Friday, 3 November 2017

Shahidi adai kufungiwa tofali sehemu za siri


MSHTAKIWA wa pili wa kesi ya mauaji ya kukusudia ya mfanyabiashara tajiri na bilionea wa madini ya Tanzanite, Erasto Msuya, Shaibu Said (Mredii), amedai mahakamani kuwa alipelekwa Kituo cha Polisi kinachoitwa Guantamano, nje kidogo ya Jiji la Arusha na kuteswa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.

Pia alidai kuwa baada ya kuhamishiwa Moshi alifungiwa nusu ya kipande cha tofali kwenye sehemu zake za siri, ili akubali kutia saini maelezo ya kukiri kosa la mauaji.

Shahidi huyo wa kwanza wa upande wa utetezi katika kesi ndani ya kesi, aliieleza mahakama hiyo kuwa wakati analazimishwa na polisi kusaini maelezo hayo akiwa Moshi, alinyweshwa pia maji ambayo yanafanya tumbo kuwaka moto na mwili mzima kuwasha.

Akitoa utetezi wake katika Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mredi alidai kuwa mateso mengine aliyokutana nayo ni kufungiwa bomba la chuma katikati ya miguu na kuning’inizwa kwenye paa la nyumba akiwa amefungwa pingu mkononi, kuchomwa na singe ya bunduki ya SMG kwenye fundo la mguu karibu na unyayo na kuchokonolewa na singe hiyo ndani yake ili akubali kosa na baadaye kuchomwa na pasi ya umeme miguuni.

Alidai mateso hayo ya polisi yamemfanya awe mlemavu mkono wake wa kushoto ambao kutokana na madhila hayo, hivi sasa anatumia dawa za mifupa na maradhi mengine tangu alipokamatwa mwaka 2013 hadi leo.

Aidha, alidai kutokana na madhila hayo, askari polisi waliokuwa wakimtesa ili akubali kutia saini maelezo ya kukiri kosa la kumuua Msuya, walikuwa wakimkanda kila siku kwa maji ya moto ili apate nafuu na kutia saini kama walivyotaka.

Akiwa mbele ya Jaji Salma Maghimbi anayesikiliza kesi hiyo namba 12 ya mwaka 2014, Mredii aliieleza mahakama hiyo kwamba wakati anakamatwa na kuhusishwa na mauaji ya Bilionea Msuya, hakuwapo Mererani, Arusha wala Orkolili kulikofanyika mauaji hayo, kwa vile alikuwa shambani kwake mkoa wa Manyara.

Alidai kwamba hata taarifa za kuuawa kwa kupigwa risasi, Erasto Msuya (Bilionea), alizipata kwa njia ya simu akiwa shambani kwake baada ya kupigiwa simu na shemeji wa marehemu, aliyemtaja kwa jina moja la Shujaa.

Msuya aliuawa kwa kupigwa risasi 22, Agosti 7, mwaka 2013, majira ya saa 6:30 mchana katika eneo la Mijohoroni, kandokando ya barabara kuu ya Arusha-Moshi, karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Mbali na Mredii, wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Sharif Athuman (31), ambaye ni mfanyabiashara wa madini na mchimbaji mdogo, mkazi wa Kimandolu mkoani Arusha na Mussa Mangu (30), mkazi wa Shangarai Kwa Mrefu.

Wengine ni Jalila Said (28), mkazi wa Babati, Sadiki Jabir a.k.a “Msudani” (32), mkazi wa Dar es Salaam na Lang’ata, Wilaya ya Hai, Karim Kihundwa (33), mkazi wa Lawate, Wilaya ya Siha na Alli Musa maarufu “Majeshi”, mkazi wa Babati, mkoani Manyara.

Kesi hiyo ndani ya kesi iliibuliwa wiki iliyopita na Wakili wa Utetezi, Majura Magafu, baada ya mshtakiwa wa pili katika kesi hiyo, kudai aliteswa na kulazimishwa kutia saini maelezo bila ridhaa yake.

