Sunday, 10 December 2017

Audio | Msaga Sumu – Mwache Adange | Mp3 Download

Audio | Msaga Sumu – Mwache Adange | Mp3 Download

Audio | Msaga Sumu – Mwache Adange | Mp3 Download

DOWNLOAD

Tundu Lissu afunguka



Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu ambaye anaendelea na matibabu nchini Kenya jijini Nairobi amefunguka na kusema kuwa wanaendelea kupigana na watashinda vita hiyo.

Lissu amesema hayo baada ya kukutana na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa CUF, Ismail Jusa Ladhu alipomtembelea jijini Nairobi katika hospitali anayopatiwa matibabu kufuatia kushambuliwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.

"Leo nina furaha sana kwa kupata fursa ya kumtembelea sahib na ndugu yangu, Tundu Lissu, Nairobi Hospital anakoendelea kupata matibabu baada ya kupigwa risasi zipatazo 16 mwilini Septemba 7, mwaka huu. Amenambia nikufikishieni ujumbe huu: "We keep up the fight and we shall win" alindika Jussa kwenye mtandao wake wa twitter

Mbali na hilo Jussa amedai kuwa afya ya Tundu Lissu kwa sasa inaendelea vizuri sana

"Anaendelea vizuri sana. Mimi leo nilivyomuona sikuamini jinsi anavyopata nafuu. Kwa hakika ni Qudra ya Mwenyezi Mungu. Tuendelee kumuombea dua apone haraka arudi kwenye shughuli zake"

FULL VIDEO: Babu Seya na Papi Kocha wakitoka Gerezani



Mwanamuziki Mkongwe Nchini Nguza Viking ' Babu Seya' na mwanae Papii Kocha leo wameachiwa huru gerezani walipokuwa wakitumikia kifungo cha maisha jela. Babu Seya na Papii ambao walihukumiwa kifungo hicho mwaka 2004 ni miongoni mwa wafungwa zaidi ya 8000 waliopata msamaha huo katika siku ya Uhuru kutoka kwa Rais Dk John Magufuli.
TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE


Wakili wa Babu Seya afunguka



Wakili Mabere Marando aliyekuwa akimtetea mwanamuziki mkongwe nchini, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’, amesema uamuzi wa Rais John Magufuli kuwasamehe umekuwa ni ‘surprise’ (jambo la kushtukiza) kwake.

Babu Seya na Papii Kocha ambaye pia ni maarufu kama Mtoto wa Mfalme walikuwa wakitumikia kifungo cha maisha jela kwa kosa la kuwabaka na kuwalawiti watoto 10 wa kike ambao walikuwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Mashujaa, Sinza Dar es Salaam.

Tayari walishatumikia kifungo hicho kwa miaka 13 na miezi minne.

Wakili Marando ambaye aliwatetea katika rufaa yao ya pili Mahakama ya Rufani alisema uamuzi wa Rais Magufuli umemshangaza na ameupokea kwa furaha kubwa.

Marando ambaye alifanikiwa kuwatoa kifungoni watoto wawili wa Babu Seya, Mbangu na Francis katika rufaa hiyo alisema hakutarajia uamuzi kama huo.

“Asante sana, asante sana, asante sana, namshukru sana Rais Magufuli kuwasamehe, kwa kweli sikutarajia hili. Hii imekuwa ni surpirise, asante sana,” alisema Wakili Marando ambaye alikuwa hajapata taarifa za uamuzi huo hadi alipoulizwa na mwandishi wetu.

Mwananchi:

Wakili wa Babu Seya afunguka


Wakili Mabere Marando aliyekuwa akimtetea mwanamuziki mkongwe nchini, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’, amesema uamuzi wa Rais John Magufuli kuwasamehe umekuwa ni ‘surprise’ (jambo la kushtukiza) kwake.

Babu Seya na Papii Kocha ambaye pia ni maarufu kama Mtoto wa Mfalme walikuwa wakitumikia kifungo cha maisha jela kwa kosa la kuwabaka na kuwalawiti watoto 10 wa kike ambao walikuwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Mashujaa, Sinza Dar es Salaam.

Tayari walishatumikia kifungo hicho kwa miaka 13 na miezi minne.

