Wednesday, 27 December 2017

Baada ya Askofu Kakobe kuikashifu Serikali , CCM yamjibu



Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema Askofu Zakaria Kakobe wa Kanisa la FGBF lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam amekosa hekima na busara kwa kugeuza madhabahu ya kanisa kuwa jukwaa la kisiasa na kuanza kukashifu viongozi wa serikali akiwemo Rais Dkt John Pombe Magufuli.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam, Frank Kamugisha alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku moja baada ya Aksofu Kakobe kukosoa namna serikali inavyotenda mambo yake, akisisitiza kwamba Tanzania si nchi ya chama kimoja kama ambavyo viongozi wanataka kuigeuza na hivyo kuwataka viongozi wa serikali waanze kutubu.
Kamugisha amesema kuwa, wao kama viongozi wa CCM hawaweza wakakaa kimya wanapoona chama kinachafuliwa na viongozi wake ambao wanafanya kazi kwa niaba ya watanzania wakikashifiwa.
Aidha, alisema kuwa, siasa ni kwa ajili ya wanasiasa, na kama kiongozi wa dini ana jambo lolote analotaka kuzungumzia, kuna busara za kutumia na sio kutumia kanisa kusema hayo.

Marekani Yawawekea kikwazo wataalamu Wa kutengeneza Makombola korea Kaskazini




Marekani imewawekea vikwazo maafisa wawili wa Korea Kaskazini ambao inasema kuwa wamechangia kuundwa makombora ya nchi hiyo.
Wizara ya fedha nchini Marekani iliwataja Kim Jong-sik na Ri Pyong-chol na kusema kwua wote walikuwa viongozi wakuu katika mpango wa makombora ya masafa marefu wa Korea Kaskazini.
Baraza la ulianzi la Umoja wa Mataifa liliiwekea vikwazo vipya Korea Kaskazini siku ya Ijumaa kujibu majaribio yake ya makombora ya masafa marefu, Korea Kaskazini ilisema kwa hatua hiyo ni kama ya vita.
Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vitazuia shughuli zozote za wanaume hao wawili zinazofanywa nchini Marekani, na hata kutwaliwa kwa mali yao yaliyo nchini Marekani.


Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

Video | Mr Flavour Ft Zoro – Ijele | Mp4 Download

DOWNLOAD


Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Thamani Ya Mama | Mp3 Download

DOWNLOAD

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

Audio | Moni Centrozone Ft Country Boy – Mwaaah.| Mp3 Download

DOWNLOAD

Tuesday, 26 December 2017

Video | Kiss Daniel _ No Do | Mp4 Download

Video | Kiss Daniel _ No Do | Mp4 Download



DOWNLOAD

Nyumba ya Rais Yachomwa moto



Nyumba ya Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila imechomwa moto katika shambulizi linaloshukiwa kufanywa na waasi, ambapo askari mmoja aliuawa
Tukio hilo limetokea Desemba 25, 2017, ambapo taarifa zinasema kuwa waasi wa kundi lijulikanalo Mai Mai walijaribu kuiba mali kutoka makazi hayo ya rais yaliyoko eneo la Musienene, katika jimbo la Kivu ya Kaskazini.
Wakati wa tukio Rais Kabila hakuwa kwenye nyumba hiyo ambayo iko kijijini maili 1,680 Mashariki mwa mji wa Kinshasa, huku kundi la Mai Mai na kundi la waasi wa ADF wakiwa washukiwa wa kwanza juu ya tukio hilo.
Hivi karibuni Rais Kabila amekuwa akipingwa na wanasiasa mbali mbali kwa kitendo chake cha kutaka kugombea nafasi ya urais kwa muhula mwengi

