Friday, 3 November 2017

Mawaziri wawekwa kizuizini Catalonia



Raia wa jimbo la Catalonia wanaotaka kujitenga wameandamana nje jengo la bunge la jimbo hilo mjini Barcelona baada ya jaji mjini Madrid kuwaweka kizuizini mawaziri nane wa serikali ya jimbo la Catalonia.

Taarifa zinasema kuwa hadi sasa kuna jumla ya wanasiasa kumi wa Catalonia waliowekwa kizuizini nchini Hispania wakiwemo pia viongozi wa kitamaduni wawili ambao nao wanashikiliwa.

Jaji Carmen Lamela amesema kuwa aliamua kuwaweka kizuizini viongozi hao nane kwa kuhofia kwamba wanaweza kutorokea nje ya nchini ama kuharibu ushahidi.

Waendesha mashitaka wanawatuhumu wanasiasa hao kwa makosa mawili ambayo ni mapinduzi na uchochezi katika jaribio la kutaka kujitenga na Hispania.

Hata hivyo jaji bado hajatoa kibali cha kukamatwa nje y nchi kwa kiongozi wa watu wa jimbo la Catalonia Carles Puigdemont na wenzake wane ambao wote wapo nchini Ubelgiji.



MAGAZETI YA LEO 3/11/2017


MAGAZETI YA LEO 3/11/2017




Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download


Enock Bella - Sauda

Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download

                                       
https://my.notjustok.com/track/download/id/287696/by/eM_J1W76fP

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download

Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees - Double Double

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download


https://my.notjustok.com/track/download/id/287534/by/6NAtshXQUW

Audio | Ibrah Nation Ft. Switcher Baba – Batani | Mp3 Download

Audio | Ibrah Nation Ft. Switcher Baba – Batani | Mp3 Download

Ibrah Nation Ft. Switcher Baba - Batani

Audio | Ibrah Nation Ft. Switcher Baba – Batani | Mp3 Download


https://my.notjustok.com/track/download/id/287525/by/EaKQ6xEaRm

Video | Enock Bella – Sauda | Download Mp4

                          Video | Enock Bella – Sauda | Download Mp4

Video Enock Bella - Sauda



Video | Enock Bella – Sauda | Download Mp4





Thursday, 2 November 2017

Jela miezi 6 kwa kuoa mke wa pili Pakistan




Mahakama nchini Pakistan imemfunga mwanamume mmoja miezi sita jela ya kuoa mke wa pili bila ya idhini kutoka kwa mke wake.

Mahakama hiyo ya mjini Lahore pia ilimuamrisha Shahzad Saqib, kulipa faini ya dola 1,900, na kukataa maoni yake kuwa dini ya kiislamu inamruhusu kuoa hadi wake wanne.

Mke wa kwanza wa Sadiq Ayesha Bibi, alikuwa amefanikiwa kujitetea kuwa kuoa bila idhini yake ulikuwa ni ukiukaji wa sheria za familia nchini Pakistan.

Wanaharakati wa masuala ya wanawake wabasema kuwa kesi hiyo ni pigo kwa ndoa za wake wengi.
Mfasiri wa FBI afunga ndoa na mwajiri wa IS

Pia walisema kuwa itawapa wanawake zaidi walio katika hali kama hizo motisha ya kupeleka kesi mahakamani.

Nchini Pakistan, wanaume wanaotaka kuoa wanawake kadhaa hufanya hivyo baada ya miaka kadhaa na ni lazima wapate idhini kutoka kwa mke wa kwanza.

Baraza la kiislamu nchini Pakistan ambalo hutoa ushauri wa serikali kuhusu masuala ya kiislamu, mara kwa mara limekosoa sheria za familia nchini humo.

Sadiq ana haki ya kukata rufaa kupinga hukumu hiyo ya siku ya Jumatano.

Watu 34 wahukumiwa kunyongwa



Watu 34 wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, (Albino), ambapo matukio 67 ya ukatili dhidi ya albino yakiwa yameripotiwa.

