Thursday, 18 January 2018

Mashindano ya elimu kuanza kutimua vumbi Februari 28



Katika kuonesha kwamba wanaunga mkono suala la elimu bora nchini Taasisi ya Teacher's Junction imeandaa mashindano kwa shule za binafsi nchini ambapo wanafunzi wa darasa la nne, sita la saba watafanya mitihani ya kujipima nguvu lengo likiwa ni kuongeza ufanisi baina ya wanafunzi hao na pia kuwarahisishia walimu kujua wapi wanapaswa kuongeza nguvu.

Mashindano hayo yamepangwa kufanyika kuanzia Februari 28 hadi Machi 1 na kushirikisha takribani shule 120 nchini.

Akizungumza na wandishi wa habari leo, Afisa Mradi wa taasisi hiyo, Njama Salum alisema walianzisha mradi huo ili kuongeza kiwango cha elimu nchini kwa wanafunzi wa shule za msingi lakini pia wakiwa na mpango wa kupeleka mradi huo hadi kwenye shule za Sekondari.

" Kiu ya taasisi yetu ni kuona kiwango cha elimu kinaongezeka nchini, hivyo kwa kushirikiana na wadau wa elimu hasa wamiliki wa shule tukaja na wazo hili la kufanya mashindano ambayo tunaamini yanawajenga wanafunzi kuanzia kiakili hadi kujiamini pale wanapofanya mitihani ya Kitaifa.

" Kikubwa tunatoa zawadi za medali kwa wanafunzi wanaofanya vizuri lakini shule ambazo zitafanya vizuri tunatoa zawadi za ngao. Na mitihani hii hufanyika mara tatu kwa mwaka ambapo kwa kuanzia tunaanza mwezi Machi kisha tutafanya mwingine Mei halafu Agosti tutafanya mwingine," alisema Njama.

Alisema tayari washapata zawadi lakini bado anatoa fursa kwa wadau wengine wa elimu kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono ili kuweza kuzalisha kizazi bora cha vijana wenye elimu ambao watakuja kuwa msaada mkubwa kwa Taifa hapo baadaye.

Akizungumzia sababu za kutohusisha Shule za Serikali, Njama alisema sio kwamba wamezitenga shule hizo lakini wao kama taasisi waliangalia ni wapi wanaweza kupenyeza wazo lao kwa haraka zaidi na kwamba taratibu za kuonana na viongozi wa kiserikali ili kuangalia uwezekano wa kupeleka mradi huo kwenye shule hizo unafanikiwa kusudi kila mwanafunzi nchini aweze kunufaika nao.

Kwa upande mwingine Njama alisema taasisi yake pia imekuwa ikisaidia walimu ambao wapo mitaani bila ajira kwa kuwatafutia kazi kwenye shule za binafsi ambazo wana ushirika nazo lengo likiwa ni kumaliza tatizo la ajira nchini.

" Sisi pia tunasaidia vijana wenzetu ambao wana taaluma ya ualimu ambao wapo mitaani ambapo kwa mwaka uliopita zaidi ya vijana 356 ambao wana taaluma ya ualimu tuliwatafutia kazi katika shule mbalimbali nchini," alisema Njama.

Mwanamke mjamzito atolewa kopo la mafuta sehemu za siri



Veronica Paschal (29) mkazi wa Kishili jijini Mwanza ametolewa kopo la mafuta ya kujipaka mwilini katika sehemu za siri, ikiwa ni muda mfupi baada ya kuwaeleza ndugu zake kuwa anataka kujifungua kopo.

Licha ya kutolewa kopo hilo, daktari aliyekuwa zamu katika kituo cha afya Igoma jijini hapa, Zaitun Lionge amelieleza Mwananchi leo Januari 18, 2018 kuwa mimba ya miezi sita ya mwanamke huyo ipo salama.

