Friday, 19 January 2018

Linah afunguka sababu za kunenepa


MKALI kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Esterlina Sanga ‘Linah’ amefungukia sababu ya kuwa mnene kupitiliza ‘bonge nyanya’ kiasi cha kusababisha mijadala mbalimbali katika mitandao ya kijamii.

 Linah ameweka wazi sababu iliyomfanya kuwa mnene ni kutokana na kutoka kwenye uzazi hali iliyomfanya mwili na nafsi yake kuridhika na kujikuta bonge nyanya.

“Nimetoka kwenye kipindi kifupi mno cha uzazi, hii ndio sababu kubwa iliyonifanya niwe bonge, baada ya kujifungua mtoto nafsi na mwili wangu viliridhika, ndio maana nimekuwa na mwili mkubwa na wenye afya,” alisema Linah.


Waziri Mkuu Majaliwa ajitwisha mgogoro wa Nyamongo


Mapokezi ya mabango yaliyobebwa na wananchi wa eneo la Nyamongo yamesababisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kujitwisha mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 15 kati ya wakazi hao na Mgodi wa Dhahabu Acacia North Mara.

Serikali imeahidi kutatua mgogoro huo kati ya mgodi na wananchi wanaozunguka eneo hilo, ili kumaliza uhasama na kurejesha amani kati ya makundi hayo mawili yanayohasimiana kwa kipindi kirefu.

Ahadi hiyo ilitolewa jana na Majaliwa alipotembelea eneo la Nyamongo wilayani Tarime katika ziara yake ya siku saba inayoendelea mkoani Mara.

Hiyo ni baada ya kupokewa na mabango aliyosema hayapungui 400 alipofika eneo la Nyamongo, jambo alilosema ni ishara tosha ya kuwapo tatizo linalowachukiza wananchi linalohitaji ufumbuzi wa Serikali na viongozi wa ngazi zote.

Kikao cha kwanza cha kujadili na kutafutia ufumbuzi mgogoro huo kitakachohusisha wajumbe watano wa watakaowakilisha wananchi, uongozi wa mgodi, mbunge wa Tarime vijijini (John Heche) na wataalami wa Wizara ya Madini kitanatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 27.

Mambo muhimu yatakayojadiliwa na kupatiwa ufumbuzi kwa mujibu wa Waziri Mkuu ni malipo ya fidia kwa mali ya wananchi, maeneo ya uchimbaji kwa wachimbaji wadogo, upatikanaji wa mawe (mabaki) ya dhahabu maarufu kama magwangala.

Mengine ni upatikanaji wa maji safi na salama eneo la Nyamongo (vyanzo vya maji vya asili vinadaiwa kuchafuliwa na kemikali), na udhibiti wa matumizi ya nguvu kupita kiasi, ikiwamo kupiga mabomu ya machozi na risasi panapotokea mgogoro au vurugu kati ya wananchi na mwekezaji.

“Nimepokewa na mabango tangu nianze ziara mkoani Mara Januari 15; lakini mabango ya Nyamongo yametisha. Hayapungui 400 na yote yanaonyesha uhusiano mbaya kati yenu (wananchi) na mwekezaji. Nitalibeba hili na kulimaliza,” alisema Majaliwa akiamsha shangwe na nderemo kutoka kwa wananchi.

Licha ya amani na utulivu eneo la Nyamongo, uamuzi huo wa Serikali pia unalenga kuondoa kuviziana kati ya wananchi na vyombo vya dola vinavyotumika kudhibiti na kurejesha amani na utulivu nyakati za uvamizi unaofanywa na makundi ya watu, hasa vijana wanaoingia eneo la mgodi kuchukua mawe au mchanga wa dhahabu.

“Mgogoro huu unakwamisha juhudi za wananchi, Serikali na wawekezaji katika kujiletea maendeleo kupitia rasilimali ya madini yanayopatikana Nyamongo, lazima tuutafutie ufumbuzi wa kudumu kwa faida na masilahi ya pande zote,” alisema Majaliwa.

