Monday, 22 January 2018

Ronaldo apasuliwa uso



LICHA ya ushindi wa bao 7-1 dhidi ya Derpotivo la Coruna walioupata Real Madrid katika La Liga, mshambuliaji wake, wa Kimataifa Raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo alikutana na dhoruba baada ya kuumia kwa kupasuka usoni.

Ronaldo aliumia kwa kuchanipa sehemu ya usoni baada ya kugongwa wakati akijaribu kufunga.

Alikuwa ameruka kichwa kwa lengo la kufunga lakini akagongana na mchezaji wa Derpotivo. Hata hivyo, Ronaldo alipata huduma nzuri na kilichovutia zaidi ni yeye kutumia simu ya daktari kuangalia kama alikuwa ameumia au la.

Nduda awasihi mashabiki na wapenzi wa Simba SC



Mlinda mlango wa kimataifa wa klabu ya Simba Said Mohamed Nduda amewataka mashabiki na wapenzi wa wekundu wa msimbazi kuwa na subira katika kipindi hiki kwa madai ana matumaini timu yake watachukua ubingwa safari hii.

Nduda ameeleza hayo wakati akizungumza na mwandishi wa 'East Afrika Television' baada ya kuwepo nje ya uwanja kwa kipindi kirefu kutoka na matatizo ya goti aliyoyapata akiwa mazoezini pindi timu yake ilipokuwa ikijiandaa kwa mchezo dhidi ya watani wao jadi.

"Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu hali yako kwa sasa naendelea vizuri na ninafuata maelekezo ya daktari ya kufanya mazoezi kama anavyoniambia, hapa nasubiri tu kauli yake kama ataniruhusu nianze mazoezi uwanjani ili niungane na wenzangu", alisema Said Nduda.

Pamoja na hayo Nduda aliendelea kwa kusema "nahisi mwezi Februari utakaoanza ninaweza nikawa nimerejea uwanjani, napenda kuwaambia mashabiki wa Simba kuwa na subira katika kipindi hichi kwa kuwa nina imani timu yetu itafanya vizuri na kukinyakua kikombe"

Kwa upande mwingine timu ya Simba itarajia kushuka dimbani alasiri ya leo (Jumatatu) kuvaana na Kagera Sugar katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara mzunguko wa 14.

Sunday, 21 January 2018

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

Audio | Best Nasso – Sabuni Ya Roho | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Audio | Best Nasso _ SABUNI YA ROHO | Official Song

Faiza ampa somo Diamond



Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Faiza Ally amempa ushauri msanii wa muziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz kuwa kwa sasa ni muda wake wa kula ujana na kuizunguuka dunia na sio muda wa kujipa majukumu mazito ile hali umri wake bado mdogo.

Faiza Ally amesema Diamond bado hajamaliza hata robo ya dunia hivyo ingawaje ana jina kubwa barani Afrika hivyo angefanya kwanza vitu kama hivyo kuizunguuka dunia ikibidi ajiweke kando na mambo ya mahusiano.

“Diamond kijana mdogo sana anahitaji kuhave funny na watoto wenzie na sisi wadada wazima lazima taungalie watu wa kutoka nao, Go baba have a funny enjoy the world ndio useto down,“ameandika Faiza Ally kwenye ukurasa wake wa Instagram na kumshauri kuwa ikibidi ajiweke mbali na mahusiano.

“Jiachie uwe huru ikibidi usiwe na mahusiano, bado hujaiona dunia hata robo wewe ni star hela ipo there is alot to see nasema with clean heart no hate kwa Zari au kwa yeyote.“ameandika Faiza.

Ushauri huo umekuja ikiwa ni wiki sasa imepita tangu kuenee tetesi kuwa Diamond Platnumz yupo kwenye mahusiano na msichana maarufu kwenye mitandao ya kijamii anayejulikana kwa jina la Tunda.

Waziri Mkuu atoa agizo kwa TAKUKURU

Waziri Mkuu .Mhe Majaliwa Kassim Majaliwa ameaagiza TAKUKURU kumkamata Meneja wa TBA wilaya ya Butiama mkoani Mara kutokana na uzembe na kutumia fedha za Serikali kinyume na maelekezo.

Waziri Mkuu amefanya maamuzi hayo baada ya Serikali kupeleka fedha zaidi ya milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la halmashauri lakini mpaka sasa fedha ujenzi huo haujaanza na fedha hizo kutumika katika miradi mingine ambayo haijapangwa na Serikali.

