Saturday, 21 October 2017

Wanafunzi watishia kuchoma shule Geita

Geita. Vurugu kubwa zimeibuka katika Shule ya Sekondari Geita baada ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita kutishia kuchoma shule kushinikiza wenzao wanne wanaoshikiliwa na polisi waachiwe.
Polisi Geita inawashikilia wanafunzi wanne wa shule hiyo tangu Alhamisi baada ya kumpiga, kumjeruhi na kutishia kumuua mwenzao wa kidato cha tano.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Isaya Busagwe amesema mwanafunzi huyo alipigwa Jumamosi iliyopita na walimu waligundua tukio hilo baada ya aliyepigwa kuugua na kuomba ruhusa ya kwenda nyumbani kutibiwa.
Jana Ijumaa Oktoba 20, wanafunzi hao waligoma kuingia darsani, badala yake, waliandamana kwenda kituo cha polisi kushinikiza wenzao kuachiwa huru.
Baada ya juhudi zao kugonga mwamba kwa polisi kuendelea kuwashikilia wenzao, wanafunzi hao walirejea shuleni na kuanza kurusha mawe wakitishia kuchoma moto majengo wakishinikiza wajumbe wa bodi waliokua wakiendelea na kikao shuleni hapo kutatua suala hilo.
Leo Jumamosi asubuhi, wanafunzi hao walianzisha vurugu zingine, hali iliyolazimisha jeshi la polisi kuingilia kati na kufanikiwa kuzidhibiti.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita(OCD), Ally Kitumbo aliyeongoza kikosi cha kutuliza ghasia kudhibiti vurugu hizo hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo akisema yeye siyo msemaji na kazi yake ni kulinda amani na utulivu.
Katika vurugu hizo mwandishi wa habari hii naye amejikuta akiwekwa chini ya ulinzi na kunyang'anywa simu na askari polisi kabla ya kunusuriwa na OCD na kuruhusiwa kuendelea na kazi.

Friday, 20 October 2017

AUDIO | Come Dash _ Haitowezekana | Download

https://my.notjustok.com/track/download/id/283017/by/vJHK6UaW3X

Breaking News: Matokeo ya darasa la saba yatangazwa


Bonyeza link hapo chini kuanaglia matokeo ya Darasa La Saba mwaka 2017

http://www.necta.go.tz/matokeo/2017/psle/psle.htm

Juma Nature Awafungukia Wasanii Wachanga

Msanii Juma Nature ambaye ni mkongwe kwenye game ya bongo fleva, amewataka wasanii wachanga kufuata sheria pale wanapotaka kutumia nyimbo za wasanii wakongwe jukwaani, ikiwemo kuomba kibali kwa muhusika na ikiwezekana amlipe fedha
Juma Nature ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa East Africa Radio, na kueleza kwamba msanii mchanga kuimba nyimbo za msanii mkongwe jukwaani sio jambo baya na inaonyesha heshima, lakini ni vyema wakawa na makubalino maalum kabla hajafanya hivyo kuepusha migogoro.

Askofu Afariki Akiwa Safarini

Dar es Salaam. Jimbo Katoliki la Tunduru Masasi limempoteza askofu wake, Castory Msemwa aliyefariki jana Alhamisi Oktoba 19,2017 saa saba mchana nchini Oman.
Kwa mujibu wa Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Tunduru Masasi, Padri Jordan Liviga, Askofu Msemwa amefariki dunia mjini Muscat akiwa safarini kwenda nchini India kwa matibabu.
Taarifa ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) imesema Askofu Msemwa alikuwa na tatizo la kiafya kwa kipindi cha miaka miwili na amekuwa akipata tiba na kuendelea na utume kama kawaida.
TEC imesema Askofu Msemwa aliondoka nchini Jumatano Oktoba 18,2017 kuelekea nchini India kwa matibabu kabla hajafariki dunia.
Padri Liviga amebainisha kuwa utaratibu wa kuuleta nchini mwili wa marehemu Askofu Msemwa Jumapili Oktoba 22,2017 unafanyika. Amesema taarifa zaidi za utaratibu wa mazishi zitatolewa baadaye.
Askofu Msemwa amezaliwa mwaka 1955 katika Kijiji cha Kitulira, Parokia ya Matola Jimbo Katoliki Njombe.
Alipata elimu ya msingi katika shule ya Motola, kisha sekondari katika Seminari Kuu ya Peramiho ambako alisomea Falsafa na Teolojia kati ya mwaka 1981 na 1987. Alipata daraja ya upadri Juni 7,1987. Amekuwa Paroko Msaidizi, kiongozi wa vijana parokiani jimboni Njombe, mwalimu na amesoma katika Chuo cha Teresianum Pontifical College for Spirituality huko Roma na kuhitimu mwaka 1996.
Alipata Daraja ya Uaskofu Januari 30,2005 kisha kusimikwa kuliongoza Jimbo Katoliki Tunduru Masasi Agosti 25,2005.