Aliyemlawiti Mtoto Tarime Matatani



Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, linamshikilia Said Selemani 30-40 mkazi wa Mtaa wa Kebasa Halmashauri ya Mji Tarime mkoani Mara kwa tuhuma za kulawiti mtoto wa miaka minne.
Kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Rorya, Henery Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa amefunguliwa shtaka kituoni hapo namba TAR/IR/5034/2017 na kuwa atafikishwa mahakamani baada ya
upelelezi kukamilika.
Aidha, Kamanda huyo aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo anatarajia kupelekwa mahakamani kesho ili kujibu shtaka linalomkabili kwa kuongeza kuwa mtuhumiwa huyo pia amatuhumiwa kumsababishia maumivu makali mtoto huyo.
Akizungumzia tukio hilo nyumbani kwake, mama mzazi wa mtoto huyo (jina limehifadhiwa), amesema tukio hilo lilibainika Disemba 14, 2017 wakati mtoto aliposhindwa kula na kuanza kuharisha mara kwa mara.
“Kugundua kuwa mtoto wangu ameathirika na kitendo hicho ni baada ya kuwa ameshindwa kula huku akiwa anaharisha mara kwa mara, kitendo ambacho kilinishtua moyo wangu na mtoto hakuwa na dalili ya kuugua ikabidi nianze kufanya ufuatiliaji wa kina ili kujua kilichompata,” alisema.
Ameongeza kuwa tukio hilo amelipokea kwa masikitiko makubwa na kuwa hakuwa na habari kuwa mwanaye wa miaka minne anaweza kutendewa kitendo cha kinyama kiasi hicho na mtuhumiwa ambaye ni mpangaji mwenzake.
Akizidi kufafanua, amesema kuwa baada ya kugundua mwanaye amekuwa akilawitiwa mara nyingi kwa nyakati tofauti, alichukua hatua za kwenda kwa wataalamu ili kuchukuliwa vipimo kwa ajili ya kijiridhisha.
“Hatua nilizochukua baada ya kugundulika kuwa mwanangu alikuwa ameathirika kwa muda mrefu ni kwenda kituoni polisi ili kutoa taarifa kwa hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya mtuhumiwa,”alisema mama huyo..
”Baada ya kwenda polisi ilibidi twende hospitalini kwa uchunguzi ambapo daktari alisema hakuona dalili zozote ila nikasema kuwa haiwezekani kuna mchezo unafanywa, andipo niliomba kwenda Bugando kwa uchunguzi zaidi ambapo polisi walitoa askari wa kwenda kujiridhisha,” aliongeza.
Alibainisha wakati wakiwa Bugando, daktari aliyemfanyia vipimo alisema mtoto huyo amelewitiwa mara nyingi zaidi ya mwaka mmoja.