Alisema yeye binafsi ataongoza mazungumzo ya kutatua mgogoro huo hadi mwafaka utakapopatikana na kuagiza pande zote kuunga mkono juhudi hizo kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu huku maslahi na maendeleo ya wananchi yakipewa kipaumbele.

Awali, mbunge wa Tarime vijijini, John Heche alimweleza Majaliwa kuwa uhasama kati ya wananchi na wawekezaji, kukosekana kwa huduma bora za kijamii kulinganisha na ya utajiri wa madini eneo hilo na matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya wakazi kwa faida ya mwekezaji bila kujali uhalali wa madai ya wenyeji ni miongoni mwa changamoto zinazowakabiliwa wakazi wa Nyamongo.



Mambo ambayo Trafiki atakiwi kufanya kwa Dereva



Kama ulikuwa unaudhika kila ukiona askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, angalau sasa unaweza kuwa na ujasiri wa kukabiliana nao kisheria.

Ni kwa kutumia elimu iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa ambaye jana alitoa ufafanuzi wa jinsi askari hao, maarufu kwa jina la Trafiki, wanavyotakiwa kufanya kazi.

Amezungumzia jinsi trafiki anavyotakiwa kufanya iwapo atasimamisha gari yako, makosa anayotakiwa kuyahoji na hatimaye kukutoza faini kulingana na wakati na hata utendaji wa polisi wanaozunguka na pikipiki, maarufu kwa jina la tigo.

Na faraja zaidi ni kauli yake kwamba si kila kosa linastahili faini na kuwataka trafiki kuwa makini ili kuondoa malalamiko ya uonevu na kuwakandamiza raia.

Mambosasa alitoa kauli hiyo jana katika kipindi cha 360 kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds FM na baadaye kuzungumza na Mwananchi kufafanua maelezo yake.

Alishangazwa na askari wanaokamata gari mchana kwa kosa la kutowaka taa na kutoza faini.

Alitaja makosa mengine kuwa ni askari kukamata gari bila kujua kosa la msingi na kulazimika kuanza kulikagua kwa lengo la kubaini kosa.

Pia alieleza kwamba askari wanaotumia pikipiki maarufu kama ‘tigo’, hawaruhusiwi kutoza faini baada ya kukamata gari.

Trafiki aeleze sababu

“Akisimamisha gari ni lazima akueleza sababu za kukusimamisha; kwamba anataka kukagua nini katika gari lako,” alisema Kamanda Mambosasa baada ya kuombwa na Mwananchi kufafanua kauli yake jana jioni.

“Nilichokimaanisha ni ile kusimamisha gari na kuanza kutafuta makosa bila kueleza sababu ya kukusimamisha.”

Trafiki wamekuwa na tabia ya kusimamisha gari, kuomba leseni na baadaye kuanza kukagua vitu kama stika ya bima, taa, gurudumu, mtungi wa kemikali za kuzimia moto na viakisi mwanga kwa ajili ya kuashiria gari bovu lililosimama barabarani.

Akipata kosa, askari huandika kuanzia Sh30,000 kwa kosa, jambo ambalo limesababisha madereva wengi kuingiwa na hofu kila wanapoona askari hao barabarani.

“Akisimamisha gari ni lazima aeleze sababu za kulisimamisha,” alisema Kamanda Mambosasa kujibu swali “trafiki atatambuaje kama gari lina bima au vitu vingine vya lazima katika gari.

Trafiki atumie busara

Mambosasa pia alisema trafiki pia anatakiwa kutumia busara kumtoza faini mtu ambaye gari lake lina matatizo ya taa kwa kuwa huenda hatumii gari hilo usiku unapoingia.

“Yapo makosa ambayo askari yeyote wa usalama barabarani anayesimamia sheria anaweza kujitathmini mwenyewe na kuona haina ulazima wa kumtoza mtu faini,” alisema.

“Kwa mfano gari langu nimeamua kutembelea mchana tu, ikifika usiku naliegesha. Kuna sababu gani ya kuwa na taa?

