Saturday, 9 December 2017

Tambua Madhara ya Ulaji Wa chipsi



Chips ni aina ya chakula ambacho hupendwa na watu wengi na pia ni miongoni mwa vyakula vyenye mafuta mengi. chips pia inasemekana ni miongoini mwa vyakula ambavyo hupikwa katika joto la juu zaidi ya 300 degree.
Chips ni chakula chenye mafuta mengi na mafuta yanapoingia mwilini huenda kuzunguka sehemu ya mwili wa mwanadamu. kama ni mtu ambaye mazoezi pia hufanyi madhara yake ni kupata magonjwa ya moyo. hivi sasa idadi kubwa ya vijana wanaugua magonjwa mengi yanayo sababishwa na mkusanyiko wa mafuta katika miili yao amabayo huchangiwa na kuto kufanya mazoezi madhara yake mafuta kuziba mirija
Mafuta yakiliwa sana husababisha kuzidi mwilini.
Pia inasadikika mafuta yaliyopo katika chipsi katika sahani moja ya chisi ya moto endapo utaamua kuchuja kuna uwezekano wa kupata nusu glasi ya mafuta ya kupikia. Kwa hali hii ujue ni hatari.
Na mwili huwa hatupi kinachofaa, na badala yake kama hakitumiki wakati huo basi huhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye. Ndio maana tunapokula vyakula vyingi vyenye mafuta mengi hutupelekea kuongeza unene na uzito.
Unene huwa ni chanzo cha magonjwa mengi ,Kwani (High Blood pressure) hutokana na kuwa na mafuta mengi mwilini ambayo hupelekea mirija ya kusafirisha damu kuwa na mafuta. Hii husababisha njia ya kupitia damu kuwa nyembamba hivyo kusababisha nguvu ya ziada itumike kusukuma damu hiyo ili isambae mwilini kama inavyotakiwa. Nguvu hii ya ziada huongeza au kupunguza mapigo ya moyo.
Mapigo ya moyo yanapoongezeka sana ni hatari na yanapo pungua sana pia ni hatari.
Hivyo basi ni vizuri kwa watumiaji wa chipsi kujitahidi kutumia kwa kiasi kidogo au kuacha kabisa vile vile mazoezi pia ni muhimu ili kupunguza mrundikano wa mafuta katika mwili.
Pia inasemekana kuwa wanasayansi wamegundua kuwa chipsi husababisha kukuza hips hivyo kwa wanaume wengi hawatapenda kuwa katika hali hiyo, hivyo ni muhimu kujiepusha na pia isije ikawa kichocheo kwa wanawake kutumia sana ili kukuza sehemu hizo za maumbile bali wapunguze kutumia chipsi pamoja na kufanya mazoezi ili kuweka mwili katika hali ya kuepuka magonjwa yasiyo ya lazima.pia ulaji wa chips kupita kiasi husababisha wanaume na wanawake kuzeeka mapema.

Friday, 8 December 2017






Mwanza. Sakata la mwanamke aliyemvisha pete ya uchumba mwanamke mwenzake limechukua sura mpya baada ya jeshi la polisi kufanikiwa kuwatia mbaroni watu wengine watatu akiwemo aliyevishwa pete.
Sura mpya ya kwanza ni mtuhumiwa Milembe Suleiman (36), anayedaiwa kumvalisha pete mwanamke mwenzake Janeth Shonza, aliyekuwa akishikiliwa na polisi mkoani Geita kuhamishiwa mkoani Mwanza.
Pili, jeshi la polisi pia limefanikiwa kumtia mbaroni mwanamke aliyevishwa pete, Janeth Shonza (25), mwanafunzi wa mwaka wa nne wa sheria katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa akiwa mafichoni eneo la Puma mkoani Singida.
Amewataja wengine wanaoshikiliwa na kutarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote uchunguzi utakapokamilika kuwa ni Richard Fabian (28), mkazi wa Buzuruga jijini Mwanza aliyepiga na kusambaza mitandaoni picha za wanawake hao wakivishana pete mitandaoni.
Kamanda Msangi amemtaja mwingine anayeshikiliwa kuwa ni Aneth Mkuki (24), mkazi wa Nyasaka jijini Mwanza, mpenzi mwingine wa Janeth aliyemsaidia kutoroka kukwepa kutiwa mbaroni na polisi baada ya video yao kusambazwa mitandaoni.