Amana yaongoza kwa idadi kubwa ya watoto waliozaliwa krismas



Dar es Salaam. Watoto 102 wameripotiwa kuzaliwa katika hospitali mbalimbali nchini wakati wa mkesha wa sikukuu ya Krismasi. Dar es Salaam wamezaliwa 50, Kanda ya Ziwa 29, Arusha 18, na Handeni mkoani Tanga watano.
Hospitali ya Amana ndiyo iliyokuwa na idadi kubwa ya watoto waliozaliwa na Ofisa Muuguzi wa zamu, Agnes Simon alisema kati ya watoto 32, watano waliozaliwa kwa upasuaji.
Alisema afya za watoto hao ni njema na baadhi yao huenda wakaruhusiwa kurudi nyumbani.
“Hakuna mtoto mwenye tatizo, wote wana afya nzuri, hata wazazi wao wanaendelea vizuri pia, hivyo tunatarajia kuwaruhusu wakasherehekee sikukuu nyumbani,” alisema Agnes.
Kaimu Mkuu wa Jengo la Wazazi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Mariam Mlawa alisema jana kwamba watoto waliozaliwa hospitalini hapo wana afya njema na wanaendelea vizuri na idadi hiyo haijapishana na waliozaliwa katika mkesha wa Krismasi mwaka jana.
Alisema kina mama sita walijifungua na kati yao, wawili kwa upasuaji na wengine kwa njia ya kawaida. Pia kati yao, wawili wamejifungua watoto pacha.
“Tunashukuru watoto wote wapo vizuri, mama zao pia wapo vizuri na kwa hawa waliojifungua kwa njia ya kawaida huenda wakaruhusiwa muda wowote,” alisema Mlawa.
Ofisa Muuguzi Kiongozi katika Hospitali ya Temeke Rashidi Nyombiage alisema watoto 12 walizaliwa kwa njia ya kawaida na kwamba hakuna aliyejifungua kwa njia ya upasuaji.
“Hatukupata pacha, watoto wote walizaliwa mmojammoja na hakuna mtoto mwenye tatizo lolote wote wanaendelea vizuri na afya zao pamoja na mama zao zinazidi kuimarika,” alisema Nyombiage.
Katika Kanda ya Ziwa, watoto 16 walizaliwa katika Hospitali ya Mkoa ya Sekou Toure. Muuguzi msimamizi wa zamu, Rhoda Lissu alisema kati ya hao wa kike ni 10 na wakiume sita.
“Watoto wawili kati ya hao wamezaliwa kwa njia ya upasuaji, lakini tunamshukuru Mungu wapo salama na afya za mama zao zipo vizuri, “ alisema Rhoda.
Wilayani Serengeti, muuguzi mkuu wa Hospitali ya Teule ya Nyerere, Neema Machara alisema watoto watatu wa kiume walizaliwa kwa njia ya kawaida.
Arusha, watoto 18, walizaliwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Jackline Urio alisema kati yao 12 ni wa kiume.
Akizungumza jana, Mwamvua Barua mkazi wa Mtoni Kijichi aliyejifungua Muhimbili alisema hakutarajia maishani mwake kujifungua katika siku hiyo akisema atamlea mtoto wake huyo aliyempa jina la Emmanuel katika maadili.
“Huyu ni mtoto wa pili na wote nimewazaa mwezi wa 12, ila uzao huu umeangukia kwenye mkesha wa sikukuu,” alisema.