"Tumeleta fedha milioni 600 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la halmshauri lakini mmezipeleka kwenye shughuli nyingine, kwanini hajajenga jengo hili ikiwa fedha zimeshaletwa? Tumeleta fedha milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya, DAS na nyumba ya watumishi lakini mmejenga nyumba moja tu ya DC, nyumba zingine mbona hamjaanza kujenga?

Waziri Mkuu baada ya kukosa majibu yanayoridhisha kutoka kwa viongozi hao ndipo alipoagiza TAKUKURU kumchukua moja ya mtumishi wa halmshauri hiyo na kusema kuwa serikali haiwezi kuwavumilia watumishi na namna hiyo.

"Meneja TBA upo? Umepata fedha toka mwezi wa nne mwaka jana mpaka leo hii 21 Januari 2018 miezi mingapi ishapita? Msingi wa jengo upo? Kamanda wa PCCB hebu ondoka na huyu bwana, mchukue huyu hatuwezi kuchelewesha kazi, tumeleta fedha kujenga jengo la halmashauri watumishi wanahangaika wewe una hela mpaka leo unazo tu. Kwanini tuwe na watumishi wa namna hii? Alihoji Majaliwa.

Kamati ya Bunge yashtushwa na bei nyumba za NSSF



Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wameshtushwa na bei ya kuuza nyumba za mradi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizoko eneo la Dege Kigamboni jijini Dar es Salaam wakisema haziendani ya hadhi na hali ya wananchi walio wengi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara, bei za nyumba za Dege ni kati ya Dola za Marekani 110,000 (Sh220 milioni) hadi Dola 250,000 (Sh500 milioni) kulingana na aina ya nyumba.

Wakizungumza jana baada ya kutembelea miradi ya NSSF jijini Dar es Salaam, wabunge hao walitilia shaka uuzwaji wa nyumba hizo huku shirika hilo likikiri kutozitangaza mapema kwa wateja.

Mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka alisema nyumba za mradi wa Dege hazina hadhi ya kuuzwa bei hiyo.

“Ukiangalia nyumba zenyewe zina ‘poor quality’ (kiwango cha chini), hata ukiangalia ‘design’ yake sio nzuri. Vyumba ni vidogo, hivi kweli mtu atashawishika kutoa Sh200 milioni kununua nyumba hiyo?” alihoji Kaboyoka.

Hoja hiyo, iliungwa mkono na Mbunge wa Magomeni Zanzibar, Jamal Kassim akisema hazikujengwa kwa kuwalenga watu wa kipato cha chini.

“Hizi nyumba hazikujengwa kwa ajili ya watu wa kipato cha chini, bali wenye kipato cha juu hasa wageni. Hata hivyo, kwa kuwa wameshawekeza fedha lazima mradi ukamilike na nyumba ziuzwe,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu Dodoma, Felister Bura alihoji upatikanaji wa wateja ikiwa watumishi wa umma wanaotegemewa wengi wao wanahamia Dodoma ambako ndiko makao makuu ya nchi.

Akijibu hoja na maswali ya wabunge, Profesa Kahyarara alisema nyumba hizo za Dege zitauzwa kati ya Dola 110,000 hadi Dola 125,000 kwa moja na Dola 195,000 hadi Dola 250,000 kwa nyumba aina ya villa.

Alisema mteja atatakiwa kulipa kwa muda wa miaka sita.

Mbali na mradi wa Dege, NSSF pia iliwaonyesha wajumbe hao wa PAC mradi wa Dungu, ambao Profesa Kahyarara alisema una nyumba 439 na umegharimu jumla ya Sh89.5 bilioni.

“Mradi wa nyumba hizo utakamilika Juni mwaka huu na mpaka sasa tumeshatumia Sh50 bilioni,” alisema Profesa Kahyarara.

Kuhusu mradi wa Toangoma wenye nyumba 161, mkurugenzi huyo alisema umetumia gharama ya Sh61 bilioni.

Hata hivyo, Profesa Kahyarara alikiri kutozitangaza nyumba hizo mapema jambo lililozua maswali kwa wabunge kuhusu uhakika wa kuziuza.