“Kwa hiyo ukinikamata kwa kosa la kutokuwa na taa mchana, nitakushangaa kwa kuwa sijavunja sheria. Wakati mwingine askari anapaswa kufikiria uamuzi wa kumtoza faini mchana kwa sababu ya taa.”

Alisema kama ni usiku ni wazi kuwa mhusika atakuwa amefanya kosa.

“Ili tusiingie kwenye malumbano, tunaomba wananchi watii sheria na pale inapotokea udhaifu wa askari kumbambikia kosa mhusika, (mwananchi) anatakiwa kutoa taarifa haraka iwezekanavyo ili hatua zichukuliwe,” alisema.

Aliwataka askari kuacha kutafuta makosa kwa madereva kwa kusimamisha magari na kuanza kuyakagua.

“Unakamata gari halafu unaanza; mara washa taa; mara zima. Tunaendelea kuwaeleza wenzetu kuwa busara inahitajika wakati wa kusimamia sheria,” alisema.

Askari wa pikipiki

Kuhusu polisi kikosi cha pikipiki, Kamanda Mambosasa alisema wana haki ya kukamata gari au chombo chochote barabarani na kukikagua, lakini kuhusu utozaji wa faini jukumu hilo si lao, bali ni la trafiki.

“Anaweza kukukagua lakini linapokuja suala la kutoza faini, hana kitabu. Lazima akupeleke kwa wahusika ambao ni trafiki,” alisema.

Katika maelezo yake Clouds, Mambosasa alisema Jeshi la Polisi ni kwa ajili ya kulinda raia na mali zao, kusimamia sheria na si kukandamiza wananchi.

“Hawana mamlaka ya kutoza faini kwa mtu aliyevunja sheria za barabarani. Jukumu lao ni kumfikisha mtu huyo kwa askari wa usalama barabarani,” alisema.

Alisema kikosi hicho hakikuanzishwa kwa ajili ya kukamata na kutoza faini, bali kupambana na uhalifu. “Kutokana na foleni za Dar es Salaam, polisi ikaona busara kuwaweka askari hao tayari kwa ajili ya kuwahi kwenye matukio ya uhalifu na sio kukamata magari kama wanavyofanya sasa ingawa wanawajibika kushughulikia uvunjaji sheria unapotokea mbele yao,” alisema.

Aliwataka wananchi kutokubali kutoa fedha bila kupatiwa risiti kwa kuwa kufanya hivyo ni sawa na kutoa rushwa.

Alisema jeshi hilo linaendelea kuwaelimisha askari wake kusimamia sheria na si kuwaonea watu.

Kauli yake imepokewa vizuri na wadau wa vyombo vya moto.

“Binafsi naona askari wa usalama barabarani wana haki ya kukagua magari kwa kuwa hilo ndilo jukumu lao,” alisema mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Mkoa wa Dar es Salaam (Darcoboa), Sabri Mabrouk alipoulizwa na gazeti hili kuhusu kauli ya Mambosasa.

“Lakini nasisitiza kuwe na busara. Lengo si kuumizana, bali ni kuhakikisha sheria zinazingatiwa. Nitoe wito kwa wamiliki kuhakikisha magari yao yapo katika hali nzuri na madereva nao wasiingize magari mabovu barabarani.”

Kamanda Mambosasa pia alifafanua kuhusu tamko la kuzuia nguo fupi, akisema hilo ni kosa la kimaadili na si kisheria na hivyo Jeshi la Polisi haliwezi kulishughulikia kwa kuwa hakuna sheria inayozuia mavazi hayo. 

Samia ataka mpango wa kuiboresha Dar


Makamu wa Rais, Samia Suluhu amewataka viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuanzia ngazi za wilaya, halmashauri kuwa na mpango mmoja wa kuboresha mazingira ili kujikinga na maafa yatakayotokana na mvua hasa mafuriko.

Mama Samia amesema hayo leo Ijumaa wakati akifungua mkutano unaokutanisha wadau wa mazingira wa jiji hili ambao una lengo la kuja na mpango kazi wa kuondoa majanga hasa mafuriko.

