Tuesday, 30 January 2018

Wachimbaji wanne wa mchanga wafariki Arusha



Watu wanne wamefariki dunia huku mmoja akijeruhiwa vibaya baada ya mawe kuporomoka na kuwafukia wachimbaji  watano ambao walikuwa wakichimba mchanga kwenye eneo la mlima CCM Kata ya Muriet, Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha (RPC), Charles Mkumbo akiongea na www.eatv.tv amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kudai kuwa majeruhi amepelekwa katika hospitali ya Mount Meru huku hali yake ikiwa ni mbaya sana.

"Kuna eneo lipo huku Kata ya Muriet ambapo huwa wanachimba mchanga mkavu hivyo wakati wanaendelea na kuchimba kuna sehemu nyingine huwa haichimbwi sasa wanasayansi wanatuambia dunia huwa inazunguka hivyo kuna mpasuko ulikuwa umetokea kwenye eneo ambalo wala halichimbwi huo mchanga, hivyo hilo gema lilipopasuka likaangukia upande ambao watu wanachimba mchanga huo na kuwafukia watu watano, wanne walipoteza maisha pale pale huku mmoja akiwa amejeruhiwa vibaya na kupelekwa hospitali ya Mount Meru kupatiwa matibabu" alisema Mkumbo.

EATV

Rostand aiokoa Yanga na aibu kombe la FA


Kipa Youthe Rostand ameibuka shujaa baada ya kupangua penalti 3 na kuiwezesha Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Ihefu ya Mbeya.

Yanga ilikuwa ikiivaa Ihefu katika mechi ya Kombe la Shirikisho iliyochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, leo.

Kipa huyo wa Cameroon amepangua mikwaju mitatu ya penalti wakati wa changamoto za mikwaju hiyo.

Al manusura Yanga ing’olewe baada ya Obrey Chirwa kukosa penalti, lakini kipa huyo Mcameroon akapangua penalti iliyofuata na kuifanya Yanga iendelee.

Yanga ililazimika kuingia kwenye changamoto hizo na timu hiyo ya daraja la pili baada ya kusawazisha katika dakika za majeruhi baada ya kuwa imefungwa bao.

Chirwa ndiye aliyesawazisha kwa mkwaju wa penalti huku Ihefu wakiwa wanaamini mechi ilikuwa imeisha.

'Kama Mollel atashinda Serikali itatatua tatizo la Kilelepori'


Chama cha Mapinduzi (CCM), kimeahidi kumuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba na Waziri wa Ardhi   William Lukuvi, kufika Siha kutatua tatizo la Kilelepori na wananchi wanaozunguka eneo hilo, endapo Dk. Godwin Mollel atashinda.

Akimnadi Dk.Mollel, katika kata ya Donyomurwak, Katibu wa itikadi na uenezi CCM Taifa, Humphrey Polepole, amesema  eneo la Kilelepori ni mali ya Siha, hivyo Chama hicho kikishinda, Serikali itafika ili kuona namna ya kushughulikia mgogoro uliopo kati ya wananchi na  eneo hilo la Kilelepori ambalo limekuwa likitumiwa na shule ya Taaluma ya Polisi Moshi (MPA) kwa mazoezi ya kijeshi.

"Natambua mnakabiliwa na changamoto kubwa na eneo la kilelepori, na hii ni kutokana na wananchi kuendelea kuongezeka na mji kupanuka sasa nipeni Dk.Mollel ili Serikali iweze kushirikiana naye kutatua changamoto hii ambayo inawasumbua muda mrefu" amesema  polepole.

Polepole amesema  siasa za matukio na uongo zimepitwa na wakati hivyo ni vyema wananchi wakatambua Serikali ya chama cha mapinduzi ina dhamira ya dhati ya kuwasaidia na kutatua changamoto zote zinazowakabili.

Akiomba kura Dk.Mollel aliwaomba wananchi wamchague ili aweze kushughulikia tatizo la maabara kwa shule za kata na kuhakikisha zinakuwa na vifaa ili kuwezesha masomo ya sayansi kusomwa kwa vitendo.

Mollel  amesema  pia atashughulikia tatizo la maji na kuhakikisha wananchi wa kata ya Donyomurwak wanasambaziwa huduma ya maji safi na salama kwa matumizi ya kunywa, pamoja na kushughulikia tatizo la umeme na migogoro ya Ardhi.

 Akiomba kura Mgombea udiwani wa Kata ya Donyomurwak, Lwite Ndosi, ambaye hivi karibuni alijiondoa Chadema na kugombea tena nafasi hiyo kupitia chama Tawala, amewaomba  wananchi wamchague tena ili kuweza kushughulika na changamoto zao ambazo ni miundombinu ya barabara, ujenzi wa Bweni la wasichana shule ya Sekondari Sikilari pamoja na ujenzi wa zahanati katika vijiji vilivyopo katika Kata hiyo.

Ndosi ambaye anachuana vikali na aliyekuwa meneja kampeni wake 2015,Sione Mollel (Chadema)alisema akipewa nafasi hiyo, pia atashughulikia mgogoro uliopo baina ya wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka kambi ya Jeshi (Kilelepori) pamoja na kutoa elimu ya mpango mji kijiji cha Munge ambacho kinakua kwa kasi.