Tukio hilo la aina yake limetokea jana Januari 17, 2018 baada ya Veronica kufikishwa katika kituo hicho cha afya na ndugu zake waliomtoa kwenye zahanati binafsi.

“Mwanzoni hawakuonyesha ushirikiano ndio tukawambia tutafanyaje. Wakasema kuna kopo kwamba ndugu yao anataka kujifungua kopo, tukauliza kopo linazaliwaje? Amehoji na kuongeza,

“Tukawambia hilo kopo halijaingia lenyewe mtakuwa mmeliweka wenyewe. Kopo lilikuwa halionekani lakini anavyojaribu kusukuma likatokezea.”

Amesema walipomchunguza kwenye vipimo ndipo walipolibaini kopo hilo la mafuta ya kujipaka mwilini, kwamba baada ya kulitoa waliita Polisi kuchukua maelezo ya mhusika na ndugu zake.

Amesema ujauzito wa mwanamke huyo uko salama kutokana na njia kutofunguka baada ya kuondolewa kopo hilo.

Bunge lahoji mkataba wa UDSM na Kampuni ya Mlimani Holding



Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeutaka uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kurekebisha mkataba kati yake na kampuni ya Mlimani Holding Ltd kutokana na upungufu uliojitokeza, huku ikihoji sababu ya mwekezaji huyo kuja na mtaji wa Sh150,000 tu.

Wakizungumza katika kikao cha kamati hiyo kilichoketi eneo la Mlimani City jijinj Dar es Salaam leo Januari 18 wajumbe wa PAC walikosoa pia gawio la asilimia 10 la mapato yote kwa mwaka ambapo Mlimani  City wamekuwa wakikata gharama zao kabla ya kulipa.

Jambo la tatu lililolalamikiwa ni umri wa mkataba ambapo UDSM imetaka upunguzwe kutoka miaka 50 hadi miaka 35.

Mbunge wa Magomeni (CCM) Zanzibar, Jamal Kassim amehoji sababu za chuo hicho kumpokea mwekezaji akiwa na mtaji wa Sh150,000.

"Ukisoma mkataba huu utaona mtaji wa mwekezaji ni Sh150,000 yaani Dola 75. Maana yake mwekezaji hakuja na pesa bali alichukua pesa za upangishaji na kuzifanya kuwa mkopo na anajilipa riba ya mabilioni ya fedha," amesema Kassim.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Naghenjwa Kaboyoka amehoji: "Je, Chuo kikuu cha Dar es Salaam kilimkubalije mwekezaji mwenye mtaji wa Dola 75 tu? Dhamana ilikuwa nini?"

Hoja hiyo ilimwibua Mbunge wa CCM (Vijana)  , Khadija Naasir akihoji sababu ya mwekezaji huyo kutuma barua pepe kila anapotakiwa kutoa maelezo na UDSM.

Mbunge wa Ulanga Magharibi Dk Haji Mponda amesema mkataba huo ni mbovu kwa sababu umeshindwa kuna ardhi iliyopangishwa bila kutumika kwa muda mrefu.

Baada ya hoja za wabunge hao, Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Hilal Aeshi ameitaka kamati kuwaita watumishi wa UDSM walioshiriki kusaini mkataba huo ili wahojiwe na kuchukulia hatua.

"Kwa kuwa waliotia saini mkataba huo wapo, tuwaite Dodoma, wajieleze ili wachukuliwe hatua na Rais. Mimi nilikuwa mjumbe wa kamati ya madini ya Spika, tuliwaita waliohusika wakajieleza," amesema Aeshi.

Hata hivyo baadhi ya wabunge walitaka viongozi wa sasa wa UDSM  wajieleze kabla ya kuwaita wa zamani.

Tofauti na mtazamo wa wabunge hao, Naibu Makamu mkuu wa chuo hicho anayeshughulikia utawala, Profesa David Mfinanga amekiri kuwa mkataba huo una mapungufu na kwamba wana mgogoro na Mlimani Holding.

