Saturday, 9 December 2017

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day



DOWNLOAD

MTL Waanika Sababu za Kupotea kwa Mwandishi Azory Gwanda!

MTL Waanika Sababu za Kupotea kwa Mwandishi Azory Gwanda!


FULL VIDEO:Makomandoo Wakishuka kwenye Helkopta katika Maonesho ya Miaka 56 ya Uhuru

FULL VIDEO:Makomandoo Wakishuka kwenye Helkopta katika Maonesho ya Miaka 56 ya Uhuru

BREAKING NEWS: Babu Seya, Papii Kocha Waachiwa Huru kwa Msamaha wa JPM

BREAKING NEWS: Babu Seya, Papii Kocha Waachiwa Huru kwa Msamaha wa JPM



BABU SEYA AACHIWA HURU NA RAIS MAGUFULI LEO!

BABU SEYA AACHIWA HURU NA RAIS MAGUFULI LEO!


BREAKING: JPM ameagiza kuachiwa huru kwa Babu Seya na Familia yake


Maadhimisho ya Miaka 56 ya Uhuru - DODOMA


RC aagiza kusakwa kwa mwanaume aliyepanga njama za kumuua mkewe



Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanry ameliagiza Jeshi la polisi mkoani humo kumsaka na kumtia nguvuni mwanaume mmoja mkazi wa wilaya ya Urambo anaedaiwa kupanga njama za kumuua mke wake kwa kutumia jambazi ambae hakuweza kutimiza jukumu hilo.

RC Mwanry ametoa agizo hilo katika kilele cha kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizofanyika katika uwanja wa Chipukizi mkoani humo zilizoandaliwa na kituo kimoja cha redio mkoani humo.

Kituo hicho baada ya kuandaa kampeni hiyo kilirekodi mkasa wa huyo mama aliofanyiwa na mumewe na kukiweka kipande hicho cha sauti kwenye redio. Huku mama huyo hakutakiwa kuonekana kwasababu za usalama wake.

Kufuatia kusikika kwa mama huyo redioni ndipo RC huyo akatoa maagizo kwa jeshi la polisi kumsaka popote alipo.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kufuatia kuuawa kwa askari 14 DRC


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha askari 14 wa Jeshi la JWTZ kuuawa walipokuwa katika operesheni ya kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).



Waziri Kigwangalla ateua kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Tanzania



Waziri wa Maliasili na Utalii Dk.Hamisi Kigwangalla  jana Desemba 8,2017 Mjini Dodoma, ameunda kamati ya kuongoza maandalizi ya namna watanzania na wageni wa Tanzania watakavyosherehekea Utanzania wao  kwenye mwezi maalum utakaojulikana kama ‘TANZANIA HERITAGE MONTH’.

Akielezea wakati wa kutangaza kamati hiyo iliyojumlisha wadau mbalimbali wakiwemo wanahabari, wanamichezo na wadau wengine mbalimbali na wafanyabishara, alisema:

“Kwenye mwezi huu kila kitu kitakuwa cha kitanzania na tutataka kwenye kila ofisi ya umma, ofisi binafsi, shule, chuo, hotel, balozi zetu n.k mtu akifika tu, ‘utanzania’ wetu uonekane!” alieleza Dk.Kigwangalla.

Utanzania huo ambapo kila mwezi huo utakapofika ambapo moja ya mambo hayo ni pamoja na aina ya mavazi maalum, vyakula,  na mambo mengine yanayobeba na kujumuisha Utanzania.


Zitto Kabwe azungumzia hatima ya ACT- Wazalenddo



Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe amefunguka kuwa  ndani ya chama chake (ACT) kuna watu wengi wakiwemo wanachama wa kutosha  akimaanisha hajabaki mwenyewe.

Zitto amefunguka hayo akimjibu mfuasi wake wa kwenye mtandao wa kijamii ambaye alitoa maoni yake kwa kumuuliza Mh. Kabwe haoni kama amebaki peke yake, ikiwa ni muda mfupi baada ya aliyekuwa Mgombea urais wa chama chake Anna Mghwira kujiunga na CCM huko Dodoma.

Akimjibu mfuasi huyo Zitto amesema "Chama chetu ACT Wazalendo kina madiwani 42, kina wenyeviti wa mitaa, vitongoji na wajumbe wa Serikali za Vijiji/Mitaa 507, Viongozi kila mkoa na jimbo, wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu. Ni dhahiri tuna watu wengi na wanachama wengi wa kutosha"

Hivi karibuni CCM ilijivunia wanachama wapya ambao waliwahi kuwa na nafasi ya uongozi ACT Wazalendo ambapo baadhi yao ni Prof Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba, Alberto Msando na jana  Anna Mghwira.

