Tuesday, 23 January 2018

Arsenal na Liverpool zaingia vitani

Liverpool na Arsenal zimeingia vitani kuwania saini ya mchezaji wa AS Monaco, Thomas Lemar mwishoni wa msimu huu.

Taarifa zinaweka wazi kwamba makocha wa timu hizo mbili, Jurgen Klopp na Arsene Wenger wote wana fedha za kufanya usajili wakati dirisha la majira ya kiangazi litakapofunguliwa na kwamba, kila mmoja ametenga Pauni 90 milioni kuinasa huduma ya staa huyo wa Ufaransa.

Liverpool na Arsenal zote zimeondokewa na mastaa wake wa maana katika dirisha hili la usajili, ambapo Philippe Coutinho ameachana na wababe hao wa Anfield akitimkia Barcelona, wakati Alexis Sanchez aliondoka Emirates kwenda Manchester United. Kuna mastaa wengi wanaosakwa na makocha hao, lakini vita inaripotiwa kwamba, itakuwa kali kwelikweli kwa Lemar.

Hata hivyo, Arsenal na Liverpool si wao tu watakaoitaka huduma ya Lemar baada ya Manchester City nao kutajwa kwenye vita kutokana na kumkosa Sanchez, huku matajiri wa Paris, PSG wakimweka kwenye mipango yao ya msimu ujao Mfaransa huyo.

Wenger alikaribia kumnasa Lemar katika dirisha lililopita baada ya kukubali kulipa Pauni 92 milioni, lakini staa huyo mwenyewe aligoma kuihama Monaco katika dakika za mwisho na kubaki katika timu hiyo ya huko kwenye Ligue 1.

Chin Bees bifuni na Mganda


Chin Bees.

MSANII wa Bongo Fleva, Chin Bees amejikuta akiingia kwenye bifu zito na msanii wa Muziki wa Uganda, Fik Fameica kwa kumuibia ‘beat’ la wimbo wake wa Pepeta.

Akizungumza na Full Shangwe, Chin Bees amesema kuwa ameshtushwa na kitendo cha msanii huyo kutumia beat lake na kuuita Mafia bila kuzungumza naye.

Fik Fameica

Inaumiza sana kuona msanii anatumia beat lako bila kukushirikisha kwa chochote. Huyo msanii wala simjui na sijaongea naye ila tumewasilisha malalamiko yetu Cosota ili hatua stahiki zichukuliwe.

Full Shangwe ilimtafuta Fik Fameica kwa njia ya WhatsApp na kumsomea mashtaka yake lakini hakujibu chochote zaidi ya kutuma wimbo wake wa Mafia.

BREAKING NEWS: Nabii Tito akamatwa na polisi Dodoma


IGP Sirro akizungumza na Nabii Tito mjini Dodoma leo.

JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma inadaiwa limemtia mbaroni mkazi mmoja wa mkoani humo anayejitangaza kama nabii, Tito Machija, ambaye amekuwa akionekana mitandaoni akifanya mambo yasiyoendana na maadili ya dini na injili anayodai kuihubiri.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro,  amezungumza na ‘mhubiri binafsi’ huyo licha ya jeshi hilo kutotoa taarifa rasmi ya kilichojiri na utaratibu unaoendelea iwapo ni kumhoji au kumfikisha mahakamani.

Nabii huyo ambaye video zake zimesambaa akihamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, ikiwa ni pamoja na kutembea na wafanyakazi wa ndani,  anatumia pombe kunasa waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, ambazo nyingi hufanyikia baa.

Aidha ameonekana akicheza nyimbo za Bongo Fleva akiwa ‘madhabahuni’ badala ya kwaya na huku akieleza kuwa wafadhili wake wanatumia pombe,  hivyo na yeye lazima waumini wake watumie pombe ambazo amezifanyia upako.

VIDEO: Sakata la Nyoso Latua TFF


Sakata la Mchezaji wa Kagera Suger Juma Nyoso la kumpiga mshabiki na kuzimia leo limeibuka kwenye mkutano wa waandishi wa Shirikisho la Soka Nchini TFF na Kulitolea ufafanuzi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Monday, 22 January 2018

Nabii Tito bado anaota kumuoa Wema


Mkazi mmoja wa Dodoma anayejitangaza kama nabii, Tito Machija amesema watu wasimuone kuwa hana akili kutokana na mahubiri yake ambayo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa na imani za waumini wa dini nyingine, hasa Wakristo.

