Friday, 3 November 2017

Mtandao wa WhatsApp ulikwama kufanya kazi kwa masaa kadhaa



Mtandao wa kutuma mafaili mbalimbali kama Picha, Video na Sauti wa WhatsApp umekwama kufanya kazi kwa masaa kadhaa kwenye baadhi ya nchi duniani ikiwemo Tanzania.

Ripoti zinasema tatizo hilo limeanzia nchini Uingereza kisha kuendelea katika nchi za Marekani, Italia, Ujerumani India na sasa nchi za Afrika Mashariki nazo zimepitia changamoto ya kukosa huduma ya mtandao huo.

Tatizo hilo limeelezwa kuanza majira ya saa mbili asubuhi ambapo maelfu ya watumiaji wa WhatsApp wameeleza kukosa huduma. Wengi wao wamelalamika kukwama kwenye baadhi ya majukumu yao kutokana na kutegemea mtandao huo kwaajili ya kuhamisha na kupokea mafaili yao.

Hadi sasa bado wamiliki wa mtandao huo ambao ni kampuni ya Facebook chini ya Mkurugenzi Mark Zuckerberg hawajatoa tamko juu ya tatizo hilo.

Lakini kwa sasa mtandao wa WhatsApp umerejea kwenye hali ya kawaida hapa Tanzania, wakati huo nchi zingine kama Uingereza bado zinalalamika kukosa huduma hiyo ambapo watumiaji wanasema inafunguka na kuonesha kuwa kuna ujumbe umeingia lakini hauwezi kuufungua ili kuusoma au kuona kama ni Picha au Video.

Nape Nnauye amfungukia Nyarandu

Baada ya Mbunge wa Singida Kaskazini kujivua ubunge na kujiondoa katika chama cha Mapinduzi(CCM), Lazaro Nyalandu hatimae Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema kuwa Chama cha siasa ni Itikadi.

Nape kupitia ukurasa wake wa twitter ameweka picha inayomuonyesha mbunge huyo na Katibu Mkuu wa Chama hicho, Ndg Kinana wakiwa wameweka kwa pamoja alama ya kidole gumba.

Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa ndani sio NJE!

Nyalandu alikihama chama cha Mapinduzi Oktoba 30 mwaka huu ambapo alieleza kuwa amechoshwa na mwenendo wa siasa wa sasa.

Mahakama yaamuru DC kukamatwa

Mwanza/Bukoba. Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba imetoa hati ya kumkamata na kumfikisha mahakamani Mkuu wa Wilaya ya Misenyi, Dennis Mwira kwa kosa la kupuuza amri ya Mahakama.

Amri hiyo imetolewa Novemba 2 na Hakimu Mkazi, Samuel Maweda baada ya mkuu huyo wa wilaya kukaidi amri ya kuachia ng'ombe 541 wa wafugaji wa kitongoji cha Rwenkuba wilayani humo waliokamatwa isivyo halali.

Septemba 22, mahakama hiyo ilitoa amri ya ng'ombe hao kuachiwa baada ya wananchi kufungua shauri la madai namba 21/2017 kupinga ng'ombe wao kukamatwa katika eneo lenye mgogoro unaoendelea katika mahakama kuu kitengo cha ardhi kwa shauri namba 14/2017.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu jana Alhamisi usiku, Wakili wa wananchi143 waliofungua kesi mahakamani, Danstan Mutagahywa amesema baada ya Mkuu wa Wilaya na mdaiwa mwenzake, Ladislaus Martin ambaye ni Meneja wa Ranchi ya Misenyi baada ya kukaidi kutekeleza amri hiyo, waliwasilisha ombi la watu hao kukamatwa kwa kudharau amri ya Mahakama.

"Siyo tu wamekaidi kutekeleza amri halali ya Mahakama, DC na mwenzake pia wamegoma kupokea hati za wito na kufikia hatua ya kumkamata na kumweka mahabusu dalali wa Mahakama aliyepewa amri ya kutekeleza zoezi la kurejesha ng'ombe wanaoshikiliwa isivyo halali," amesema Mutagahywa.

