Saturday, 27 January 2018

Ujenzi wa reli ya kisasa watarajiwa kuanza Machi mwaka huu


Serikali imesema ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) kutoka Morogoro hadi Makutopora mkoani hapa ambao utaanza kabla ya Machi mwaka huu, utagharimu dola 1.923bilioni za kimarekani (sawa na Sh4.3 trilioni).

Meneja Mradi huo wa Kampuni Hodhi ya Raslimali za Reli (Rahco) Mhandisi Maizo Mgedzi amesema mradi huo unatarajia kuanza wakati wowote kabla ya Machi.

Amesema  treni hiyo ina uwezo wa kwenda kilometa 160 kwa saa itahifadhi mazingira na kwamba itaweza kubeba mzigo mkubwa kwa zaidi ya mara tano ya reli ya sasa.

“Pia itaweza kubeba watu na mizigo kwa usalama kwa maana  hakutakuwa na ajali zinazosababishwa na ubovu wa miundombinu,” amesema

Meneja wa Kampuni ya Yapi Merkezi iliyopewa zabuni ya mradi huo, Abdullah Kilic amesema kuwa jiwe la msingi la mradi huo litawekwa wakati wowote kuanzia sasa.

“Tunachosubiri ni utaratibu wa Ikulu lakini jiwe la msingi tutaliweka wakati wowote kuanzia sasa,”amesema.

Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini, Antony Mavunde amesema Serikali ingependa mradi huo ulete matokeo chanya kwa watu wa Dodoma na si laana.

“Matokeo haya yasiwe laana kwa maana tusije kuiacha reli hii ipite tu hapana. Sisi tunataka kwa watu wa Dodoma reli hii iwe kichocheo cha kwanza cha uchumi ikiwezekana kubadilisha mji,”amesema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Deogratius Ndejembi amesema viongozi watawapa ushirikiano wa kutosha katika kipindi cha miaka mitatu cha ujenzi wa reli hiyo na kurekebishana kwa baadhi ya mambo.

“Wamesema asilimia 80 (watu 3000) watachukua watu wa Dodoma kwa hiyo ni jambo kubwa sana. Hii ni fursa kubwa hata kipindi hiki cha ujenzi,”amesema.

Friday, 26 January 2018

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Lava Lava – Tattoo | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Audio | Foby – Ngangana | Mp3 Download

Rais Trump aombwa kuchukua choo cha dhahabu


 
Choo cha dhahabu alichopendekezewa rais Donald Trump
Jumba la kumbukumbu la Guggenheim mjini New York limekataa ombi kutoka kwa rais Donald Trump la kutaka kupewa mchoro wa msanii Van Gogh ili kuwekwa katika ikulu ya Whitehouse kulingana na vyombo vya habari.

Jumba hilo liliomba msamaha kwa kutoweza kupeana picha hiyo na badala yake likaomba kumpatia rais Trump choo cha dhahabu kulingana na gazeti la The Washington Post.

Lakini jumba hilo la kumbukumbu lilipendekeza limpatie rais Trump kiti hicho cha choo chenye dhahabu karati 18.

Ikulu ya Whitehouse haijatoa tamko lolote.

Kulingana na gazeti hilo,mhifadhi wa vitu katika jumba hiloi Nancy Spector aliojibu ombi hilo la Ikulu mwezi Septemba.

''Naomba msamaha...kukujulisha kwamba hatuwezi kushiriki katika kukupatia picha hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa mkusanyiko wa Thannhauser ambao hawaruhusiwi kutoka nje ijapokuwa kwa maswala yasio ya kawaida'', aliandika katika barua pepe.

Picha hiyo ya 1888 ya Van Gogh, barua hiyo iliongezea itaonyeshwa katika taasisi dada kutokana na ruhusa kutoka kwa wamiliki wake.

