Monday, 11 December 2017

Tundu Lissu: Madaktari wamesema nitasimama na kutembea


Mbunge wa Singida Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu amefunguka na kusema kuwa ameambiwa na madaktari wake kuwa atasimama, atatembea na kurudi tena Tanzania kuendelea na majukumu yake kama kawaida.

Tundu Lissu amesema hayo leo alipofanya mahojiano na DW na kusema kuwa kwa sasa anaendelea vizuri kiafya na kuwa madaktari wamemweleza kuwa atasimama na kutembea tena kama zamani na kurudi nyumbani kwake Tanzania.

Aidha Tundu Lissu amesema hajapoteza matumaini ya kuwapata na kuwatambua watu ambao walishambulia kwa risasi kwa kuwa anaamini sehemu ambayo tukio hilo lilitokea kulikuwa na ulinzi na walinzi wa serikali.

"Matumaini hayajapotea kwa vile nakaa kwenye nyumba za serikali hizi nyumba zinalindwa masaa 24, Je, siku hizo napigwa risasi walinzi walikuwa wapi? Walinzi wa geti kubwa nao walikuwa wapi? Ile sehemu yote tunayoishi imezungushwa ukuta na kuna geti kuu lenye ulinzi masaa 24 nao walikuwa wapi? alihoji Tundu Lissu

Mbali na hilo Tundu Lissu ameelezea jinsi ambavyo tukio hilo lilitokea mnamo Septemba 7, 2017 pale Dodoma msikilize hapa chini akitolea maelezo hilo.

Hii ndio droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya



Droo ya Hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya maarufu kwa jina la Champions League imepangwa na kuna michezo mitatu ambayo imeonekana kuwavutia watu wengi.

Juventus wanatarajia kukutana na Tottenham Hotspur wakati ambapo wababe wa Hispania Real Madrid wao watakula sahani moja na wababe wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.

Ratiba hiyo inamaanisha kuwa staa wa PSG, Neyamr atakutana na Real Madrid kwa mara nyingine baada ya mchezaji huyo kukuna nao mara kadhaa lipokuwa akiitumikia Barcelona.

Gumzo zito ni juu ya  Chelsea wanaonolewa Kocha Antonio Conte ambapo wanatarajiwa kukutana na Barcelona.

Manchester City wao wataanzia ugenini ambapo huko watakipiga dhidi ya Basle wakati Porto wataikaribisha timu nyingine ya England, Liverpool katika hatua hiyo.

Sevilla wao wataanza nyumban I kuikaribisha Manchester United kabla ya timu hizo kurudiana wiki moja baadaye.

Michezo ya hatua hiyo itachezwa Februari, mwakani.

Ratiba kamili ya hatua hiyo ni hii hapa:
Juventus vs Tottenham Hotspur

Basle vs Manchester City

Porto vs Liverpool

Sevilla vs Manchester United

Real Madrid vs Paris Saint-Germain

Shakhtar Donetsk vs Roma

Chelsea vs Barcelona

Bayern Munich vs Besiktas

Pole Pole Amchana Lowassa



Humphrey Polepole ameibuka na kusema kuwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa serikali ya awamu ya nne Edward Lowassa alishindwa kuzuia Babu Seya asifungwe na kudai pia alishindwa mshawishi Mhe. Jakaya Kikwete ili awatoe watu hao.

Polepole amesema hayo baada ya watu kuanza kusema kuwa jambo alilofanya Rais Magufuli kuwatoa Babu Seya na mwanaye Papi Kocha ni jambo ambalo Lowassa aliahidi katika kampeni zake za 2015 kuwa endapo angechaguliwa kuwa Rais wa Tanzania angewaachia huru watu hao.

"Huyu mzee ambaye amezungumza kwamba hii ilikuwa ahadi yake kipindi cha kampeni ni mzee ambaye amehudumu kwenye serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kipindi ambacho Babu Seya anafungwa huyu mzee alikuwa Waziri Mkuu mwenye nguvu sana, kama alijua Babu Seya labda hakutendewa haki kwa namna yoyote kwa fikra zake angaliweza kumshauri Rais wake kipindi hicho kwamba huyu mtu hastahili kufungwa asamehewe" alisema Polepole

Polepole aliendelea kusisitiza kuwa Lowassa alishindwa kuzuia Babu Seya na watoto wake wasifungwe "Kashindwa kuzuia Babu Seya asifungwe, kashindwa mwaka wa kwanza kumshawishi Rais wake amsamehe Babu Seya, ameshindwa kufanya hivyo kwa miaka mingi iliyopita.