Amesema amri hiyo inatarajiwa kufikishwa ofisini kwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa (RCO), wa Kagera leo Ijumaa Novemba 3.

Amemtaja dalali wa Mahakama aliyekamatwa na kuswekwa mahabusu kwa amri ya DC Oktoba 31, kuwa ni Ignatus Bashemela aliyeachiwa huru baada ya yeye kuwasilisha suala hilo ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera akionyesha nyaraka halali za Mahakama kuhusu jambo hilo.

Wakati shauri la madai dhidi ya DC na mwenzake Ladislaus likitarajiwa kusikilizwa mara watakapokamatwa na kufikishwa mbele ya mahakama, ile ya ardhi ambayo bado inatajwa mbele ya Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Seif Musa, itatajwa tena Machi 8, 2018.

Kauli ya DC

Akizungumza kwa njia ya simu mkuu huyo wa wilaya amesema aliagiza kukamatwa kwa dalali wa wafugaji wa ng'ombe kutoka Uganda ambaye alifika bila kutoa taarifa yoyote kwa mamlaka za Serikali.

Amesema kuwa mtu huyo alikwenda moja kwa moja katika eneo wanapotunzwa ng'ombe zaidi ya  80 walioingizwa nchini kutoka Uganda bila kufuata utaratibu.

"Hilo suala la dalali wa Mahakama nalisikia kwako niliyeagiza akamatwe ni dalali wa wafugaji wa ng'ombe kutoka Uganda ambao tumewakamata alifika bila kufuata taratibu nikaagiza akamatwe,"amesisitiza Kanali Mwila.

Ameongeza kuwa alikamata ng'ombe zaidi ya 400 na wamiliki wake kutoka Uganda walilipa faini na kuwarudisha kwao na kubaki ng'ombe 88 aliosema alipata taarifa kuwa wanataka kuchukuliwa kwa nguvu na watu ambao hata hawakupita kwenye ofisi yake.

Pia amesema hana taarifa yoyote ya kuwepo kwa hati ya Mahakama dhidi yake na kuwa anaendelea kuwasaka raia wawili wanaodaiwa kushirikiana na wafugaji wa Uganda kuingiza mifugo hiyo bila utaratibu

Mourinho:Nahitaji pongezi kuifunga Tottenham



Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho

Meneja wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho amesema kikosi chake cha mashetani wekundu (The Red Devils) kinastahili kupongezwa kwa kuifunga Tottenham ambayo imefanya vizuri katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.

Mourinho ambae nimiongoni mwa makocha wachache wenyemaneno mengi katika ligi ya Uingereza ameyasema hayo hii leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

“Tottenham imeifunga Liverpool mabao 4-1 ikaifunga Real Madrid 3-1,lakini wameshindwa kufanya hivyo dhidi yetu bila shaka wachezaji wamgu wanastahili pongezi,”amesema Mourinho.

Timu ya Tottenham hapo jana usiku imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa jumla ya mabao 3-1 mbele ya mabingwa watetezi klabu ya Real Madrid katika dimba la Wembley huku Dele Alli akitupia mawili na Christian Eriksen akimalizia karamu hiyo ya mabao.

Spurs imechomoza na ushindi huo wa kihistoria ndani ya klabu hiyo ikiwa ni sikuchache tu toka ikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Manchester United lilofungwa na Anthony Martial mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza.

Mourinho amesisitiza United inastahili pongezi kwa kuishushia kipigo Tottenham ambayo imechomoza na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Liverpool mwezi uliyopita

Maduka yanaodurufu CD za wasanii yafungiwa na TRA

Maduka yanaodurufu CD za wasanii yafungiwa na TRA

       

              



MAMLAKA ya mapato nchini (TRA) ikishirikiana na kampuni ya Msama Auction Mart ambao ni wasimamizi na wasambazaji wa kazi za muziki wa Injili, chini ya Mkurugenzi wake, Alex Mwita Msama, imefanya oparesheni ya kuwafungia maduka na kuwahoji watu wanaodurufu CD feki yaani zisizofuata utaratibu uliopo.