Wakili Marando ambaye aliwatetea katika rufaa yao ya pili Mahakama ya Rufani alisema uamuzi wa Rais Magufuli umemshangaza na ameupokea kwa furaha kubwa.

Marando ambaye alifanikiwa kuwatoa kifungoni watoto wawili wa Babu Seya, Mbangu na Francis katika rufaa hiyo alisema hakutarajia uamuzi kama huo.

“Asante sana, asante sana, asante sana, namshukru sana Rais Magufuli kuwasamehe, kwa kweli sikutarajia hili. Hii imekuwa ni surpirise, asante sana,” alisema Wakili Marando ambaye alikuwa hajapata taarifa za uamuzi huo hadi alipoulizwa na mwandishi wetu.

Mwananchi

Mnyika awaombea askari 14 wa JWTZ



Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amejitoa na kuwaombea askari 14 wa JWTZ ambao wamefariki dunia nchini Congo wakati wakilinda amani huku askari wengine 44 wakiwa wamejeruhiwa.

Mbunge wa Kibamba ameitumia Jumapili ya leo Disemba 10,2017  kuwaombea mashujaa hao na kuwapa pole wanafamilia wote ambao ndugu zao wamepoteza maisha katika tukio hilo.

"Kwa kipekee naitoa ibada ya leo kuwaombea Mashujaa wetu,askari 14 wa JWTZ waliojitoa mhanga na maisha yao kuitetea amani Congo, 44 ambao wamejeruhiwa na wale wawili (2) ambao hawajulikani walipo. Mungu awajalie pumziko jema kwa wale waliopoteza uhai kupigania amani"
Mnyika aliendelea kusema kuwa
"Awape uponyaji majeruhi na kusaidia kupatikana kwa Askari wawili. Aijalie faraja na ustawi familia za wahanga na wote ambao wameguswa kwa moja kwa moja au namna ingine yeyote na tukio baya hilo" aliandika John Mnyika 

Wachezaji Zanzibar Heroes kupimwa mkojo kama wanatumia dawa



Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) yaingiwa na hofu kwa kiwango bora wanachoonyesha timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) katika Mashindano ya Cecafa Senior Chalenj Cup yanayoendelea nchini Kenya.

Hofu hiyo imekuja jioni ya leo katika uwanja wa Kenyatta Mjini Machakos mara baada ya kutoka sare ya 0-0 na Wenyeji Kenya na kupelekea Zanzibar kutinga moja kwa moja nusu fainali wakiwa na alama 7 wakiongoza kundi lao A lenye Mataifa kama Kenya, Libya, Rwanda na kaka zao Tanzania bara.

Baadhi ya wajumbe wa CECAFA wakiongozana na wakaguzi wanaopinga dawa za kuongeza nguvu Michezoni walikwenda kwenye vyumba vya kubadilisha nguo vya Zanzibar Heroes kwa kusema haiwezekani timu ya Zanzibar icheze michezo mitatu mfululizo bila ya kuonekana kuchoka.

“Mechi tatu mfululizo Zanzibar wanacheza kwa kiwango bora, tena wachezaji wao ndo wale wale kila siku wanaoanza labda abadilike mmoja tu, itakuwa wanatumia dawa za kuongeza nguvu lazima wachunguzwe”. Alisema mmoja wa Afisa.


Uongozi wa Zanzibar Heroes ukakubali wachezaji wake kwenda kupimwa kama kweli wanatumia dawa za kuongeza nguvu au kiwango chao tu,ukatokea mtafaruku baina yao wenyewe viongozi wa CECAFA na mwisho wakakubali kuwaachia wachezaji hao waende zao wachezaji ambao walishangazwa mno kusikia kuwa wanatumia dawa.

Mbunge Lema atuma ombi hili kwa Rais Magufuli



 Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. John Magufuli kuwafuatilia mahabusu waliokaa magereza muda mrefu bila kesi zao kukamilika.

Mh. Lema amefunguka hayo kwenye ukurasa wake Twitter ambapo amechukua hatua hiyo baada ya kumshukuru rais Magufuli kwa kitendo cha kutoa msamaha kwa watu 8157.... waliokuwa wamehukumiwa katika magereza tofauti nchini.