Kanisa la Mch Gwajima Labomolewa usiku

Kufuatia zoezi la serikali la kupanua na kuboresha miundo mbinu mbalimbali nchini hususan ya barabara katika jiji la Dar es Salaam ambapo imelazimu baadhi ya maeneo kubomolewa ili kupisha zoezi hilo la upanuzi, Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Josephat Gwajima nalo limekumbwa na kadhia ya kubomolewa.
Kanisa hilo lililoko jirani kabisa na Barabara ya Morogoro ambayo serikali imepanga kuipanua ili kurahisisha usafiri na kupunguza foleni, lilitakiwa kubomolewa kutokana na kuwa ndani ya eneo la hifadhi ya barabara hiyo.
Mchungaji Biyagaza wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko chini ya Askofu Gwajima, ameeleza kuwa serikali iliwapatia notisi ya siku 30 ili wabomoe kipande cha jengo la kanisa hilo kilichopo ndani ya eneo la hifadhi ya barabara.
“Ni kweli tunayo notice ya mwezi mmoja ya kuhakikisha kwamba eneo ambalo ni hifadhi ya barabara tunaliacha. Na hifadhi ya barabara ni mita 90 kuanzia katikati. Bahati nzuri wale waliokuja kuweka alama zao walipofika hapa na wahandisi , mafundi na baadhi ya watu wa kanisani walikuwepo. Basi tukawaambia wapime mita 90 zinapoishia. Kwa hiyo wakapima mita 90 zilipoishia wakaweka alama, wakasema basi nyie mnaweza mkabomoa upande huu na upande huu mkauacha kwa ajili ya hifadhi ya barabara,” alisema Mchungaji Biyagaza.
“Sisi baada ya hapo tukaona tujipange kwa ajili kuachia eneo la barabara ili shughuli nyingine ambazo ni mpango wa maendeleo ya serikali ziweze kuendelea na sisi tuweze kuendelea na eneo letu vizuri. Kwa hivyo kile kipande chote ambacho ni cha barabara na tukaongeza ndani kidogo chote tumekiondoa. Na hili eneo linalobaki tunapaimarisha ili nyumba ya Bwana iweze kufanya kazi yake ya kutoa huduma za kiroho,” aliongeza.
Mchungaji Biyagaza alieleza japokuwa eneo la jengo limepungua, eneo lililobakia linaimarishwa ili kanisa hilo liweze kuendelea kutoa huduma za kiroho kwa waumini wake.
Aidha kufuatia zoezi hilo la upanuzi wa barabara ya Morogoro ambalo linaenda sambamba na ujenzi wa barabara za juu (fly-over) katika makutano ya barabara eneo la Ubungo, umepelekea kubomolewa kwa majengo mbalimbali ikiwemo majengo ya wizara ya Maji na Umwagiliaji pamoja na jengo la Makao Makuu ya Shirika la Umeme Tanzania ambayo yamebomolewa kufuatia agizo la Rais Dkt. John pombe Magufuli.

Jerry Muro amesema uwezowake ajilinganisha na Wabunge 10 Chadema




Aliyekuwa Msemaji wa Yanga SC, Jerry Muro amesema kutokana na uwezo wake katika mambo mbali mbali anaweza kujilinganisha na wabunge 10 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katika mahojiano na kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm, Jerry amesema kutokana na uwezo wake suala la ubunge kwake ni jambo rahisi tu sawa na kubofya button.

“Mimi Jerry Muro mmoja ni sawa na wabunge 10 wa Chadema, nimewazidi kifikra, kinguvu, kipesa, maadili, kihoja na mambo mengine mengi sana” amese Jerry.