Hatahivyo , muhifadhi huyo ameongezea kwamba choo hicho cha dhahabu kilichotengezwa na msaani wa Itali Maurizio Cattelan kiko tayari kwenda Ikulu kwa ''mkopo wa muda mrefu''.

Ni jambo la kawaida kwa marais wa Marekani na wake zao kuomba kazi za usanii ili kupamba baadhi ya vyumba katika Ikulu ya Whitehouse.

Tambwe kuivaa Azam FC kesho?


Straika wa Yanga, Amissi Tambwe raia wa Burundi ameshindwa kufanya mazoezi ya pamoja na wenzake kutokana na majeraha ya goti.

Hali hiyo imekuja ikiwa ni siku chache tangu arejee na acheze mechi dhidi ya Mwadui FC kabla ya kuwavaa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar. Mshambuliaji huyo akiwa amekaa nje ya uwanja huku wenzake wakiendelea na mazoezi.

Mshambuliaji huyo, alipata majeraha hayo juzi Jumatano katika mazoezi ya timu hiyo baada ya kugongana na beki wa pembeni, Juma Abdul na kushindwa kuendelea na programu nyingine.

Kutokana na Tambwe kushindwa kufanya mazoezi ya mwishoni ikiwa ni siku moja kabla ya mchezo huo, upo uwezekano wa Mrundi huyo kuikosa mechi dhidi ya Azam FC.

Katika mazoezi hayo ya jana, benchi la ufundi la timu hilo, lilionekana kuwaandaa baadhi ya washambuliaji watakaocheza nafasi yake ambao ni Juma Mahadhi na Yohana Nkomola.



Rais Magufuli,Mama Janet wamchangia Wastara Fedha za matibabu




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mke wake Mama Janet Magufuli hii leo wamemchangia muigizaji wa filamu Tanzania Wastara Juma shilingi milioni 15, kumsaidia katika matibabu yake.

Fedha hizo ambazo Wastara amekabidhiwa na Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike , sambamba na kiasi kingine cha milioni moja na laki tisa ambayo ni michango kutoka kwa wasaidizi wa Rais.

Msanii huyo amekuwa akisumbuliwa na mguu kwa muda mrefu na alikuwa kaomba msaada wa watanzania mitandaoni ili aweze kwenda nchini India kupatiwa matibabu.

Rais Magufuli anakuwa mtu wa kwanza kutoa fedha nyingi kwa msanii huyo, tangu aanze kutoa rai ya kuomba michango, ambapo wiki iliyopita waziri wa Habari, sanaa, michezo na utamaduni Dkt. Harison Mwakyembe alimkabidhi shilingi milioni moja.
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akimkabidhi fedha Wastara

Kesi ya Tido Mhando yaahirishwa hadi Februari 23


Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando amepata dhamana baada ya kukidhi masharti na kutakiwa kurejea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Februari 23, mwaka huu.

Tido alifikishwa mahakamani hapo saa 5:22  asubuhi na aliingizwa katika ukumbi wa mahakama ya wazi kabla ya kusomewa mashtaka matano.

Leo Januari 26, mwaka 2018 wakili wa Takukuru, Leonard Swai amedai mbele ya hakimu mkazi mkuu wa makahama hiyo,  Victoria Nongwa kuwa Mhando anatuhumiwa kwa mashtaka matano.
Swai amesema Juni 16, 2008 katika maeneo ya Dubai, United Arab Emirates (UAE), Tido akiwa mwajiriwa wa TBC kama Mkurugenzi Mkuu kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa makubaliano kwa ajili ya kuendesha na utangazaji wa vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 group Corporation ( BV1) bila ya kupitisha zabuni kinyume  na sheria ya manunuzi na kuisababishia BVl kupata manufaa.

Shtaka la pili, Tido anadaiwa Juni 20, 2008  katika maeneo ya utekelezaji wa kazi yake alitumia madaraka vibaya kwa kusaini makubaliano (wakuu wa makubaliano) kwa utangazaji wa digital duniani kati ya TBC na BVl.

