Wednesday, 18 October 2017

Audio | DJ Olu ft Davido, Mayorkun & Danagog – Bambiala | Mp3 Download

Audio | DJ Olu ft Davido, Mayorkun & Danagog – Bambiala | Mp3 Download

https://hearthis.at/baraka-matara-junior-vu/dj-olu-ft-davido-mayorkun-danagog-bambiala/download/

MAGAZETI YA LEO 18/10/2017













Mji Wa Raqqa Wa Syria Wakombolewa,,,,

Bendera ya wanamgambo wa kupambana na kundi la wanamgambo wenye msimamo mkali la I-S imekuwa ikipepea juu ya mji wa Raqqa, baada ya kuuweka mji huo wa Syria katika himaya yake baada ya mapambano ya nguvu ya miezi minne mfululizo.
Wanamgambo hao wenye asili ya Kurdi na Uarabuni wametoa tamko la kwamba sasa wanaudhibiti mji wa Raqqa, lakini wasaidizi wao Marekani wameonya kuwa wapiganaji hao wa Kiislam wanaokadiriwa kufikia mia moja wanaishi katika mji huo na kwamba Marekani imesema kwamba iko tayari kutoa usaidizi wowote utakao hitajika.
Tatizo lingine kubwa lililopo kwa sasa ni ukusanyaji na uondoaji wa mabomu yaliyosimikwa kwatika makazi ya watu na kwenye mji wote wa Raqqa.
Waangalizi wa masuala ya kimataifa wamearifu kuwa zaidi ya watu elfu tatu wameuawa katika kipindi cha mapambano ya kuukomboa mji huo, na miongoni mwao theluthi moja ni raia.

Nassari Awavimbia Takukuru......

MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (Chadema), amepinga onyo alilopewa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) la kutoweka hadharani taarifa anazowafikishia kuhusiana na flashi za tuhuma za rushwa na kusisitiza kuwa hataacha kufanya hivyo.
Akizungumza jana ikiwa muda mfupi baada ya kupata taarifa za onyo alilopewa na Takukuru, Nassari alisema haoni kama anavunja sheria kwa kuuarifu umma juu ya kila hatua anayoichukua kuhusiana na taarifa za rushwa anazozifikisha Takukuru.
Hivi karibuni, kwa nyakati tofauti, Nassari amekuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea anavyofikisha taarifa Takukuru kuhusiana na kile anachodai kuwa ushahidi juu ya tuhuma za rushwa za baadhi ya viongozi mkoani Arusha.
Jana, Takukuru kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake, Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola, ilitoa onyo lililotajwa kuwa la nne kwa mbunge huyo kuhusu mwenendo wake wa kuzungumza na vyombo vya habari juu ya tuhuma za rushwa anazowafikishia na kumtaka kukaa kimya wakati uchunguzi wa suala lake ukiendelea.
Nassari amekuwa akiwasilisha kwenye ofisi za Takukuru ‘flashi’ na CD zenye video anazodai zinaonyesha jinsi viongozi wa serikali jijini Arusha walivyokuwa wakiwashawishi kwa rushwa madiwani kadhaa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ili wahamie Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Siwezi kukaa kimya. Nitaendelea kuzungumza na vyombo vya habari… wananchi wana haki ya kupata taarifa,” alisema Nassari kuiambia Nipashe jana baada ya kusikia onyo alilopewa na Takukuru.
Katika hoja yake, Nassari alidai kuwa aliamua kuwasilisha ushahidi Takukuru kuthibitisha madai yake kwamba kuna madiwani wawili wa Chadema waliotangaza kujiunga na CCM hivi karibuni walishawishiwa kwa rushwa.
Nassari aliwasilisha kile alichodai kuwa ni ushahidi wa vitendo vya rushwa kwa mara ya kwanza Oktoba 2, 2017 akisindikizwa na wabunge wenzake wa Chadema, Peter Msigwa (Iringa Mjini) na Godless Lema (Arusha Mjini). Alienda tena Takukuru kuwasilisha ushahidi wake wa pili Oktoba 4, 2017 kabla ya juzi kuwasilisha ushahidi wake wa tatu.
ONYO LA TAKUKURU
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna Mlowola alisema wameshamwonya Nassari mara tatu juu ya kitendo chake cha kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kile kinachojiri wakati wa mazungumzo kati yao na mbunge huyo.
Mlowola alimtaka mbunge huyo kukaa kimya na ‘akome’ kuzungumzia suala hilo kwenye vyombo vya habari kwa sababu vinginevyo, anaweza anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Kamishna Mlowola alisema:
"Oktoba 2 mwaka huu, Nassari akiwa na wabunge wenzake Mchungaji Peter Msigwa na Godbless Lema, walikuja ofisini kwetu. Wakatoa taarifa zao na tukapokea… na tukawaambia hicho kilichowasilishwa tutafanyia kazi.
