Thursday, 28 December 2017

Serikali yapiga hodi mgodi wa Geita



Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi ameunda kamati maalumu ya kuchunguza wanaofuja fedha za wananchi, huku akiwaagiza mkuu wa wilaya hiyo Herman Kapufi, Mkurugenzi wa mji Modest Apolinary kuwasiliana na mgodi wa Geita (GGM) waharakishe kuikabidhi serikali ya mkoa huo majengo yaliyojengwa kwa ufadhili wa mgodi huo yaliyopo magogo ili yabadilishwe kuwa chuo kikubwa cha ufundi kwa lengo la kuwasaidia vijana na watoto katika mkoa wa Geita.

Amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya kalangalala katika shughuli ya uchimbaji misingi ya majengo ya shule ya secondary GEITA,na kwamba baada ya GGM kukabidhi majengo hayo,ndani ya mwezi mmoja watahakikisha wanakamilisha taratibu za kuwa chuo ili watoto wapate kujiunga hasa wale wanaotaka kusomea kozi mbalimbali zikiwemo computer ,makanika,ujenzi, kuchomelea vyuma na madini hakuna haja ya kuwatoa mkoani hapa kuwapeleka kusoma kwenye mikoa mingine.

Katika hatua nyingine baadhi ya wananchi wa kata ya Nyankumbu wamelalamikia baadhi ya viongozi kukwamisha shughuli za maendeleo na kumlazimu mkuu wa wilaya kuahidi kula nao sahani moja.


Manyara bado inasumbuliwa na uhaba wa Walimu



Waalimu na wanafunzi katika shule ya Umbur iliyopo wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wanakabiliwa na changamoto kutembea umbali mrefu upatao kilomita 20 kufuata shule,ikiwemo kukosekana uwiano wa walimu na wanafunzi ambapo mwalimu mmoja anafundisha darasa moja lenye watoto zaidi ya 100.

Akizungumza kwa njia ya simu na kunukuliwa na channel ten Mkuu wa wilaya ya mbulu Chelestino Mofuga ameiambia kituo hiki kuwa sera ya elimu inaeleza juu ya uwiano wa wanafunzi wanaopaswa kufundishwa katika chumba kimoja cha darasa kuwa ni kati ya 45 kwa shule za sekondari na 35 kwa shule za msingi ambapo shule ya umbur hali hiyo ni mara tatu zaidi kwa mujibu wa waalimu shuleni hapa wameeleza kuwa wanakailiwa na upungufu wa vyumba vitatu vya madarasa pamoja na waalimu ambapo wanafundisha hadi wanafunzi zaidi ya mia moja.

Umburu shule ya msingi pia kwa sasa inakumbwa na wasi wasi juu ya umiliki wa eneo la shule kwakuwa shule hii haina hati miliki ya ardhi ya eneo iliyopo shule hii.

Watoto hawa licho ya umri wao hutembea kilomita zaidi ya 20 kufuata huduma itakayowapa mwanga kwenye maisha yao jambo linalowaacha wazazi katika maswali mengi wakijiuliza uwezekano wa watoto wao kufanya vizuri katika masomo.

Uzinduzi wa madarasa mawili kwenye shule hii inayofanywa na halmashauri kupitia mkurugenzi wa mbulu vijijini inaongeza idaidi ya vyumba vya madarasa na kufikia vinne lakini haimalizi tatizo uhitaji wa vyumba zaidi vya madarasa kutokana na watoto kutoka wilaya ya karatu mkoa wa arusha pamoja na wilaya ya mbulu mkaoni Manyara kuendelea kuongezeka zaidi.

Benki Kuu yaipa Serikali Bilioni 300


Benki Kuu ya Tanzania imetoa gawio la Shilingi Bilioni 300 kwa Serikali kutokana na faida iliyopatikana kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.

Taarifa iliyotolewa na Benki Kuu imesema kwamba gawio hilo kutoka benki kuu kwenda kwa Serkali linafikisha jumla ya Bil 780  kwa kipindi cha miaka mitatu (2014/2015- 2016-2017)

Hata hivyo taarifa hiyo imewekwa wazi kwamba majukumu ya msingi ya Benki Kuu siyo kutengeneza faida na inapotokea faida imepatikana , sehemu kubwa hutolewa kama gawio kwa serikali.



