Sunday, 26 November 2017

Maagizo ya simu aliyopiga Rais Magufuli kwenye FIESTA leo Alfajiri

Maagizo ya simu aliyopiga Rais Magufuli kwenye FIESTA leo Alfajiri



Mziki wa G, Nikk na Joh... Mtu 3 FIESTA DSM

Mziki wa G, Nikk na Joh... Mtu 3 FIESTA DSM




"JUX KANIWEZA" - VANESSA MDEE

"JUX KANIWEZA" - VANESSA MDEE




"Bado siamini, nisingependa iwe hivyo kwa Vanessa" - JUX

"Bado siamini, nisingependa iwe hivyo kwa Vanessa" - JUX



Nguvu ya Darassa FIESTA ya Dar es salaam

Nguvu ya Darassa FIESTA ya Dar es salaam




Nguvu ya Aslay FIESTA Dar es salaam

Nguvu ya Aslay FIESTA Dar es salaam



Moto wa Rich Mavoko FIESTA DSM

Moto wa Rich Mavoko FIESTA DSM



Performance ya Fid Q Tigo Fiesta Grand Finale Dar es Salaam

Performance ya Fid Q Tigo Fiesta Grand Finale Dar es Salaam



Ben Pol Afunga Ndoa, Afumaniwa Jukwaani Tigo Fiesta Dar, Ebitoke Amuamshia Dude la Mwaka


Saturday, 25 November 2017

RC Aggrey Mwanri aamua kuwapa fursa hii vijana




Vijana Mkoani Tabora wametakiwa kuacha tabia ya kukaa vijiweni na kusikiliza maneno ambayo hayawasaidii wala kuwafundisha namna ya kupata maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri katika maeneo mbalimbali ya Kata za Wilaya ya Kaliua kwenye zoezi la uhamasishaji wa kilimo cha kisasa cha zao la Pamba na mazao mengine.

Aidha mkuu huyo wa mkoa amewataka vijana kutumia muda wao kujiajiri katika sekata ya kilimo na uzalishaji wa pamba pamoja na mazao mengine yatakayowasaidia kujipatia kipato na kuinua maisha yao.

“Kijana uliyekuja hapa leo ninakuambia kuwa kama unarafiki yako unashinda nae kijiweni na kucheza karata, Pool kuanzia leo achana naye, kwani hana nia njema nawewe, mwambie kuwa mkuu wa mkoa amenifundisha juu ya kulima pamba kisasa kuanzia sasa urafiki wangu mimi na wewe bye bye”, amesema RC Mwanri.

Mkuu wa Tabora yuko katika ziara mkoani mwake kuhamasisha kilimo cha kisasa cha zao la pamba na mazao mengine ambayo yatawasaidia wakulima kupata pesa zitakazoboresha maisha yao.

Lema amueleza Mrisho Gambo maneno haya



Mbunge wa Arusha Mjini, Mh. Godbless Lema amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutojaribu kufanya hila zozote za kuisababishia CCM ipate ushindi kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika hapo kesho, Nov 26.

Lema amesema kwmba anafahamu kila hatua na vikao ambavyo Mkuu huyo wa Mkoa na kwamba ana ushahidi wa kutosha wa kila kitu kunachopangwa.

"Mrisho Gambo,unapaswa kujua kwamba huna mamlaka wala  uwezo wa kushinda huu uchaguzi kwa nguvu/hila, hakuna kikao umekaa ambacho sina taarifa zake na ushahidi wa kila kitu".  Lema
Aidha Lema ameongeza kwa kumkanya kiongozi huyo asijaribu kufanya hivyo.

"Unataka kushinda uchaguzi huu kwa gharama yoyete ile ?sababu polisi wako nyuma yako ? usijaribu" Lema ameandika kupitia ukurasa wake wa Twitter asubuhi ya leo
Kesho kata 43 zinatarajiwa kufanya uchaguzi wa marudio wa kuwapata madiwani.