"Magufuli hakuwa kwenye nafasi ya uamuzi kipindi hicho alikuwa Waziri wa kawaida kabisa baada ya tafakuri ya kina ya miaka miwili akaona katika watu ambao wamejirudi huyu anastahili msamaha, huyo mzee anaibuka oohh nilifanya mimi, huyu mzee aache hizi tabia za kinafiki, kizandiki kwani Watanzania wanataka upinzani unaojenga hoja" alimalizia Polepole.

Babu Seya na mtoto wake Papii Kocha waliachiwa huru katika kifungo cha maisha jela baada ya Rais John Pombe Magufuli kuwapa msamaha katika siku ya Uhuru wa Tanzania bara, ambapo kila mwaka Disemba 9 zinafanyika sherehe za kumbukumbu.

Rais Kenyatta amuandikia barua Rais Magufuli



Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kupinga kitendo cha mauaji ya askari wake 15 waliokuwa wakilinda amani nchini Kongo, na kumpa pole kufuatia msiba huo mkubwa.

Katika barua hiyo, Rais Kenyatta amesema kushambuliwa kwa askari, ambao walikuwa wakihudumia kwa sababu nzuri ya kuanzisha amani ya kudumu nchini DRC ilikuwa mbaya, huku akiwapa pole watanzania na ndugu wa marehemu, na kuwaombea wale waliojeruhiwa waweze kupona haraka.

Uhuru Kenyatta ameendelea kwa kusema kwamba Kenya itaendelea kushirikiana na watu na serikali ya Tanzania katika kulinda amani ya Kongo na maeneo ya maziwa makuu, na kuangalia kesho bora ya maeneo hayo.

Rais Kenyatta amesema Kenya inathamini jukumu muhimu lililofanywa na watunza amani tangu imehusika katika mipango mingi ya kulinda amani.

Mwishoni mwa wiki iliyopita askari 15 wa Tanzania waliokuwa wakilinda amani nchini Kongo waliuawa na askari waasi wanaoendesha ampigano nchini humo, huku 44 wakijeruhiwa, 8 wakiwa mahututi na wawili hawajulikani walipo.


Babu wa Loliondo aoteshwa tena kikombe



Ngorongoro. Mchungaji Ambilikile Mwasapile maarufu Babu wa Loliondo aliyehudumia maelfu ya watu ndani na nje ya nchi kwa dawa aliyoitoa kwa kipimo cha kikombe amedai ameoteshwa kuwa umati utarudi kijijini Samunge kupata dawa.

Amesema ana uhakika wa jambo hilo kwa kuwa hata mwaka 2011 kabla ya maelfu ya watu kufika nyumbani kwake alioteshwa, hivyo amejiandaa kuweka miundombinu bora zaidi na hasa ujenzi wa vibanda atakavyovitumia kutoa huduma.

Mchungaji Mwasapile alisema hayo jana Jumapili Desemba 10,2017 mbele ya ujumbe wa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Joseph Kakunda aliyekuwa mkoani Arusha kukagua miradi ya maendeleo, ikiwemo ya kuwawezesha wananchi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Miongoni mwa waliofika kupata ‘kikombe’ kwa gharama ya Sh500 mwaka 2011 walikuwemo wafanyabiashara maarufu, wanasiasa na viongozi waandamizi serikalini.

Akizungumzia dawa yake anayodai inatibu maradhi mengi amesema kwa sasa anaitoa kwa watu wachache wanaofika kijijini hapo.

Miongoni mwao amesema ni watalii wanaofika kutembelea vivutio vya kitalii vilivyopo katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

"Huwa nawauliza watalii namna walivyoifahamu dawa yangu wanasema habari za ‘kikombe cha Babu’ imeenea katika nchi zao za Ulaya na Amerika," amesema Mwasapile.

Naibu Waziri wa Tamisemi, Kakunda akiwa na ujumbe wake baada ya kupata kikombe alimshukuru Mchungaji Mwasapile kwa alivyolifanya Taifa kujulikana na kusababisha maendeleo ya kijamii katika Kijiji cha Samunge.

Ametoa mfano wa barabara ya kutoka wilayani Longido na Kigongoni wilayani Monduli ambazo zimeboreshwa kutokana na idadi kubwa ya watu waliokuwa wakifika kupata huduma ya dawa.

Amesema hata huduma ya mitandao ya mawasiliano ya simu ilifika eneo hilo kwa haraka kutoka na watu wengi waliohitaji kuwasiliana na ndugu zao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Raphael Siumbu amesema Mwasapile amechangia shughuli za maendeleo kutokana na idadi kubwa ya waliokwenda kijijini hapo na kusababisha mzunguko wa fedha kuwa mkubwa.