Takwimu hizo zimetolewa katika muendelezo wa mkakati wa kitaifa wa kupiga vita ukatili, mauaji na unyanyasaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi ambapo Wakili kutoka Ofisi Mkurugenzi wa Mashtaka, Beatrice Isembo, amesema, pamoja na adhabu za vifo, watuhumiwa 17 wamehukumiwa vifungo tofauti huku kesi nyingine zikiendelea.

"Tumegundua mikoa ya kanda ya Ziwa ndiyo iliyoongoza kwa matukio ya aina hii  na yote ni kutokana na imani za kishiriki kama kutaka utajiri kwenye uvuvi, mazao nk." Mwanza inaongoza kwa kuwa na kesi za aina hii 15, na jumla ya matukio 67 yameripotiwa katika kipindi cha miaka 11" amesema Bi. Isembo.

Kwa upande wake, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Ralph Meela, kutoka Makao Makuu ya jeshi la polisi Idara ya Upelelezi kitengo cha makosa dhidi ya binadamu na usalama barabarani, amesema, asilimia kubwa ya mauaji hayo yanatokana na imani za kishirikina hasa maeneo ya migodini na uvuvi pembezoni mwa ziwa Victoria.

Julio aanza majigambo




KOCHA MKUU WA TIMU YA DODOMA FC YA DODOMA, JAMHURI KIHWELU ‘JULIO’,.

KOCHA Mkuu wa timu ya Dodoma FC ya Dodoma, Jamhuri Kihwelu ‘Julio’, amesema matokeo mazuri ambayo timu yake inapata katika mechi za Ligi Daraja la Kwanza yanatokana na wao kujipanga na si kubebwa kama baadhi ya wadau wanavyosema.

Akizungumza na gazeti hili jana, Julio, alisema kuwa anaamini kikosi chake kina nafasi ya kupanda daraja na kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao kwa sababu wamejipanga kuendelea kupambana ili watimize malengo waliyoyaweka.

Beki na kocha huyo wa zamani wa Simba alisema pia ligi hiyo ni ngumu na ina changamoto mbalimbali huku akiweza wazi kukukutana na ushindani kwenye michezo yote wanayocheza.

“Hakuna mechi rahisi, tunapambana katika kila mechi, hatubebwi, hata ukiangalia matokeo yetu, mechi nyingi tulizoshinda tumecheza ugenini, tutaendelea kupambana tutakaporudi kumalizika michezo ya nyumbani," alisema Julio.

Baada ya juzi kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Toto Africans, Dodoma FC imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa na pointi 18, ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine katika kundi lao ikiwamo Alliance ambayo imekuwa mshindani.

Timu sita kutoka katika Ligi Daraja la Kwanza zitapanda daraja na kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao wa 2017/18

Omog hafukuzwi ng’o: Simba



KAIMU RAIS WA KLABU HIYO, SALIM ABDALLAH "TRY AGAIN.

WAKATI mkataba wa Kocha Mkuu wa Simba, Joseph Omog, ukiwa umebakiza miezi minne kumalizika na hakuna mazungumzo yoyote ya kusaini mkataba mpya yaliyofanyika, Kaimu Rais wa klabu hiyo, Salim Abdallah "Try Again", ameibuka na kusema kuwa kocha huyo hafukuzwi.

Minong'ono ya kutimuliwa kwa Omog imeendelea kwa kasi baada ya kutua kwa Mrundi Masoud Djuma Irambona, ambaye amerithi mikoba ya Jackson Mayanja aliyeamua kuachia ngazi na kurejea kwao Uganda kumaliza matatizo ya kifamilia.

Akizungumza na Nipashe jana, Salim, alisema kuwa Omog bado ni kocha wa Simba na hakuna kikao chochote ambacho kimefanyika na kufikia uamuzi wa kumtimua kocha huyo raia wa Cameroon.

Salim alisema kuwa mpaka sasa timu yao haijapoteza mchezo wowote kwenye ligi na anawaomba wote ambao wanafikiria Omog ataondoka kwenye klabu hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Kubashiri Matokeo Michezoni ya SportPesa, kwa sasa waache kuwaombea "mabaya".