Machija, ambaye anajulikana kama ‘Nabii Tito’ anahamasisha kuoa mke zaidi ya mmoja, ikiwa ni pamoja na kutembea na wafanyakazi wa ndani; anatumia pombe kunasa waumini na anadai hataki nyimbo za injili kwenye ‘ibada’ zake, ambazo nyingi hufanyikia baa.

‘Nabii’ huyo anaonekana kwenye mitandao ya kijamii akiwa amevalia kanzu nyeupe yenye misalaba miwili, chupa ya bia na kitabu kitakatifu aina ya Biblia.

“Nawashangaa wanaoniona mimi sina akili, niko timamu kabisa na ninaelewa ninachokifanya,” alisema alipozungumza na MCL Digital.

“Narudia tena kusisitiza kuwa walevi ndio watakaoingia ‘mbinguni’ na mafundisho ninayoyatoa ni sahihi,”

Tito amekuwa akionekana kwenye mitandao ya kijamii, hususani kwenye video fupifupi za Instagram, akiwa amevalia mavazi kama ya kichungaji na kucheza muziki huku akinywa bia na akiwa ameshika biblia.

‘Nabii’ huyo, mwenye wake watano na watoto 12, amedai kuwa kwa sasa hitaji lake kubwa ni kumuoa mwigizaji Wema Sepetu ili aungane naye katika huduma zake.

“Wema ni msichana mzuri wa sura na umbo nataka nimuoe awe sehemu ya kanisa langu na nina imani watu wengi wataongezeka kwenye ibada ili kuja kumuona yeye na wake zangu hawana tatizo na hilo hata mmoja wao ananisaidia kumshawishi ili tuungane naye,” alisema Tito.

Tito anakiri kuwa ‘kanisa’ lake halijasajiliwa ila anadai kwamba anapata ufadhili kutoka kwa walevi mbalimbali.

Tito amedai  kuwa ‘kanisa’ lake lipo karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma na mara nyingi ibada zake huwa anazifanya kwenye baa na ana wafuasi  wengi kiasi cha kutojua  idadi yao.

Amesema kabla ya ibada kufanyika kwenye baa husika, huanza kwa kupeleka vipeperushi kwa mmiliki ili kuwapa taarifa waumini wake siku hasa ya ibada kufanyika katika baa hiyo.

“Siku ya ibada ikifika naenda pale nikiwa na bia zangu za (anaitaja aina ya bia) ambazo nimeshaziombea. Zina ‘upako’. Kila anayetaka kuingia kwenye ibada analipa kiingilio cha Sh12,500. Ukilipa pesa hiyo unapata bia zako tano ndiyo huduma inaendelea usipotoa unafukuzwa,” alisema.

Tito anajinasibu kuwa ana waumini wengi ambao hujitokeza kusikiliza mafundisho yake ambayo kwa kiasi kikubwa yanahamasisha ulevi na mapenzi kwa wasichana wa kazi wa majumbani.

Amesema kwenye huduma zake nyimbo za injili hazina nafasi kwa kuwa huwaburudisha waumini wake kwa nyimbo za kisasa.

“Mtu akishaweza safari zake kichwani ukimuwekea bongofleva anacheza na kufurahi huku ibada inaendelea,” alisema.

Nabii huyo amedai kuwa hakuna anachokizungumza kutoka kichwani mwake bali anasimamia mistari ya vitabu vitakatifu.

 “Wapo wengi wanaopinga huduma zangu ila nawaambia sijakurupuka nafanya kitu ambacho kipo na wala sioni kama ninakosea,” alisema.

Kwanini ‘ibada’ kwenye baa

Tito amedai kuwa anaingia makubaliano na wenye baa kwa kuwa ndiyo sehemu ambayo walevi hukutana na kwake ni mahali sahihi pa kutoa huduma.

“Pale nakwenda na bia zangu kadhaa kwa ajili ya waumini watakaoingia kwenye ‘ibada’. Zikiisha naondoka zangu, nawaacha wanaendelea kununua za baa hapo ndipo mwenye baa anaponufaika,” alisema.

