Baada ya Mbunge wa Singida Kaskazini kujivua ubunge na kujiondoa katika chama cha Mapinduzi(CCM), Lazaro Nyalandu hatimae Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema kuwa Chama cha siasa ni Itikadi.Nape kupitia ukurasa wake wa twitter ameweka picha inayomuonyesha mbunge huyo na Katibu Mkuu wa Chama hicho, Ndg Kinana wakiwa wameweka kwa pamoja alama ya kidole gumba.
Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa ndani sio NJE!
Nyalandu alikihama chama cha Mapinduzi Oktoba 30 mwaka huu ambapo alieleza kuwa amechoshwa na mwenendo wa siasa wa sasa.



Dar es Salaam. Mwanamuziki Dogo Janja amekiri kuwa amefunga ndoa na mwigizaji Irene Uwoya na kwamba amembadilisha dini kuwa muislamu ingawa amegoma kujibu maswali muhimu ikiwamo uwepo wa wazazi wa mwanamke huyo katika tukio hilo.
Taarifa zinaeleza hali si shwari katika klabu ya Chelsea na sasa mmiliki wa klabu hiyo Roman Abromovich hana maelewano mazuri na kocha Antonio Conte na siku za usoni hawajawahi kuonana.