Miradi Mikubwa itakayo kumbukwa mwaka 2017



Dar es Salaam. Mwaka 2017 ukielekea ukingoni, miradi mikubwa saba itaendelea kuutaja kila itakapikuwa ikizungumziwa.
Miradi hiyo ni ujenzi wa bomba la mafuta, uboreshaji Bandari Dar es Salaam, upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) na ujenzi wa Daraja la Furahisa, Mwanza, bandari mpya ya Bagamoyo na mradi wa kuzalisha megawati 2,100 za umeme wa Stiegler’s Gorge.
Ikiwa imetangaza kuzikaribisha taasisi zinazoweza kufanya utafiti wa namna ya kufanikisha azma ya uchumi wa viwanda, Serikali inatekeleza miradi hiyo mikubwa na kati yake ipo iliyofikia hatua za mwisho.
Bomba la mafuta
Agosti 5, Rais John Magufuli pamoja na mwenzake, Yoweri Museveni wa Uganda walizindua ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima hadi Bandari ya Tanga. Ajira zaidi ya 1,000 zinatarajiwa kupatikana katika mradi huo.
Bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,450 litapita katika mikoa minane ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga. Ndani ya mikoa hiyo, bomba hilo litakalogharimu Sh8 trilioni, litapita katika vijiji 184 vilivyomo katika wilaya 24.
Mbali na ajira kwenye mradi huo, kutakuwa na fursa za kibiashara kwa wauzaji na wasambazaji wa vyakula na vifaa vya ujenzi.
Bomba hilo litajengwa na kuendeshwa na kampuni za Total ya Ufaransa, CNOOC ya China na Tullow ya Uingereza kwa ubia na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (Unoc) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
Bandari ya Dar
Julai 2, ulifanyika uzinduzi wa kuboresha Bandari ya Dar es Salaam ambao unatekelezwa na Kampuni ya China Harbour Engineering Company (CHEC) utakaogharimu Sh336 bilioni ambazo ni mkopo kutoka Benki ya Dunia. Kazi hiyo inatarajiwa kukamilika baada ya miezi 36.
Uboreshaji huo unahusisha ujenzi wa gati jipya la kuhudumia magari pekee, uboreshaji wa gati namba moja hadi saba na kuongeza kina cha maegesho ya meli kutoka mita 8.2 hadi 15 na kina cha mlango wa bahari ili meli kubwa na za kisasa ziweze kufika katika bandari hiyo.
Upanuzi huo unatarajiwa kuongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam hivyo kuiwezesha kuhudumia kiasi kikubwa cha mizigo hivyo kukuza uchumi.
Licha ya kuboreshwa kwa miundombinu, huduma nazo zinatarajiwa kurahisishwa. Mamlaka zote zinazohusika na uondoshaji au usafirishaji wa mzigo zimetakiwa kuwa na ofisi bandarini hapo. Hizo ni pamoja na benki zote zinazopokea fedha za Serikali ambazo ni na tozo za aina tofauti zinazopaswa kulipwa.
Taasisi zote muhimu zimewekwa chini ya dirisha moja ili kupunguza muda wa kukamilisha mchakato huo na kuharakisha biashara kwa waagizaji wa ndani na nchi jirani zinazoitumia bandari hiyo.
Upanuzi JNIA
Katika kuimarisha usafiri wa anga kwa wasafiri wa ndani na kimataifa, Serikali inapanua uwezo wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), mradi huo unaotekelezwa na Kampuni ya Bam International ya Uholanzi, kwa gharama ya Sh560 bilioni.
Wakati upanuzi huo ukitarajiwa kukamlika mapema mwakani na kuongeza idadi ya abiria kutoka milioni 2.5 hadi milioni 6.4 kwa mwaka, Serikali pia inaimarisha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).
Ndege mbili zikiwa zimeanza kutoa huduma, nyingine nne zipo kwenye mpango wa kuwasili. Mpaka mwakani, Serikali imesema ndege zote zitakuwa zimewasili nchini ili kuimarisha usafiri wa anga na sekta ya utalii kwa ujumla.
Bandari mpya Bagamoyo
Baada ya kusuasua kwa muda mrefu, mwaka huu Serikali imekamilisha taratibu za ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo pamoja na eneo maalumu la uwekezaji (SEPZ). Tangu Oktoba 15, 2015 Rais mstaafu Jakaya Kikwete alipoweka jiwe la msingi la utekelezaji wa mradi huu, hapakuwa na uendelezaji.