Amesema watu wengi kijijini Samunge  wamepanda miti inayotumika kutengenezea dawa hivyo kuchangia utunzaji wa mazingira na huduma za kijamii kuongezeka.

Takukuru yamfikisha Mahakamani Sadifa kwa makosa mawili


Dodoma. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma imemfikisha mahakamani aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis.

Sadifa ambaye pia ni mbunge wa Donge, Zanzibar amefikishwa leo Jumatatu Desemba 11,2017 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma kwa makosa mawili.

Kamanda wa Takukuru mkoani Dodoma, Emma Kuhanga alisema jana Jumapili Desemba 10,2017 kuwa Sadifa angefikishwa mahakamani leo.

Alisema kiongozi huyo alikamatwa nyumbani kwake akituhumiwa kwa kuwapa soda wajumbe wa UVCCM kutoka Mkoa wa Kagera kitendo ambacho ni kinyume cha maadili.

Kuhanga akithibitisha kukamatwa kwa Sadifa alisema alikamatwa Jumamosi Desemba 9,2017.


VIDEO: Tanroad yasaini mikataba nane



Makampuni nane ya kichina yamesaini mikataba ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 402.97.

Kampuni hizo zimesaini mikataba hiyo na Wakala wa Barabarani TANROADS mbele ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof Makame Mbarawa.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI........USISAHAU KUSUBSCRIBE

VIDEO: UKAWA yafunguka kuhusu Serikali ya awamu ya tano



Umoja wa katiba ya wananchi UKAWA umesema kuwa umejiridhisha kuwa Serikali ya awamu ya Tano sio serikali ambayo inafuata utawala bora,  kuzingatia haki za binadamu huku ikivunja katiba.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSBUSCRIBE

Akizungumza na  waandishi wa habari, Mwenyekiti mwenza wa Umoja huo,  Freeman Mbowe amesema vipo viashiria vingi vinavyoonesha kuwa uongozi wa awamu ya Tano hauzingatii katiba ikiwemo kuzuia mikutano ya kisiasa Pamoja na kushambulia Kwa viongozi wa vyama vya upinzani.

" Serikali inabana wazi  kuzungumzia na kuikosoa,  hata nyinyi wandishi hampo Salama, ndio maana mwenzenu azory Mpaka sasa hajapatikana na serikali haijatoa tamko lolote" amesema Mbowe.

Mbowe pia alizungumzia uchaguzi mdogo wa madiwani ambapo Kata 43 zilifanya uchaguzi huku ccm ikishinda Kata 42 na Chadema walishinda moja.

Alisema viongozi  wao wakiwemo wabunge, madiwani na wagombea wa upinzani walikua wakikamatwa na kuwekwa ndani huku wasimamizi wao wakitolewa nje ya vyumba vya Kura jambo ambalo ni kinyume na katiba ya nchini.

Papa Francis, Guterres watoa maoni uamuzi wa Trump juu ya Israel



Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guterres amesema hatua ya rais Trump kuutambua mji wa Jerusalem kama makao makuu ya Israel inaleta wasi wasi katika jitihada za kuleta amani katika mzozo wa Israel na Palestina.
Akizungumza na CNN Guterres ametoa msimamo huo siku ambayo pia msemaji wa makamu wa rais wa Marekani Mike Pence ameishutumu serikali ya Palestina.
Msemaji huyo ameongeza hakufurahiswa na kitendo cha rais wa Palestina Mahmoud Abbas kushindwa kukutana na kiongozi huyo wa Marekani kwa sababu ya mzozo wa mji wa Jerusalem.
Waandamanaji wameendelea kukusanyika mitaani katika nchi za Kiaarabu wakipinga hatua hiyo ya raia Trump.
Naye Papa Francis ambaye ni kiongozi wa kidini wa wakatoliki wapatao billion moja duniani ametoa maoni yake,akisema kuwa Jerusalem ni mji mtakatifu kwa wakristo,Wayahudi na Waislam.
Amesema ni mazungumzo pekee yanayoweza kuleta suluhu katika mzozo huo wa Irael na Palestina.

Sunday, 10 December 2017

Video ya Babu Seya yampiku Diamond kwenye Trending za Youtube



Siku moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli kutangaza msamaha wa kumwachia huru Mkongwe wa Muziki wa Dansi nchini Nguza Viking 'Babu Seya'  na mtoto wake Johnson Nguza 'Papii Kocha' video yao wakionekana wanatoka gerezani imeshika namba moja kwenye Trending za Youtube hivyo kuishusha video mpya ya Diamond.