Harmorapa amuomba msamaha Master Jay


Msanii wa muziki wa bongo fleva Harmorapa amefunguka na kumuomba radhi mtayarishaji mkongwe wa muziki wa bongo fleva na mmiliki wa studio za Mj Records, Master J na kusema kuwa amegundua kuwa alimkosea mkongwe huyo kwenye muziki.

Harmorapa alifunguka hayo alipohojiwa kwenye kipindi cha eNewz cha EATV na kusema katika mwaka 2017 amemkosea sana Master J kufuatia kauli yake aliyoitoa kipindi cha nyuma kupitia kipindi hicho kuwa hamjui wala hamtambua mtayarishaji huyo mkongwe wa bongo fleva.

"Nimegundua kuwa nilifanya makosa sana, unajua kipindi kile nasema vile nilikuwa bado sijamjua vizuri Master J hivyo naomba anisamehe tu kwani ulikuwa ugeni katika tasnia hivyo nilikuwa sijamjua vizuri" alisikika Harmorapa.

Harmorapa alishawahi kumkana mtayarishaji huyo kuwa hamfahamu baada ya Master J kunukuliwa akisema kuwa msanii huyo hana kipaji cha muziki na kuimba labda kama atakwenda kufanya vichekesho, jambo ambalo lilionesha kumkwaza Harmorapa.


Serikali yawapiga mkwara viongozi wa Dini




Serikali imewaonya viongozi wa dini wanaotumia mahubiri yao kuchambua masuala ya kisiasa, ikiwataka kuheshimu msingi wa uanzishwaji wa taasisi zao la sivyo taasisi zao zitafutwa.

Taarifa iliyotolewa leo Desemba 28 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali mstaafu Projest Rwegasira imesema taasisi za dini zinapaswa kuzingatia sheria na masharti ya kuanzishwa kwake ambayo yapo kwenye Katiba za taasisi husika.

"Baadhi ya jumuiya zimekuwa zikifanya shughuli zao kinyume na malengo yaliyomo kwenye Katiba zao bila kuiarifu Ofisi ya Msajili wa Jumuiya za kidini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, " amesema na kuongeza,

"Hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi wa jumuiya kutumia mahubiri yao wakati wa ibada kuchambua masuala ya siasa kinyume na Katiba zao. Hakuna jumuiya iliyosajiliwa chini ya sheria ya jumuiya ili kufanya siasa."

Amesema kufanya hivyo ni kwenda kinyume na malengo na ukiukwaji wa Kanuni ya 7 ya Kanuni za Jumuiya zilizoundwa chini ya sheria ya Jumuiya, inayotamka pamoja na mengine kuwa Jumuiya yoyote hairuhusiwi kufanya mabadiliko ya malengo yake bila kibali cha msajili.

“Ofisi ya Msajili inazikumbusha Jumuiya zote kwamba ukiukaji wowote wa Sheria ni kosa ambalo linaweza kupelekea Jumuiya husika kufutiwa usajili wake kama ilivyoelezwa kwenye kifungu cha 17 cha Sheria husika," amesema.

Mwananchi.

Rais Magufuli akutana na kamati ya uhakiki CCM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  John Magufuli amekutana na kamati maalum aliyoiunda kwa lengo la kuhakiki mali za chama hicho, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais amekutana na kamati hiyo leo Desemba28 kwa mara ya kwanza tangu alipoitangaza  Desemba 20, Mkoani Dodoma ambayo inaongozwa na Dk. Bashiru Ally.

Katika Mazungumzo hayo  Rais Magufuli amewataka wajumbe wa kamati hiyo kufuatilia na kuhakiki mali zote za chama, kumhoji mtu yeyote ambaye atahitajika kutoa taarifa juu mali za chama na kubaini thamani ya mali, mahali zilipo, makusanyo ya mapato na wanazozishikilia ama kutumia mali hizo.

Rais Magufuli pia ametoa wito kwa wanachama wa CCM na wananchi wengine kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zote zinazohusu mali za chama kwa kamati hiyo, na watakaoitwa kuhojiwa waitikie wito huo.

“Nataka mali za chama zikinufaishe chama, nataka mkamhoji mtu yeyote, awe kiongozi, awe mwanachama, awe mfanyabiashara, mtu yeyote. Mkazihakiki mali zote ili chama kipate haki yake” amesema  Rais Magufuli.