Lakini Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema taratibu zimekamilika na ujenzi utaanza Januari 2018. Utekelezaji wa mradi huo utaifanya Bagamoyo kuwa bandari kubwa zaidi Afrika Mashariki na Kati.
Utekelezaji wake utagharimu Dola 10 bilioni za Marekani (zaidi ya Sh22.3 trilioni), na waziri Mwijage alisema utafanywa kwa ushirikiano wa Kampuni ya China Merchants Holdings International (CMHI) ya China na State General Reserve Fund ya Oman. Eka 3,000 zimetengwa na viwanda 190 vinatarajiwa kujengwa kabla ya mwaka 2020.
Utakapokamilika, mradi huo utakuwa na viwanda 700 na kuufanya kuwa eneo la kimkakati kwa uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na kuchangia kuinua uchumi wa Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa za ujenzi huo, awamu ya kwanza itahusu meli kubwa zinazobeba hadi makontena 8,000 ya futi 20 hivyo kupunguza foleni ya meli za mzigo katika Bandari ya Dar es Salaam huku kukiwa na uwezekano wa kuitanua zaidi.
Stiegler’s Gorge
Mipango iliyomshinda Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na awamu tatu zilizofuata baada yake imewezekana hivi sasa. Agosti 30 Serikali ilitangaza zabuni ya ujenzi wa mradi mkubwa wa kuzalisha megawati 2,100 za umeme katika maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge).
Zaidi ya kampuni 80 zimejitokeza kuomba kutekeleza mradi huo unaoelezwa kwamba utapunguza uhaba wa nishati hiyo nchini na kuweka mazingira rafiki ya ujenzi wa viwanda. Utakapokamilika, utaifanya Tanzania kuwa na jumla ya megawati 5,000 ifikapo mwaka 2021.
Mradi huo unatekelezwa huku Wakala wa Nishati Vijijini (Rea) ukiwa unaendelea kusambaza umeme nchini. Mwaka jana, jumla ya vijiji 4,000 viliunganishwa. Pamoja na hiyo, mradi wa Kinyerezi I na II ipo kwenye hatua tofauti. Upanuzi wa Kinyerezi I uliokamilika kwa zaidi ya asilimia 50 unatarajiwa kuzalisha megawati 185 utakapokamilika wakati Kinyerezi II uliokamilika kwa zaidi ya asilimia 86 ukitegemewa kuzalisha megawati 250.
Ujenzi reli ya kisasa (SGR)
Ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway) kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma na Mwanza tangu utekelezaji wake ulipoanza mwaka huu, unatarajiwa kuanza kufanyakazi baada ya miezi 36.
Ujenzi wa awamu ya kwanza kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro utakaogharimu Sh2.7 trilioni wa reli hiyo ya mwendo wa kasi ya kilomita 160 kwa saa, umeanza na utaifanya Tanzania kuwa ya pili kwa kasi hiyo baada ya Morocco.
Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (Rahco) imetiliana saini mkataba wa ujenzi wa awamu ya kwanza ya reli hiyo na Kampuni ya Yapi Merkenzi Instant Ve Sanayi A.S ya Uturuki na Mota-Engil, Engenharia E and Construcao S.A ya Ureno kujenga kilomita 205 za njia kuu na kilomita 95 za kupishania.
SGR itakuwa na uwezo wa kusafirisha tani milioni 17 za mzigo ambalo ni ongezeko karibu mara mbili na nusu ya uzani uliopo.
Daraja la furahisha
Licha ya kujenga barabara zenye urefu wa kilomita 1,500 kwa kutumia Sh1.2 trilioni nchini kote mwaka huu, Serikali imekamilisha ujenzi wa Daraja Furahisha lililopo jijini Mwanza kwa kutumia Sh4.7 bilioni. Rais Magufuli alilizindua Oktoba 30.
Daraja hilo lina urefu wa mita 46, upana mita 3.6 na kimo cha mita 5.8 na njia za kuingia na kutoka zenye jumla ya meta 700. Fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe za Muungano mwaka 2016 zilijenga daraja hilo baada ya kuzibadilishia matumizi.
Kujengwa kwa daraja hilo kumeokoa kwa kiasi kikubwa maisha ya wapita katika eneo hilo kwani lilikuwa na matukio mengi ya ajali.

