Friday, 15 December 2017

Guardiola aweka rekodi kushinda tuzo ya kocha bora

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ameendelea kuweka rekodi katika ligi kuu ya soka nchini England (EPL) baada ya kushinda tuzo ya kocha bora wa mwezi Novemba.


Kwa kushinda tuzo hiyo leo, Guardiola sasa ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kuchukua tuzo hiyo mara tatu mfululizo. Mhispania huyo ameshinda katika miezi ya Septemba, Oktoba na Novemba ambayo ameshinda leo.

Pep amechukua tuzo hiyo leo akiwashinda waliokuwa wapinzani wake kwenye kuwania tuzo hiyo Antonio Conte, Sean Dyche, Jurgen Klopp, Jose Mourinho na Arsene Wenger.

Jumatano wiki hii Pep aliweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kushinda michezo 15 mfululuizo kwenye EPL na kuzikaribia rekodi zake mwenyewe ambazo amewahi kuziweka kwenye ligi za La Liga (16) na Bundesliga (19).

Ulega akamata tani 11 za samaki wakiandaliwa kusafirishwa nje

Mwanza. Naibu Waziri wa Uvuvi, Abdalla Ulega, leo Ijumaa amefanya ziara ya kushtukiza katika soko la kimataifa la samaki la Kirumba jijini Mwanza na kukamata tani 11 za samaki waliokuwa wakiandaliwa kusafirishwa nje ya nchi kinyume cha sheria.

Shehena hiyo ya samaki  ambao hawaruhusiwi kuvuliwa kisheria, wanadaiwa kuwa walitaka kusafirishwa kwenda nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) kupitia mpaka wa Rusumo mkoani Kagera.

Pamoja na kukamata samaki hao, naibu waziri huyo pia ameagiza kuondolewa mara moja kutoka sokoni hapo maofisa uvuvi kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waliokuwa na dhamana ya kusimamia ukaguzi katika soko hilo kwa kushindwa kutimiza wajibu.

Iniesta hana tatizo na Neymar kwenda Madrid

KIUNGO mkongwe wa Barcelona, Andres Iniesta amesema hana hofu kuhusu Neymar kujiunga na Real Madrid lakini akakiri kuwa ikitokea hivyo haitampendeza kutokana na uhusiano wa Neymar na mastaa wengine wa Barcelona wakati alipokuwa akiichezea timu hiyo.

Iniesta amecheza na Neymar kwa miaka minne kabla ya mchezaji huyo kuondoka na kuhamia Paris Saint- Germain lakini kumekuwa na taarifa za kuwaniwa kwa ukaribu na Real Madrid.
 “Chochote kinaweza kutokea kwenye soka, kuna mambo ambayo yalionekana ni magumu kutokea na yakatokea, sitashangaa lakini haitapendeza kwa kuwa kwa kuwa ni mchezaji mzuri lakini sina hofu,” alisema Iniesta.

Mwenyekiti wa zamani wa CCM apata dhamana

Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na wenzake watano wamefanikiwa kupata dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Ni baada ya Wakili wa Serikali, Shedrack Kimaro kuwasilisha cheti kutoka Kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ambapo kimeipa mamlaka mahakama hiyo ya Kisutu kusikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo, washtakiwa hao walisomewa mashtaka mapya matano mahakamani hapo leo Ijumaa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa.

Katika mashtaka hayo mawili ni ya kusambaza dawa bandia za kufubaza makali ya ukimwi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, uzembe wa kuzuia kosa kutendeka na kusababisha hasara.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa walikana na wapo nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili wanaominika, kila mdhamini akisaini bondi ya Sh 12 milioni.

Pia washtakiwa hao watoe fedha taslimu Sh 12 milioni ama mali isiyo hamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.
Facebook Tw

Diamond azidi kukimbiza Afrika Mashariki


Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.

Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.
 

Diamond azidi kukimbiza Afrika Mashariki


Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.

Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.

Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k , Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Kwa sasa wimbo wa ‘Waka’ unaweka rekodi ya kuwa wimbo wa kwanza kutrend namba moja kwa nchi tatu za Afrika Mashariki kwenye mtandao wa YouTube.

Video hiyo mpaka jana usiku ilikuwa ndiyo video inayotazamwa zaidi mtandaoni (Trending) kwa kushika namba moja kwa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania.

Wimbo wa ‘Waka’ awali ulipotoka ulikaa siku mbili kwenye mtandao wa YouTube hapa Tanzania  bila kukaa kwenye namba 1 ya video zinazotrend hapa nchini. Lakini mpaka sasa video ya wimbo huo yenye siku saba mtandaoni ipo namba moja kwenye Trending.