Madai hayo ya mateso yaliyosababisha afya ya mteja wake (Mredii) kuwa mbaya na kulazimika kupelekwa Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi) na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC kwa matibabu zaidi, ndiko kulikoibua mgongano wa kisheria na kuanza kesi ndani ya kesi.

Shahidi huyo wa upande wa utetezi (Mredii), aliongozwa kutoa ushahidi na Wakili wake Majura Magafu kuhusu uelewa wake tangu alipokamatwa hadi kufanyiwa mateso hayo na kisha kulazimishwa kusaini maelezo ya kukubali kushiriki mauaji ya Bilionea Msuya. Mahojiano hayo yalikuwa kama ifuatavyo:

Wakili Magafu: Walipokuchukua askari kutoka Mererani kuja KIA, ulipofika hapo kulitokea kitu gani?

Shahidi: Walipaki gari chini ya mti wa mjohoro na kuniamuru nilale chini kifudifudi.

Wakili Magafu: Baada ya hapo ikawaje?

Shahidi:  Nililala hivyo hadi saa 12 jioni nikasikia wanasema twende hivi na nilihisi wanakwenda barabara ya Arusha.

Wakili Magafu: Ulijuaje uko barabara ya KIA kuelekea Arusha?

Shahidi:  Nimeizoea hiyo barabara kwa sababu naipita kila siku.

Wakili Magafu: Mlienda mpaka wapi?

Shahidi: Nilipelekwa mpaka Arusha

Wakili Magafu: Ulipofikishwa Arusha nini kilifanyika?

Shahidi: Nilikaa kwenye gari la Polisi kwa saa mbili hivi hadi waliponishusha kwa amri ya afande Samuel ambaye alitoa ushahidi
hapa mahakamani.

Wakili Magafu: Umesema Arusha ulipelekwa ukumbini, hebu tuambie ni jambo gani lilifanyika?

Shahidi: Nilimkuta RPC (Kamanda wa Polisi wa Mkoa) Arusha na baadhi ya askari wengine wenye vyeo vikubwa.

Wakili Magafu: Huyo RPC ulikuwa unamfahamu majina yake kabla?

Shahidi: Hapana, nilikuwa namfahamu kwa sura tu

Wakili Magafu: Wakati unapelekwa pale ukumbini Arusha, kulikuwa na askari wangapi?

Shahidi: Walikuwa kama sita au saba

Wakili Magafu: Tusaidie, wakati huo ulikuwa katika hali gani?

Shahidi: Nilikuwa katika hali nzuri, lakini walikuwa wamenifunga pingu za mikono na miguu.

Wakili Magafu: Ulipofikishwa ukumbini uliambiwa nini na hao uliowakuta?

Shahidi: RPC Arusha aliniambia Shaibu tunachotaka hapa ni ushirikiano wako.

Wakili Magafu: Alikwambia anaomba ushirikiano kuhusiana na jambo gani?

Shahidi:  Mauaji ya Erasto Msuya

Wakili Magafu: Huyo Erasto Msuya ulikuwa ukimfahamu?

Shahidi: Ndiyo nilikuwa namfahamu ingawa sikuwa na ukaribu naye.

Wakili Magafu: Ulipowajibu kwamba hutambui chochote kuhusiana na tukio hilo, walikuambiaje?

Shahidi: Niliwaambia kwamba sifahamu jambo hilo na siku ya tukio linapofanyika mimi sikuwapo Mererani, Kia wala Arusha.

Wakili Magafu: Baada ya kuwaambia hivyo walikujibu nini?

Shahidi: Waliniuliza taarifa za kuuawa kwa Erasto nilizipata wapi.

Wakili Magafu: Ukawajibu nini?

Shahidi: Niliwaambia nilizisikia baada ya kupigiwa simu kwamba Erasto ameuawa.

Wakili Magafu: Unaweza kukumbuka ni nani alikwambia kwamba Erasto ameuawa?

Shahidi: Nilipata taarifa baada ya kupigiwa simu na shemeji yake Erasto, anaitwa Shujaa.

Wakili Magafu; Ukiwa kule ukumbini Arusha walikwambia nini hao kina RPC na askari wengine?