Nassari ashangaa kuwaona viongozi ofisini


Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari amesema kuwa bado anashangaa kuendelea kuwaona ofisini viongozi ambao aliowataja kwenye ushahidi wa kutumia rushwa kununua madiwani wa Chadema mkoani Arusha kwani watakuwa na nafasi kubwa ya kuharibu ushahidi huo. Mh. Nassari amesema kwamba hofu yake kwa viongozi hao ni kwamba watakuwa na nafasi kubwa ya kuuharibu ushahidi huo kwa kuwa bado wamekalia madaraka hivyo wanaweza kufanya lolote kuhakikisha ushahidi ulioneshwa unaharibika ikiwa ni pamoja na upelelezi kufanyika kwa mashaka. "Kinachonishikisha ni kuendelea kuwaona viongozi wale bado wapo ofisini. Huko nyuma tumeona watu wakiwajibika kisiasa pale wanapopata tuhuma kuhusu rushwa, huwa wanawajibika au kuwajibshwa. Hapa naona inakuwa ngumu kidogo kuhusu upelelezi wa kesi hii kufanyika . Mfano tunaona sehemu kwenye video Mkurugenzi anasikika akieleza ni namna gani ataelekeza wale madiwani waanze kulipwa kidogo kidogo lakini bado yupo ofisini hii inanisikitisha kwani upelelezi unakuwa na mashaka kidogo" Nassari Aidha Nassari amesema ameshangazwa na kauli ya Mkurugenzi wa Takukuru, Valentino Mlowola kwamba yeye anaingilia upelelezi wao na kudai kwamba anachoamini yeye ni kwamba hajavunja sheria wala hajaingilia upelelezi wao kwani anachokifanya ni kuutaarifu umma kila hatua anayokua anaifanya. Nassari ameongeza kwamba kauli zinazotolewa na Mlowola kama zina lengo la kumtia hofu basi kwake hofu hiyo anaamini haitafanya kazi kwake kwani kama ni kuzungumza na wanahabari wakati akiwa anapeleka ushahidi hataacha kwani huwa hazungumzii ushahidi alioubeba bali huwa anazungumzia hatua anazopiga. Pamoja na hayo Nassari amesema hawezi kuzungumza kama haki itapatikana au la bali anachoamini Takukuru ni taasisi inayojitegemea hivyo hawataona haya kutenda haki ili ijulikane wateule wa rais wana hatia au vinginevyo.

Mexime asema Kagera Sugar bado inatafuta ushindi

Kocha wa klabu ya Kagera Sugar ya mkoani Kagera inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara Meck Mexime amesema timu yao bado inatafuta ushindi.
Meck ameyasema hayo leo kuelekea mchezo wa raundi ya 7 dhidi ya Mwadui FC utakaopigwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga.
“Kikubwa sisi tunatafuta ushindi kwasababu hatujaupata tangu ligi ianze, hivyo tumejiandaa kutafuta ushindi na pointi tatu”, amesema Meck Mexime.
Mexime ambaye ni mchezaji na kocha wa zamani wa timu ya Mtibwa Sugar ameshindwa kuonesha makali ya msimu uliopita tangu ligi ya msimu wa 2017/18 ianze ambapo hajafanikiwa kupata ushindi kwenye mechi Sita za mwanzo.
Hadi sasa Kagera Sugar inaburuza mkia kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 2. Wakata Miwa hao wa Kaitaba wamepoteza mechi 4 na kutoa sare mechi mbili. Wakati Mwadui wanashika nafasi ya 12 ikiwa na alama 6 baada ya michezo Sita.