"Kuna watu wana ndoto na matarajio ambayo hatuwezi kuwazuia kuyafikiria, hatujafungwa, tunaongoza ligi, ligi ni ngumu msimu huu, sio ya kawaida, timu nne zote zinalingana pointi, haijawahi kutokea," alisema Salim ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kundi la Friend's of Simba.

Hata hivyo, Salim alikataa kuweka wazi kama klabu ina mpango wa kumpa mkataba mpya Omog ambaye aliwahi kuifundisha Azam FC, lakini akikiri kuwa waliwahi kufanya mazungumzo na Kocha Mkuu wa Lipuli FC, Selemani Matola ili kuchukua nafasi ya Mayanja.

"Mkataba ni siri kati ya sisi na kocha, hatuwezi kuweka hadharani, ila tuna mkataba naye mrefu, hatuna mpango wa kumfukuza, pia siwezi kusema kesho kitatokea nini, anaweza yeye akaamua kuachana na sisi na kwenda mahali kwingine," alisema Salim.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa Omog na msaidizi wake wanafanya kazi kwa ushirikiano na tayari wameshaanza kutoa mapendekezo ya kuimarisha kikosi cha timu hiyo kuelekea dirisha dogo la usajili.

"Omog ametupa ubingwa wa FA, tukamaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita, kwa sasa Simba iko vizuri, hakuna migogoro na viongozi tunajenga mifumo imara na sahihi, tunataka kuiendesha klabu kisasa, tunaachana na kufanya mambo kwa mazoea," aliongeza kiongozi huyo.

Kikosi cha Simba kinatarajia kuondoka jijini kesho kuelekea Mbeya kwa ajili ya kuwafuata wenyeji wao Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kupigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Sokoine jijini humo

Nafasi za kazi leo November 2

Basi lagonga kichwa cha tren




Kada Maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Jimbo la Mtera Mkoani Dodoma amewasihi Watanzania kumpuuza Mwanasiasa Lazaro Nyalandu ambaye juzi ametangaza kujivua nyadhifa zake zote katika CCM ikiwemo ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa kile alichodai Serikali kukigandamiza Chama na CCM kupoteza mwelekeo.

Lusinde amesema Bw. Lazaro Nyalandu hakuwahi kunyimwa nafasi yoyote ya kutoa maoni yake ama dukuduku zake ndani ya chama wala bungeni na kwamba uamuzi huo unaashiria kuwa anatafuta kinga ya kutochukuliwa hatua kutokana na tuhuma nzito zinazomkabili.

Kada huyo wa CCM amesema ana wasiwasi ndani ya Serikali wapo watendaji ama viongozi wasio waaminifu ambao watakuwa wamevujisha taarifa za hatua ambazo Serikali inatarajia kuzichukua dhidi kutokana na makosa makubwa aliyoyasababisha alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na alipokuwa Naibu Waziri

Lusinde Amchana Nyalandu



Kada Maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge wa Jimbo la Mtera Mkoani Dodoma amewasihi Watanzania kumpuuza Mwanasiasa Lazaro Nyalandu ambaye juzi ametangaza kujivua nyadhifa zake zote katika CCM ikiwemo ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini kwa kile alichodai Serikali kukigandamiza Chama na CCM kupoteza mwelekeo.

Lusinde amesema Bw. Lazaro Nyalandu hakuwahi kunyimwa nafasi yoyote ya kutoa maoni yake ama dukuduku zake ndani ya chama wala bungeni na kwamba uamuzi huo unaashiria kuwa anatafuta kinga ya kutochukuliwa hatua kutokana na tuhuma nzito zinazomkabili.

Kada huyo wa CCM amesema ana wasiwasi ndani ya Serikali wapo watendaji ama viongozi wasio waaminifu ambao watakuwa wamevujisha taarifa za hatua ambazo Serikali inatarajia kuzichukua dhidi kutokana na makosa makubwa aliyoyasababisha alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na alipokuwa Naibu Waziri