Mbali na bei hizo, pia imeelezwa kuwa mvutano wa hisa kati ya NSSF na kampuni ya Azimio ni chanzo mojawapo cha kucheleweshwa kwa mradi wa nyumba zaidi ya 7,000.

Profesa Kahyayara aliiambia kamati hiyo kuwa mradi huo umeshatekelezwa katika awamu mbili na nyumba 3,750 zimeshakamilika kati ya 7,160 za mradi mzima.

Kwa mujibu wa mkataba huo, kampuni ya Azimio iliyotoa ardhi ya hekta 300 inamiliki hisa asilimia 55 huku NSSF iliyowekeza zaidi ya Dola 500 ikimiliki hisa asilimia 45.

Alisema mradi huo ulitarajiwa kukamilika mwisho wa mwaka huu lakini haitawezekana kutokana na dosari za mkataba. Baadhi ya wajumbe wa PAC walihoji sababu ya mkurugenzi wa kampuni ya Azimio kutoonekana kila anapotafutwa.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Kilimanjaro, Shaly Raymond alisema kuchelewa kwa mradi huo kutapandisha gharama kutoka Dola 544 milioni hadi 700 na kuhoji nani atakayelipa, huku pia akihoji sababu za mwekezaji wa Azimio kutokuwapo katika ziara hiyo.

“Angalia hiyo meza kuu, mwekezaji hayupo, wewe mkurugenzi umekuja peke yako, wenzako wako wapi?” alihoji Shaly.

Mbunge Bura alisema kama Azimio hawataki kuonyesha ushirikiano, atafutwe mwekezaji mwingine. “Tulipozungumza na mwekezaji huyu alikubali kupunguza hisa zake kwa sababu amewekeza kidogo. Kama anasumbua, NSSF waangalie namna ya kupata mwekezaji mwingine.”

Akijibu hoja za wabunge, Profesa Kahyarara alikiri kucheleweshwa kwa mradi huku akisema bado wanajadiliana na kampuni ya Azimio.

Alimtetea mwekezaji huyo akisema amekuwa na safari nyingi nje ya nchi na kwamba atakuwepo kwenye kikao cha Januari 26 na mambo yote yatajadiliwa na kutolewa uamuzi.

Kamanda wa trafiki aunga mkono kauli ya Mambosasa



Kamanda wa Kikosi cha Polisi wa Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Muslim ameunga mkono kauli ya kamanda wa jeshi hilo Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kuhusu utendaji kazi wa trafiki.

Haukuishia kuunga mkono tu, Kamanda Muslim amesema askari wa usalama barabarani wanatakiwa kuangalia makosa hatarishi yanayoweza kusababisha kutokea kwa ajali na kuachana na yale yasiyokuwa ya msingi.

Juzi, Kamanda Mambosasa aliwataka askari hususan wa usalama barabarani kutumia busara katika utendaji kazi wao ili kuondoa malalamiko ya uonevu na kuwakandamiza raia na kusisitiza kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda raia na mali zao na kusimamia sheria.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda Muslim alisema askari wote wa kikosi hicho wanaelekezwa kuzingatia makosa hatarishi kwa kuwa kazi kubwa ya kikosi hicho ni kuhakikisha sheria za barabarani zinazingatiwa ili kupunguza ajali zinazogharimu maisha ya watu.

Alisema kuna makosa ambayo hayana athari kulingana na mazingira husika hivyo askari hawana sababu ya kuyapa kipaumbele.

“Naungana kabisa na Mambosasa ila mimi nisitumie neno busara labda niseme askari wakamate makosa hatarishi, mnamkamata vipi dereva kwa kosa la taa mchana au wiper mbovu wakati wa jua kali? Hayo yote hayawezi kusababisha ajali kwa nyakati hizo. Hapo ndipo linapokuja suala na mazingira, wiper zinatakiwa kufanya kazi kipindi cha mvua.”

Kuhusu askari wa usalama barabarani kumsimamisha dereva na kuanza kutafuta kosa, Kamanda Muslim alisema ni muhimu kwa madereva kuzingatia sheria si muda wote wanasimamishwa kwa sababu ya makosa.

“Tatizo ni kwamba madereva wenyewe wameshajenga mtazamo hasi, sio kila wakati askari anapokusimamisha lazima uwe na kosa inawezekana anataka kukupa tahadhari huko unakoelekea sio kuzuri hivyo uongeze umakini.

