Thursday, 1 February 2018

Umuhimu wa Kujiongeza katika maisha ya mafanikio


Habari za muda huu mpenzi msomaji wa mtandao huu wa dira ya mafanikio, ni matumaini yetu mazima u mzima wa afya tele na unaendelea vyema katika harakati zako za kuweza kulisukuma gurudumu hili la maendeleo.  Ni siku nyingine tulivu ambayo sina budi nikukaribishe kwa moyo mkunjufu tuweze kujifunza kwa pamoja.

Siku ya leo nataka ttuzungumzie namna ambayo una uwezo mwingine wa kutenda jamno jingine ambalo linaweza kukupa mafanikio makubwa kwa upande wako tofati na hilo ulitendalo sasa. Unajua nataka tuzungumzie hili kwa sababu wetu wengi hawafahamu uwezo mwingine walionao, ambao unaweza kuutumia ili uweze kukamilisha jambo jingine ambalo Mwenyezi mungu kakujalia kiulitenda.

Watu wengi hudhani ya kwamba hicho ambacho wanakifanya ndicho ambacho wamepangiwa kufanya. Kwa mfano mtu ni mfanyabishara fulani, labda huenda mtu akawa amesomea kitu fulani, basi baada kuweza kubobea katika kipengekle hicho, basi anaweka mipaka katika kitu hicho pekee.

Ukweli haipo hivyo hata chembe, kwani kila binadamu binadamu kaumbwa  na uwezo mwingine wa kufanya vitu vingi ambavyo vitaweza kumuinua kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ya kimafanikio. Hata kanuni ya kufanya mazoezi ya mwili inasema ya kwamba huwezi kutengeneza six park kwa kufanya mazoezi ya aina moja pekee kila wakati, bali unaweza kutengeza six park kwa kufanya mazoezi ya aina tofauti tofauti.

Kwa  muktadha huo kama kweli unataka kufanikiwa zaidi ya hapo ulipo sasa, unachotakiwa kufanya ni kuweza kutambua uwezo mwingine ambao mwenyezi Mungu kakuwekea ndani yako, ili uweze kujipatia mkate wako wa kila siku.

Hata mwandishi mmoja aitwaye Antony Robbison aliwahi kuandika ya kwamba “if you do what you have done you will get what you always gotten” hii ikiwa na maana “kama utafanya mambo yaleyale ambayo umekuwa  ukifanya siku zote, utapata yale yele ambayo siku zote umeyapata”. Naomba urudie kusoma tena aya hii ili uielewe vizuri.

Kwani aya hiyo ipo wazi kabisa kama umezoea kufanya mambo yale yale kwa njia ile ile basi matokeo yake, yatakuwa ni yaleyale. Hivyo ili uweze kupata matokeo ya iana tofauti  na uliyoyazoea, unachotakiwa kufanya kubomoa uzio wako wa kufikiri kwa kuanza kubadili ratiba ya kutenda mambo yako ya msingi. Lakini pia ongeza uzio wa kufanya mambo yako  kwani binafsi naamini una kitu kingine cha kufanya zaidi ya hicho ambacho unakifanya.

Mwisho nimalizie makala haya kwa kusema ukitaka kwenda mbali zaidi katika mambo yako ya msingi acha kujenga uzio ambao utakufanya ushindwe kuona fursa nyingine,  bali unachotakiwa kufanya ni kubomoa uzio huo ili uweze kuona fursa mbalimbali ambazo zimejificha, kwani pindi unavyoacha ukuta huo ni kule kutengeneza uwezo wako wa kulalamika, na mwisho wa siku kuelekea jehenamu ya umasikini.

Narudia kwa kusema tena pale unaposhindwa kujiongeza ni kutengeneza jehanamu ya umaskini. Usiogope na kusema afisa mipango anakutisha hapana,  ila kazi yangu ni  kukwambia ukweli ambao upo wazi, kwani nafasi uliyonayo sasa unachotakiwa kufanya ni kuwaza ni namna gani utaweza kufika mbali zaidi.

