Tuesday 12 December 2017

Waziri Jafo ampa wiki sita Mkandarasi wa mradi wa maji Muheza



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Selemani Jafo amempa wiki sita Mkandarasi wa mradi wa maji wa Kivindo Wilayani Muheza mkoani Tanga, kuhakikisha anakamilisha mradi huo na uanze kutoa huduma.

Waziri Jafo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo wilayani Muheza,  ambapo alikagua miradi katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo ukiwemo mradi huo wa maji.

“Sitegemei kusikia sababu zozote zitakazofanya mradi huu usikamilike ndani ya wiki sita, ni mategemeo yangu wananchi wataanza kufaidi matunda ya mradi huu baada ya muda mfupi tu kuanzia sasa, Mkandarasi fanya kazi yako” amesema Jafo.

Aidha Waziri Jafo alimtaka Mkandarasi wa Mradi huo ambao umefikia asilimia 90 ya utekelezaji wake kuwaahidi wananchi kuwa ataukamilisha ndani ya muda wa wiki sita ambao amepewa na waziri.

Mbali na mradi huo wa maji wa Kivindo pia Waziri Jafo amefanikiwa kutembelea Miradi ya afya na
 elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu.

elimu katika kituo cha afya Mkuzi na Ubwari pamoja na kutembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Msingi Kilulu.

No comments:

Post a Comment