Shtaka la tatu, Agosti 11, 2008  na Septemba 2008 katika maeneo hayo, Tido anadaiwa kutumia  vibaya madaraka yake kwa kusaini mkataba wa makubaliano (kuongeza wakuu wa mkataba ) kwa ununuzi, usambazaji kufunga vifaa vya usambazaji na mnara wa utangazaji kati ya TBC na BVI na kuisababishia BVI kupata faida.

Shtaka la nne, Tido anadaiwa Novemba 16,2008 akiwa Dubai, United Arab Emirates alitumia vibaya madaraka yake kwa kusini mkataba wa makubaliano (kuongeza wakuu wa mkataba ) kwa kuendesha miundombinu ya utangazaji (DTT broadcast infrastructure) kati ya TBC na BVI na kusababisha BVI kupata manufaa.

Katika shtaka la tano, Tido anadaiwa kati ya Juni 16 na Novemba 16, 2008 katika maeneo hayo ya United Arab Emirates aliisababishia hasara TBC ya Sh 887, 122,219.19.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Tido ambaye anatetewa na wakili Ramadhani Maleta alikana mashtaka yote.

Swai alidai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Hakimu Nongwa alimtaka mshtakiwa kutoa fedha taslimu mahakamani hapo Sh444 milioni ama hati ya mali isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Mbali na sharti hilo, pia awe na wadhamini wawili ambapo watasaini hati ya dhamana ya maneno yenye thamani ya Sh500 milioni na asitoke nje ya nchi bila ya kuwa na kibali cha mahakama.
Mshtakiwa alikamilisha masharti hayo kwa kuwasilisha hati za mali na wadhamini wawili nyakati za saa sita mchana na kuondoka.

Kesi imeahirishwa hadi Februari 23, 2018 kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali (PH).
Kuhusu dhamana hiyo, DPP alipeleka hati ambayo inaipa mamlaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuisikiliza kesi hiyo.

Mhando ni miongoni mwa waandishi wa habari na watangazaji mahiri na wakongwe ndani na nje ya nchi ambaye amewahi kufanya kazi Shirika la Utangazaji Uingereza (BBC).
Pia amewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, Mwanspoti na The Citizen na sasa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Azam Media.

Nyumba za Askari Magereza zatakiwa kukamilika ndani ya miezi mitano


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali mstaafu, Projest Rwegasira ametoa miezi mitano kwa Wakala wa Majengo (TBA) kukamilisha ujenzi wa nyumba za askari wa Jeshi la Magereza zilizoko Ukonga jijini Dar es Salaam.

Ametoa agizo hilo leo Ijumaa Januari 26,2018 alipofanya mazungumzi na maofisa wa TBA na wa Jeshi la Magereza baada ya kukagua ujenzi huo.

“…fanyeni juu chini mhakikishe mradi huu unakamilika ndani ya miezi hiyo mitano mliyosema. Ongezeni nguvu ili mkamilishe mradi huu kwa wakati,” amesema katika taarifa iliyotolewa na wizara.

Fedha za ujenzi wa nyumba hizo unaogharimu  Sh10 bilioni zilitolewa na Rais John Magufuli baada ya kufanya ziara Ukonga mwishoni mwa mwaka 2016.

Soma: Waziri Mkuu aagiza wakala wa majengo Mara kukamatwa

Ujenzi ulianza mwaka jana badala ya Desemba 19, 2016.

NEC yatoa orodha ya wagombea wa udiwani



Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa majina 27 ya wagombea udiwani walioteuliwa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kuwania nafasi hizo katika kata 10.

Uchaguzi mdogo katika kata hizo utafanyika Februari 17,2018 kutokana na baadhi ya madiwani kujiuzulu nyadhifa zao na vifo.