Kwani umuhimu wa kujiongeza kunamsaidia mtu kuweza kuwa milango mingi ya kuweza kufanikiwa zaidi. Pia faida nyingine ya kujiongeza humsaidia mtu kuweza mbunifu zaidi kwa kile akifanyacho. Na ubunifu humsaidia mtu aweze kujilikana na ukijulikana ndo mwanzo wa mafaniko yenyewe. Mpaka kufikia hapo sina la ziada naomba kazi ibaki kuwa kwako kwa kuamua kwenda kuyatekeleza hayo ambayo nimekwambia. Asante.Ni wako katika ujenzi wa mafaniko.


MAGAZETI YA LEO 1/2/2018


















Wednesday, 31 January 2018

UNHCR Yadai wakimbizi 1,200 wakimbilia Tz kutoka Congo


Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi la UNHCR, limedai kuwa jumla ya wakimbizi 1200,raia wa jamhuri ya Demokrasia ya Congo,wameyakimbia mapigano yanayoendelea Mashariki mwa nchi hiyo na kuingia Tanzania.

Aidha shirika hilo limedai Maelfu ya watoto, wanawake na wanaume, wameacha makazi yao kukimbia mapigano dhidi ya makundi yenye silaha ya Mai Mai yanayoendelea Kusini mwa Jimbo la Kivu.

Aidha shirika hilo la umoja wa mataifa limedai mbali na Tanzania,wakimbizi wengine wamekimbilia nchi za Burundi, na Uganda.

Wakati huo huo, inaamika kwamba, kuna wimbi kubwa zaidi la wakimbizi ambao wapo Kivu Kusini wakiwa katika hali mbaya ya kukosa chakula na makazi.


TID: Kuwa karibu na Makonda kumenifanya nikose Show


Msanii wa muziki, TID amelalamika kuwa baadhi ya watu wanamfanyia figisu figisu ili asipate show kutokana na ukaribu wake na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Muimbaji huyo amefunguka hayo katika kipindi cha Eight cha TVE kwa kudai kuwa hali hiyo inampa tabu sana.

“Kuna watu wananibania kupata dili, wengine wanaenda mpaka kwa waandaaji sipati show. Napata dabu kweli,” amesema TID.

TID ameongeza kuwa Mhe. Makonda ni mtu ambaye yuko poa sana na watu na kila anachokifanya anakuwa na uhakika nacho.

Wadau wajadili changamoto ya wataalamu wa dawa za usingizi


Upungufu wa wataalamu wa dawa za usingizi nchini umepelekea Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas) kuanza kufikiria kutoa mafunzo ya uuguzaji wa dawa hizo kwa ngazi ya shahada.

Hatua hiyo ya Muhas kuanza kutoa mafunzo hayo imetokana na upungufu wa madaktari wenye utaalamu huo hasa wakati wa huduma ya upasuaji kuwa mdogo ambapo kwa sasa waliopo ni asilimia 1.2.

Hiyo maana yake ni kwamba katika idadi ya madaktari 2000 ambao wanahitajika kutoa huduma hiyo Tanzania inayo madaktari 30 pekee.

Kufuatia changamoto hiyo leo wadau mbalimbali wa afya na elimu walikutana na kujadili mtaala utakaotumika kufundishia chuoni hapo kabla ya kuupeleka kwa Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU).

" Ni kweli kumekuwepo kwa changamoto hiyo ya watalaamu wa dawa hizo lakini sasa mpango huu ukikamilika maana yake tutaongeza idadi ya madaktari kamili maana hawa waliopo wengi ni wale ambao wamesoma kozi kwa mwaka mmoja au miwili.

" Mafunzo yakianza kutolewa hapa chuoni Muhimbili wataweza kuchukua wanafunzi 200, Bugando 50 na KCMC 50 jambo ambalo litaongeza idadi kubwa ya watalaamu ili kuweza kufikia lengo letu la kuwa na wataalamu 2000 nchi nzima," Alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Mpoki Ulisubisya.