Watu wengi wamekuwa wakilaumu mafundisho ya Tito kuwa yanapotosha na wameiomba Serikali kuchukua hatua.


Ushirika Mara kukaguliwa mali zake


Waziri Mkuu,  Kassim Majaliwa amesema Serikali itatuma wakaguzi kwa ajili ya kukagua  mali za chama cha ushirika mkoa wa Mara.

Amesema Serikali imeanza kufuatilia mali za vyama vya ushirika nchini zikiwemo za chama hicho.

Waziri Majaliwa ametoa kauli hiyo jana, Januari 21 mwaka 2018 katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya kikazi mkoani hapa.

Amesema ukaguzi huo utakwenda sambamba na kufuatilia fedha wanazodai waliokuwa watumishi wa chama hicho.

“Kumekuwa na matatizo makubwa ndani ya vyama vya ushirika kiasi cha kudumaza maendeleo ya wananchi,” amesema.

Pia, amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), mhandisi  Elius Mwakalinga kufanya tathimini  ya ubora ya jengo la kituo cha pamoja cha forodha cha Sirari kilichopo mpakani mwa Tanzania na Kenya.

Amesema mkurugenzi huyo afanye tathmini na kuishauri Serikali kama jengo hilo linafaa kutumika.

Januari 17, Waziri Mkuu alikagua kituo hicho kilichopo wilaya ya Tarime mkoa wa Mara na kusema hajaridhishwa na ujenzi wake  kwa kuwa upo chini ya kiwango.

Kituo hicho kilianza kujengwa mwaka 2011 na kukamilika mwaka 2014.

Basi la Mkombozi laua wawili na kujeruhi watatu Mwanza


Watu wawili wamefariki dunia na wengine watatu wamejeruhiwa katika ajali ya gari baada ya basi dogo la abiria kampuni ya Mkombozi kugongana uso kwa uso na basi la kampuni ya Walawi katika eneo la Kamanga jijini Mwanza.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza kamishna msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa dereva wa basi la Mkombozi pamoja na abiria mwingine wamepoteza maisha hapo hapo.

"Ni kweli imetokea ajali hiyo na kusababisha vifo vya watu wawili akiwepo dereva la basi dogo la kampuni ya Mkombozi ambaye alifariki hapo hapo baada ya ajali pamoja na abiria mwingine, lakini pia wapo majeruhi watatu ambao wamepelekwa kwa matibabu zaidi"

Jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi kujua chanzo za ajali hiyo

Makumbusho ya Taifa yamzungumzia binadamu wa kwanza

Makumbusho ya taifa la Tanzania iliyopo jijini Dar es salaam imeandaa mafunzo ya onesho la chimbuko la binadamu Afrika yanayotarajiwa kutolewa kesho.

Mkurugenzi wa Makumbusho ya taifa Prof. Audax Mabula  mafunzo na onesho hilo yanatokana na tafiti mbalimbali zinazofanyika bonde la hifadhi ya Olduvai na Laetol katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro.

Aidha Prof. Audax  ameeleza onesho hilo litafanyika kesho jijini Dar es salaam na litafunguliwa na waziri wa Mali asili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na litahudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Katika onesho hilo wananchi pia wataweza kuona mambo mbalimbali ya kale ambayo binadamu wa kwanza aliweza kuyafanya katika nyanja tofauti katika maisha yake.

Mwenyekiti UVCCM amtupia kombora Salum Mwalimu


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Kheri James amemfananisha Mgombea Ubunge, Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CHADEMA, Salum Mwalimu sawa na bibi harusi na kuwa wao CCM watashinda uchaguzi huo.

James amesema kuwa Watanzania wanakipenda sana Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati huu kuliko wakati mwingine wowote hivyo ni lazima Mgombea ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya (CCM), Maulid Mtulia ashinde.

"Kinondoni tunakwenda kushinda nimesikia Kamati ya harusi imemchagua Bibi harusi mmoja, hawa wanacheza siasa ya diblo dibala mara wamo mara hawamo lakini faida tuliyopata safari hii wametuletea mtu mwenye historia ya kushindwa, kaomba Ubunge kwao huko visiwani kapigwa, kaomba Ubunge wa Afrika Mashariki kapigwa na Kinondoni atapigwa, nachohitaji Kinondoni nataka kipigo kitakatifu ili baada ya kushindwa Salum Mwalimu aache siasa atafute biashara nyingine" alisema Kheri James

Mbali na hilo Mwenyekiti wa UVCCM amedai kuwa Salum Mwalimu ni mbuzi wa kafara wa CHADEMA kuwa kila shughuli ngumu wanamtuma yeye ili akafe wao wabaki.