Shahidi: RPC Arusha aliniambia tunakuonea huruma kwa sababu tukikukabidhi kwa hawa vijana waliokuja na wewe, sijui kama utarudi salama.

Wakili Magafu: Kutokana na kauli hiyo au ushauri huo wa RPC Arusha uligundua nini?

Shahidi: Kwa sababu hao walioniambia hivyo ni viongozi wakubwa niliingiwa na hofu sana.

Wakili Magafu: Baada ya hapo nini kiliendelea?

Shahidi: RCO Ramadhan Ng’anzi (Mkuu wa Upelelezi Mkoa) alitoa amri kwa afande Samuel na kumwambia ondokeni naye.

Wakili Magafu: Baada ya kutolewa hapo ukumbini mlielekea wapi?

Shahidi: Tulielekea kama tunaenda Babati.

Wakili Magafu: Mlienda hadi wapi?

Shahidi: Tulienda hadi uwanja wa Ndege Kisongo, mkoa wa Arusha na tulienda tukaingia upande wa kushoto.

Wakili Magafu: Safari yenu huko iliishia wapi?

Shahidi: Tulienda hadi kwenye mashamba makubwa ambako kuna kituo cha Polisi kule.

Wakili Magafu:  Hicho kituo kinaitwaje?

Shahidi: Wao wenyewe Polisi waliniambia unaijua Guantanamo wewe?

Wakili Magafu:  Ehee mlipofika huko Guantanamo nini kiliendelea?

Shahidi: Hapo kituoni tulimkuta dada mmoja askari akiwa kaunta na akaambiwa chomoa hiyo redio ya Sub Uffer na switch yake ilete.

Wakili Magafu:  Ni nani aliomba hiyo redio ya Sub Uffer?

Shahidi: Ni askari mmoja toka Arusha aliyekuwa ameongozana na askari wa Moshi anaitwa Faustine Mafwele.

Wakili Magafu: Nini kilifuata?

Shahidi: Waliifungulia kwa sauti kubwa hiyo redio na wakanifungua pingu zote za mikononi na miguuni na kuniambia nivue nguo na kubaki kama nilivyozaliwa.

Wakili Magafu: Baada ya kuvua hizo nguo na kubaki kama ulivyozaliwa, walikufanyaje?

Shahidi: Waliniweka chini ya sakafu wakaniambia wao hawana ombi kama wale maofisa wakubwa zao ila wao wana amri tu.

Wakili Magafu: Wakafanyaje sasa?

Shahidi: Waliniambia sisi hatutaki maelezo wala kinachohusiana na mauaji ya Erasto.

Wakili Magafu: Wakati wakikueleza hayo walikuwa wana nini na nini?

Shahidi: Walikuwa na makaratasi mengi sana

Wakili Magafu: Walikuambia kitu gani kuhusiana na hayo makaratasi?

Shahidi: Waliniambia tunachotaka hapa ni sahihi yako tu.

Wakili Magafu: Baada ya kuwajibu hivyo walifanya kitu gani?

Shahidi: Nilisikia maumivu makali baada ya kupigwa na kitu kizito kichwani.

Wakili Magafu: Baada ya kukupiga kichwani kuna nini kingine walifanya?

Shahidi: Niliingizwa bomba la chuma katikati ya miguu na yule shahidi aliyetoa ushahidi wake jana (afande Dereck) na mwenzake afande Chilumba akanishika kiuno na kuniweka kwenye meza na kilichoendelea hapo mheshimiwa nilikuwa nakomeshwa na waliniambia hapa salama yako ni sahihi.

Wakili Magafu: Baada ya kuingizwa bomba walifanyaje?

Shahidi: Afande Chilumba alimwambia Dereck jisevie.

Wakili Magafu: Baada ya hapo walifanya kitu gani?

Shahidi: Nilipigwa kwenye nyayo kwa juu (kwenye kifundo) na nilipiga kelele sana.

Wakili Magafu: Sasa hebu tusaidie ile redio ilikuwa na kazi gani?