"Mh Rais Magufuli, Mungu akubariki sana kwa msamaha uliotoa jana kwa wafungwa haswa wale waliokaa magereza muda mrefu pamoja na wazee, msamaha ni ibada, pia wako mahabusu wamekuwa magereza kwa muda mrefu sana bila kesi zao kukamilika. Mh Rais fuatilia watu kama hawa pia" Lema.

Jana katika maadhimisho ya siku ya Uhuru wa miaka 56 ya Tanganyika yaliyofanyika Mkoani Dodoma Rais Magufuli alitangaza  msamaha kwa wafungwa 8,157.  ambapo baada ya msamaha huo, 1828 watatakiwa kuondoka Magereza kabisa na wengine 6329 wamepunguziwa muda wa kukaa gerezani.


Takukuru yamshikilia mwenyekiti wa UVCCM



Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma inamshikilia Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis kwa tuhuma za kugawa rushwa kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa uchaguzi.

UVCCM leo Jumapili Desemba 10,2017 inachagua viongozi wapya wa ngazi ya Taifa watakaoongoza jumuiya hiyo ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano.

Sadifa ambaye pia ni mbunge wa Donge, Zanzibar amekamatwa nyumbani kwake karibu na mnada wa zamani mkoani Dodoma.

Kamanda wa Takukuru mkoani Dodoma, Emma Kihanga amethibitisha kukamatwa kwa mwenyekiti huyo na kwamba watatoa taarifa zaidi baadaye.

"Ni kweli tumemkamata tangu jana usiku tumekesha tunafanya uchunguzi, nitatoa taarifa baadaye kuhusu tukio hilo," amesema.

Mkutano mkuu wa uchaguzi wa UVCCM unaendelea mjini Dodoma na miongoni mwa waliohudhuria ni Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akifunga mkutano mkuu wa uchaguzi wa Umoja wa Wanawake (UWT) jana Jumamosi Desemba 9,2017 alisema hawajapokea malalamiko mengi kutoka umoja huo na kuzitaka jumuiya nyingine za CCM kujifunza UWT.

Manchester United v Manchester City, nani kutoka kifua mbele leo


Manchester United wanawakaribisha majirani zao Manchester City hii leo katika mchezo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa sana, vilabu hivi viwili vinaongoza mbio za ubingwa jambo ambalo linaufanya mchezo huu kuwa mgumu sana.

Mchezo hii sio mrahisi kwa upande wowote ule na United wamepoteza michezo saba kati ya michezo kumi na mbili ambayo wamekutana na katika siku za hivi karibuni Man City wanaonekana kuimarika kuliko United.

Derby ya leo ni tofauti sana na derby nyingi zilizopita kati ya timu hizi kwani kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2013 Manchester United na Manchester City zinakutana huku wakiwa katika nafasi mbili za juu.

Wakati City wakiwa wamefunga mabao mengi ugenini (27) msimu huu, wenzao United wanaringa na rekodi ya uwanja wao wa nyumbani ambapo michezo 42 hawajafungwa huku wakiwa wameshinda 30.

Jose Mourinho anaonekana kuijenga na kuiimarisha sana United katika eneo lao la ulinzi ambapo hadi sasa wameruhusu nyavu zao kuguswa mara 9 tu katika uwanja wao wa Old Traford msimu huu.

Tayari Manchester City wameshashinda michezo 13 mfululizo na kama watakwenda kushinda mchezo wa leo dhidi ya United baasi wataifikia rekodi waliyoweka Arsenal 2001/2002 ya kushinda michezo 14 mfululizo.

Lakini Jose Mourinho ana rekodi mbovu mbele ya Pep Gurdiola ambapo michezo 19 waliyokutana Mou ameshinda 4 tu na tena ni mchezo 1 tu wa ligi alioshinda, akisuluhu 7na vipigo 8.

Mkuu wa mkoa aagiza waliotia mimba wanafunzi 20 wakamatwe



MKUU wa Mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo ameitaka polisi mkoani humo kuwakamata watu waliowatia mimba wanafunzi 20 ambao walishindwa kufanya mitihani yao ya kumaliza darasa la saba mwaka huu.