Halmashauri ya Kigamboni yapitisha rasmi sheria zake


Baada ya Halmashauri ya Kigambini kugawanywa mwaka juzi kutokea Temeke, Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo limekutana na kupitisha sheria ndogo tisa ambazo zitatumika kuendesha halmashauri hiyo.

Sheria hizo mpya ambazo ndani yake kuna kanuni ni sheria ndogo za ushuru na huduma, ada na ushuru, matangazo, maegesho, uvuvi na rasimali za bahari ya hindi, masoko na magulio, usafi wa mazingira, burudani na sheria ya kudumu ya halmashauri.

Madiwani hao wamepitisha sheria hizo katika kikao chao cha pili cha robo cha baraza hilo kilichokuwa na ajenda 10 ikiwemo kupitisha sheria hizo na kanuni zake ili kuachana na sheria zilizokuwa zikitumika hapo awali ambazo zilikuwa ni za Halmashauri ya Temeke kabla ya kutenganishwa.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Stephen Katemba alisema mchakato wa kubadilisha sheria na kanuni hizo umepitia ngazi mbalimbali ikiwemo kushirikisha wadau na wananchi kuanzia ngazi ya mtaa hadi ya kata.

" Hizi sheria zikianza kutumika lazima wananchi watambue kuwa zitakua na adhabu kwa wale ambao watazikiuka, na faini ya makosa yake itaanzia Sh 200,000 hadi Milioni moja punde tu ambapo sheria na kanuni hizi zitaanza kutumika miezi michache ijayo," Alisema Katemba.

Kagame aanza kibarua chake cha AU kwa kasi


Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Paul Kagame ameanza kazi yake hiyo haraka baada ya kukutana na viongozi wa jukwaa la Biashara na Uwekezaji ambapo alisisitiza umuhimu wa sekta binafsi kushikishwa kikamilifu kwenye masuala ya utawala.

Kagame ambaye pia ni Rais wa Rwanda alisema Serikali nyingi za Kiafrika awali ziligundua kuwa ni ngumu kuwatumikia wananchi kwa haraka na ubora bila sekta binafsi hivyo akaomba ziungwe mkono ili ziweze kurahisisha maendeleo.

Alisema anaamini mazungumzo yake hayo na wataalamu hao yataenda sawa na vitendo hivyo kutaka sekta binafsi ziungwe mkono ambapo anaamini sasa ushirikiano mkubwa baina ya watawala na sekta binafsi utaendelezwa ili kuongeza chachu ya mafanikio.

" Mfano sisi Rwanda tumeongeza ushirikiano na makampuni ya nje katika kusaidia sekta ya afya hii haina maana kuwa tunabinafsisha hapana bali tunaongeza ubora wa huduma ili kuweza kuwasaidia wananchi wetu kwa haraka zaidi," Alisema Rais Kagame

Sosopi asema dawa ya muhuni ni kuwa muhuni zaidi yake


Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema, BAVICHA, Patrick Ole- Sosopi amekiri kuwa Chama chake kimeamua kurudi kwenye uchaguzi mdogo haswa wa Kinondoni na Siha kwa kuwa wamegundua dawa ya muhuni ni kuwa muhuni zaidi.

Akizungumza kwenye Kampeni za kumnadi Mgombea Ubunge wa Kinondoni Salum Mwalimu Ole-Sosopi amesema kwamba kilichowafanya kususia uchaguzi mara ya kwanza ni kwamba hakukuwa na faida kubwa ya kupatikana kiongozi kwa wananchi wasio na hatia kwa kumwaga damu.

Ole-Sosopi amesema kwamba baada ya kususia uchaguzi ambao uligomewa kupelekwa mbele sasa wagundua kuwa "dawa ya muhuni ni kuwa muhuni zaidi hivyo ifahamike na iwekwe rekodi kuwa CHADEMA tumerudi kushiriki na kufanya uchaguzi".

Mbali na hayo Ole-Sosopi ameongeza kuwa hataki chama chake au kingine kisipendelewe bali waachwe wabishane kwa hoja na mwishowe wananchi waachiwe kufanya maamuzi.