Shahidi: Yule askari wa Arusha Faustine Mafwele alikuwa anaongeza sauti ili kuzima sauti yangu ibaki ya redio.

Wakili Magafu: Tusaidie ukiwa Moshi, unasema RCO aliondoka kwa hasira baada ya kuambiwa hujasaini, kwani mliondoka kuelekea wapi?

Shahidi: Mashamba ya miwa TPC

Wakili Magafu:  Mlipofika mashamba ya miwa kulitokea nini?

Shahidi: Waliniambia sali sala yako ya mwisho

Wakili Magafu:  Ulisali?

Shahidi: Nilisali kwa sababu kwenye moyo wangu nilishamwambia Mungu lolote linaweza kutokea na tayari nilikuwa nimeshaweka nadhiri.

Wakili Magafu: Baada ya wewe kumaliza kusali walifanya nini?

Shahidi: Askari mmoja alitoa kitu kama kisu kwenye ncha ya bunduki ya SMG (singe) na kunichoma nayo kwenye unyayo wa mguu.
Wakili Magafu: Walipoingiza hiyo singe kwenye mguu wakafanyaje sasa?

Shahidi: Walikuwa wanaichezesha huko ndani katikati ya mfupa na nyama huku wakiishindilia.
Wakili Magafu: Nini kiliendelea tena?

Shahidi: Walisema wananipeleka kwenye tocha ya mwisho (mateso) na walinipeleka kwenye kituo cha polisi kilichopo karibu na kiwanda cha TPC

Wakili Magafu: Mlipofika kulifanyika kitu gani?

Shahidi: Waliipiga kisu suruali yangu niliyokuwa nimevaa na ikatolewa mwilini.
Wakili Magafu: Wakafanya kitu gani sasa?

Shahidi: Niliona wana kipande cha tofali za block (mchanga) kimefungwa kamba.

Wakili Magafu: Hicho kipande cha tofali kazi yake ilikuwa nini?

Shahidi: Walikichukua wakanifunga kwenye …(sehemu za siri) wakaliacha likiwa linaning’inia huku mimi nikiwa nimefungwa pingu juu ya paa la nyumba.

Wakili Magafu: Hilo zoezi lilichukua muda gani?

Shahidi: Sikuwa najielewa baada ya hapo.

Wakili Magafu: Wakati huo hizo document ulikuwa umeshazisaini?

Shahidi: Kwa sababu niliona nakufa ilibidi nisaini

Baada ya Wakili Magafu kumaliza kumwongoza shahidi huyo, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Abdallah Chavula, alisimama na kumwomba Jaji Salma upande wa utetezi wamwite mahakamani Daktari wa Hospitali ya Mawenzi aje kuhojiwa kuhusiana na matibabu ya Mredii anayedaiwa kuteswa.

“Mheshimiwa Jaji, chini ya kifungu cha 291 (3) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), Sura ya 20 ya Sheria ya Mwaka 2002 iliyofanyiwa marejeo, Daktari Massam E ambaye ana cheo cha AMO (Assistant Medical Officer) aliyejaza fomu namba tatu ya Polisi, aletwe mahakamani kwa ajili ya cross examination (mahojiano),” alidai Chavula.

Kutokana na hoja hiyo ya upande wa mashtaka, Wakili Magafu aliiambia mahakama hiyo kwamba wanatarajia kuleta mashahidi wawili mahakamani akiwamo daktari huyo wa Mawenzi na daktari wa Magereza, hivyo wanaomba wenzao wawe wavumilivu.

Dakika chache baadaye, Wakili Chavula alianza kumhoji shahidi huyo wa kwanza wa upande wa utetezi (Mredii) na mambo yalikuwa hivi:

Wakili Chavula: Nairejesha mahakama nyuma kidogo kwenye kumbukumbu zake, tarehe 10/2/2015 wakati wa PH (Preliminary Hearing), shahidi ukiwa na mawakili wako, kwa nini ulisema ulikamatwa tarehe 15/8/2013, Je, uliidanganya mahakama?