Aliyasema hayo mjini Kibaha wakati wa kikao cha bodi ya uteuzi wa wanafunzi waliofaulu na wanaojiunga kidato cha kwanza mwaka 2018 na kuongeza kuwa wanafunzi hao wa kike ndiyo walioshindwa kufanya mitihani yao ya kumaliza darasa la saba kutokana na kupata ujauzito kwenye mkoa huo.

“Naagiza polisi kuwakamata watu hao waliowatia mimba wanafunzi wakashindwa kufanya mitihani yao ya kumaliza darasa la saba mwaka huu,” alisema Ndikilo na kuongeza kuwa sheria ziko wazi kwa wanaowatia mimba wanafunzi hivyo wahusika hao wakamatwe wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma hizo.

Alisema haiwezekani kuwakalia kimya wahusika kwani wamewaharibia maisha watoto hao ambao ndoto zao zimeyeyuka kwa kukatishwa na watu wasio na utu hivyo.

Mvua yaharibu makazi Mtwara



Baadhi ya wakazi wa Kiangu na Chuno mjini Mtwara wamelazimika kuyahama makazi yao yaliyojaa maji baada ya mvua kunyesha.

Mvua ilinyesha usiku wa kuamkia jana Jumamosi Desemba 9,2017 saa nane usiku pasipo kukata hadi saa kumi na moja jioni. Mvua ilikata kwa muda na kuendelea kunyesha usiku hadi leo Jumapili Desemba 10,2017.

Katika maeneo hayo MCL Digital imeshuhudia wananchi wakiokoa mali zao ambazo zilikuwa zimelowa.

Miongoni mwa mali zilizoharibika ni magodoro, samani, majokofu na televisheni.

Baadhi ya vijana wamekuwa wakiwasaidia wazee kuhamisha mali na kuwaondoa maeneo yaliyozingiwa maji.

Mkazi wa Kiangu, Edith Mboni ameiomba Serikali kujenga mitaro itakayopeleka maji baharini ili kuwaondolea adha hiyo.

Amesema mtaro uliopo ni mdogo hivyo kutokana na wingi wa maji unashindwa kuhimili.

Mkazi mwingine, Hassan Mbarali  ameiomba Serikali kujenga miundombinu imara ili kuwaepusha na maafa ambayo yamekuwa yakijirudia mvua kubwa inaponyesha.

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Desemba 8,2017 ilitoa taarifa kwa umma ikieleza kuwapo vipindi vya mvua kubwa katika  maeneo ya ukanda wa Pwani.

Maeneo hayo ni mikoa ya Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Mtwara. Pia,  visiwa vya Unguja na Pemba.

Viongozi wakuu wa TFF kumzika Bendera



Viongozi wakuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Rais Wallace Karia na Makamu Rais Michael Wambura wataongoza ujumbe wa shirikisho katika mazishi Kocha wa zamani wa Taifa Stars, marehemu Joel Nkaya Bendera.

Bendera aliyefariki dunia Desemba 6, mwaka huu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, atazikwa leo Jumapili Desemba 10, 2017 makaburi ya Kijiji cha Manundu, Korogwe mkoani Tanga.

Ujumbe huo pia utamjumuisha Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la TFF, Mhe. Mohammed Abdulaziz, Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madadi, Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Vedastus Lufano pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Kanda ya 12 (Mikoa ya Tanga na Kilimanjaro), Khalid Mohammed.

Khalid Mohammed atakuwa na wenyeji wengine ambao ni viongozi wa mpira wa miguu mkoa na wilaya za Tanga ambao wataungana familia pamoja na waombolezaji wengine kumpumzisha Mbunge huyo wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1995 hadi 2005) katika Jimbo la Korogwe Mjini.

Mwili wa marehemu Bendera umeagwa Jumamosi Desemba 9, mwaka huu asubuhi kwenye Viwanja vya Hospitali ya Jeshi la Lugalo, Dar es Salaam. Enzi zake Joel Nkaya Bendera alifikia cheo cha Naibu Waziri Michezo mbali ya kuongoza mikoa ya Morogoro na Manyara kwa cheo cha Mkuu wa  mkoa.