“Ninachosisitiza madereva wafuate sheria, waache kulalamika. Wakizingatia sheria sidhani kama hao askari watakuwa wanawasimamisha ovyo kama wanavyodai,” alisema Kamanda Muslim.

Pia aliungana na Mambosasa kuwataka madereva wasikubali kutoa fedha kwa askari bila kupata risiti zinazotokana na mashine au fomu namba 101 ya polisi inayofahamika kama ‘notification’.

Kadhalika alisema askari wa pikipiki maarufu kama tigo wataendelea kufanya kazi yao ya kuzuia uhalifu unaohusisha makosa ya jinai na usalama barabarani na kusisitiza kuwa hawana mamlaka ya kutoza faini.

Ukusanyaji wa mapato

Kamanda Muslim alionyesha kukerwa na watu wanaohusisha tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na ukusanyaji wa mapato.

Alisema kazi ya kukusanya mapato inafanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tofauti na tozo zinazokusanywa na kikosi hicho kutokana na uvunjifu wa sheria barabarani.

“Nashangaa wanaosema tunakusanya mapato kwani Jeshi la Polisi lina biashara gani? Sisi tunatoza tozo zinazotokana na makosa ya barabarani na lengo letu ni kuzuia ajali na kuhakikisha usalama unakuwa wa kutosha katika barabara zetu.

“Tozo hizo zipo kwa mujibu wa sheria na anayepaswa kulipa ni yule aliyevunja sheria na inasimama badala ya kifungo kwa hiyo watu wanapaswa kutambua askari wa usalama barabarani hawakusanyi mapato.”

Hali ya usalama barabarani

Kamanda hiyo alisema hali ya usalama barabarani nchini imeimarika na ajali zinaendelea kupungua kwa kiasi kikubwa.

Alisema hiyo inatokana na askari wa kikosi hicho kuimarisha ukaguzi na usimamizi wa sheria.

“Nikitolea mfano wa leo (jana) yaani ndani ya saa 24, nchi nzima kuna ajali tatu pekee. Hii ni hatua kubwa na siku nyingine hakuna ajali kabisa hayo ni matokeo ya usimamizi wa sheria kazi inayofanywa vizuri kabisa na askari wa kikosi cha usalama barabarani.

“Usimamizi wa sheria umeongezwa maradufu kwenye maeneo ya kuvukia watembea kwa miguu, nimesisitiza lazima dereva asimame aangalie pande zote ndipo apite hata kama hakuna mtu anayevuka. Kwa magari yanayosafiri ukaguzi unafanyika kabla hayajatoka vituoni na madereva tunawapima ulevi, huko njiani askari nao wanajipanga vizuri.”

Kamanda Muslim alisema jitihada zote hizo zinafanyika kuhakikisha ajali zinapungua au kutokomezwa kabisa.

Alisema, “Hatuwezi kuvumilia watu wapoteze maisha sababu ya madereva wazembe, hatutafungua ‘tuition’ barabarani ya kutoa elimu. Kama unataka elimu acha gari lako nyumbani ukija nalo barabarani na ukavunja sheria neno ni moja tu “kamata” na watalipa faini na wale ambao watakuwa wagumu zaidi kuelewa neno lao ni “funga” hawa tutawafungia leseni zao.”

Wakazi wa Kilimanjaro waiomba Serikali kuweka matuta kuepusha ajali



WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali  kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.

WAKAZI wa Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, wameiomba serikali  kupitia Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), kuweka matuta katika barabara ya Sanya Juu- Bomang’ombe, ili kuzuia ajali ambazo zimekuwa zikitokea na kusababisha watu kupoteza maisha.

Wakazi hao wamesema barabara hiyo kwa muda mrefu imekuwa na ajali nyingi za watu kugongwa na magari na kupoteza maisha papo hapo na hakuna jitihada zozote ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali kuzuia ajali hizo.

Mmoja wa wakazi wa Majengo Sanya Juu, Idrisa Mndeme, alisema serikali kupitia Tanroads inapaswa  kuwawekea matuta katika barabara hiyo kwenye maeneo ya kuanzia Standi Kuu ya Sanya hadi Fuka, kwa kuwa madereva wa magari wamekuwa wakiendesha kwa mwendo kasi bila kujali watembea kwa miguu.

“Ndani ya mwezi huu kuna ajali mbili zimetokea. Mtu mmoja aligongwa na gari na kupoteza maisha na mwingine ambaye ni mwendesha pikipiki aligongwa na gari na kufariki papo hapo,”alisema.