Akizungumza wakati wa oparesheni hiyo iliyofanyika jana jioni Kariakoo jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Kodi za Ndani (TRA), Elijah Mwandubya, alisema wamekuwa wakiwatahadharisha watu hao kuachana na kazi hiyo ya kudurufu CD feki hivyo lakini wamekuwa hawaitikii tahadhari hiyo na sasa mamlaka hiyo.

Aliongeza kwamba, kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, wamejidhatiti vilivyo kuhakikisha kazi za wasanii nchini zinalindwa na serikali inapata mapato yake kutokana na wengi wao kukwepa kulipa kodi na kuuza CD feki.

Alisema serikali inatengeneza mazingira safi na wafanyabiashara waaminifu wanaofuata utaratibu sahihi, ukiwemo ulipaji wa kodi kwa wakati na hivyo wataendelea
kuhakikisha kazi za wasanii zinalindwa na kuheshimika ipasavyo, kwani zoezi litaendelea maeneo mbalimbali nchin

Dogo Janja anyoosha maelezo kuhusu ndoa yake na Uwoya

Dogo Janja anyoosha maelezo kuhusu ndoa yake na Uwoya

Dar es Salaam. Mwanamuziki Dogo Janja amekiri kuwa amefunga ndoa na mwigizaji Irene Uwoya na kwamba amembadilisha dini kuwa muislamu ingawa amegoma kujibu maswali muhimu ikiwamo uwepo wa wazazi wa mwanamke huyo katika tukio hilo.

Dogo Janja ambaye jina lake halisi ni Abdulaziz Chende wakati akihojiwa na Kipindi cha Leo Tena cha leo Ijumaa kinachorushwa na kituo cha redio Clouds FM, amekiri kufunga ndoa na mwigizaji huyo na kusema kuwa sasa anaitwa Sheillah.

Akisaidiwa kutoa maelezo na mwanamuziki Keisha amesema ndoa hiyo ilifungwa kwa kupata baraka kutoka kwa ndugu wa pande zote baada ya kutoa posa wiki mbili zilizopita.

Amesema Uwoya alibadili dini wiki tatu kabla ya ndoa na kwamba barua ya posa, mahari na ndoa vilichukua muda wa wiki tatu tu.

Mtangazaji wa kipindi hicho, Husna Abdul maarufu Da Huu amemuuliza mwanamuziki huyo mahali ilipofungwa ndoa hiyo naye alijibu kwa Madee lakini Keisha aliingia kati na kusema ilikuwa eneo la siri.

Mtangazaji huyo aliendelea kuwabana kwa maswali kuwa inawezekana vipi ndoa ikafungwa eneo la siri wakati ilipaswa kufanyika nyumbani kwa wazazi wa Irene, Keisha amesema walikwenda kumchukua bibi harusi na kwenda kufunga ndoa katika eneo hilo.

Kitilya na wenzake waendelea kusota rumande

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa kampuni inayoshughulikia  uwekezaji wa mitaji na dhamana (Egma), Harry Kitilya na waliokuwa maofisa wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon bado wanaendelea kusota rumande kutokana na upelelezi wa kesi inayowakabili  bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi ameeleza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa  leo Ijumaa kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Soma: Wakili aomba kesi ya utakatishaji fedha dhidi ya akina Kitilya ifutwe

Pia ameeleza kuwa bado wanasubiri awamu ya pili ya upelelezi kutoka nchini Uingereza, kutokana na hilo ameomba kesi hiyo ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Baada ya ombi hilo Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 10, 2017 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la

Mmiliki wa timu ya Chelsea na kocha mkuu hawaongei

Mmiliki wa timu ya Chelsea na kocha mkuu hawaongeiTaarifa zinaeleza hali si shwari katika klabu ya Chelsea na sasa mmiliki wa klabu hiyo Roman Abromovich hana maelewano mazuri na kocha Antonio Conte na siku za usoni hawajawahi kuonana.


Mmiliki wa Chelsea Roman Abromovich huwa ana mahusiano ya karibu sana na makocha wa timu yake na hupenda kuwaweka karibu yake na ndivyo alivyofanya wakati Antonio Conte akijiunga na Chelsea.