Mkutano huo ambao umeudhuriwa na viongozi na mawaziri mbalimbali akiwamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na wakuu wa wilaya.

Samia amesema katika maafa yanayotokea katika jiji la Dar es Salaam kumekuwa na mipango tofauti katika wilaya zote jambo ambalo sio sawa kwani lazima kuwe na mkakati wa kunusuru jiji zima.

"Lazima tuwe na mkakati kabambe wa kufanya usafi wa mifereji na hatuwezi kusubiri maafa ndio tuanze kufanya kazi ya uokoaji sio sawa kabisa," amesema Samia.

Katika mkutano huo ambao mwenyekiti wake ni Makamba amesema kikao hicho kitatoka na azimio moja katika kukabiliana na majanga hayo.


Madiwani waliohama Upinzani kugombea tena kupitia CCM Ruangwa


Madiwani wa Kata za Namichiga na Nachingwea Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi Bakari Omari Mpanyangula na Mikdadi Ibadi Mbute, ambao walihama vyama vya Chadema na CUF na kujiunga na Chama cha Mapindizi CCM kwa kukiunga mkono Chama hicho.

Madiwani hao wananafasi kubwa ya kugombea tena nafasi hiyo kupitia CCM kwani umedhihirishwa Leo na Katibu wa CCM mkoa wa Lindi Bw, Loti Olelesele kwenye hafla ya kuwakabidhi kadi za chama hicho iliyofanyika kwa nyakati tofauti katika kata za Nachinwea na Namichiga.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya Wanachama na wapenzi wa CCM katika kata hizo Olelesele alisema Mpanyangula na Mbute ndio wanachama wanaofaa kugombea nafasi hiyo tena kupitia chama hicho, kwakuwa wameonesha uwezo mkubwa wa Uongozi walipokuwa Madiwani kupitia Vyama walivyohama.

Pia Olelesele alisema licha ya kuonesha uwezo wa uongozi lakini pia wanakubalika na Wananchi hali ambayo ilisababisha wawabwage wagombea wa CCM katika uchaguzi Mkuu uliopita "Tunakubaliana na uamuzi wa Vikao halali vya Chama vya kata za Namichiga na Nachingwea vilivyopendekeza wawe wagombea wetu wakati wa uchaguzi mdogo kwenye kata hizo kwani wananchi wameendelea kuwaamini," alisema Olelesele.

Lakini pia alitumia hafla hiyo kuwahakikishia Wananchi kwamba Chama hicho kimeweza kudhibiti vitendo vya rushwa  hivyo Viongozi wanapatikana kutokana na uwezo wao na kukubalika kwao mbele ya Wananchi


Nae Katibu wa Mkoa wa Lindi wa Jumuia ya Wazazi wa Chama hicho Tatu Hamisi, ameipongeza Serikali kwa kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa vitendo ikiwamo sera ya Elimu bila malipo, alitoa wito kwa wazazi kutumia vyema fursa hiyokwa kuwapeleka watoto wao Shule.

Hata hivyo Wanachama 15 kutoka upinzani walihama vyama vyao na kujiunga na CCM na kukaribishwa na makada wa chama hicho, nae Mpanyangula akifuatwa na watu sita wa Familia yake walimuunga mkono, Mpanyangula alisema"pamoja na kuridhishwa na Serikali ya awamu ya tano lakini mgogoro wa Uongozi ndani ya CUF umesababisha chama hicho kukosa muelekeokuanzia juu mpaka chini hivyo huu ni mwanzo tu wanachama wengi wanajiandaa kuhama," alisema Mpanyangula.

Madiwani hao walitangaza kuvihama vyama vyao vya awali wiki iliyopita kwa madai kwamba wamehamia CCM ili kuungana na Serikali ya awamu ya tano na Mbunge wao Mheshimiwa Kassim Majaliwa katika kuwaletea Wananchi maendeleo.