Mwanasheria wa Chuo hicho, Profesa Bonaventure Rutinwa amesema tangu alipoteuliwa alianza kuupitia mkataba huo.

"Tangu nilipoteuliwa mwaka jana nilifika ofisini kwa Profesa Rwekaza Mukandala nikamuomba vipaumbele vitano vya kisheria, mojawapo akaniambia ni kuupitia mkataba wa Mlimani," amesema Profesa Rutinwa.

Akifafanua zaidi, Kaimu Katibu wa Baraza la Chuo hicho, Dr Saudin Mwakaje alikiri kuwepo tatizo la mtaji na kwamba walishaiambia kamati hiyo.

Awali Mkurugenzi wa mipango na maendeleo wa chuo hicho, Pancras Pujuru amesema Mlimani Holding iliingia mkataba huo mwaka 2004 ukiwa katika sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza ulihusu kati yake na UDSM na sehemu ya pili ilikuwa kati yake na Serikali kupitia kituo cha

Mkali wa tennis Uingereza atupwa nje ya michuano



Mchezaji tennis namba moja kwa viwango vya ubora nchini Uingereza mwanadada, Johanna Konta ameondolewa kwenyemichuano ya Australia Open baada ya kufungwa na mchezaji anaeshikilia nafasi 123 duniani, Bernarda Pera.

Mmarekani, Bernarda Pera amemshinda Konta kwa jumla ya seti 6-4 7-5 katika kipindi cha pili cha mchezo.

Mara baada ya kutolewa katika mashindano hayo Konta amesema “Ni jambo la kusisimua lakini tunaendelea vizuri na benchi langu la ufundi, siji sikii vizuri lakini kwa namna yoyote lazima nikubali matokeo,”Konta.

Konta ameongeza “Nimecheza kila namna mpaka kufikia pale kwa hakika sikuhitaji rejea nyumbani mapema.”

Video | Korede Bello – Melanin Popping | Mp4 Download

Video | Korede Bello – Melanin Popping | Mp4 Download
Video | Korede Bello – Melanin Popping | Mp4 Download



Audio | Korede Bello – Melanin Popping | Mp3 Download

Audio | Korede Bello – Melanin Popping | Mp3 Download
Audio | Korede Bello – Melanin Popping | Mp3 Download


Audio | Belrino Ft Nana – Si Umesema | Mp3 Download

Audio | Belrino Ft Nana – Si Umesema | Mp3 Download

Audio | Belrino Ft Nana – Si Umesema | Mp3 Download

DOWNLOAD

Waziri Mkuu amewaasa Wanaume wa Wilaya ya Tarime


Tarime.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaasa wanaume wa wilaya ya Tarime kujiepusha na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuachana na kilimo cha bangi.

Ametoa  kauli hiyo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Waziri Mkuu amesema  vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kilimo cha bangi vinaitia doa wilaya hiyo, hivyo hawana budi wakaepukana navyo.

“Serikali inakemea vitendo vya ukatili, achaneni navyo. Mtu unamchapa mtoto makofi hadi anazimia, kitendo hicho hakiwezi kuvumilika na pia kinaitia doa wilaya yenu.”

Wakati Huohuo, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa wilaya hiyo, Glorious Luoga kuendelea na msako wa mashamba ya bangi na mirungi na kuchukua hatua kwa watakaobainika kuendesha kilimo hicho.

Amesema ardhi ya wilaya hiyo ni nzuri na inahimili kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na biashara kama mahindi, mihogo, ndizi, kahawa, pamba, ni marufuku kulima bangi.

Pia Waziri Mkuu ameagiza kuchukuliwa hatua kwa wakandarasi waliotekeleza ujenzi wa maji mkoani Mara kwa sababu miradi hiyo wameijenga chini ya kiwango.