Shule ya Makuti Mtwara yaanza kukarabatiwa


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mtwara QS Omary Kipanga, amesema ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi Mitambo iliyopo kata ya Msimbati ambayo iliripotiwa kuwa na madarasa ya makuti, unaendelea shuleni hapo.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Bw. Kipanga mesema ujenzi huo ni wa vyumba vitatu vya madarasa ambao serikali inasimamia, na kimoja ambacho kinajengwa kwa nguvu ya wananchi, pamoja na nyumba ya mwalimu.

“Vyumba vipo na vya matofali na vimeezekwa majengo matatu, lakini kuna ujenzi ambao unaendelea kwa nguvu za wananchi wa darasa moja, lakini na sisi halmashauri katika bajeti yetu ya mwaka 2017/18 tumetenga bajeti kwa ajili ya madarasa mawili na nyumba ya mwalimu, mpaka sasa vyumba vya madarasa vinavyotumika ni vyumba viatu, vingine vitatu vipo kwenye ujenzi”, amesema Mkurugenzi Kipanga.

Sambamba na hilo Mkurugenzi amekiri uwepo wa upungufu wa walimu, ambapo amesema tatizo hilo ni la nchi nzima na sio kwenye halmashauri yake peke yake, hata hivyo serikali inafanya jitihada za kutatua changamoto hiyo.

“Tuna changamoto ya walimu sio kwenye halmashauri yangu tu, ni nchi nzima, kwa sababu mimi katika halmashuri yangu nina upungufu karibu mia 5 na kitu, pale walimu 7, wanafunzi 437 na madarasa 7 yaani la kwanza mpaka la saba”, ameendelea kufafanua Mkurugenzi huyo.

Kwa upande wa elimu ya sekondari Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mtwara amesema ana tatizo kubwa la kuwepo kwa upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi, kwani kwenye halmashauri yake ina uhaba wa walimu 71 wa masomo ya sayansi.

“Kwa upande wa sekondari masomo ya sanaa hatuna tatizo sana, ila kwa masomo ya sayansi mimi kwenye halmashauri yangu ina upungufu wa walimu takriban 71 kwa shule zote, lakini bado tuna mikakati ya kuhakikisha tunapata walimu wa mazoezi ili tuweke priority kwenye masomo ya sayansi”, amesema Mkurugenzi huyo.

Shule ya Mitambo ilianzishwa mwaka 2009, ambapo mwaka 2015 walihitimu wanafunzi wa darasa la saba kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa.

EATV.

Rais Magufuli apokea hati za mabalozi sita nchini


Rais Dkt John Magufuli amepokea hati za utambulisho kutoka Mabalozi 6 walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Vanessa kuinufaisha familia ya Mbaraka Mwishehe


Msanii wa muziki Vanessa Mdee amebainisha kwa nini familia ya marehemu Mbaraka Mwishehe itanufaika kwa mauzo ya albamu ya Money Monday kwa njia ya mtandao na sio kwa mauzo ya kawaida (CD).

Mrembo huyo amebinbisha hayo kupitia mahojiano aliyofanya na Bongo5 na kusema kuwa ameamua maamuzi hayo yamekuja baada ya kutoa kionjo katika ngoma ya ‘Jogoo la Shamba’ ya marehemu Mbaraka na kukitumia katika ngoma yake ya ‘ Pumzi ya Mwisho’ aliyowashirikisha marapa wawili amabo ni Cassper Nyovest na Joh Makini.

“Familia ya mubaraka itanufaika kwa mauzo ya kimtandao kwa sababu soko letu lina hamia kimtandao Zaidi hivyoi ni meona ni busara kutumia njia hiyo,” amesema Vanessa.

AUDIO Audio | Lava Lava – Kizunguzungu | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Lava Lava – Kizunguzungu | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Lava Lava – Kizunguzungu | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3