Shahidi: Labda nilikuwa nimesahau.

Wakili Chavula: Umeileza mahakama kwamba tarehe 18/8/2013 ukiwa kizuizini pale Polisi Mererani, baadaye ukapelekwa Polisi Kia, kweli si kweli?

Shahidi: Kweli
Wakili Chavula: Ni sahihi kwamba shahidi wa nne, afande Dereck alikuwa miongoni mwa waliokutesa kutoka Guantanamo hadi mashamba ya TPC?

Shahidi: Ni sahihi.

Wakili Chavula: Kwa nini jana, hamkumuuliza maswali wakati anaitwa kutoa ushahidi wake kwamba alihusikaje kukutesa?
Shahidi: Jaji ndio anajua kwa sababu alikuwa hajaruhusu hilo.

Wakili Chavula: Ni sahihi kwamba wakati Erasto anauawa haukuwa Mererani, Arusha wala Orkalili?
Shahidi: Sahihi.

Jopo la mawakili wa utetezi katika kesi hiyo linaongozwa na wakili Hudson Ndusyepo anayemtetea mshitakiwa wa kwanza, Majura Magafu anayemtetea mshitakiwa wa pili na wa tano, Wakili Emmanuel Safari anayemtetea mshitakiwa wa tatu na John Lundu anayemtetea mshitakiwa wanne, sita na saba.

Upande wa mashtaka katika kesi hiyo ambayo ni gumzo katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini, unaongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Abdala Chavula.

Hadi sasa jumla ya mashahidi 10 wa upande wa mashtaka, wameshatoa ushahidi wao mahakamani hapo akiwamo aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Hai, (OC-CID) Joash Yohana, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Hai (DMO) Dk. Paul Chaote (39) na Khalid Sankamula (49) ambaye ni Mganga wa Kienyeji na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Limbula, Wilaya ya Kaliua, mkoani Tabora.

Wengine ni Anase Khalid (37), mkulima na mkazi wa Kaliua, Tabora, Mbazi Steven (32), mkazi wa Arusha na Ofisa Upelelezi, Kitengo cha Intelijensia ya Jinai mkoa wa Kilimanjaro, Herman Ngurukisi (40), Inspekta Samueli Maimu (45) ambaye alikuwa kiongozi wa timu ya ukaguzi ya Polisi (CRT) kutoka Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) wa mkoa wa Kilimanjaro na Ofisa Upelelezi (Detective), Sajenti Atway Omari ambaye aliyekuwa katika timu ya CRT. Kesi hiyo itaendelea tena leo

Simba watanguliza "mashushushu" Mbeya

KOCHA MKUU WA SIMBA, MCAMEROON, JOSEPH OMOG.

KOCHA Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog, amesema kikosi chake hicho kitatua jijini Mbeya kikifahamu wazi kuwa wapinzani wao Mbeya City ni "imara" na wanatakiwa kutumia nguvu za ziada ili kuhakikisha wanapata pointi zote tatu.

Mbeya City inatarajia kuwakaribisha vinara Simba katika mechi ya raundi ya tisa ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayofanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu Sokoine jijini Mbeya.

Akizungumza na gazeti hili jana, Omog, alisema kuwa mechi zote za ligi kwa Simba ni sawa na fainali, lakini za ugenini huwa ni zaidi kutokana na kubadilisha mazingira ya uwanja.

Omog alisema kuwa bado amewaandaa wachezaji wake kuendeleza kasi waliyoionyesha kwenye mechi zilizopita licha ya kupata matokeo ya sare.

"Hakuna mechi rahisi, hakuna timu ndogo, tunacheza ligi moja na hivyo tunatakiwa kupambana katika kila mchezo ili kufikia malengo, lengo letu kubwa ni kutwaa ubingwa na ikiwezekana iwe mapema kabla ya mechi ya mwisho ya msimu," alisema Omog.

Naye Mratibu wa Simba, Abbas Ally, alisema kuwa kikosi cha Simba kitawasili Mbeya leo na kuweka kambi nje ya jiji hilo ili kuendelea na mazoezi kabla ya kuwavaa wenyeji wao.