Katika hatua nyingine Jerry amesema mwaka 2020 si ajabu kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Edward Lowassa wakirejea katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Watu wawili waliokutwa na Mayai ya Mbuni wahukumiwa miaka 25 Jela



Serengeti. Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya  Serengeti imewahukumu kifungo cha miaka 25 washitakiwa wawili na gari lao kutaifishwa kwa kosa la kukutwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni.

Waliokumbwa na adhabu hiyo ni Marwa Matiko(32) na Julius Marwa (42) wakazi Tarime mjini.

Akitoa hukumu leo Ijumaa katika kesi ya uhujumu uchumi namba 128/2016 hakimu wa mahakama hiyo, Ismael  Ngaile amesema kila mshitakiwa atahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela na gari lao kutaifishwa liuzwe.

Mapema mwendesha mashitaka wa Jamhuri, Emmanuel Zumba ameiambia Mahakama kuwa, washitakiwa hao walikamatwa Desemba 7, 2016 wakiwa kwenye nyumba ya kulala wageni Serengeti wakiwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni kinyume cha sheria.

Amesema mayai hayo walikuwa wameyaficha ndani ya gari lao.

Amesema washitakiwa wakidai kuwa walikuwa wanapeleka nchini Kenya kwa ajili ya kuuza kwa watu wanaotengeneza dawa ya ukimwi.

Akamatwa na Polisi baada ya kumuua nesi



Polisi siku ya Jumatano walimkamata mgonjwa aliyemuua nesi kwa kumpiga risasi ya kichwa kwenye kituo cha afya cha Chiromo huko Westlands, Nairobi

Mgonjwa huyo aliyetambuliwa kwa jina la Joseph Njoroge Mungai mwenye kibali cha kumiliki silaha alimpiga risasi ya kichwa daktari huyo aliyefahamika kwa jina la Faustine Mwandime Mwandilu

Kamanda wa polisi wa Nairobi Japheth Koome amesema mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kwa kesi ya mauaji

Mtuhumiwa huyo mwenye matatizo ya akili alipelekwa na kulazwa hospitalini hapo akiwa na bunduki baada ya kukataa kuiwasilisha kwa walinzi wa hospitali

Askari Mgambo Kizuizini kwa kujifanya Maofisa Uhamiaji



Mwanza. Idara ya uhamiaji jijini Mwanza inawashikilia kwa mahojiano askari mgambo wawili wa jiji la Mwanza kwa tuhuma za kujifanya maofisa wa idara hiyo na kupita maeneo ya biashara ikiwemo mahoteli kukagua vibali vya ukaazi wa wageni.

Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Paul Eranga akitoa taarifa leo Ijumaa amesema mgambo hao walikamatwa walipofika kwenye moja ya hoteli za kitalii jijini Mwanza kwa lengo la kukagua wageni waliofikia hapo iwapo wana nyaraka na vibali halali vya kuingia nchini.

Amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni Chacha Kichele, mkazi wa Bugarika Wilaya ya Nyamagana na mwenzake Michael Julius, mkazi wa Kiloleli wilayani Ilemela.

“Walitumia mwanya wa sare zao kufanana na zile za idara ya Uhamiaji kupita kwenye mahoteli kukagua wageni wakijifanya ni maofisa Uhamiaji hadi uongozi wa hoteli moja ulipowashtukia na kutoa taarifa,” amesema Eranga

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download


DOWNLOAD

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download

Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download
Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download



Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download

Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download

Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download


Thursday, 7 December 2017

Shilole afunga pingu za maisha na mchumba wake



Ashraf Uchebe akiwa na mkewe, Shilole.

Hatimaye msanii wa Bongo Fleva, Shilole amefungua ndoa na mpenzi wake Ashraf Uchebe huko Masaki usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam.

Staa huyo alikuwa akisisitiza kufunga ndoa mwaka huu lakini watu walikuwa wakichukulia poa kwa sababu si mara ya kwanza kutoa kauli kama hiyo lakini jana Desemba 6 akafanya kweli.