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo, Dk Bashiru Ally amesema kamati imeanza kazi rasmi na ametoa wito kwa wanachama, wananchi na wote wanaozitumia mali za chama kutoa ushirikiano watakapoitwa kuhojiwa.

“Tumezungumza na Mwenyekiti kwa karibu saa mbili, katueleza matarajio yake, sababu za kuunda tume hii, kazi zake na faida zake kwa chama na kwa nchi, kwa hiyo ametukabidhi vitendea kazi na taarifa mbalimbali na ametuambia kazi yetu ni kuhakiki mali zote za chama kwa kushirikiana na wanachama na wale wanaoshirikiana na chama kuzitumia hizo mali kama vile wapangaji, wasimamizi, nakadhalika” amesema Dk  Ally.


Kiwanda cha Alizeti chafungwa Singida


Serikali imekifungia Kiwanda cha kukamua mafuta cha  Alizeti Mount  Meru Millers Ltd kwa  muda usiojulikana kwa madai ya kukaidi agizo la kulipa faini ya Sh20milioni.

Uamuzi wa kukifunga kiwanda hicho umetolewa jana Jumatano na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira ,Kangi Lugola  alipokuwa kwenye kwanda hicho kilichopo  kijiji cha Manguanjuki Manispaa ya Singida.

Kabla ya kutoa uamuzi huo  mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Singida, Lugola alisema Novemba 29 mwaka jana, mtangulizi wake Luhaga  Mpina, aliuagiza uongozi wa  kiwanda hicho ulipe  faini ya Sh20milioni kwa kosa la kutiririsha  maji taka yenye kemikali kwenye makazi ya watu .

“Maji taka yameelekezwa kwenye makazi ya wananchi wanaokizunguka kiwanda .Pia maji  hayo yenye kemikali, yameelekezwa kwenye ziwa la Singidani lenye viumbe hai wakiwemo samaki. lakini hadi leo, agizo la Waziri  Mpina, halijatekelezwa’’ amesema Lugola na kuongeza kwamba

‘’Kutokana na  ukiukwaji wa  sheria za mazingira, Mpina alikipa adhabu ya kulipa faini  Sh20milioni ambayo haijalipwa hadi leo”, amesema Waziri Lugola kwa masikitiko.

Lugola amesema kwamba  kiwanda hicho kimetekeleza agizo la kununua mashine ya kutibu maji taka, lakini maji taka hayo, hayajaelekezwa kwenye mashine hiyo.

 “Maji hayo yenye kemikali bado yameendelea kuwa kero kwa wananchi hadi leo, na yanaathiri viumbe hai vilivyopo kwenye ziwa Singidani. Hii dharau kwa serikali haikubaliki”, amesema

Naibu waziri huyo, amesema  wananchi wanaozunguka kiwanda hicho wamekuwa wakitoa kilio chao serikalini kwa miaka minne, kwamba wanaathiriwa na maji yenye kemikali  na moshi mnene wa kiwanda cha Maount Meru.

“Binafsi leo nimefika kwenye kiwanda hiki na baada ya kufanya ukaguzi wa kina, nakiri kwamba kilio cha wananchi wa Manguanjuki ni cha kweli na kinahitaji tiba ya kudumu. Mkuu wa wilaya ya Singida, naagiza kuanzia sasa, usimamie kufungwa kwa kiwanda hiki”,amesema na kuongeza;

“OCD pia nakuagiza uwatafute Wakurugenzi wa kiwanda hiki Atul Nittal, Arvind Mittal na Tarsem Aggarwal, popote walipo na kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria kwa kukaidi agizo la Serikali”.

Kwa upande wake meneja Uhusiano, Nelson Mwakambuta, amesema kiwanda hicho kimekuwa kikifanyiwa ukaguzi mara kwa mara na mamlaka mbalimbali. Lakini  wamekuwa wakiwaambiwa na viongozi hao kuwa   kiwanda hicho, hakina tatizo lolote linalohusiana na kwenda kinyume na sheria za  mazingira.

“Kufungwa kwa muda usiojulikana kwa kiwanda hiki, kutaathiri ustawi wa watumishi wengi wa kiwanda na familia zao. Pia  wakulima wa zao la alizeti ndani na nje ya mkoa wa Singida, nao watakuwa wamepata pigo. Hatupingani na serikali tutatekeleza yale yote tuliyoagizwa”,amesema meneja huyo.