Gazeti maarufu la masuala ya michezo la Marca limechapisha habari inayosema kwamba watu hao wawili hawaongei moja kwa moja kwa sasa na kama Conte akitaka kuongea na Abromovich ni lazima amtumie Secretary wake.

Mahusiano kati ya wawili hao yalianza kuwa katika hali mbaya wakati wa dirisha la usajili huku sababu kubwa ikidaiwa ni Conte kutoridhishwa na namna ambavyo klabu ya Chelsea inaendesha dirisha la usajili.

Mbaya zaidi Marca wamesema tayari kuna kikundi cha wachezaji ndani ya Chelsea ambao hawamuungi mkono Antonip Conte na wengi wakichukizwa na kitendo alichomfanyia Diego Costa baada ya msimu kuisha.

Kwa mambo yanayoendelea Chelsea inaonesha wazi huenda huu ukawa msimu wa mwisho kwa Conte kuitumikia Chelsea na kipigo cha bao 3 kwa 0 toka kwa As Roma kimezidi kuchafua hali ya hewa kwa meneja huyo.

Chelsea wana kibarua kigumu zidi ya Manchester United mchezo ambao utamlazimu Conte kushinda laa sivyo muda wake wa kuwa Chelsea unaweza kuisha mapema zaidi kuliko watu wanavyoamini.m

Tazama full video ya harusi ya Dongo Janja na Irene Uwoya


Wakati mjadala ukiendelea kuhusu taarifa zinazodai Dogo Janja na Irene Uwoya kufunga ndoa, hatimaye Dogo Janja ametuletea video hii inayoonyesha tukio zima la sherehe yake.

Tazama video hapa chini

Anaswa na wananchi akimbaka mtoto wa miaka miwili

Anaswa na wananchi akimbaka mtoto wa miaka miwili



Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba 

Polisi wanamshikilia mkazi wa Kijiji cha Magamba wilayani hapa kutokana na tuhuma za kumbaka mtoto mwenye miaka miwili.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, tukio hilo lilitokea juzi Kitongoji cha Komkola Chang’ombe.

Wakazi wa kitongoji hicho waliozungumza na gazeti hili, walisema walisikia mtoto akilia nyumbani kwa mtuhumiwa na walipokwenda walikuta akimbaka mtoto huyo.

“Huu ni unyama umevuka kiwango kijana anathubutu kumbaka mtoto mdogo kama yule, sijui tunaelekea wapi vijana wa namna hii hawastahili kuishi na jamii,” alisema Hussen Juma.

Kamanda Wakulyamba alisema mtoto aliyebakwa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni akiendelea na matibabu na kwamba, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Alitoa wito kwa wazazi kutowaacha watoto wao kuzurura mitaani, ili kuwalinda wasitendewe vitendo vya kikatili kama hivyo

Akaunti ya Twitter ya rais Trump ''yapotea kwa muda




Akaunti ya mtandao wa Twitter ya rais Donald Trump ilipotea kwa muda siku ya Alhamisi lakini, ikarudishwa baadaye , kampuni hiyo imesema.

Twitter imesema kuwa akaunti hiyo kwa jina @realdonaldtrump iliondolewa na mfanyikazi mmoja na baadaye kuelezea kuwa ilikuwa siku yake ya mwisho kazi.

Akaunti hiyo iliondolewa kwa muda wa dakika 11 na sasa kampuni ya Twitter inachunguza.
Bwana Trump ambaye ni mtumizi wa mtandao wa Twitter wa mara kwa mara akiwa na wafuasi milioni 41.7 hajatoa tamko lolote kuhusu swala hilo.

Siku ya Alhamisi jioni, wale waliotembelea akaunti ya rais Trump waliona ujumbe uliosema ''pole ukurasa huu hauko kwa sasa!''

Baada ya akaunti kurejeshwa , ujumbe wa kwanza wa bwana Trump ulikuwa kuhusu ule mpango wa Republican wa kupunguza kodi.

Hatahivyo@POTUS ambayo ndio akaunti rasmi ya rais Trump haukuathiriwa.