Umoja wa Mataifa Umesitisha Shughuli Zake Zote Nchini Kenya Kuhofia Uchaguzi

Umoja wa Mataifa (UN) umesitisha shughuli zake zote nchini Kenya katika kipindi cha kuelekea uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26.
Taarifa iliyotolewa Ijumaa na Msaidizi wa Katibu mkuu kanda ya Afrika Mashariki, Peter Drennan imesema umoja huo utasitisha kwa muda programu zake zote ambazo hazikuwa muhimu sana.
“Baada ya kufanya tathmini ya hali ya usalama nchini Kenya, ofisa mteule (DO) kwa ushauri kutoka Timu ya Usimamizi wa Usalama, ameshauri kusitishwa kwa warsha, mikutano, semina na makongamano na jumbe mbalimbali zisizo za lazima nchini Kenya walau kwa wiki moja kabla na wiki moja baada ya uchaguzi wa marudio kwa kura ya urais,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
“Ninakubaliana na ushauri wa DO na mamlaka husika kusitishwa kwa programu hizo ambazo hazina ulazima kuanzia leo Oktoba 19 hadi Novemba 2.”
Jana Alhamisi serikali ilitangaza kwamba Alhamisi ya Oktoba 26 itakuwa siku ya mapumziko kwa ajili ya kuruhusu wananchi kushiriki uchaguzi wa marudio.
Kaimu Waziri wa Mambo ya Ndani, Fred Matiang’i alitangaza kwamba siku hiyo imeandikwa katika Gazeti la Serikali kwamba itakuwa siku ya mapumziko kuwezesha Wakenya kushiriki kwa uhuru uchaguzi huo.
Tangazo hilo limekuja katikati ya mnyukano wa kisiasa na kuiweka uchaguzi huo katika hatihati ya kufanyika.
Jumatano, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati alielezea kukerwa kwake katika maandalizi ya uchaguzi wa marudio na akatangaza wazi kuwa hawezi kuhakikisha uchaguzi wa kuaminika.
Chekubati alisema kutokana na kupanda sana kwa hofu ya kisiasa nchini, alipendekeza Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakutane kwa mazungumzo kabla ya uchaguzi huo

BAD NEWS ! Ajali ya Hiace na lori Yaua Watu watano

Muleba. Watu watano wamefariki dunia baada ya gari aina ya Toyota Hiace kugongana na lori kisha kuwaka moto.
Ajali hiyo imetokea katika Kijiji cha Kyamyorwa wilayani Muleba mkoani Kagera.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Olomi amesema ajali hiyo imetokea leo Ijumaa Oktoba 20, saa 12:00 asubuhi.
Amesema mwendo kasi wa dereva wa gari dogo la abiria ni chanzo cha ajali hiyo.
Ingawa Kamanda Olomi hakuwataja waliokufa, Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Richard Ruyango amesema miongoni mwao ni dereva wa gari dogo, kondakta na abiria watatu.
Amesema watu hao walishindwa kujiokoa kutokana na mlango wa gari kubanwa hivyo kushindwa kufunguka.