Yassin Kimaro kwa upande wake aliwatupia lawama madereva wenye magari makubwa kwa kuendesha kwa mwendokasi na mara nyingine hudharau alama za pundamilia kwa kupitisha magari bila kujali watu wanaovuka.

“Madereva wa magari huendesha magari kwa kasi mno, hali ambayo imekuwa ikichangia sana ajali ambazo zinaweza kuepukika iwapo matuta yangekuwa yamewekwa,”alisema.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Siha, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Onesmo Busweru, alikiri kuwapo kwa baadhi ya madereva ambao wamekuwa wakiendesha kwa kasi, hivyo kusababisha ajali ambazo zingeweza kuepukika

Kutokana na hali hiyo aliagiza Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani  kuweka kidhibiti mwendo (tochi) katika maeneo hayo ili kuwadhibiti madereva ambao wamekuwa akiendesha kwa kasi.
 

Joyce Kiria amwaga siri za mumewe hadharani

Mwanaharakati na mwanamke shujaa nchini Tanzania, Joyce Kiria ameweka hadharani kuwa mahusiano yake kwa sasa na mumewe Henry Kileo ambaye alishawahi kushika nyadhifa mbalimbali CHADEMA.

Joyce Kiria amesema kuwa kwasasa mahusiano yake hayapo sawa kwani yeye amekuwa ndiye baba na mama wa familia kwa kila kitu yaani kuhudumia familia nzima pamoja na mumewe.

Akitoa taarifa hiyo kwa umma kupitia ukurasa wake wa Instagram huku akibubujikwa na majozi, Kiria amesema huwa anamshauri mumewe atafute japo kazi itakayowaingizia kipato ili kusaidiana kutunza familia lakini mumewe anakuwa mkali na kumpiga.

“Sikutegemea kama ipo siku kwa mkono wako ungeunyanyua kunipiga (@kilewo2020mwanga) ukasahau kabisa! ukasahau yooote. Nimeharibu career yangu kupigania ndoto yako kwa kugawa watu wangu kwenye biashara zangu, nimepoteza ndugu jamaa na marafiki, umeniachia nimebeba mzigo wa familia kwa muda wote, Malipo yako ni kunipiga/ kunidhalilisha na kunitoa machozi, umenipiga kwa sababu Mimi ni mnyonge siyo! sina nguvu, kwa sababu ni MWANAMKE Sina nguvu za kupigana na MWANAUME. Umeniumiza mwili wangu unauma kila mahali, ukanigongesha kwenye gari, ili iweje? Nia yako ilikuwa ni nini? kuniua??,“ameandika Kiria huku akielezea jinsi alivyompigania mumewe hadi kwenye kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015 hadi akaingiza deni kubwa na kufungiwa kipindi chake cha Wanawake Live kilichokuwa kinaruka EATV.

“Haya MACHOZI yangu namlilia Mungu wangu aliye juu, yeye ndo ataamua, kama ni mimi niliandamana na watoto, nikakufanyia kampeni na deni kubwa nikaingia mpaka nikafungiwa Kipindi hewami, ninakutunza wewe na Watoto wako kwa miaka yote Mungu yupo. Leo umenipiga (@kilewo2020mwanga)?? Sawa watakusifia hao wanaokusifu ujinga, wanaokuambiaga Mimi sikuheshimu, badala wakwambie ufanye kazi utunze familia, Leo watakuona wewe ni mwanaume kwa kunipiga.“amemaliza Kiria.

Mumewe na Joyce Kiria ni moja ya vigogo wa CHADEMA na kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 aligombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Mwanga, Kilimanjaro lakini kwa bahati mbaya alishindwa kupata nafasi hiyo.

Jafari Maganga: Watanzania wameanza kukubali falsafa ya Azam FC


Kuelekea mchezo wa leo wa ligi kuu soka Tanzania Bara kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Azam FC, msemaji wa wa Azam FC Jafar Idd Maganga amesema watanzania wameanza kukubali falsafa ya timu hiyo ya kutumia vijana.

Jaffar amesema kocha mkuu wa timu hiyo Aristica Cioaba, amekuwa muumini wa kutumia vijana kitu ambacho awali kilionekana kupingwa na mashabiki wengi wa soka wakiamini kuwa timu hiyo haitafanya vizuri.