Nafasi za kazi leo Jan 19

Saed Kubenea Aachiwa Huru na Mahakama na Kukamatwa Tena



DODOMA: Mahakama ya Wilaya mapema leo imemuachia huru Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea(CHADEMA)

Hata hivyo Jeshi la Polisi limemkamata tena. Yadaiwa atafunguliwa mashtaka upya

Mbunge huyo kabla ya kuachiwa leo alikuwa akituhumiwa kwa kumshambulia kwa mateke, ngumi na makofi, Juliana Shonza(Mbunge wa Viti Maalum) ambaye kwasasa ni Naibu Waziri

New VIDEO: Lava Lava – Utatulia

New VIDEO: Lava Lava – Utatulia

New VIDEO: Lava Lava – Utatulia


DOWNLOAD

New VIDEO: Justin Timberlake – Supplies

New VIDEO: Justin Timberlake – Supplies
                      
                              New VIDEO: Justin Timberlake – Supplies

Justin Timberlake delivered a video teaser for his new Pharrell-produced song “Supplies” yesterday and now the pop icon is back with the full thing, directed by Dave Meyers.

Watch below:




MAGAZETI YA LEO 19/1/2018

























Pretty Kindy afunguka kupata funzo



Suzan Michael ‘Pretty Kindy’.

MSANII wa filamu Bongo, Suzan Michael ‘Pretty Kindy’ ambaye siku chache zilizopita alipewa kibano cha kufungiwa asifanye sanaa miezi sita na Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza, amesema kuwa jambo hilo limempa funzo kubwa na kuamua kubadilika kimavazi.

Akizungumza na paparazi wetu, Pretty alisema tangu naibu waziri ampe adhabu hiyo kwa kosa la kuweka picha ya utupu mtandaoni, amekuwa akiwaza mengi na kuona kuna haja ya kuufyata kwa kubadili mfumo wa mavazi yake, sababu amegundua mavazi ya utupu yanamshushia heshima.

“Kwa upande mwingine kanipa funzo kubwa maishani mwangu, tangu ile adhabu itokee, hata ukikutana na mimi utagundua hiki ninachokisema, nimebadilika mno kimavazi, navaa kiheshima, nimegundua nguo za nusu utupu zinanifanya nidharaulike tu,” alisema.

Kenya: Daktari ataka ukeketaji uhalalishwe

Daktari mmoja nchini Kenya amewasilisha kesi mahakamani akitaka upashaji tohara wa wanawake ambao hufahamika pia kama ukeketaji uhalalishwe.

Dkt Tatu Kamau anasema sheria inayoharamisha ukeketaji wa wanawake na wasichana inakiuka utamaduni katika jamii nyingi za Kiafrika.

kadhalika, amesema ni ubaguzi dhidi ya wanawake ikizingatiwa kwamba upashaji tohara wa wanaume unakubalika kisheria.

Daktari huyo anataka pia bodi ambayo iliundwa nchini humo kukabiliana na upashaji tohara wa wanawake ivunjiliwe mbali.

Aliwasilisha kesi hiyo katika Mahakama Kuu mjini Machakos, mbele ya jaji David Kemei.

Kesi hiyo itaanza kusikilizwa mwezi ujao.

Dkt Kamau, akizungumza na wanahabari baada ya kuwasilisha kesi yake, alisema wanawake wote, sawa na watu wazima popote pale, wanafaa kuruhusiwa kufanya uamuzi kuhusu miili yao wenyewe bila kuwekewa vikwazo na sheria.

Amesema ukeketaji ni neno ambalo lilitetwa na watu kutoka nchi za Magharibi

Lakini sasa amesema raia wa nchi za Magharibi wanafanya jambo sawa na ukeketaji, kufanya upasuaji kwenye uke kurekebisha maumbile.

"Upashaji tohara ulikuwa sehemu ya utamaduni wa Waafrika kabla ya kufika kwa wakoloni na haifai kuharamishwa," amesema.