Katika uteuzi huo wanaume waliojitokeza kugombea nafasi hizo ni 24 na wanawake ni watatu.

Taarifa iliyotolewa na NEC leo Ijumaa Januari 26,2018 imesema wagombea wa kata nne waliteuliwa Januari 20 na wengine wa kata sita waliteuliwa Januari 24,2018.

Wagombea waliojitokeza kuwania udiwani katika kata ya Buhangaza iliyoko wilayani Muleba mkoani Kagera na vyama vyao ni Jenitha Tibihenda (CCM), Nelson Makoti (Chadema) na Grayson Aniceth (NCCR Mageuzi).

Katika Halmashauri ya Siha iliyoko mkoani Kilimanjaro ambako kuna kata tatu zitakazofanya uchaguzi mdogo, wagombea katika kata ya Gararagua ni Zakaria Lukumai (CCM) na Agness Lasway (Chadema). Kata ya Donyomuruak wagombea ni Lwite Ndossi (CCM) na Daniel Molle (Chadema), wakati katika kata ya Kashashi wagombea ni Suzan Natai (CCM) na Immanuel Saro (Chadema).

Mkoani Mwanza ambako kuna kata mbili, wagombea wa kata ya Kanbyelele iliyoko Halmashauri ya Misungwi ni Marco Yela (ACT Wazalendo), Daniel Makoye (CCM) na George Mhoja (Chadema). Kata ya Isamilo iliyoko wilayani Nyamagana wagombea ni Nyamasiriri Marwa (CCM), John Kisyeri (Chadema), Hashim Ramadhan (CUF), Georgina Kibendegele (DP) na Ramadhani Mtoro (UDP).

Kwenye kata ya Mitunguruni iliyoko wilayani Singida wagombea ni Abdallah Mkoko (CCM), Manase Kijanga (Chadema) na Abdallah Kinga (CUF).

Wagombea wa Kata ya Madanga iliyoko wilayani Pangani mkoani Tanga ni Mohamed Abdallah (ACT Wazalendo), Athuman Tunutu (CCM) na Swaibu Mwanyoka (CUF).

Mkoani Dodoma ambako pia kata mbili zitafanya uchaguzi, kata ya Manzase iliyoko wilayani Chamwino wagombea ni Amos Mloha (CCM), Alex Chalo (Chadema) na Ndahani Mazengo (Chaumma), wakati kata ya Kimagai wilayani Mpwapwa mgombea ni Noah Lemto aliyepita bila kupingwa.


Hospitali ya Bugando yanufaika na mashine za CT-SCAN


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amezindua huduma za mashine ya CT – SCAN katika hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa Bugando jijini Mwanza,ambazo zilisimama kwa muda wa miaka minne iliyopita, baada ya mashine iliyokuwepo awali kuharibika mwaka 2014.

Mashine hiyo ya kisasa,iliyonunuliwa nchini Ujerumani kwa gharama ya shilingi Bilioni 1.7,imesimikwa na kufanyiwa majaribio na uhakiki kutoka tume ya mionzi Tanzania na kuthibitika kuwa na uwezo wa kufanya kazi ipasavyo.Mashine hiyo kwa mujibu wa daktari bingwa wa mionzi Dk.Godfrey Kasanga itakuwa na uwezo wa kuhudumia wagonjwa 100 kwa siku.

Askofu wa jimbo katoliki la Geita,Mhashamu baba askofu Flavian Kasala,ambaye amemwakilisha Mwenyekiti wa bodi ya uendeshaji ya hospitali hiyo,Mhashamu Askofu Mkuu jimbo kuu la Mwanza Yuda Thadei Rwaichi,amewataka watumishi wa kitengo kitakachosimamia huduma za mashine hiyo kuitunza na kuacha kuihujumu.