CHADEMA walitangaza kugomea uchaguzi mdogo uliofanyika January 13 kwa madai mbalimbali ikiwepo kufanyia hujuma za wazi katika uchaguzi uliofanyika Novemba 26 huku tume ikilalamikiwa kutofanyia kazi malalamiko hayo.

King Majuto ammwagia sifa Rais Magufuli kwa uimara wake


Msanii mkongwe wa filamu za bongo, Mzee Majuto amefunguka na kudai yeye ndio mtu wa kwanza kutabiri ujio wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi ya Tanzania huku akisisitiza kwamba anajisikia faraja kuona ana misimamo iliyokuwa imara.

Mzee Majuto amebainisha hayo muda mchache alipotembelewa na Rais Magufuli leo katika hospitali aliyolazwa ya Tumaini iliyopo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa tezi dume unaomsumbua kwa kipindi kirefu.

"Mimi ndiyo mtu wa kwanza kumtabiri kwamba akiwa Rais itakuwa shughuli. Nilishukuru sana kuchaguliwa huyu bwana, tumepata Rais sio masihara watu wote sasa hivi wana adabu zao wanajua nini maana ya kazi ukisema jambo watu wanatekeleza, wezi wanakamatwa, wala rushwa wanakamatwa, wenye vyeti feki hata kama amefanya kazi miaka 20 fukuza, hii safi", alisema Majuto.

Pamoja na hayo, Mzee Majuto aliendelea kwa kusema "sisi wazee tunafarijika sasa hivi, viwanda kila kona vimetapakaa na leo amekuja kutembea hospitalini hapa sijui kama wengine hawajikojolea huko kwa uoga maana hataki masihara. Hii ndio raha ya kupata viongozi wenye msimamo".

Kwa upande mwingine, Mzee Majuto amesema kupata sio rahisi kupata Rais mwenye misimamo na asiyekuwa na masihara kama Dkt. John Magufuli.


Nabii Nyakia aeleza jinsi alivyotekwa na watu wasiojulikana


Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Jerusalem lililopo Kitunda jijini Dar, Nabii James Nyakia amesimulia alivyonusa kifo baada ya kutekwa na kuteswa kwa siku kadhaa na watu wasiojulikana.

Tukio hilo la kutisha lilimtokea nabii huyo mwaka jana alipokuwa akitangaza Injili huko Mkuranga mkoani Pwani.

Akizungumza na gazeti hili katika kanisa hilo baada ya kukimbia huko, Nabii Nyakia alisema kuwa, alikuwa katika program ya kutangaza habari njema wilayani humo ndipo siku moja akakutana na kundi ambalo baadaye alisikia ndilo lile la watu wasiojulikana ambao walimkamata akiwa msituni na kuanza kumtesa.

“Nilikuwa nimeamua kwenda kupeleka neon la Mungu vijiji mbalimbali vya Mkuranga.

“Nakumbuka siku moja nilikuwa katikati ya msitu mkubwa kwani Mkuranga imezungukwa na mapori na misitu.

“Nikiwa njiani kwenda kufanya mkutano wa Injili, ghafla walitokea vijana waliokuwa na silaha za kijadi kama marungu na mapanga. Pia kulikuwa na wachache waliokuwa na bunduki.

“Walinieleza kuwa hawakutaka kusikia habari za kueneza injili kwani walisema wao wanataka dini yao tu na nadhani walishanijua kwa sababu muda mwingi kazi hii ya Mungu niliifanyia huko.

“Niliwaomba sana wasiniue, lakini cha moto nilikiona maana kama ni kupigwa, nilipigwa sana. Kwa kifupi mateso hayakuwa ya kawaida.

“Nilichokifanya ilikuwa ni kumuomba Mungu kimoyomoyo na kumwita aniokoe au anipokee mikononi mwake kwani niliamini kama ni kufa, ningekufa nikiwa ninaitenda kazi ambayo Mungu ameniita kwayo.