"Punde tu itakapohalilishwa, tutaweza kufanya tohara kwa njia iliyo bora Zaidi, mojawapo ikiwa njia ya hospitali. Tukifanya hivyo basi itakuwa salama kabisa. Na njia hii ni mojawapo wa upasuaji wa kawaida duniani kote."

Anasema wanawake wengi wamekuwa wakisumbuliwa na maafisa wa dola au hata kufungwa jela kwa sababu ya ukeketaji.

"Ingawa tunataka sana kumlinda mtoto msichana, kuna wanawake wengi sana ambao wamekamatwa na kufungwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita," anasema.

"Unapokuwa mtu mzima, hakuna sababu yoyote ya kuzuia kufanya uamuzi (iwapo ungependa kupashwa tohara)" alisema.

Takwimu muhimu kuhusu ukeketaji Kenya

Asilimia 21 ya wanawake wa umri wa kati ya miaka 15-49 Kenya wamepashwa tohara

Kuna ushahidi kwamba siku hizi, wasichana wamekuwa wakikeketwa wakiwa na umri mdogo.

Asilimia 28 ya wanawake wa miaka 20-24 walikeketwa wakiwa na miaka 5-9, ikilinganishwa na asilimia 17 ya wanawake wa miaka 45-59.

Kuhusu aina ya ukeketaji, asilimia 2 ya wanawake wa miaka 15-49 hawakutolewa sehemu yoyote kwenye uke wao, asilimia 87 walikatwa na kuondolewa sehemu fulani, nao asilimia 9 walikatwa kisha kushonwa.

Wasichana wa miaka 0-14 wana uwezekano wa juu wa kukeketwa ikiwa mama zao wamekeketwa.
Wanawake na wanaume asilimia 11 huamini kwamba ukeketaji unahitajika kwa mujibu wa jamii yao au dini na kwamba unafaa kuendelea.

Chanzo: Takwimu ya Utafiti kuhusu Afya na Watu Kenya ya mwaka 2014

Dkt Kamau alisema jamii nyingi zimekuwa zikifanya upashaji tohara kwa njia nyingi na kwamba si aina zote za tohara hiyo ambayo ina madhara kwa mwanamke.

Alisema sawa na jinsi watu huonywa dhidi ya athari za uvutaji sigara au ungwaji pombe, kampeni ya kuwahamasisha watu kuhusu madhara ya ukeketaji inafaa kuendelea lakini wale wanaoamua au wangependa kupashwa tohara wanafaa kuruhusiwa.

Dkt Kamau ameshutumu hatua ya Bunge nchini Kenya la kupitisha sheria ya kuharamisha ukeketaji akisema Bunge lilivuka mipaka na kuingilia masuala ya utamaduni.

"Iwapo wanaweza kuharamisha utamaduni, kesho wataharamisha dini au kitu kingine. Dada anastahili kutetewa akifanya maamuzi yake, na wala si kulazimishwa kufanya mambo mengine," amesema.

Makundi yanayokabiliana na ukeketaji yameshutumu hatua ya Dkt Kamau.

Mwenyekiti wa bodi ya kukabiliana na ukeketaji Bernadette Loloju amesema ukeketaji hupingwa kwa sababu ya madhara yake kwa wanawake, hasa wakati wa kujifungua.

Amesema kampeni hiyo imefanikiwa kupunguza visa vya ukeketaji kutoka asilimia 37 mwaka 2008 hadi 21 mwaka 2014 kwa mujibu wa takwimu za serikali.

Kwa sasa hata hivyo, ukeketaji hutekelezwa kisiri.

Watoto wamekuwa pia wakipashwa tohara wakiwa wadogo kinyume na zamani ambapo ulifanywa wasichana wakibalehe.

Wasichana takriban 140 milioni wamekeketwa maeneo ya Afrika, Mashariki ya Kati na Bara Asia.

Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo pia zimeathiriwa pakubwa na ukeketaji wa wasichana.

Inakadiriwa kwamba nchini Tanzania, wasichana na wanawake 7.9 milioni wamekeketwa.