UN yatoa Dola160 milioni nchini

Mratibu mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez
Dar es Salaam. Umoja wa Mataifa (UN) umetoa Dola 160 milioni za Marekani kati ya Dola 200 milioni zinazitakiwa kutolewa mwaka huu kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwamo kuwahudumia wakimbizi waliopo kambi mbalimbali Kigoma.
Nusu ya fedha hizo zimeelekezwa kwenye mradi wa Kigoma wa kuwahudumia wakimbizi na kiasi kingine kimeelekezwa kwenye miradi mingine ya maendeleo inayofadhiliwa na mashirika mbalimbali ya UN.
Oktoba 24, UN itaadhimisha miaka 72 tangu kuanzishwa kwake na sherehe za maadhimisho hayo kitaifa zinatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wageni zaidi ya 500 wakiwamo na mabalozi, wanafunzi na vyombo vya ulinzi na usalama.
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ‘Maendeleo ya Viwanda na Utunzaji Mazingira kwa Maendeleo Endelevu.’
Akizungumzia maadhimisho hayo jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kimataifa na kikanda, Dk Susan Kolimba alisema wameamua kuunganisha kauli mbiu ya Serikali ya kuendeleza viwanda na mpango wa UN wa kutekeleza Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDGs).
Mratibu mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez alisema programu ya Kigoma imebuniwa ili kukidhi vipaumbele vya maendeleo ya mkoa huo na hasa kuzilenga jamii katika wilaya za Kasulu, Kibondo na Kakonko.

Yanga yaipiga mkwala stand UTD

KOCHA MSAIDIZI WA KLABU YA YANGA, SHADRACK NSAJIGWA.
KOCHA msaidizi wa klabu ya Yanga, Shadrack Nsajigwa, amesema maandalizi waliyoyafanya kuelekea mchezo wao dhidi ya Stand United ni ya kiwango cha juu na wenyeji hao wasitegemee urahisi.
Yanga itashuka kwenye Uwanja wa Kambarage, ulioko Shinyanga keshokutwa ili kusaka pointi nyingine muhimu za kutetea ubingwa wanaoushikilia.
Akizungumza na gazeti hili jana kutoka Tabora walipokuwa wameweka kambi ya muda kujiandaa na mchezo huo, Nsajigwa, alisema kuwa, wamejiandaa vizuri na mchezo wao wa kirafiki waliocheza juzi dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora umewaongezea nguvu.
“Tulijiwekea mikakati katika michezo miwili ule wa Bukoba na huu tunaokwenda kucheza Shinyanga, tuondoke na pointi zote sita, tumefanikiwa mchezo wa kwanza, tunaenda Shinyanga kukamilisha kile tulichokianza Bukoba,” alisema Nsajigwa.
Aliongeza kuwa wanajua watakutana na ushindani kutoka kwa wenyeji wao, ambao watataka kutumia vyema uwanja wa nyumbani, lakini wamejipanga kuondoka na ushindi.
Kuhusu wachezaji watakaoanza kwenye mchezo huo hasa kuepuka wale wenye kadi mbili za njano ambao wanaweza wakapelekea kuukosa mchezo dhidi ya Simba, Nsajigwa alisema suala lipo chini ya Kocha Mkuu, George Lwandamina.
“Tuna siku ya leo (jana) kesho (leo) na Jumamosi kuangalia nani ataanza kwenye mchezo wa Shinyanga, tunafahamu tunatakiwa kuwa na tahadhari, si tu kwa kadi lakini pia kuepuka wachezaji wetu wasiumie kwa sababu ya mchezo wa Oktoba 28, hilo suala linafanyiwa kazi,” alisema Nsajigwa.
Wachezaji wa Yanga ambao wana kadi mbili za njano na wako katika hatari ya kuikosa Simba kama wataonyeshwa kadi yoyote Jumapili ni Kelvin Yondani na Juma Abdul.