Matukio ya Mauwaji yaliyotikisa Mwanza 2017



Mwanza. Tukiwa tunaelekea kuhitimisha mwaka 2017, mkoa wa Mwanza na viunga vyake vilitikiswa na matukio mbalimbali.
Miongoni mwa matukio yaliyobamba na kutikisa nyoyo za wakazi mkoani hapa ni vifo vya watu mbalimbali pamoja na mamilioni ya fedha ambayo idadi yake haikujulikana kuteketea ndani ya nyumba.
Juni 10 mwaka huu wakazi wa Mwanza waligubikwa na simanzi ya kifo cha milionea mmoja mkazi wa jiji la Mwanza, Maduhu Masunga (76) maarufu kwa jina la Mzee Shinyanga kuteketea kwa moto ndani ya nyumba aliyokuwa anaishi pamoja na mamilioni yake.
Mzee huyo inadaiwa alifariki dunia wakati anajaribu kuokoa mamilioni hayo ya fedha aliyokuwa ameyaficha ndani ya nyumba hiyo.
Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi ilisema thamani ya mali na fedha zilizoteketea katika ajali hiyo haijafahamika na kwamba jeshi la polisi lilikuwa linaendelea na uchunguzi kubaini kiasi cha fedha hizo.
Pamoja na kiasi cha fedha kilichokutwa ndani hakijaweza kujulikana, Meneja wa Idara ya Uchumi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Kanda ya Ziwa, James Machemba alisema kisheria fedha zote zinapaswa kuhifadhiwa kwenye taasisi za fedha ili zirejee kwenye mzunguko na hivyo kusisimua uchumi.
“Hata kama ni fedha zinazomilikiwa kihalali, ni kosa kisheria kuhifadhi kiasi kikubwa nyumbani; fedha zinatakiwa kuwa kwenye mzunguko na anayezihifadhi ndani anakwamisha maendeleo na uchumi wa Taifa,” alisema Machemba.
Akizungumza na gazeti hili akiwa nyumbani kwake mtaa wa Kirumba wilayani Ilemela, mke wa marehemu, Mariam Masanja (68) alisema pamoja na kuwa mzee huyo alikuwa akimiliki mali nyingi yakiwamo maghorofa na magari lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa anajua kiasi cha fedha alichokuwa nacho na mahala alipoweka fedha zake.
Mke wa marehemu pamoja na baadhi ya watoto waliozungumza na gazeti hili kila mmoja alidai kuwa hafahamu ni kiasi gani cha fedha alichokuwa anamiliki.
“Mzee Shinyanga alikuwa anatoa mahitaji yote muhimu kwenye familia, ikiwamo kusomesha watoto lakini hatukuwahi kujua kama fedha zote zinakaa ndani tena kwenye ndoo, hadi pale siku ya tukio zilipobainika zimeteketea kwa moto,” alisema Mariam.
Majambazi wauawa Mwanza
Tukio jingine lililoibua hisia kwa wakazi wa Mwanza ni baada ya jeshi la polisi mkoani Mwanza kufanikiwa kuwaua majambazi sita katika mtaa wa Fumagila, kata ya Igoma jijini Mwanza.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Julai 8 mwaka huu baada ya majambazi hao kurushiana risasi na askari waliokuwa doria, hivyo kufanikiwa kuyaua huku wawili wakifanikiwa kutoroka.
Kutokana na tukio hilo, wakazi wa mtaa huo waliingiwa na hofu hivyo kusababisha shughuli zao za kila siku kusuasua.
Mauaji ya wanandoa
Mauaji ya wanandoa nayo yalileta taswira mbaya kwa wakazi wa mkoani Mwanza baada watu wawili wakazi wa mtaa wa Kanyerere, kata ya Butimba kuuana kwa risasi.
Tukio hilo lilitokea Mei 25, mwaka huu baada ya Maximilian Tula (40) kumuua kwa kumpiga risasi mkewe Teddy Malulu kabla ya yeye kujimaliza.
Chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi kati yao.
Mbali na tukio hilo, matukio ya wanandoa kuuana yaliendelea baada ya wakazi wa kijiji cha Mwagiligili wilayani Sengerema, Kwilokeja Boniphace (35) kumuua mkewe Shija Luchagula (30) kwa kumpiga na kumnyonga kisha naye kujinyonga kwa kile kinachosemekana kuwa ni wivu wa mapenzi.
Matukio mengine yanayofanana na hayo zaidi ya saba yaliendelea kutokea katika maeneo mbalimbali mkoani humo.
Hiace yatumbukia ziwani
Oktoba 9 mwaka huu, wakazi wa mkoa wa Mwanza pia waliingiwa na simanzi kutokana na vifo vya watu 12 waliofariki dunia baada gari dogo la abiria maarufu kama daladala aina ya Toyota Hiace kutumbukia Ziwa Victoria katika Kivuko cha Kigongo wilayani Misungwi.
Baadhi ya majeruhi walitoka salama na kulazwa katika Kituo cha Afya Bukumbi.
Majeruhi Yohana Ngabula alisema ajali hiyo ilisababishwa na dereva kuwa kwenye mwendo mkali.
“Tulimshauri dereva asiendeshe kwa kasi lakini hakutusikiliza hali iliyosababisha gari kufeli breki na kusababisha vifo hivyo,” alisema Ngabula.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya Bukumbi, Dk Robert Shija alithibitisha kupokea miili ya watoto watatu na watu wazima tisa.
Miezi mitatu baadaye watu watano walifariki dunia na wengine 13 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea jijini Mwanza ikihusisha gari aina ya Coaster na lori eneo la Buhongwa.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema ajali hiyo ilitokea Desemba 16, saa 3:30 usiku katika barabara ya Mwanza-Shinyanga kata ya Buhongwa wilayani Nyamagana.
Wanawake wavishana pete
Tunaweza kusema kuwa ni tukio la funga mwaka baada ya jeshi la polisi mkoani hapa kuwatia nguvuni wanawake wawili waliodaiwa kuvishana pete za uchumba kinyume cha sheria.
Washtakiwa hao ambao ni, Milembe Suleiman (35) na Janeth Shonza (25) Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Gway Sumaye na kusomewa shtaka la kufanya vitendo vinavyoashiria mapenzi ya jinsia moja.
Wakili wa Serikali, Emmanuel Luvinga alidai kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo Agosti 31 wakiwa katika Hoteli ya Pentagon jijini Mwanza, kinyume cha kifungu cha 138 A cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura ya 16 kama na marekebisho yake ya mwaka 2002.
Katika shauri hilo namba 548/2017, Wakili Luvinga alidai kuwa washtakiwa hao waligusanisha ndimi zao ikiwa ni shara ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi kinyume cha sheria.
Aneth Mkuki (24) mkazi wa jijini Mwanza, naye alifikishwa mahakamani kwa shtaka hilo hilo na kifungu hicho hicho cha sheria baada ya kudaiwa kuwa mshereheshaji siku ya tukio hilo.
Mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni Richard Fabian (28) Mkazi wa Buzuruga Mwanza yeye ameshtakiwa kwa kosa la kusambaza picha ya video za tukio hilo la kuvishana pete, kinyume na Sheria ya Mtandao Kifungu cha 20 Kifungu Kidogo cha (1) (a) cha Sheria ya Mitandao namba 14 ya mwaka 2015.
Wakili Jebra Kambole anayewatetea washtakiwa hao aliiomba mahakama iwape dhamana kwa sababu mashtaka yanayowakabili yana dhamana.
Ombi hilo lilikubaliwa na Hakimu Sumaye lakini akasema kwamba hawezi kutoa masharti ya dhamana kwa sababu shauri hilo lilipangwa kusikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilbert Chuma ambaye hakuwapo.