"Lakini kwa mshtuko baada ya kupokea taarifa, tukashangaa wanaongea na waandishi wa habari kuhusu kilichojiri wakati awali tuliwaambia tukio hili wasilifanye kisiasa. Na tuliwaonya wasiongee na waandishi.”
Mlowola alisema kuwa kwa mara nyingine, Oktoba 4, 2017, Nassari alifika tena Takukuru na kutoa maelezo kwao na alipotoka ofisini kwao, aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza yale yaliyojiri kwenye mazungumzo yao, licha ya ukweli kuwa awali walishamkanya aache kufanya hivyo.
Alisema Oktoba 16 (juzi), Nassari alifika tena katika ofisi za Takukuru kuwasilisha taarifa zingine na alipomaliza, alifanya kitendo kile kile cha kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza hatua ambazo zimeshanza kuchukuliwa, ijapokuwa alipewa angalizo kwa mara nyingin e la kutokufanya jambo hilo.
“Tunamwonya Nassari, ameshaleta taarifa kwetu na atuache tufanye kazi kwa mujibu wa sheria na siyo kutushinikiza,” alisema Kamishna Mlowola na kuongeza:
“Natoa onyo lingine… endapo ataendelea na tabia hii tutazingatia sheria na tutachukua sheria dhidi yake, bila kuathiri taarifa yake aliyotupa kuifanyia kazi."
Mlowola aliongeza kuwa Sheria ya Takukuru inawapa mamlaka ya kufanya kazi kwa uhuru bila ya shinikizo.
Alisema Takukuru inapokea taarifa zinazohusiana na rushwa au makosa ya rushwa kutoka vyanzo mbalimbali vikiwamo vya wazi na vya siri.
Alisema taarifa wanaipokea kutoka kwa mtu yeyote na anaweza kuwa mtakatifu, shetani, mwendawazimu au mwenye akili timamu, lakini hatua ya kwanza kwao inakuwa ni kupokea taarifa na mengine hufuata baadaye.
Alisema Takukuru inapopeleleza huwa inaangalia kama kuna kosa limetendwa na kufikishwa katika chombo kingine kilichotengwa ambacho ni mahakama kupitia kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
“Hatukutarajia kuwa na drama (maigizo) na watu wanapaswa kufahamu kuwa Nassari ameleta taarifa na siyo ushahidi… ushahidi una sifa zake,” alisema Kamishna Mlowola.
Alibainisha kuwa kifungu cha 37 cha makosa ya rushwa, kinaeleza kuhusu makosa ya jinai yanayoweza kutendwa na mtoa taarifa.
Alisema Nassari alikuwa ni mtoa taarifa na Takukuru ina wajibu wa kumlinda mtoa taarifa na kwamba kinyume chake, Nassari amejionyesha mwenyewe katika vyombo vya habari kuwa ndiye aliyewapatia taarifa.
“Tunachokiona sisi hapo, Nassari na wenzake wanataka kulifanya suala hili kama la kisiasa badala ya sheria. Tuzingatie sheria. Chombo chenye mamlaka tukiache kifanye kazi yake,” alisema Kamishna Mlowola.
Alisema kuihusisha Takukuru katika malumbano na ulingo wa kisiasa si vizuri kwa kuwa jukumu la Takukuru siyo kufanya siasa.
Alisema uchunguzi unaweza kuonyesha kilichotokea katika tukio hilo ni kosa au siyo kosa kwa kuwa inawezekana kuna makosa yanafanyika mtu akadhani ni ya jinai, kumbe ni makosa ya kawaida ambayo yanahitaji utaratibu mwingine wa kuyashughulikia.

