
Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross
kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na
kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.
Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.
Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na
nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k ,
Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio
unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika
Mashariki.
Wakati wimbo mpya wa Diamond Platnumz aliomshirikisha Rapper Rick Ross
kutoka Marekani unatoka haukuwa na nguvu kubwa pengine kutokana na
kuahirishwa kwa tarehe iliyotakiwa kutoka video ya wimbo.
Lakini hiyo haikuwa kigezo kikubwa kwa wimbo huo wa ‘Waka’ kwani ndani ya siku tatu ulikuwa tayari umefikisha views milioni 1.
Ukweli ni kwamba ‘Waka’ ulipata mapokezi ya kawaida ukilinganisha na
nyimbo nyingine za Diamond Platnumz kama Hallelujah, Salome, Kidogo n.k ,
Lakini kitu cha kushangaza wimbo huo kadri siku zinavyozidi kwenda ndio
unazidi kutazamwa zaidi sio tu Tanzania bali na nchi nyingine za Afrika
Mashariki.
Kwa sasa wimbo wa ‘Waka’ unaweka rekodi ya kuwa wimbo wa kwanza kutrend
namba moja kwa nchi tatu za Afrika Mashariki kwenye mtandao wa YouTube.
Video hiyo mpaka jana usiku ilikuwa ndiyo video inayotazamwa zaidi
mtandaoni (Trending) kwa kushika namba moja kwa nchi za Kenya, Uganda na
Tanzania.
Wimbo wa ‘Waka’ awali ulipotoka ulikaa siku mbili kwenye mtandao wa
YouTube hapa Tanzania bila kukaa kwenye namba 1 ya video zinazotrend
hapa nchini. Lakini mpaka sasa video ya wimbo huo yenye siku saba
mtandaoni ipo namba moja kwenye Trending.
Awali rekodi ya video iliyotrend namba 1 kwa nchi mbili tofauti tofauti
ilikuwa ilikuwa inashikiliwa na video ya wimbo wa ‘Zilipendwa’ wa WCB ,
Salome ya Diamond Platnumz na Video ya wimbo wa ‘Seduce Me’ wa Alikiba
ambapo video zote wakati zinatoka zilishika namba moja Tanzania na Kenya
kwa muda tofauti tofauti.