TEHAMA yawanufaisha watoto




Maadhimisho ya tamasha la kufunga mwaka la TEHAMA yanayohusu kuwafundisha watoto elimu ya kompyuta kwa vitendo yamefanyika jijini Da es salaam yakiwa na lengo la kuonyesha kwamba watoto wakifundishwa kwa kufuata silabasi sahihi iliyowekwa na serikali inamafanikio kwa asilimia 100.
Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkurugenzi Kiongozi wa mpango huo wa Tehama class, Rajab Mustafa amewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao katika vituo vilivyo sehemu mbalimbali jijini Dar es salaam ili wapate elimu hiyo kwani watoto kuanzia darasa la kwanza hadi la tatu ni bure kwa siku ya jumamosi na juma pili inapotelewa elimu hiyo kulingana na ratiba za nasomo.
Aidha katika mpango huo watoto watapata elimu ya kompyuta kwa vitendo ikiwa ni dhamira ya kufanya watoto waelewe kuhusu Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
''Tunawafundisha Ngamizi ili baadae watakapojiendeleza na elimu zao wapate kuelewa kuhusu teknolojia pia waweze kujiajili'' Alisema Mustafa

Barnaba Kufanya Kolabo Na Ben Pol



MKALI wa Bongo Fleva, Elias Barnaba amefunguka kuhusu kufanya kolabo la maana na msanii mwenzake Ben Pol, mwakani 2018. Akizungumza na Full Shangwe, Barnaba alisema kuwa, Mungu akibariki, watafanya kolabo moja ya ukweli mwakani.
“Kikubwa ni kumshukuru Mungu na kumuomba atufikishe salama lakini naamini kolabo langu na Ben Pol litakuwa ni la hatari sana, maana mafundi wanakutana, unadhani nini kitatokea kama siyo nyasi kuwaka moto,” alisema Barnaba.