Waziri Kigwangalla awajibu wanaosema vyuma vimekaza



Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Hamisi Kigwangalla amesema maisha yataendelea kuwa magumu kwa watu wasio na shughuli maalum ambao wamezoea kuishi kwa ujanja ujanja.

Ameyasema hayo wakai akijibu maswali ya wananchi kupitia mtandao wa ‘Twitter’ ambao wengi walitaka kujua kuhusu utendaji kazi wake na hali halisi ya maisha yalivyo wakidai kuwa ni magumu.

“Wanaofanya shughuli zao halali hawatoona vyuma vimekaza, badala yake watafurahia sema watoto wa mjini, wasanii sanii na wajanja wajanja ndiyo watapata shida! Hawa wajanja wajanja ni wangapi? Na wenye shughuli halali ni wangapi?”, alisema Kigwangalla akiacha maswali kwa mmoja wa watu waliomuuliza.

Waziri Kigwangalla aliendelea kwa kutoa ufafanuzi juu ya namna ya kujenga uchumi kupitia kufanya kazi na sio kutegemea kupata pesa kwa njia rahisi rahisi.

“Mfumo wa uchumi unataka watu tufanye kazi kwa ubunifu ndipo tupate maisha mazuri siyo kufanya usanii kidogo tayari ukatajirika! Kukaza vyuma maana yake kuziba mianya ya wasanii ili walio kwenye uchumi halisi na wasanii wawe sawa siyo kuonea watu!” alimaliza.

Waziri Kigwangalla hivi sasa yupo jimboni kwake Nzega vijijini akiwa amepiga kambi kwaajili ya kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Nata.

Bwana harusi afariki, mkewe ajeruhiwa katika ajali wakitoka kufunga ndoa



Watu 12 wamekufa na wengine 22 kujeruhiwa katika ajali iliyotokea kijiji cha Ighuka wilayani Ikungi kwenye Barabara Kuu ya Singida – Manyoni baada ya Toyota Hiace waliyokuwa wakisafiria kutoka kumchukua bibi harusi kugongana uso kwa uso na Toyota Noah iliyokuwa imepakia watu kutoka msibani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba alisema kuwa ajali hiyo ilitokea juzi saa mbili usiku kwa kulihusisha gari lenye namba za usajili T 581 BBV iliyokuwa ikitokea Singida kwenda Manyoni na T 423 CFF iliyokuwa ikitokea Manyoni kwenda Singida.

Alisema kuwa ingawa uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha ajali hiyo bado unaendelea, taarifa za awali zinaonesha kuwa sababu kuu ni mwendo kasi na uzembe wa madereva.

“Baadhi ya majeruhi walituambia dereva wa Toyota Hiace aliyekuwa anatoka Singida mjini alihama kutoka upande wake na kwenda upande wa pili wa barabara ambako aligongana uso kwa uso na Noah iliyokuwa imebeba watu waliokuwa wakitoka msibani na kusababisha vifo vya abiria 10 hapo hapo na majeruhi 24,” alisema.

Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa mkoa wa Singida, Dk Ng’hungu Kusenza alisema kuwa majeruhi wawili waliofikishwa Hospitali ya Misheni Puma kwa ajili ya matibabu pia walikufa hivyo kufanya idadi ya watu waliokufa kuwa 12.

Aliwataja waliokufa ambao miili yao imehifadhiwa Hospitali ya mkoa kuwa ni John Duma, Jasson Nsunza, Abubakar Omari, Mary Kinku, Mwanaidi Juma na Husna Juma, Wengine ambao miili yao imehifadhiwa Hospitali ya Misheni Puma wilayani Ikungi ni Ezekiel Joseph, Mussa Daniel, Namtaki Daniel, Hamis Omari, Jumanne Mganga na Wansola Shalua. Habari ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa Bwanaharusi na madereva wa magari yote mawili ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Chanzo: Habarileo