Uongozi wa Trump wakosolewa na Marais hawa

Marais wa zamani George Bush na Barrack Obama
Marais wawili wa zamani nchini Marekani wameonyesha wasiwasi wao kuhusu hali ya kisiasa nchini humo bila kumtaja rais Donald Trump kwa jina.
Barrack Obama aliwataka wapiga kura kukataa kile alichokitaja kuwa siasa za kuwagawanya watu mbali na siasa za hofu.
Alikuwa akimfanyia kampeni mgombea wa chama cha Democrat anayewania wadhfa wa gavana wa jimbo la New Jersey.
Matamshi yake yanajiri saa chache baada ya mtangulizi wake George W. Bush kukosoa unyanyasaji na chuki katika maisha ya kawaida ya raia Marekani.
Katika hotuba, alisema chuki dhidi ya wale wanaokupinga zimeongezwa nguvu huku maadili ya kiraia yakisahaulika.
Bwana Trump ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa mtangulizi wake bado hajatoa tamko lolote.
Marais wa zamani nchini Marekani kwa kawaida huwa nadra kutoa maoni yao kuhusu hali ya kisiasa na ilionekana kuwa makosa makubwa kwa rais aliyetangulia kumkosoa mrithi wake katika ikulu ya Whitehouse.
lakini maadili na viwango vya tabia ambazo awali zilikuwa zikifuatwa sasa zimesahaulika katika mazingira ya kisiasa ya wakati huu.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni za chama cha Democrat , mjini New Jersy, Obama alisema kuwa Wamarekani wanapaswa kutuma ujumbe kwa ulimwengu kwamba tunakataa siasa za kugawanywa na siasa za hofu.
Aliongezea: Kile ambacho hatufai kuendelea nacho ni kuwa na siasa za zamani za kugawanyana ambazo zimekuwepo nyakati za wali.
Siasa tunazoziona sasa tulidhani zimepitwa na wakati, hiyo ni kurudi miaka 50 nyuma.Ni karne ya 21 sio 19. jamani!.

Korea Kaskazini yaionya Australia

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Serikali ya Australia imesema kuwa imepokea stakhabadhi kutoka Korea Kaskazini ikiitaka Canbera kutojihusisha na utawala wa rais Trump.
Barua hiyo imeshutumu onyo la Marekani kwamba itaiangamiza Korea Kaskazini iwapo italazimika kujilinda.
Waziri mkuu wa Australia PM Malcolm Turnbull amesema kuwa barua hiyo pia ilitumwa kwa mataifa mengine.
Amesema inaonyesha kuwa shinikizo za kidiplomasia dhidi ya Korea Kaskzini zimeanza kufanya kazi, licha ya barua hiyo kuwa na ufyozi na malalamishi ya kawaida ya taifa hilo.
Barua hiyo yenye ukurasa mmoja ilitumwa kupitia ubalozi wa Korea Kaskazini nchini Indonesia na inadaiwa kutoka kwa kamati ya maswala ya kigeni ya Korea Kaskazini.
Imezitaka serikali nyengine kujitenga na hatua zisizokuwa na heshima za rais Trump ikisisitiza kuwa Marekani inaweza kusababisha janga kubwa la kinyuklia.
Bwana Turnbull amesema kuwa Korea Kaskazini ndio inayosababisha wasiwasi kwa kutishia kuyashambulia mataifa ya Japan, Korea Kusini na Marekani kwa kutumia silaha za kinyuklia.
''Wametuma barua hizi kwa mataifa mengi , kama barua iliosambazwa'', alisema Bwana Turnbull kwa kituo kimoja cha redio 3AW.
Waziri wa maswala ya kigeni Julie Bishop aliitaja barua hiyo kuwa hatua isiokuwa ya kawaida ya Korea Kaskazini.
Baadaye bwana Turnbull alionekana kutojali umuhimu wake akiifananisha na ufyozi na malalamishi kuhusu Donald Trump unaotolewa na Korea Kaskazini.
Hatahivyo wote wanakubaliana kwamba huenda ni ishara kwamba shinikizo za kimataifa dhidi ya taifa hilo zimeanza kuzaa matunda na kuwa na matumaini kwamba kutakuwa na majadiliana ya kimataifa.
Siku ya Jumamosi Pyonyang iliionya Australia kwamba haitaweza kuzuia janga iwapo itashirikiana na sera za Marekani dhidi ya utawala wa Kim Jong Un.
Korea Kaskazini imekiuka makubaliano ya kimataifa katika miezi ya hivi karibuni kupitia kufanyia majaribio kombora lake la kinyuklia mbali na kurusha makombora mawili juu ya anga ya taifa la Japan.
Marekani imejibu kwa vitisho vya kijeshi , lakini waziri wa maswala ya kigeni wa Marekani Rex Tillerson anasisitiza kuwa bwana Trump yuko tayari kuutatua mgogoro huo kupitia diplomasia.