“Baada ya maombi na mateso ya saa zaidi ya sita, wale jamaa nilisikia wakiambizana kwamba waliachie, lakini kwa onyo kwamba nisiendelee na shughuli hiyo.

“Waliponiachia nilirejea kwa mwenyeji wangu, lakini tulizidi kumwomba Mungu hadi tuliposikia baadhi yao walikamatwa na polisi na wengine kuuawa na sasa kuna utulivu wa kutosha,” alisema Nabii Nyakia akiwa na makovu ya mateso hao kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake.

Chama cha Mitindo chazinduliwa rasmi leo



Baada ya Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) miezi mitatu iliyopita, kutaka wabunifu nchini kuanzisha chama kitachowakutanisha pamoja katika shughuli zao, leo Januari 31, Chama cha Mitindo Tanzania (FAT) kimezinduliwa rasmi.

Akizindua chama hicho, Katibu Mtendaji Basata, Godfrey Mngereza amesema uanzishwaji wake licha ya kuwainua wabunifu wachanga na wakubwa kutambulika kimataifa, utakuza viwanda vya pamba na ngozi nchini ambavyo vitategemea malighafi za ndani.

Mngereza amesema wabunifu wakijengewa utamaduni wa kutumia bidhaa za ndani kama ngozi na nguo kutengeneza mavazi yenye utamaduni wa ndani, wataendana na kauli ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Tanzania ya viwanda. Mngereza amesema Serikali inafanya kazi na chama kinachotambulika kisheria kikiwa kimesajiliwa hivyo kupitia chama hicho wataweza kuelekeza matatizo yao.

Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi (TAFCA), Adrian Nyangamalle amesema watahakikisha wanawasaidia katika changamoto mbalimbali zitakazotokea katika chama hicho.

“Tutatoa ushirikiano sehemu yoyote inayohitajika kuisukuma Serikali ili malengo ya chama hiki yatimie kwa haraka,” amesema Nyangamalle.

Mwanzilishi wa FAT, Asia Idarous amesema wamekuwa na changamoto mbalimbali katika tasnia hiyo, hivyo wanaishukuru Serikali kwa kutaka kuanzisha chama hicho kitakachowaunganisha na Serikali ili kuifikisha Sanaa hiyo kimataifa.

Gigy money aponda utaratibu wa Basata kuhusu video vixen



Gigy Money ameonyesha kutokubaliana na utaratibu wa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) uliowataka ma-video vixen kujisajili katika Baraza hilo.

Muimbaji huyo ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa Basata walimueleza hilo lakini anaona kuna ma-video vixen wengi ambao hawajasalijiwa na wanafanya kazi hiyo.

“Waliniambia hivyo, lakini sasa Hamisa Mobetto anafanya nini, Tunda tuseme anafanya nini, officialnai anafanya nini, ma-video vixen unataka kuniambia wanajulikana Basata, why Gigy kwa sababu umeonekana ashapata chochote kitu,” amesema Gigy Money.

“Basata mtajalije utamaduni wa msanii mkiwa hamjali Ugali wake, haujali mfuko wake, wewe unaniona tu napendeza unajua mimi napoteza shilingi ngapi,”

Gigy Money kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Mimina baada ya kutamba na ngoma ‘Papa’.


Akutwa ameuwawa na mwili wake ukichunwa ngozi



Mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Mpande mkoani Songwe amekutwa amekufa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani huku akiwa amechunwa ngozi na kutolewa baadhi ya viungo vya mwili wake na watu wasiojulikana.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani hapo Yusuph Sarungi amesema ni kweli tukio hilo limetokea na wameweza kubahatika kumtambua kwa jina marehemu huyo kuwa ni Luntinala Tunyepa mwenye umri wa miaka ipatayo 75.

Aidha, Sarungi amesema mpaka sasa chanzo cha tukio la kuuawa mwanamke huyo hakijafahamika huku akisema wanaendelea na msako mkali ili kuweza kuwabaini watu hao waliotenda hivyo.

Msikilize hapa chini Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani Songwe Yusuph Sarungi akielelezea mkasa mzima wa tukio hilo.