Mtambo Wa kuchomea taka unavyohatarisha afya za wananchi Mkuranga,,,

Wakazi wa kijiji cha Dundani wilayani Mkuranga wako katika hatari ya kupata magonjwa yanayosababishwa na moshi mzito unaozalishwa na mtambo mkubwa wa kuchoma takataka za hospitali ulio jirani na makazi yao.
Uchunguzi wa Mwananchi umegundua kuwa mtambo huo mkubwa kuliko yote nchini kwa kazi hiyo ulijengwa kabla ya kufanyika kwa tathmini ya athari ya mazingira (EIA) na sasa umegeuka kero kwa wakazi hao. Mbali na uchomaji wa taka za hospitali, tanuru hilo linaloendeshwa na kampuni ya Safe Waste Incinerator linatumika pia kuchomea dawa zilizoisha muda wa matumizi na zile zinazogundulika kuwa si halisi (feki).
Kutokana na hali hiyo, wakazi wa Dundani wameziomba mamlaka zinazohusika kuingilia kati ili kunusuru afya zao na mazingira.
Kabla ya kiwanda hicho kuanza kuteketeza kiwango kikubwa cha taka hizo hakuna mkazi aliyehisi hatari iliyokuwa mbele, lakini sasa uteketezaji wa kiwango kikubwa umewafanya wakasirishwe.
Wakati mwekezaji huyo akijenga mtambo huo kati ya mwaka 2013 na 2014 hakukuwa na wakazi eneo hilo, lakini kwa sasa mtambo huo umezungukwa na makazi ya watu ambao sasa wanataka ama uhamishwe au zibuniwe mbinu mpya za kudhibiti moshi na harufu kali.
Kadhia hiyo imewaweka viongozi wa kisiasa na maofisa afya wilayani Mkuranga katika wakati mgumu kutokana na lawama za wananchi.
Malalamiko kila kona
“Hatujui hizi takataka ni kabila (aina) gani kwa sababu hatushirikishiwi na wala hajafika mwenye kiwanda kutuambia anachoma kitu gani,” alisema Mbarka Salumu mkazi wa Dundani.
“Ile harufu tunayoisikia ukisema ni mtu anachomwa ni sawa tu! Ukisema wadudu wanachomwa sawa! Na ukisema sumu inachomwa sawa tu kwa sababu ni harufu chafu kabisa.” Kwa mujibu wa Salumu, mtambo huo unapowashwa, moshi husambaa na kuingia mpaka ndani ya nyumba zao. “Tunataka tusaidiwe ili hii kero itutoke, ifike wakati huyu bwana atolewe sehemu hii ili tusidhurike,” anaongeza.
Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) linasema halijapokea taarifa rasmi kuhusu kero hiyo. “Hili tatizo tumelisikia juzi tu na ndio tunakwenda kukagua. Ni mpaka tutakapofika na kuona hali halisi ndipo nitakapokuwa katika nafasi ya kulizungumzia hili zaidi,” alisema ofisa wa NEMC, Alfred Msokwa.
Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga ilimpa kibali mwekezaji kujenga mtambo huo, ambao hauwashwi kila siku kabla ya kufanyika kwa tathmini ya athari za mazingira. “Halmashauri zetu wakati mwingine huruhusu kujengwa kwa mitambo kama hii zikilenga kuongeza mapato na kusahau suala la mazingira na afya za watu. Wakati mwingine vibali vinatolewa katika ngazi ya halmashauri, halafu wanashindwa kuwasimamia,” alisema. Ofisa mmoja wa kampuni inayolalamikiwa aliyeomba kutotajwa jina, alisema wamepata malalamiko hayo kupitia vyombo vya habari, akisema ni “changamoto za kawaida katika biashara”.
“Tumepigiwa simu na watu kadhaa kutoka Mkuranga wakitaka tu-surrender documents (tusalimishe nyaraka). Tumewaandikia kutafuta muda mwafaka ili tukae na mamlaka zote husika na kuwajibu wanayoyataka kwetu kwa pamoja,” alisema ofisa huyo. Mkazi mwingine wa Dundani, Saidi Hamisi, alisema haelewi kinachochomwa.
“Ni kama (harufu) ya dawa za hospitali. Na watu ukiwauliza wengine wanasema zinachomwa simu za zamani, wengine wanasema dawa za hospitali zinazotoka Bohari Kuu, sasa hatuelewi ni kitu gani,” alisema. “Moshi ni mzito sana na harufu inayokuja inakuwa ya mchangayiko, sasa kwa kuwa lile bomba halijaenda juu sana ule moshi unaishia kusambaa chini.
“Kipindi alivyonunua huku palikuwa bado pori, kwa ushauri wangu kwa sababu huku mji umeshaingia basi hiki kiwanda kihamishwe au bomba liende hewani ili ule moshi unapotoka sisi tusiathirike.”
Kero ya moshi mzito na harufu kali imelalamikiwa pia na wanawake wakiwemo wajawazito.
“Harufu kama hii inatuumiza sana sisi wajawazito, tunaumia, tunaombwa tusaidiwe,” alilalamika mwanamke mjazito aliyeomba kutotajwa jina. Malalamiko ya mjamzito huyo yaliakisiwa pia na Rajma Saidi.
“Mtu unaweza kupika chakula na usikile kwa sababu harufu inayotoka huko ni mbaya kupita kiasi kwa hiyo tunakereka sana. Tunashukuru umefika ukatoe salamu huku hali si nzuri,” alisema Rajma
Ofisa msaidizi wa afya wilayani Mkuranga, Juma Shari alisema wamefuatilia malalamiko na kuthibitisha kuwa ni ya kweli.
“Kiwanda kipo kwa chini na maeneo ya makazi yako juu. Kwa hiyo katika uchomaji wao, moshi husambaa kwa urahisi zaidi kwenye eneo la makazi,” alisema Shari.