Kwa nini imekuwa vigumu kukabiliana na ukeketaji?
Katika baadhi ya jamii Afrika Mashariki, ni utamaduni unaoathiri hadhi ya mwanamke katika jamii. Baadhi ya jamii, mwanamke haruhusiwi kuolewa au kutangamana na wasichana wengine wa rika lake iwapo hatapashwa tohara.

Katika jamii ya Wamaasai kwa mfano, mwanamke huwa na wakati mgumu kuthibitisha kwamba yeye ni mwanamke kamili iwapo hajapashwa tohara.

Aidha, watoto wake huchukuliwa na jamii kama wasiokubalika.

Sherehe ambazo huambatana na upashaji tohara na wazazi wa msichana kutambuliwa kama wazee katika jamii iwapo binti mabinti wao wamepashwa tohara huwafanya kutaka sana mabinti wao wakeketwe.

SOURCE: BBC

Wamiliki wa Mabasi waomba kukutana na Rais Magufuli

WAMILIKI wa mabasi yaendayo mikoani, wameomba kukutana na Rais John Magufuli kumweleza matatizo yanayowakabili ikiwamo  vipengele wanavyodai kuwa ni kandamizi katika kanuni mpya za leseni za usafirishaji.

Wamefikia hatua  hiyo baada ya kutofikia mwafaka katika kikao kilichofanyika jana  jijini Dar es Salaam kati yao  na maofisa kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa  Usafiri wa Nchi kavu na Majini (Sumatra), Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, na Jeshi la  Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani.

Akitangaza azimio hilo kwa niaba ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo, Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi hayo (Taboa), Enea Mrutu, alisema wataandika barua kuomba kukutana na Rais  Magufuli ili kumweleza matatizo yanayowasibu.

"Tukimaliza kikao hapa na kwa kuwa wote mmekubali na mnataka kukutana na Rais  Magufuli, sekretarieti itakutana tutaandika hiyo barua na tutaipeleka nyumba nyeupe (Ikulu)," alisema Mrutu.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Taboa , Mohammed Hood, alisema kabla ya kuandikia barua ya kuomba kukutana na Rais, watafanya utaratibu wa kuonana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.

"Hatuwezi kufika kwa Rais  moja kwa moja bila  kupitia kwa Waziri, hivyo mimi  nitampigia Waziri ili nimwombe tuonane na baada ya hapo ndipo  tutakwenda  Ikulu," alisema Hood.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Udhibiti wa Usafiri wa Barabara, Johansen Kahatano, alisema hakuna uadui kati ya Sumatra na wamiliki wa mabasi na kwamba suala la faini inayotozwa kuanzia Sh. 250,000 hadi 500,000 haliwezi kuingiliwa kwa sasa kwa sababu ni la  kisheria.

"Jambo hili litafutiwe namna nyingine ya kuzungumza kwa sababu lipo kisheria. Hakuna mmiliki atakayeshitakiwa  au kupelekwa mahakamani kwa kosa la  gari kwenda kasi, dereva ndiye atakayeshitakiwa," alisema Kahatano.

Kahatano aliwataka Taboa kwenda Tume ya Ushindani kulalamika endapo wanaona kanuni au sheria hizo mpya zinawakandamiza.

Kuhusu  kuzuia gari kwa kosa la  dereva, Kahatano alisema sheria ya Sumatra inasema endapo gari litakamatwa, mmiliki wa gari atapewa siku 14 za kulipa faini hiyo na endapo siku hizo zikipita bila kulipa, mmiliki anaweza kufika Polisi au Sumatra na kutaka kesi iende mahakamani.

Alisema hakuna gari lolote litakalozuiwa kwa kosa alilofanya dereva na kwamba makosa ya dereva na mmiliki yametenganishwa.

Wakichangia katika mkutano huo, wajumbe wa Taboa wengi wao  walilamikia kanuni zilizokuwapo katika leseni za usafirishaji kuwa zinawakandamiza, huku wakipendekeza faini za viwango vipitiwe upya pamoja na makosa ya dereva na mmiliki yatenganishwe.