Orodha ya wachezaji wanaolipwa mkwanja mrefu EPL



Ligi Kuu ya Uingereza ni miongoni mwa Ligi Kubwa Ulaya lakini ni miongoni pia mwa Ligi za Ulaya zenye mashabiki wengi ukanda wa Afrika husani Afrika Mashariki, inawezekana kuna mambo mengi ambayo huyafahamu katika Ligi Kuu England.

Hii hapa chini ni orodha ya mastaa wa Soka kwenye Ligi hiyo wanaolipwa mkwanja mrefu zaidi kwa wiki.

1- Paul Pogba analipwa pound 290000/Tsh 872,087,739 (ManUnited)

2- Romelu Lukaku pound 250000/Tsh 752,068,375 (ManUnited)

3- Sergio Aguero pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManCity)

= Yaya Toure pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManCity)

= Zlatan Ibrahimovic pound 220000/Tsh 661,820,170 (ManUnited)

6-Kevin De Bruyne pound 200000/Tsh 601,609,900 (Man City)

= David De Gea pound 200000/Tsh 601,609,900 (ManUnited)

= Eden Hazard pound 200000/Tsh 601,609,900 (Chelsea)

9-Virgil van Djik pound 180000/Tsh 541,448,910 (Liverpool)

= Philippe Coutinho pound 180000/Tsh 54,1448,910 (Liverpool)


Familia yafukua kaburi la Baba yao




Familia ya watoto wanne wakiongozwa na mama yao mzazi Julieta Majaliwa wamelazimika kufukua kaburi la baba yao Stanford Gombo, wakidai kuwa na mashaka na sababu ya kifo cha baba yao.

Tukio hilo limetokea huko katika cha kijiji cha Kilimani wilayani Gairo mkoani Morogoro ikiwa ni utekelezaji wa amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani humo baada ya familia hiyo kutaka mwili huo kufanyiwa uchunguzi.

Wanafamilia hao walifika kijijini hapo wakiwa na ulinzi wa polisi kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa amri ya mahakama inayoelekeza kufukuliwa kwa kaburi hilo, ili watoto wapate nafasi ya kuhakiki mwili uliozikwa kama ni wa baba yao pamoja na kufanyiwa uchunguzi kubaini sababu zilizopelekea kifo chake.

Kwa upande wake Mke wa marehemu ,Bi. Julieta Majaliwa amesema mara ya mwisho kuwasiliana na mumewe walikua  nyumbani kwao jijini Dar es salaam ambapo alimuaga anaenda kijiji kwao kuwajulia hali lakini tangu alivyo ondoka hawa kuwa na mawasiliano hadi kifo chake.

Chifu ashambuliwa kwa kupiga vita pombe haramu



Chifu wa eneo la Elburgon, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya alijikuta akishambuliwa na kundi la vijana wenye hasira alipoongoza msako dhidi ya pombe haramu.

Chifu huyo anayejulikana kwa jina la Francis Ngacha, alikuwa ameongozana na wanachama wa kundi la nyumba kumi aliposhambuliwa na vijana hao, wakimlaumu kwa kuwaharibia sherehe zao za Krismasi.

“Nilikuwa nimeongoza kikundi hicho kufanya msako dhidi ya vijiwe vya kuuza pombe haramu katika eneo hilo, na ndipo kundi la vijana zaidi ya 10 lilipoanza kuturushia mawe,” amesema Bw. Ngacha.

Kwa upande mwengine Naibu Kamishna wa Kaunti hiyo Bw. Naftaly Korir, alituma kikosi cha polisi kufanya msako huo, lakini hawakufanikiwa kuwakamata vijana waliomshambulia chifu, kwani walitoroka eneo hilo.

Polisi wamesema wanawatafuta vijana hao waliohusika kumshambulia chifu, ili wachukuliwe hatua za kisheria.



Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download

Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download


Audio | Joh Makini – Mipaka | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download

Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download


Video | Nancy Hebron ft Vanessa Mdee, Mimi Mars – Beautiful Jesus | Mp4 Download


Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

Video | Joh Makini – Mipaka.| Mp4 Download

DOWNLOAD