Twitter imesema kuwa inachunguza tatizo hilo na kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa kisa kama hicho hakitokei tena.

Kampuni hiyo ilisema katika ujumbe wake kwamba wamebaini katika uchunguzi wao kwamba kisa hicho kilifanywa na mfanyikazi anayewahudumia wateja ambaye alifanya hivyo katika siku yake ya mwisho ya kazi.

Tunatathmini kisa chote kikamilifu.

Bwana trump alijiunga na mtandao wa twitter mnamo mwezi Machi 2009.

Amekuwa mtumiaji mkubwa wa mtandao huo kwa kukuza sera zake mbali na kuwashambulia wapinzani wake wakati wa kampeni za urais 2016 na hata baada ya kuchukua mamlaka mnamo mwezi Januari

Wahukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mpwa wao



Mahakama moja nchini India imewahukumu watu wawili kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mpwa wao mwenye umri wa miaka 10 ambaye alijifungua mtoto wa kike mnamo mwezi Agosti.

Wanaume wote wawili walikuwa wajomba wa smichana huyo.

Walihukumiwa kwa kumbaka msichana huyo siku ya Jumanne.

Uja uzito wa msichana huo ulibainika katikati ya mwezi Julai wakati alipopelekwa hospitalini baada ya kulalamikia maumivu ya tumboni.

Mjombake wa pili alikamatwa baada ya chembechembe za DNA za mtoto huyo kutofanana na kakake mkubwa ambaye ndio mshukiwa wa kwanza .

Kesi ya mshukiwa wa kwanza ilichukua mwezi mmoja huku mjombake mdogo akihukumiwa baada ya kesi hiyo kuchukua siku 18.

Kesi hiyo ya msichana wa miaka 10 imegonga vichwa vya habari kwa wiki kadhaa nchini India na kote duniani.

Alikuwa na uja uzito wa wiki 30 wakati mahakama moja ya Chandigarh ilipokataa ombi la kuavya mimba, kwa sababumimba hiyo ilikuwa kubwa.

Jopo la madaktari lilisema kuwa kutolewa kwa mimba hiyo ni hatari .

Baadaye mahakama ya juu ya India pia ilikataa kutolewa kwa mimba hiyo kwa sababu kama hizo za kimatibabu.

Sheria ya India hairuhusu kutolewa kwa mimba baada ya wiki 20 hadi pale daktari aweze kubaini kwamba maisha ya mama yapo hatarini.

Mtoto huyo hakujua kwamba alikuwa akibeba uja uzito na kwamba alielezewa kwamba tumbo lake likuwa na jiwe, kulingana na mwamndishi wa BBC Geeta Panday mjini Delhi.

Alijifungua mwezi Agosti na mtoto huyo kukabidhiwa mamlaka ya kuangalia watoto ili kulewa.

Awali msichana huyo aliwaambia maafisa wa polisi na wanaharakati wa maslahi ya watoto kwamba alibakwa mara kadhaa katika kipindi cha miezi saba iliopita na mjombake mkubwa ambaye yuko katika umri wake wa 40

Steve Nyerere amwagia sifa Aunt Ezekiel


Mchekeshaji maarufu Bongo, Steve Nyerere.

MCHEKESHAJI maarufu Bongo, Steve Nyerere amefunguka kuwa mwanamke anayemheshimu Bongo Muvi kwa sasa ni Aunt Ezekiel pekee.



Msanii wa Bongo Muvi, Aunt Ezekiel pekee.

Akizungumza na Star Mix Steve alisema kuwa, anamheshimu kwa sababu ni mwanamke ambaye hajabweteka na amejitahidi sana kukusanya hela anazopata kufanya mambo ya maana kama alivyojenga nyumba maeneo ya Kigamboni tofauti na mastaa wengine.

“Yaani kwa kweli Bongo Muvi kwa wanawake nampa heshima kubwa Aunt,ni mdada ametulia na mzazi mwenziye amepata watoto lakini pia ameweza kujituma mpaka kujenga nyumba tofauti na wengine,”alisema Steve