Waziri Mkuu amesema hayo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kupitia mabango wakidai kutonufaika na miradi ya maji katika maeneo yao licha ya Serikali kutoa fedha.



Mambosasa akanusha Polisi kuzuia Wanawake kuvaa nguo fupi




Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,  Lazaro Mambosasa amekanusha kutoa tamko la kuzuia wanawake kuvaa nguo fupi zisizo na heshima kwa maelezo kuwa  jambo hilo ni la kimaadili siyo sheria.

Amesema Jeshi la Polisi lina kazi ya kushughulikia makosa ya kisheria na si maadili.

Mambosasa ametoa kauli hiyo leo Januari 18, 2018 wakati akihojiwa katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Redio Clouds, ikiwa ni siku mbili baada ya kunukuriwa katika mkutano wake na wanahabari kuwa amezuia uvaaji wa nguo fupi jijini Dar es Salaam.

 “Niliwaeleza wazi kuwa suala la mavazi bado halijatungiwa sheria hivyo polisi hatuhusiki nalo mtu anayevaa kimini katika maeneo kama kanisani au msikitini  ni ukiukwaji wa maadili,” amesema na kuongeza,

“Niliwaeleza  kuwa katika nyumba hizo za ibada kuna kamati ya ulinzi na usalama za eneo husika wao watakushughulikia lakini si polisi.”

Amesisitiza, “Nilikwenda mbali zaidi na kuwaeleza kuwa hivyo vimini kuna mahali vinahitajika kama ufukweni, sehemu za starehe. Ikitokea mtu amepigwa, amedhalilishwa au amekamatwa na askari kwa kuwa amevaa kimini ana haki ya kulalamika kuwa ameshambuliwa.”

NHIF yakanusha taarifa hii

Waziri Mkuu atoa agizo kwa Mghwira kusitisha uuzwaji wa mali za KNCU



Tarime. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro  Anna Mghwira asitishe uuzwaji wa mali za Chama cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Januari 17, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Serengeti, wilayani Tarime.

Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL  kutimiza sharti la mtaji la Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Benki hiyo ya KCBL inatakiwa kutimiza sharti la kuwa na mtaji kamili unaotosha wa shilingi bilioni  tano (5) katika kipindi cha miezi sita tangu kutolewa kwa tangazo hilo.

Waziri Mkuu amesema  ni marufuku kuuza mali za Ushirika huo, hususan katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya uhakiki wa mali za vyama mbalimbali vya Ushirika nchini.

Amesema Serikali imedhamiria kuimarisha Ushirika nchini na sasa inafanya uhakiki wa mali za vyama vya Ushirika na watakaobainika kuhusika na ubadhilifu watachukuliwa hatua.

Januari 4, 2018 BoT ilizipa miezi sita benki tatu ili ziweze kuongeza kiwango cha mtaji unaohitajika kutokana na matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili wa kutosha.

Benki hizo ni Kilimanjaro Co-Operative Bank Limited, Tanzania Women Banki Plc na Tandahimba Community Bank Limited, zitakaposhindwa kutekeleza agizo zitachukuliwa hatua.

BoT ni itazifutia leseni na kusimamisha shughuli za kibenki chini ya ufilisi, iwapo benki hizo zitashindwa kutekeleza agizo hilo hadi kufikia Juni 30, 2018.


Katibu UVCCM Iringa afunguka alivyonusurika kufa


KATIBU wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM), Alophance Myunga amenusurika kifo baada ya kitu chenye mlipuko kurushwa dirishani kwake na kufikia kitandani huku yeye akiwa amelala na kisha kusababisha moto ulioteketeza nyumba anayoishi yote.

Amesema kutokana na kurushwa kwa kitu hicho ambacho kilisababisha mlipuko mkubwa chumbani kwake na kisha moto kuanza kuwaka alichofanikiwa ni kuchukua simu yake ya mkononi tu huku vitu vingine vyote vikiteketea kwa moto.