AUDIO | Sharpa tz Ft Brown Punch_hawa watu | Download

https://hearthis.at/djmwanga/sharpa-tz-ft-brown-punch-hawa-watu/download/

Audio | Nollady _ Hustle | MP3 Download





Bovya hapa ==> ku Download,,,,,

https://my.notjustok.com/track/download/id/281776/by/y5oWOhI88mwwww

Tuesday, 17 October 2017

AUDIO | Otile Brown _ Mapenzi Hisia | Download

Audio | Otile Brown _ Mapenzi Hisia | Download

Bovya link hii ku download ==>

https://my.notjustok.com/track/download/id/281711/by/JQbc9b8il~

Serikali imesema ufugaji kuku, samaki ni Uchumi Wa Viwanda

Naibu Waziri wa Mifugo na Kilimo, Abdallah Ulega akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mwandege wakati wa kuhitimisha ziara yake iliyokuwa ya siku mbili.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, amesema serikali ya Viwanda inakwenda na ufugaji Kuku pamoja na samaki kwa kutengeneza Viwanda vya Kuku pamoja na mabwawa ya ufugaji samaki.
Ulega aliyasema nayo wakati wa ziara yake aliyoifanya Wilaya ya Mkuranga-Pwani kwenye vijiji Vinne ,ambapo alisema hakuna sababu ya wananchi wa Mkuranga kuchukua Kuku mikoa mingine wakati wanaweza kufuga wenyewe na kujipatia kipato na maendeleo yakapatikana na kuwawezesha kuuza hata sehem nyingine.
Amesema yuko tayari kuwasaidia wananchi wa Mkuranga mbegu za Kuku pamoja na watalaam wa kuwafundisha jinsi ya kufanya ufugaji wa Kuku na samaki wa kisasa.
Amesema ajira katika Wilaya hiyo zipo ikiwa ni pamoja na ufugaji Kuku pamoja na samaki ambayo ni ajira ya kudumu na soko ni kubwa kutokana mahitaji ya vitoweo hivyo kuhitajika kwa wingi.
"Sioni sababu wananchi wa Mkuranga kuchukua kuku kutoka mikoa mingine wakati mnaweza kufanya nyinyi wenyewe kutokana na maeneo mlionayo, haitawezekana kama nyinyi hamtaweza kuonyesha mfano nikiwa ni Mbunge na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi"alisema Ulega.
Katika ziara yake alitembelea Ujenzi wa Zahanati za Kibamba, Kimazichana na Mwandege na kuahidi kuwaunga mkono wananchi katika juhudi mbalimbali wanazoonyesha katika maendeleo ya huduma za jamii.
Ulega amesema kuwa wakati uliopo ni kufanya kazi za Maendeleo kwa kuunga mkono jitihada za Rais Dk. John Pombe Magufuli juu ya dhamira ya serikali ya Viwanda.
 Naibu waziri aliaahidi kuchagiaji sh. Milioni moja na mifuko ya saruji kwa ajili ya kikundi cha VICCOBA cha wanawake waliojenga ukumbi wa mikutano na sherehe kilichopo Mwandege.

Lissu atoka ICU aona jua kwa mara ya kwanza tangu apigwe risasi

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ametoka ICU na sasa anaweza kukaa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumanne, Mbowe amesema afya ya Lissu inaimarika kwa kuwa alihitaji upasuaji mwingi sana kutokana na risasi zilizoingia kwenye mwili wake.
“Amefanyiwa upasuaji mkubwa mara 17 mpaka sasa. Ameongezewa damu nyingi kuliko mtu yeyote miaka 20 iliyopita ametoka ICU wiki iliyopita,” amesema Mbowe.
Amesema Lissu hatumii oxygen tena wala mirija na kwamba anakula chakula anachokitaka.
“Juzi kwa mara ya kwanza alikaa, anatembea Wheel Chair na aliliona jua kwa mara ya kwanza,” amesema Mbowe.
“Tunawashukuru madaktari wa Dodoma na Nairobi. Hospitali ya Nairobi imefikisha awamu ya pili ya kutibu. Tunavyozungumza baada ya wiki moja kadri madaktari watakavyoshauri atamaliza matibabu ya pili,”
“Ataanza awamu ya tatu nje ya Nairobi yatakayokuwa ya muda mrefu. Kwa usalama wake hatutataja wapi anakwenda. Siyo Tanzania na sio jirani. Hiyo ndio hali halisi ya mgonjwa.”

Wachezaji Wa Yanga waliokuwa wamebaki Dar waongeza nguvu tabora,,,,

Klabu ya soka ya Yanga itaungana na wachezaji wake waliokuwa wamebaki jijini Dar es salaam wakati timu imesafiri kwenda mkoani Kagera kucheza na Kagera Sugar wikiendi iliyopita.
Yanga tayari imeshatoka Kagera na kutua mkoani Tabora ikijiwinda na mchezo wake wa ligi kuu raundi ya 7 dhidi ya Stand United utakaopigwa wikiendi ijayo mjini Shinyanga.
Meneja wa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu Tanzania bara Hafidh Saleh amewataja wachezaji hao kuwa ni Juma Mahadhi, Pato Ngonyani, Ramadhan Kabwili, Abdallah Hajji, Juma Mahadhi na Saidi Mussa.
Aidha meneja Saleh amesema kuwa wachezaji waliokuwa majeruhi ambao ni Donald Ngoma, Thabani Kamusoko na Amisi Tambwe wataendelea na mapumziko hadi timu itakaporejea jijini Dar es salaam.
Kesho Yanga inatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora kwenye uwanja wa Al Hassan Mwinyi kabla ya kuelekea mjini Shinyanga kucheza na Stand United