"Nimerudi kwa nguvu na kasi mpya, sasa naomba nipeni tena nafasi hii ili niweze kushughulika na changamoto zenu, naahidi pia nitasaidia wananchi ambao wanalalamika maeneo yao kuchukuliwa na Kulelepori ambao ni wa vijiji vya Munge, Emboko, Loiwa na Ormelili"amesema

Akiomba kura mgombea ubunge jimbo la Cuf,Tumsifuel Mwanri, aliwataka wananchi wa Siha kumchagua, kumchagua, kwa kuwa yeye ana msimamo na anaweza kukaa bungeni kuwatumikia wananchi kwa kipindi chote bila kujiuzulu.

Mwanri amesema  katika uchaguzi huo mdogo wapo wagombea Wanne wa vyama tofauti Siha, lakini ni jukumu la wananchi wa Jimbo hilo wakachukua maamuzi sahihi ya kumchagua Mgombea wa Cuf ambaye atawatumikia kwa uaminifu.

"Ndugu wananchi, angalieni kiongozi ambaye atawatumikia kwa uaminifu, kwani mkimchagua mwingine anaweza kukaa tena mwaka mmoja na kujiuzulu na kuturudisha tena kwenye uchaguzi" amesema

Mwanri amesema  endapo atashinda, pia atashughulikia tatizo la maji na kuhakikisha, gharama zinashuka tofauti na ilivyo sasa ambapo inakuwa mzigo mkubwa kwa wananchi.

Aidha amesema  Siha ina  ardhi nzuri yenye rutuba lakini haitumiki ipasavyo, hivyo akichaguliwa atashughulika na tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kushughulikia tatizo la migogoro na kulipatia ufumbuzi.
   

Watumishi wafukuzwa kazi kwa kukaidi agizo la Rais Magufuli


Halmshauri ya wilaya ya Magu mkoani Mwanza imewasimamisha kazi walimu watatu wa shule ya msingi Nenge akiwemo Mwalimu Mkuu na Afisa Elimu Kata ya Nyanguge kwa kosa la kukaidi agizo la Rais Magufuli la kutochangisha fedha wanafunzi.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Magu Lutengano Mwalwiba, amesema kuwa baada ya agizo la Rais Magufuli la kusitisha michango katika shule za msingi, Januari 23 mwaka huu aliwaonya wakuu wa shule na walimu wote, lakini Januari 24 waliendeleza kukusanya michango.

Mwalwiba meongeza kuwa watumishi hao wamekiuka mkataba wa elimu ya msingi bila malipo ambapo wamewachangisha shilingi 500 wanafunzi 378 wa shule hiyo kwa ajili ya lebo zautambulisho wa sare za wanafunzi kinyume na maagizo ya Rais Magufuli.

January 17 mwaka huu Rais John Pombe Magufuli alipiga marufuku michango kwenye shule za msingi na sekondari za serikali, na kuwaagiza Mawaziri Joyce Ndalichako na Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jafo kusimamia agizo hilo.

Sumaye, Sosopi wamnadi Mwalimu leo


Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema, Salum Mwalimu amewaomba wananchi wa Kinondoni kumchagua awahi mkutano wa Bunge la bajeti utakaoanza Aprili, mwaka huu ili awasilishe hoja za maendeleo.

Amesema hayo leo Jumanne Januari 30,2018 alipohutubia mkutano wa kampeni Magomeni Morocco wilayani Kinondoni.

“Msifanye makosa siku ya uchaguzi, waacheni hao wengine wapige kelele. Mkimchagua mbunge dhaifu mtaendelea kubaki dhaifu katika kipindi cha miaka mitano,” amesema Mwalimu.

Amesema yeye ni mfuatiliaji  wa masuala ya  fidia na atakapokuwa mbunge, wananchi wa Kinondoni hawatapata shida kwa kuwa anajua kunusa zilipo fedha kwa ajili ya maendeleo.

Mkutano huo pia ulihutubiwa na viongozi mbalimbali wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye; mwenyekiti wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), Patrick ole Sosopi na mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea.

New VIDEO: Lulu Diva – Amezoea

New VIDEO: Lulu Diva – Amezoea

New VIDEO: Lulu Diva – Amezoea

Audio | Rosa Ree Ft. Billnass – Marathon | Mp3 Download

Audio | Rosa Ree Ft. Billnass – Marathon | Mp3 Download

Audio | Rosa Ree Ft. Billnass – Marathon | Mp3 Download

New VIDEO: Mo music ft Roma – BAJAJI

New VIDEO: Mo music ft Roma – BAJAJI

New VIDEO: Mo music ft Roma – BAJAJI

Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download

Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download

Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download

CSEE – FORM FOUR EXAMINATION RESULTS (Matokeo Kidato cha Nne) 2016/2017




CSEE – FORM FOUR EXAMINATION RESULTS (Matokeo Kidato cha Nne) 2016/2017

CSEE 2017 CLICK HERE

(QT) 2017 CLICK HERE


 

Audio | Mbosso – Alelee | Mp3 Download

Audio | Mbosso – Alelee | Mp3 Download

Audio | Mbosso – Alelee | Mp3 Download


Monday, 29 January 2018

New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are

New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are

New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are


DOWNLOAD VIDEO

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download