 Myunga amesema yeye ni moja kati ya wapangaji saba wanaoishi kwenye nyumba ambayo wanaishi na chumba ambacho kilianza kuwaka moto ni cha kwake.

Katibu huyo wa UVCCM Wilaya ya Iringa amesema kuwa kwenye mida ya saa saba usiku akiwa amelala chumbani kwake alisikia dirisha lililopo chumbani kwake likivunjwa.Hata hivyo aliogopa kuchungulia kwani hakujua wanaofanya hivyo wanalengo gani dhidi yake.

Ameongeza wakati anaendelea kutafakari huku akiwa bado yupo kwenye kitanda chake alishangaa kuona amerushiwa kitu ambacho hawezi kukielezea ni cha aina gani lakini ghafla kikaangukia chini na kusababisha kulipuka na moto kuanza kuwaka.

“Naogopa kusema ni kitu aina ya bomu au laa.Maana si mtaalamu wa kutambua aina ya kitu ambacho kimerushwa chumbani.Niseme tu baada ya kitu hicho kurushwa kitandani na kudondokea chini, moto ukaanza kufuka na kisha kulipuka.Nilichofanikiwa ni kuchukua simu na Kompyuta mpakato na kisha kukimbilia nje.

“Nilipotoka nje na wapangaji wenzangu nao wakatoka na kuanza kuulizana nani amefanya tukio hilo.Tayari tumetoa taarifa Polisi jana(juzi) usiku baada ya nyumba kuungua na hivyo tunasubiri watakachobaini kilichosababisha nyumba kuchomwa na waliohusika kufanya tukio hilo,”amesema.

Alipoulizwa anahisi nini baada ya tukio hilo, Myunga alijibu kuwa anachoamini sababu kubwa itakuwa ni mambo ya siasa kwani yeye si mfanyabashara na hana kazi nyingine zaidi ya siasa na siku za karibuni kuna moja ya kiongozi wa kisiasa wa upande wa upinzani alimtishia kwa bastola.

“Mbali ya kunitisha kwa bastola aliniambia kuwa nitakiona na lazima atanihamisha Iringa kwani najifanya mjanja kwa kuwa nimetoka Dar es salaam.Huyu kiongozi(jina tunalo) ndio atakuwa adui yangu namba moja na ndio namhisi atakuwa kafanya tukio hilo.

“Inaonesha kabisa walikuwa wamedhamiria kuniuua mimi na ndio maana walivunja dirisha la chumbani kwangu na kurusha kitu hicho ambacho kilisaabisha mlipuko uliofanya moto kuanza kuwaka.Hata hivyo acha Jeshi la Polisi Iringa nalo lifanye kazi yake ya kuchunguza na ukweli utapatikana,”amesema.


Fid Q atoa somo kwa Wasanii



Mkali wa muziki wa hip hop Bongo, Fid Q ametoa somo kwa wasanii namna ya kujiweka mbali na msongo wa mawazo (stress) kutokana na kuyumba kwa uchumi.

Rapper huyo ameiambia Dj Show ya Radio One kuwa wasanii wanatakiwa kuwa wabunifu katika kazi zao na kuwa na njia tofauti tofauti za kuwaingizia kupato.

“Katika suala la ubunifu inakupa nafasi kubwa sana kwa sababu unakuwa na akili iliyotulia ambayo haipelekwi pelekwi na stress ndogo ndogo kama za kukosa show za hapa na pale, ni kitu poa na kinapaswa kufuatwa na kila msanii,” amesema Fid Q.

“Pia kuhakikisha anakuwa na njia zaidi ya moja ya kujiingizia kipato yaani mbali na muziki awe na vitu vingine ambayo vitamsaidia kujiingizia kipato,” amesisitiza Fid Q.

Fid Q kwa sasa anafanya vizuri na remix ya ngoma Fresh aliyowashirikisha Diamond na Rayvanny.