Awali rekodi ya video iliyotrend namba 1 kwa nchi mbili tofauti tofauti ilikuwa ilikuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB , Salome ya Diamond Platnumz na Video ya wimbo wa ‘Seduce Me’ wa Alikiba ambapo video zote wakati zinatoka zilishika namba moja Tanzania na Kenya kwa muda tofauti tofauti.

Komando Jide azidi kudata na Spicy


BAADA ya mwanadada ‘lejendari’ kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ kufanya vyema na Ngoma ya Together Remix akiwa na mpenzi wake, Spicy, staa huyo amejipanga kutengeneza naye ngoma tena.




BAADA ya mwanadada ‘lejendari’ kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ kufanya vyema na Ngoma ya Together Remix akiwa na mpenzi wake, Spicy, staa huyo amejipanga kutengeneza naye ngoma tena.

 Akizungumzia stori hiyo, Jay Dee alisema kwamba ameamua kurudi tena na Spicy na ngoma mpya ya Baby baada ya kolabo ya Together Remix kufanya vizuri ambapo anaamini itampeleka mbali zaidi kimuziki kuliko alipo kwa sasa.


“Nimeamua kumganda Spicy kwa sababu ninaamini ni mwanamuziki mzuri na muungano wetu huwa unafanya vizuri, angalia ngoma iliyopita na hii utagundua kwamba tunapokuwa pamoja tunatengeneza kitu kizuri sana,”alisema Spicy.

 Akizungumzia stori hiyo, Jay Dee alisema kwamba ameamua kurudi tena na Spicy na ngoma mpya ya Baby baada ya kolabo ya Together Remix kufanya vizuri ambapo anaamini itampeleka mbali zaidi kimuziki kuliko alipo kwa sasa.

Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza








Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza  tangu awasili wiki hii nchini Singapore kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.

Kiongozi huyo aliyekuwa  madarakani kwa miaka 37 ameonekana akiwa amezungukwa na walinzi wake huku kwa mbele akionekana mwanamke ambaye inaaminika atakuwa mke wake, Grace Mugabe.

Picha za tukio hilo zinamwonyesha akiwa amevalia shati jeupe na suruali nyeusi wakati mtu anayedhaniwa kuwa mke wake akiwa katika vazi jekundu na beki ya mkononi lenye rangi ya zambarau.










Mugabe ajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza

Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza  tangu awasili wiki hii nchini Singapore kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.

Kiongozi huyo aliyekuwa  madarakani kwa miaka 37 ameonekana akiwa amezungukwa na walinzi wake huku kwa mbele akionekana mwanamke ambaye inaaminika atakuwa mke wake, Grace Mugabe.

Picha za tukio hilo zinamwonyesha akiwa amevalia shati jeupe na suruali nyeusi wakati mtu anayedhaniwa kuwa mke wake akiwa katika vazi jekundu na beki ya mkononi lenye rangi ya zambarau.

Walinzi wake pia wameonekana kuvalia katika hali ya kawaida ikiwa mashati na suruali. Mara nyingi Mugabe pamoja na walinzi wake wa karibu huonekana wakiwa wamevalia suti isipokuwa wakati alipokuwa akishiriki shughuli za chama au katika sherehe za uhuru.

Canavaro kumbe hana wasiwasi na Simba

Beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema licha ya Simba kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, lakini bado kikosi chao kina nafasi kubwa ya kutetea ubingwa.

Canavaro amesema tofauti ya pointi mbili kati yao na Simba wanaongoza ligi ni kitu kilicho ndani ya uwezo wao kuiweza kuwashusha na sasa wanajipanga vyema kwa hatua hiyo.

Mkongwe huyo alisema mazoezi wanayofanya sasa ni maalum kwa kuhakikisha ligi itakavyoanza wanakuwa tayari ambapo endapo wenzao waliokuwa katika Micchuano ya Kombe la Chalenji watajiunga mapema watakuwa na maandalizi kamili kwa ligi.

Beki Yanga awapasha wakosoaji



 

Beki Yanga awapasha wakosoaji

Beki wa Yanga Juma Abdul amesema matokeo mabaya waliyopata kikosi cha Kilimanjaro Stars, Watanzania hatupaswi kulaumiana bali tunatakiwa kujiuliza tulipokosea.

Abdul ambaye amewahi kuitumikia timu hiyo, amesema hakuna sababu ya kuendeleza lawama kwa makocha na watu wengine, ambapo tathmini ya kina inatakiwa kufanyika kujua wapi tulipokosea kama nchi katika soka letu.

Aidha Abdul amesema bado hajafikiria kuitumikia timu ya taifa, lakini ataendelea kujituma ili kusubiri kuitwa kwa mara nyingine na makocha wa timu za taifa.