''Watanzania wengi wameshaanza kukubali na wanaunga mkono uongozi wa Azam FC kuwatumia vijana na kocha huyu (Cioaba) amekuwa akiwaamini zaidi vijana tofauti na makocha wetu waliopita'', amesema Jaffar.

Kuhusu mchezo wa leo jioni, Jaffar amesema benchi la ufundi limejipanga kuhakikisha linapanga wachezaji ambao wataendana na timu ya Tanzania Prisons pamoja na hali ya uwanja wa Sokoine ili kuhakikisha timu yao inapata matokeo mazuri.

Azam inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 27 huku vinara wa ligi Simba SC, wakiwa na alama 29. Mabingwa watetezi Yanga SC watakuwa dimbani pia kucheza na Ruvu Shooting.

Kocha wa Simba afunguka kuhusu Nicholas Gyan

Kocha msaidizi wa vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC Masoud Djuma, ameweka wazi kuwa pamoja na kumpatia nafasi ya kucheza hivi sasa nyota wa timu hiyo kutoka Ghana Nicholas Gyan, lakini aliwahi kumwambia hajui kucheza.

Masoud  amesema baada ya kujiunga na Simba alimkuta Gyan na baada ya kumtazama kwenye mazoezi alimtamkia kuwa hawezi kucheza soka wala hafananii kuwa mchezaji lakini kwasasa Gyan amemjibu kwa vitendo.

"Nilimwita Gyan na kuzungumza naye na nikamwambia wewe si mchezaji, inakuwaje haupigi pasi, wala hautulizi mpira vizuri, kwa sababu haiwezekani mchezaji awe anakosa vitu hivyo, lakini kumbe mwenyewe kichwani alikuwa anafikiria kuwa  anarogwa," ameeleza Masoud.

Kocha huyo raia wa Burundi ameongeza kuwa baada ya kugundua kuwa Gyan anawaza hivyo alikaa naye na kumshauri kisha akampa nafasi ya kucheza na mwisho wa siku ameonesha kiwango kikubwa na amekuwa msaada kwa timu.

Masoud amekuwa akimtumia Gyan upande wa kulia kutokana na kasi yake ili kusaidia mfumo wake wa 4-4-2 ambao huwa unabadilika na kuwa 3-5-2 timu ikiwa inacheza hivyo Gyan mara nyingi husaidia kurudi kama mlinzi wa kulia na baadae kupanda kama winga.

Kiwanda cha Dangote chapewa siku 14


Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko ametoa siku 14 kwa uongozi wa kiwanda cha saruji cha Dangonte mkoa wa Mtwara kuingia mkataba na wachimbaji wadogo wa gypsum.

Biteko ametoa kauli hiyo leo Januari 21, 2018 baada ya kutembelea kiwanda hicho na kuzungumza na viongozi wake.

Amesema mikataba hiyo inapaswa kuwa na kipengele cha kuwalipa ndani ya siku 30 baada ya kiwanda kukusanya gypsum kutoka kwa wachimbaji hao, lengo likiwa ni kuleta ufanisi na tija katika biashara zao.

“Nimekubaliana hapa kamishna wa kanda atasimamia hili la mikataba kati ya kiwanda na wachimbaji wa gypsum. Sehemu ya malipo itakuwa ndani ya mkataba na watalipa ndani ya siku 30,” amesema.

Amesema wachimbaji hao wamekuwa wakilalamikia kucheleweshewa malipo yao baada ya kupeleka kiwandani bidhaa zao.

“Nimeambiwa wachimbaji hawa walikuwa wanalipwa baada ya miezi mitatu lakini kwa mkataba huu ambao wataingia na kiwanda sasa watakuwa wanalipwa ndani ya siku 30,” amesema Biteko.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inalenga kuwasaidia wachimbaji wadogo sambamba na wawekezaji ambao wanapaswa kufanya kazi bila kusumbuliwa.

 “Uwepo wa kiwanda hiki unawasaidia wachimbaji wetu waweze kupata bei nzuri pamoja na kupata soko la uhakika la kuuza bidhaa zao. Dangonte wameniahidi kwamba ndani ya muda mfupi watatekeleza agizo hili,” amesema.

Biteko amesema lengo la ziara yake ni kuwasaidia wachimbaji wa gypsum ambao hawana mikataba na kujikuta wakibanwa katika uuzaji wa bidhaa zao.