Video ya wimbo mpya wa Diamond aliomshirikisha mkali kutoka Marekani, Rick Ross unaokwenda kwa jina la Waka ulikuwa ukikamata nafasi ya kwanza lakini tangu Mtandao wa Muungwana Blog kuiweka video ya Seya na Papii wakitoka gerezani imejikuta ikifunika video zote.

Babu Seya na mwanae Papii Kocha ni miongoni mwa wafungwa zaidi ya 8000 waliopata msamaha wa Rais Magufuli jana katika sikukuu ya Uhuru ikiwa ni baada ya kukaa gerezani kwa takribani miaka 14 ambapo walikuwa wakitumikia kifungo cha maisha jela.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI....USISAHAU KUSUBSCRIBE

Mamia wauaga mwili wa Mwandishi wa Mwananchi



Mamia ya waombolezaji wamejitokeza kuaga mwili wa aliyekuwa mwandishi mwandamizi wa gazeti la Mwananchi, Joyce Mmasi.

Shughuli za kuaga mwili wa Joyce zimefanyika leo Jumapili Desemba 10,2017 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Ibada ya kuaga mwili iliongozwa na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Mbezi Luis, Richard Lucas.

Mchungaji Lucas amesema maisha aliyoishi Joyce yawe fundisho kwa waliobaki duniani.

"Binadamu tuna maisha mafupi ya kuishi duniani. Joyce aliyakabidhi maisha yake kwa Yesu, hivyo hakuna shaka kuwa yuko mahali salama," amesema.

Akizungumza katika shughuli hiyo, Mhariri  Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Bakari Machumu kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Francis Nanai amesema Joyce alikuwa mwandishi wa habari lakini pia mjasiriamali.

"Hili ni fundisho kwetu kwamba tunahitaji kuishi maisha ya kujiongeza maana Mmasi alikuwa mwanachama mzuri wa Saccos ya Mwananchi na alitoa mawazo ambayo yamesaidia maendeleo ya Saccos na kampuni," amesema.

Baada ya mwili wa Joyce kuagwa umesafirishwa kuelekea kijijini kwao Mbokomu wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro kwa mazishi yatakayofanyika kesho Jumatatu Desemba 11,2017.

Joyce alifariki dunia usiku wa kuamkia  Jumatano Desemba 6,2017 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Andrew Kamugisha ambaye ni mume wa Joyce alisema mkewe alifariki saa kumi usiku katika Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Alisema Joyce aligundulika kuwa na saratani ya damu. Alisema kutokana na tatizo hilo, utengenezaji wa damu ikiwemo rojorojo lililoko katika mifupa (bone marrow) na hivyo kusababisha mfumo wa chembe hai kutofanya kazi inavyotakiwa.

Mwananchi

Peter Stoger aula kibarua cha kuinoa Dortmund



Klabu ya Borussia Dortmund leo tarehe 10 Novemba 2017, imeushangaza ulimwengu wa soka baada ya kutangaza kumfukuza kazi kocha wake, Peter Bosz na kumuajiri Peter Stöger.

Peter Bosz amepoteza michezo 12 tangu ajiunge na klabu hiyo na kitu pekee cha kushangaza ni kwamba Dortmund wamemuajili kocha ambaye ametimuliwa na klabu ya inayoshika mkia wa ligi kuu nchini Ujerumani Bundesliga.

Kuchaguliwa kwa Peter  Stöger kumezua gumzo kubwa nchini Ujerumani kwani wadau wengi wa soka wanasema Dortmund wamekosea kumsajili Kocha ambaye mwenye historia mbaya kwenye kufundisha timu za Ujerumani.

Peter Stoger amepoteza mechi 8 na kupata sare 3 kabla ya kutimuliwa na klabu ya FC Cologne ambayo inashika mkia kwenye msimamo wa Bundesliga. Ambapo imeelezwa kuwa ndio kocha wa kwanza kuanza vibaya kwenye tangu ligi hiyo ianzishwe.

Na hii inakuwa ni hatua ya kwanza kwenye historia ya Ligi kuu nchini Ujerumani kwa kocha mwenye karba hiyo kuajiliwa na klabu kubwa nchini humo.

Msuva kucheza dhidi ya Yanga Klabu Bingwa?




Utamu wa vita ni kumjua adui yako, Yanga inajiandaa na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayoanza mwakani mmoja wa wapinzani wake katika kusaka taji hilo ni mshambuliaji wake wa zamani, Simon Msuva anayecheza Difaa El Jadidi ya Morocco.