Askari mbaroni kwa kumuua mwenzake kisa 'mapenzi

Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia kwa mahojiano askari Magereza wa Gereza la Kisongo jijini Arusha, Koplo Faustine Masanja kwa tuhuma za kumuua mwenzake wakiwa kazini.

Akizungumza na Vyombo vya Habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa limetokea Desemba 14,2017 majira ya saa 2:00 asubuhi.

Kamanda Mkumbo amesema baada ya Masanja kumjeruhi mwenzake kwa risasi, alipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu ambako alifariki dunia.

Mkumbo ameahidi kutoa taarifa zaidi baada ya uchunguzi kukamilika ili kubaini chanzo na sababu za tukio hilo. Ingawaje taarifa za awali zinaonesha kuwa tukio hilo linaviashiria vya wivu wa mapenzi.

Pogba kurudi dimbani na muonekano mpya


Pogba kurudi dimbani na muonekano mpya 

 

Pogba kurudi dimbani na muonekano mpya

Mshambuliaji  wa Manchester United, Paul Pogba anayetumiakia adhabu ya kukosa mechi tatu, amegeukia mitindo ya nywele ambapo ameonekana akiwa amekoleza rangi kwenye kiduku chake.

Mchezaji huyo aliikosa mechi ya watani ya Manchester United na Manchester City Jumapili iliyopita na hakuwepo kabisa uwanjani. Pia ameikosa mechi ya United na Bournemouth.

Jana Alhamisi, mchezaji huyo mwenye mika 24 alituma picha yake akionyesha mtindo mpya wa nywele kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Hata hivyo, mchezaji huyo amekuwa akijifua mazoezi binafsi ili kuhakikissha anajiweka fiti na mechi zinazofuata.

Thursday, 14 December 2017

Haya ndio majina ya Askari wa JWTZ waliouawa DRC



Haya ni majina ya wanajeshi 14 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), waliouawa katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakati wakilinda amani.

Wanajeshi hayo ni  Hamad Haji Bakari, Chazil Khatibu Nandonde, Idd Abdallah Ally, Juma Mossi Ally,  Ally  Haji Ussi, Pascal Singo, Samwel Chenga, Deogratius Kamili, Mwichumu Vuai Mohamed, Hassan Makame, Issa Mussa Juma, Hamad Mzee Kamna, Salehe Mahembano na Nazoro Haji Bakari.

Tayari miili ya marehemu hao imeshaagwa katika viwanja vya ulinzi vilivyopo makao ya jeshi yaliyopo Upanga jijini Dar es Salaam na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na viongozi wa Serikali wengine waliongoza Watanzania kutoa heshima za mwisho kwa askari hao.

Askari hao 14 walifariki dunia katika mapigano na waasi wa kikundi cha ADF nchini DRC, huku 44 wakijeruhiwa na mmoja akipotea baada ya kambi yao kuvamiwa eneo la Mashariki mwa nchi Desemba 7 wakati wakitekeleza majukumu ya ulinzi wa amani.

Kinana awaonya Viongozi wanaowagawa Wananchi



Singida. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amewaonya viongozi wa chama hicho ambao amesema wanawagawa wananchi.

Amesema endapo wataendelea kufanya hivyo watavuliwa uongozi.

Kinana amesema hayo leo Alhamisi Desemba 14,2017 akifungua mkutano wa halmashauri kuu ya jimbo unaopiga kura ya maoni kupata mgombea ubunge jimbo la Singida Kaskazini.

Katika kinyang’anyiro hicho cha marudio wagombea 22 wamejitokeza kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Lazaro Nyalandu aliyejivua ubunge alioupa akiwa CCM na sasa amejiunga Chadema.

Amesema CCM ipo imara na wapambe wamepungua kwa kiasi kikubwa. Amewataka wagombea wafanye kampeni zinazofaa na mmoja akichaguliwa, wote wawe wamoja ili chama hicho kishinde kwa kishindo.

Kinana akizungumza katika mkutano huo unaofanyika Kijiji cha Ilongero, Singida amesema uchaguzi wa awali uligubikwa na vitendo vya rushwa ndipo uongozi wa juu wa CCM ulipoamua kufuta mchakato.

Ameagiza vitendo hivyo visijirudie akiwataka wajumbe wasirubuniwe kwa aina yoyote; na wagombea wakatae maombi ya wapiga kura ambao mara nyingi huwaambia unatuachaje.

Kinana amempongeza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Hassan Kilimba akisema amekuwa mwaminifu kwa chama hicho hata baada ya kuacha ubunge.