Wakenya wawachangia damu waadhirika Wa mabomu Somalia,,,,

Mamia ya Wakenya pamoja na raia wa Somalia wanaoishi nchini humo walishiriki katika shughuli ya kutoa damu ili kuwasaidi wale waliojeruhiwa katika mlipuko wa bomu nchini Somalia uliowaua takriban watu 276.
Kampeni hiyo ya kutoa damu ilizinduliwa kupitia mitandao ya kijamii katika eneo la Eastleigh mjini Nairobi kufuatia bomu hilo.
Tayari takriban miili 165 isiotambulika imezikwa katika kaburi la pamoja mjini Mogadishu.
Chombo cha habari cha serikali kinasema kuwa ni watu 111 waliotambuliwa.
Baadhi ya waliojeruhiwa walisafirishwa hadi nchini Uturuki kwa matibabu zaidi kulingana na mpiga picha mmoja wa chombo cha habari cha AFP.
Hatua hiyo inajiri kufuatia ombi la serikali ya Somalia kuomba msaada wa damu .
Waziri wa habari nchini Somalia aliambia BBC kwamba idadi ya watu waliofariki huenda ikaongezeka na kwamba usaidizi zaidi ulihitajika.
Alisema kuwa zaidi ya watu 300 walijeruhiwa nchini Somalia kufuatia shambulio hilo ambalo limetajwa kuwa kubwa zaidi katika kipindi cha miaka 10 huku miili kadhaa ikidaiwa kufinikwa chini ya vifusi.
Ndege mbili kutoka Marekani na Qatar zimewasili mji Mogadishu.
Serikali ya Kenya imesema kuwa itatuma tani 31 za dawa mjini Mogadishu mbali na kuwasafarisha baadhi ya waathiriwa wa mlipuko huo hadi Nairobi kwa matibabu zaidi.
Serikali ya Djibout nayo tayari imetuma madaktari 30 nchini Somalia wakiongozwa na waziri wa afya nchini humo ili kutoa msaada wa dharura.
Mlipuko huo wa Jumamosi ulilenga eneo lenye watu wengi na kuwaua raia wakiwemo madaktari na wanafunzi.
Hakuna kundi ambalo limekiri kuhusika lakini serikali ya Somalia inalaumu kundi la wapiganaji wa al-Shabab.
Shghuli ya kuchangisha damu pia inaendelea nchini Somalia ambapo maafisa wa Jeshi la AMISOM wanatoa damu.

Meya wa Kinondoni atoa sababu 3 za kusaini mkataba na CRJE

Meya wa manispaa ya Kinondoni Benjamin Samweli Sita leo amesaini mkataba wa ujenzi wa kiwanda cha kuchakata takataka na kuwa mbolea kitakachojengwa na kampuni ya CRJE ambapo ujenzi huo unatarajia kuanza kesho.
Meya Sita amewaeleza waandishi wa habari kuwa sababu ya kusaini mkaba huo ni kwamba mbolea aina ya mboji itakayozalishwa na kampuni hiyo haitaharibu udongo kwani tofauti na njia ambayo imezoeleka ya Chemical Fertilizer ambayo inaharibu udongo kwa kiasi kikubwa.
Pia amesema kujengwa kwa kiwanda hicho kitaongeza ajira kwa wananchi pia kitawasaidia wakulima kutumia mbolea ambayo ni bora na ya kisasa huku ikiwa haina athari kwa udongo na hata mazao.
Aidha kupitia mkataba huo manispaa ya Kinondoni itakuwa imeunga mkono kiasi kikubwa jitihada za Rais Magufuli katika kuelekea Tanzania ya viwanda, hivyo wananchi watapata ajira mbalimbali za kutoka kiwanda hicho.