa akifanya hivyo tangu alipokuwa Zanzibar.
Akizungumza na Risasi Jumamosi, Uchebe alifunguka hivi: “Kama unavyojua kumuombea mtu dua ni jambo la kawaida lakini anayesaidia ni Mungu, hata wewe nakuombea tu dua na Mungu ndiye anasaidia ila hilo la kuwa mganga sijawahi, kazi yangu ni fundi wa magari,” alisema Uchebe
Jokate afunguka kuanzisha familia mwaka huu

Jokate Mwegelo
MWANAMITINDO ambaye ni kada wa CCM, Jokate Mwegelo baada ya kuanika kuwa mwaka huu ni sahihi kuingia kwenye maisha ya ndoa, ameibuka tena na kuanika kuwa 2018 ni mwaka wa kuwa na familia pia.
Akiongea na Risasi Jumamosi Jokate alisisitiza kuwa mwaka huu ni wa neema kwake na kufafanua kuwa ana mpango wa kuanzisha familia yake.
“Watu wajue tu kuwa mwaka huu nitaanzisha familia, sio kama ninawafumba lakini kwa uwezo wake Mungu wataona tu, wakae wakisubiri kwani lisemwalo lipo kama halipo linakuja,” alisema Jokate ambaye hakuweka wazi mwanaume atakayemuoa na kuanzisha naye familia
Mrema awatolea uvivu UKAWA

Mwenyekiti wa chama cha TLP Lyatonga Augustino Mrema amefunguka na kusema kuwa UKAWA hawampendi wala hawamtaki ndiyo maaana walifanya kila namna kuhakikisha wanampokonya jimbo la Vunjo kwa kumsimamisha James Mbatia katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Mrema amesema hayo jana Januari 2, 2018 akiwa kwenye kampeni za kumnadi mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni kupitia chama cha TLP, Dokta Godfrey Malisa na kusema kuwa wapinzani nchi hii wamekuwa wakimchukia.
"Ni kweli kwamba UKAWA hawanipendi, hawanitaki wakaninyang'anya lile jimbo wakampa James Mbatia angekuwa basi anafanya kazi za wananchi wa Vunjo wala nisingelalamika. Angelikuwa mwaminifu kwa Rais wetu wala nisingehangaika wala kulalamika, lakini walininyang'anya jimbo kwa ulaghai na utapeli kwa maneno ili kunimaliza kwa wananchi wa Vunjo wakasema Mrema ni mzee na kweli ni mzee ila kuwa mzee siyo kosa wala siyo dhambi kwamba wazee hawana manufaa" alisema Mrema
Mbali na hilo Mrema aliendelea kusema
"Hawa UKAWA wananiita marehemu mtarajiwa ndiyo wenzangu kwa hiyo wakaninyanyasa, wakanizodoa na ndiyo maana nawaambia UKAWA wakiendelea na tabia hii ya kuwakataa wazee kama Mrema kama hawana lolote, hamtakaa mpate kura za wazee wa nchi hii kwa sababu maneno yenu waliyasikia. Kwanini mnatukataa sisi wazee"
Aliyewabagua Waaafrika afutwa kazi

Klabu ya soka ya West Ham imemfuta kazi mkurugenzi wa uajiri wa wachezaji wa timu hiyo Tony Henry kutokana na kauli yake ya kuwabagua wachezaji kutoka Afrika.
Tony Henry hivi karibuni alinukuliwa akisema kuwa timu hiyo haiwezi kusaini wachezaji kutoka Afrika kutokana na wachezaji hao kutowajibika vizuri kwenye baadhi ya majukumu yao.
Taarifa ya klabu hiyo imeeleza kuwa maneno ya Tony Henry sio msimamo wa klabu kwasababu timu haiamini katika ubaguzi wa aina yoyote ndio mana imeamua kumfuta kazi Henry ili hatua zingine zichukuliwe.
West Ham ina wachezaji sita kwenye kikosi cha kwanza wenye asili ya Kiafrika ambao ni Cheikhou Kouyate, Pedro Obiang, Joao Mario, Angelo Ogbonna, Arthur Masuaku na Edimilson Fernandes.
Wengine ni mshambuliaji wa Senegal Diafra Sakho ambaye ameondoka kwenye dirisha dogo la Januari akajiunga na Rennes ya Ufaransa huku Andre Ayew wa wa Ghana akielekea Swansea.
Subscribe to:
Comments (Atom)