Kwa upande wake,Mkurugenzi mkuu wa hospitali ya rufaa ya Kanda ya ziwa Bugando Dk.Abel Makubi ameiomba serikali kuanzisha taasisi ya moyo katika hospitali hiyo ili kupunguza idadi ya wagonjwa kutoka mikoa ya kanda ya ziwa wanaokwenda Dar es Salaam kutafuta matibabu ya moyo katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete.


Wazazi wavamia shule kudai kurejeshewa michango yao


Baadhi ya wazazi katika halmashauri ya mji wa wa Mbinga mkoani Ruvuma wameshindwa kulielewa agizo la Rais John Magufuli la kufuta michango katika shule za msingi na sekondari na  kuvamia shule wakidai kurejeshewa michango yao.

Kufuatia hali hiyo Baraza la halmashauri ya mji wa Mbinga limeitisha kikao cha dharura kujadili changamoto hizo na nanmna ya kuzitatua huku Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Mbinga Donald Msigwa akiwataka madiwani kutopingana na agizo la Rais katika majadiliano hayo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Mbinga mheshimiwa egno Kipwere amesema agizo la Rais halijahalalisha wananchi kudai kurejeshewa michango waliyochangia na halijafuta michango waliyokubaliana wenyewe kuchangia.

Wenger ajigamba kuhusu usajili wake


Kocha wa Arsenal Arsene Wenger amesema timu hiyo haitauza mchezaji bila kununua mchezaji huku pia akiongelea usajili wa Aubameyang kuwa bado haujakamilika.

Kocha huyo mkongwe ameyasema hayo leo alipokuwa akitoa ripoti ya majeruhi na programu za timu kwa ujumla, ambapo amesisitiza nyota wake Olivier Giroud hauzwi kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa.

''Kwasasa hauzwi mchezaji yoyote bila kununua mchezaji wa kuchukua nafasi yake, tumemuuza Sanchez lakini tumempata Mkhitaryan hivyo timu iko vizuri na kikosi cha wachezaji waliopo'', amesema Wenger.

Pia Mfaransa huyo ameongeza kuwa milango pekeee itakayokuwa wazi ni kwa timu za vijana ambapo kuna baadhi watatolewa kwa mkopo na wengine watapandishwa kwenye kikosi cha wakubwa.

Kuhusu kumsajili nyota wa Gabon na Borussia Dortmund Pierre Aubameyang, Wenger amesema bado hawezi kusemea lolote kwasababu hakuna kilichokamilika na mchezaji huyo bado ni mali ya Dortmund.



Kumbe CCM wenyewe wanasubiri kuapishwa tu?

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka na kusema kuwa wagombea wa Ubunge kupitia chama chake katika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Kinondoni na Siha wanasubiri kuapishwa tu na kuingia bungeni.

Polepole amesema hayo alipokuwa akihojiwa na moja ya kituo cha habari na kusema kuwa kwa jinsi ambavyo wana CCM wamefanya kazi nzuri sana Kinondoni na Siha kuhakikisha wanawanadi na kuwauza wagombea wao hivyo wana uhakika wa kushinda uchaguzi huo kwa kishindo.

"Kwa utafiti tunaofanya na kazi nzuri tuliyofanya tunasubiri kutangazwa washindi katika majimbo yote mawili pale Kinondoni na Siha" alisisikika Polepole akisema

Mbali na hilo Polepole amekanusha chama hicho kuwa na mvurugano wa wenyewe kwa wenyewe kufuatia kusimamisha wagombea katika majimbo hayo ambao hawana muda mrefu katika chama hicho wakitokea upinzani na kusema kwa CCM kila mwanachama ana haki sawa na wanachama wengine.

Chama Cha Mapinduzi kimemsimamisha Maulid Mtulia kugombea Ubunge kwa jimbo la Kinondoni wakati katika jimbo la Siha kimemsimamisha Dk Godwin Mollel ambao wote walikuwa ni wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokea vyama vya upinzani, lakini walijivua uanachama kwenye vyama vyao na kujiunga na CCM.