Baada ya picha kusambaa mtandaoni aliyekuwa mpenzi wa Shilole, Nuh Mziwanda ameandika ujumbe katika ukurasa wa Instagram ambao unaweza kutafsiriwa kama ametupa kijembe kwenye ndoa hiyo.  Nuh ameandika;

Alie LaLa na BiBi harusi’wiki Moja KabLa ya harusi’Na wala sio Bwana Harusi’Bado mnanishauri harusi 😏 (all girls are pretenders )

Alichokiandika Nuh Mziwanda ni mistari kutoka kwenye wimbo wa Mwana FA ‘Bado Nipo Nipo’ ambao ulitoka takribani miaka 10 iliyopita.

Baada ya Mwandishi wa Mwananchi kupotea, OJADACT yataka uchunguzi ufanyike


Mwandishi wa kujitegemea wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Azory Gwanda.

Chama cha Waandishi wa Habari wa Kupinga Vita Matumizi Dawa za Kulevya na Uhalifu (Ojadact), kimevitaka vyombo vya dola na mamlaka nyingine serikalini kumtafuta na kumpata mwandishi wa kujitegemea wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Azory Gwanda.

Gwanda ambaye kituo chake cha kazi ni Pwani ametoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 21 na mpaka sasa hajulikani alipo.

Mbali ya Ojadact, vyombo vya habari vya kimataifa na wadau mbalimbali wa habari wamezungumzia kutoweka kwa Gwanda wakitaka juhudi za makusudi za kutafutwa na kupatikana kwa mwandishi huyo.

Akizungumza na mwaandishi wa habari jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Ojadact, Edwine Soko aliwaomba wadau wa habari nchini kuunganisha nguvu katika kumtafuta na kuvishinikiza vyombo na mamlaka husika kumtafuta mwandishi huyo.

“Hatuwezi kuendelea kuvumilia tabia inayoanza kuzoeleka nchini ya watu kupotea bila kujulikana walipo huku vyombo vya dola vyenye dhamana ya ulinzi na usalama wa raia vikichukulia kawaida, kama jamii lazima tusema hapana kwa sababu huo siyo aina ya Utanzania tuliouzoea,” alisema Soko.

Soko alisema jamii haipaswi kuendelea kufumbia macho vitendo vya watu kupotea na wengine miili yao kuokotwa katika fukwe za bahari na mito nchini kwa sababu vinakiuka Ibara ya 14 ya Katiba inayolinda haki ya kuishi kwa kila mtu.

Alisema tukio la Gwanda lina dalili zote za uovu kwa sababu muda ambao hajaonekana unazidi hata ule unaoruhusiwa mtuhumiwa kushikiliwa kisheria hata na vyombo vya dola kabla ya kumfikisha mahakamani.

Kwa mujibu wa mkewe, Anna Pinon (35), Novemba 21, Agwanda aliaga nyumbani kwake Kibiti kuwa kuwa anaenda kazini lakini hakufika wala kurejea nyumbani.

Mmoja wa waandishi wa habari jijini Mwanza, Halima Juma alisema kitendo cha Gwanda kupotea kimeibua hofu miongoni mwa waandishi wa habari nchini, hasa wanaofuatilia na kuibua habari zinazopiga vita uovu, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kwa watu wenye uwezo na mamlaka.

Kupitia kurasa zake za kujamii, mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliandika ‘’Maswali kwa @MwananchiNews 1) alikuwa ana ‘assignment’ yeyote kutoka kwenu alipotekwa huko Kibiti? 2) kama ndio kwanini hamsemi hilo? 3) Mna Habari yake yeyote hamjaichapisha gazetini?

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kilisema ‘’tunaungana na uongozi wa @MwananchiNews kutoa wito kwa Jeshi la Polisi Tanzania…kuchukua hatua ili ndugu Azory Gwanda aweze kupatikana. #MrudisheniAzoryGwanda.”

Vituo vya habari za kimataifa vya Fox News, New York Times, Daily Nation walizungumzia kupotea kwa mwandishi Gwanda.