Sunday 10 December 2017

Manchester United v Manchester City, nani kutoka kifua mbele leo


Manchester United wanawakaribisha majirani zao Manchester City hii leo katika mchezo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa sana, vilabu hivi viwili vinaongoza mbio za ubingwa jambo ambalo linaufanya mchezo huu kuwa mgumu sana.

Mchezo hii sio mrahisi kwa upande wowote ule na United wamepoteza michezo saba kati ya michezo kumi na mbili ambayo wamekutana na katika siku za hivi karibuni Man City wanaonekana kuimarika kuliko United.

Derby ya leo ni tofauti sana na derby nyingi zilizopita kati ya timu hizi kwani kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2013 Manchester United na Manchester City zinakutana huku wakiwa katika nafasi mbili za juu.

Wakati City wakiwa wamefunga mabao mengi ugenini (27) msimu huu, wenzao United wanaringa na rekodi ya uwanja wao wa nyumbani ambapo michezo 42 hawajafungwa huku wakiwa wameshinda 30.

Jose Mourinho anaonekana kuijenga na kuiimarisha sana United katika eneo lao la ulinzi ambapo hadi sasa wameruhusu nyavu zao kuguswa mara 9 tu katika uwanja wao wa Old Traford msimu huu.

Tayari Manchester City wameshashinda michezo 13 mfululizo na kama watakwenda kushinda mchezo wa leo dhidi ya United baasi wataifikia rekodi waliyoweka Arsenal 2001/2002 ya kushinda michezo 14 mfululizo.

Lakini Jose Mourinho ana rekodi mbovu mbele ya Pep Gurdiola ambapo michezo 19 waliyokutana Mou ameshinda 4 tu na tena ni mchezo 1 tu wa ligi alioshinda, akisuluhu 7na vipigo 8.

No comments:

Post a Comment