Wabunge wa Chadema waachiwa kwa Dhamana



Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro imetupilia mbali hati ya kiapo cha kupinga dhamana ya wabunge Suzan Kiwanga(Mlimba), Peter Lijualikali (Kilombero) na washtakiwa wengine 37 waliofikishwa mahakamani hapo kwa makosa nane.

Mbele ya Hakimu, Ivan Msaki mahakama ilitupilia mbali kiapo hicho na kueleza kuwa washtakiwa wote dhamana yao iko wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili kila mmoja watakaosaini dhamana ya Sh 5 milioni na pia barua za dhamana lazima zisainiwe na wenyeviti wa vijiji ama maofisa watendaji.

Katika kiapo kilichowasilishwa awali mahakamani hapo na upande wa mashtaka kupitia wanasheria wa Serikali, Sunday Hyera na Edga Bantulaki ulieleza sababu walizodai kuwa ni za msingi za kupinga dhamana na kwamba kuwepo nje kwa washtakiwa  kunaweza kuharibu upelelezi wa kesi hiyo.

Kufuatia hoja hiyo upande wa utetezi unaowakilishwa na mawakili wanne wakiongozwa na wakili Peter Kibatala uliamua kuwasilisha hati ya kupinga kiapo hicho kwa madai kuwa  kiliandikwa bila ya kuzingatia misingi na matakwa ya kisheria.

Wakili Kibatala alidai kuwa miongoni mwa mapungufu yaliyokuwemo kwenye kiapo hicho ni pamoja na kutokuonyesha majina ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Malinyi (OCD) ambaye alitajwa kwenye kiapo hicho kama chanzo kilichotoa taarifa zilizotengeneza mashtaka yanayowakabili wabunge hao na wenzao.

Alidai kuwa mapungufu mengine yaliyokuwepo kwenye kiapo hicho ni utofauti wa tarehe ya kuandika kiapo hicho na kusainiwa na hivyo waliiomba mahakama kuzingatia mapungufu hayo.

Kutokana na mvutano huo wa kisheria baina ya pande hizo mbili Hakimu Msaki aliamua kupitia hoja za msingi za kisheria na hivyo kubaini mapungufu yaliyopo kwenye kiapo hicho na kueleza kuwa mapungufu hayo hayawezi kurekebishwa na kwamba kazi ya mahakama ni kutafsiri sheria na si kufundisha namna ya kuandika kiapo.

Kwa msingi huo Hakimu Msaki alitupilia mbali hati hiyo ya kiapo cha kupinga dhamana na kueleza kuwa washtakiwa hao watakuwa nje kwa dhamana wakati kesi yao ikiendelea.

Kabla ya kupewa dhamana washtakiwa hao walikaa rumande kwa siku 12 hali iliyosababisha kesi hiyo kuvuta hisia za watu hususani viongozi na wanachama Chadema waliokuwa wakifulika mahakamani hapo.

CHUO CHA ST DAVID KIMARA DAR KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO




CHUO CHA ST DAVID COLLEGE OF HEALTH KILICHOPO KIMARA TEMBONI DSM NI CHUO CHA KIPEKEE KATIKA UKANDA HUU WA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KINACHOTOA KOZI ZA AFYA KWA NGAZI ZOTE ZA CHETI NA DIPLOMA.

SIFA KUU NI UFAULU MASOMO YA SAYANSI IKIWEO HESABU NA KIINGEREZA ANGALAU ALAMA D.

ADA ZETU NI NAFUU UTALIPA KIDOGO KIDOGO KUKIDHI UWEZO WAKO, KWA MAWASILIANO 0626 231 364 / 0783 785 747 /  0716 044 610 / 0718 229 977 AU INGIA MTANDAONI  www.stdavidcollege.ac.tc

WAHI SASA MUHULA MPYA TAYARI UMEANZA.
PIA KUNA KOZI MAALUMU KWA WOTE WASIO NA VIGEZO KAMILI KUMUWEZESHA KUPAMBANA MPAKA AFIKIE VIWANGO NA KUJIUNGA NA MEDICINE..CA/CO

JIUNGE NA KOZI INAYOTOLEWA ST DAVID COLLEGE PEKEE IITWAYO PRE-MEDICINE PROGRAME KWA KUSHIRIKIANA NA BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA NECTA TUMEKUANDALIA NJIA RAHISI KABISA.

FIKA SASA KIMARA TEMBONI ZAMANI MOA AU OFISI ZETU ZILIZOPO MWANANYAMALA A CCM MINAZINI KWA DR DAVID B.MWANGANDA.

CHUO NI CHA KUTWA NA BWENI.