
Wakulima wa Kata ya Kiberege Wilayani Kilombero mkoani Morogoro, wamejikuta katika wakati mgumu, baada ya mazao yao kuvamiwa na panya waharibifu, na kusababisha uharibifu mkubwa katika mazao ya mpunga na mahindi ambayo wameyapanda katika msimu huu.
Wakulima wa kata hiyo wamesema tatizo hilo limeanza kwa muda mrefu, na cha kushangaza licha ya mvua kunyesha bado panya hao wameendelea na uharibifu, hali ambayo inawapa mashaka juu ya hali ya chakula itakavyokuwa msimu huu.
Aidha wakulima hao kutoka katika vijiji vya Nyamwezi na Misufini, wamedai ndiyo mara ya kwanza kuwanaona panya hao wakiharibu mazao yao.
Naye Afisa Kilimo wa Kata ya Kiberege amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na ameeleza kuwa Serikali ya Wilaya hiyo imeanza kuchukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha inakabiliana na tatizo hilo.

Hitilafu ya mfumo wa umeme imetajwa kuwa chanzo kikuu cha ajali ya ndege ambayo ilisababisha vifo vya watu wawili juzi visiwani Zanzibar.
KUFUATIA skendo nzito inayofukuta ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kudaiwa kutoka kimapenzi na warembo, Wema Isaac Sepetu na Tunda Sebastian, mama mzazi wa mwanamitindo Hamisa Mobeto, Shufaa Lutigunga ‘amemtapika’ jamaa huyo kuwa vitu vyote vinavyoendelea kwenye mitandao ya kijamii havihusiani na mwanaye.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wanaosimamia usajili wa wananchi kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho wa Taifa kuwa makini.
Asasi za kiraia zimetakiwa kufuata taratibu kabla ya kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi ili kukwepa udanganyifu, ikiwa ni pamoja na kuwachangisha fedha na kutokomea kusikujulikana.
Mlinda mlango namba mbili wa Simba, Said Mohammed 'Nduda' wiki ijayo anatarajia kujiunga na wenzake tayari kuanza mazoezi baada ya kuwa nje kwa miezi mitano, kufuatia kufanyiwa upasuaji wa goti Oktoba mwaka jana nchini India.
Mbunge mwingine nchini Kenya, amekamatwa kuhusiana na mzozo unaozunguka kujiapisha kwa aliyekuwa waziri mkuu Raia Odinga kwa kile anachokitaja kama rais wa watu wa Kenya.
Msanii Radio wa nchini Uganda ambaye alifariki Februari 1, amezikwa leo kijijini kwao Nakawuka nchini Uganda, na kuhdhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali za nchi hiyo na wasanii wa nchi jirani.




Serikali mkoani Lindi imeunda timu ya kuchunguza matukio ya baadhi ya wakulima kuchanganya mchanga na korosho kwa nia ya kuongeza uzito wakati wa kupima kwenye mizani, ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika kufanya hhujuma hiyo.
Rais wa Marekani Donald Trump amewapigia simu viongozi wa Japan na Korea Kusini siku chache kabla ya michezo ya Olimpiki kuanza nchini Korea Kusini.