Saturday 16 December 2017

maji maji yaibomoa ngome ya lipuli FC


Klabu ya Majimaji imefanikiwa kuipata saini ya mshambuliaji Waziri Ramadhan kutoka Lipuli FC kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Meneja Mkuu wa Majimaji, Geofrey Mvula alisema kwa mujibu wa Kocha Mkuu wa timu hiyo Peter Mhina alihitaji kufanya usajili wa mshambuliaji pekee ili kukiongezea nguvu kikosi hicho.
"Tumefunga usajili kwa mchezaji huyo pekee na hawa wengine tutaendelea nao kwani tumeona wako vizuri.”
Mvula alisema Ramadhan amefanyiwa uhamisho kutoka Lipuli lakini alikuwa na mkataba na wanapaluhengo nao.

No comments:

Post a Comment