Shirikisho la Soka Afrika (CAF) linataraji kutangaza ratiba ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika Jumatano ijayo Desemba 13 jijini Cairo, Misri kwa michuano hiyo itakayoanza mwanzoni mwa Februari na kumalizi Novemba mwakani bingwa atajinyakulia dola 2.5 milioni.

Yanga chini ya kocha, George Lwandamina imedhamiria kufanya vizuri katika michuano hiyo na tayari imeanza kufanya usajili wachezaji mbalimbali wa kimataifa ili kutimiza lengo hilo.

Mabingwa hao wa Tanzania Bara, Yanga itaanza Ligi ya Mabingwa hatua ya awali kama ilivyokuwa kwa Difaa El Jadidi inayoshiriki mashindano hayo kwa mara kwanza tangu 2010 ilipotolewa katika raundi ya kwanza.

Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani hatua ya makundi itashirikisha timu 16, zitakazogawanywa katika makundi manne, kutokana na mabadilino hayo Yanga inaweza kupata nafasi ya kucheza dhidi ya Msuva katika hatua ya awali, au raundi ya pili kama siyo hatua ya makundi.

Msuva amekuwa katika kiwango kizuri tangu Julai 28, 2017, alipotua Difaa El Jadidi akifanikiwa kufunga jumla ya mabao 15 katika mechi zote. Msuva amefunga mabao tisa katika mechi 13 za kirafiki, mabao mawili katika Kombe la Mfalme katika Ligi Kuu Morocco ‘Batola Pro’ amefunga mabao 4, katika mechi 10.

Akizungumzia ratiba hiyo Msuva alisema sitamani tupangwe dhidi ya Yanga hata kidogo, lakini ikitokea hivyo nitawajibika kuipigania Difaa.

“Ukweli ni kwamba Yanga ni timu yangu, imenilea mpaka kufikia hatua ya kuhitajika na timu kadhaa kubwa barani Afrika, lakini Difaa nipo ni kazi si kingine.

“Pamoja na huku, lakini nimekuwa nikiwasiliana mara kwa mara na wachezaji wa Yanga, hii inaonyesha namna gani ambavyo bado ni kama nipo Yanga vile, ndiyo maana nikatangulia kusema sitamani tupangwe pamoja.

“Ila yote kwa yote ya uwanjani yatabakiwa kuwa ya uwanjani na sidhani kama yataharibu mahusiano yangu na Yanga, naipenda sana Yanga na itabaki kuwa timu yangu,” alisema Msuva.

Mbali ya Diffa El Jadidi timu nyingine zitakazokuwa kikwazo kwa Yanga katika kufuzu kwa hatua ya makundi pamoja na ubingwa ni mabingwa watetezi, Wydad Casablanca ya Morocco, mabingwa wa kihistoria Al-Ahly, na Misr Lel-Makkasa (zote za Misri).

Miamba mingine kiboko ya Yanga katika mashindano hayo ni Esperance de Tunis na Etoile du Sahel (Tunisia), kutoka DR Congo ni TP Mazembe na AS Vita Club wakati Algeria imetoa timu za ES Setif na MC Alger.

Afrika Kusini inawakilishwa na Bidvest Wits na Mamelodi Sundowns wakati Sudan watakuwa na timu za Al-Hilal, Al-Merrikh.

Naye kocha wa Yanga, Lwandamina akizungumza na gazeti dada la Mwanaspoti alisema: “Nimeziona hizo timu nazifahamu si kwa kubahatisha ni timu ngumu, lakini ubora wao zaidi unatokana na nguvu ya fedha wanayotumia kufanya maandalizi yaliyobora kabla ya mashindano.

“Najua tutashindana nao japo sijajua tutakutana na timu zipi ila katika maandalizi ni bora tukaangalia kwa ujumla washindani wetu, tunahitaji kuangalia upana na ubora wa kikosi chetu nafikiri hapa ndiyo kwenye kazi,” alisema Lwandamina.

Kama Yanga itapagwa kwenda Ivory Coast itacheza dhidi ya ASEC Mimosas au Williamsville AC.

Kutoka Zambia kutakuwa na ZESCO United na Zanaco wakati Congo kutakuwa na timu za AC Leopards, na AS Otoho. Mali watawakilishwa na timu za Stade Malien na AS Real Bamako huku Nigeria ikiwa na timu za Plateau United, na MFM.

Mbali ya miamba hiyo Yanga anatarajia kupata ushindani mkubwa wa kufuzu kwa hatua ya makundi kutoka kwa Eding Sport ya Cameroon, Al-Tahaddy (Libya), Aduana Stars (Ghana), 1º de Agosto (Angola), Saint George (Ethiopia) na Township Rollers (Botswana).