"Mimi niko Mbeya tayari kwa ajili ya kuweka mambo sawa, tumejipanga kuhakikisha tunafanya vizuri mechi yetu ya Jumapili na ile ya Prisons itakayofanyika Novemba 18, tunajua Mbeya ni pagumu, lakini tutapambana," alisema mratibu huyo.

Aliwataja wachezaji ambao Simba itaendelea kuwakosa kutokana na kuwa majeruhi ni pamoja na Salim Mbonde, Saidi Mohammed na Shomary Kapombe, ambaye bado anaendelea na kliniki maalumu.

Ili kujiandaa na mchezo huo, kikosi cha Mbeya City kilichoko chini ya kocha wake raia wa Burundi, Ramadhani Nsanzurwino, kiliingia kambi juzi huku wachezaji wake ambao ni majeruhi ni Haruna Shamte na John Kabanda

Mashabiki waYanga watolewa hofu

KOCHA WA YANGA, GEORGE LWANDAMINA.

LICHA ya kuwakosa nyota wake wanne, kocha wa Yanga, George Lwandamina, amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kwa kuwa timu yake inauwezo wa kupata matokeo mazuri kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Singida United.

Yanga ipo Singida bila ya washambuliaji wake, Donald Ngoma na Amisi Tambwe pamoja na Thaban Kamusoko na Juma Abdul.
Wakati Ngoma, Tambwe na Kamusoko wakiukosa mchezo huo kutokana na kuwa majeruhi, Abdul anakabiliwa na kadi tatu za njano zinazomfanya kukosa mchezo huo.

Akizungumza na gazeti hili muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kuelekea Singida, Lwandamina, alisema kuwa anaamini wachezaji wake ambao wapo ndani ya kikosi kilichoelekea Singida wanauwezo mkubwa wa kuwakabili wenyeji wao.

"Nina imani na wachezaji wangu wote, tunaenda kukabiliana na Singida United huku nikiamini tunauwezo wa kupata ushindi," alisema Lwandamina.

Alisema wamejitahidi kufanya marekebisho kwenye makosa madogo madogo aliyoyaona kwenye mchezo uliopita.

"Tumefanyia kazi suala la umaliziaji, yapo makosa madogomadogo ambayo niliyaona kwenye mchezo dhidi ya Simba, nataka
tutumie vizuri nafasi tunazozitengeneza ndani ya uwanja," aliongezea kusema Lwandamina.

Cannavaro: Hautakuwa mchezo rahisi

Nahodha wa timu hiyo, Nadir Haroub 'Cannavaro', aliiambia Nipashe kuwa mchezo huo wa kesho hautakuwa rahisi kutokana na ubora wa kikosi cha wapinzani wao.

Alisema Singida United wamefanya usajili mzuri na wanachezaji wenye uzoefu na ligi hivyo wao (Yanga) watacheza kwa tahadhari kuhakikisha wanapata ushindi.

“Singida si timu ya kubeza… tutapambana kuhakikisha tunapata ushindi," alisema Cannavaro.
Mchezo huo wa kesho utachezwa kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida

Nyalandu halazimiki kuandika barua bungeni: Msekwa

Nyalandu halazimiki kuandika barua bungeni: MsekwaDar es Salaam. Spika wa zamani, Pius Msekwa amesema Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu hakuwa analazimika kuandika barua kwa Spika wa Bunge wala CCM kwani kuonyesha kwake nia ya kujiunga na Chadema kulitosha kuthibitisha hilo.


Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana, Msekwa ambaye ni makamu mwenyekiti wa CCM mstaafu, alisema kilichomwondoa Nyalandu CCM ni kifungu cha 13 (f) cha Katiba ya CCM kinachoeleza kuwa mtu aliyejiunga na chama kingine chochote cha siasa anapoteza sifa ya kuwa mwana CCM.

“Kilichomwondoa Nyalandu ni kujiunga na chama kingine kinyume na kifungu cha 13 (f). Kuandika barua ni utaratibu tu wa kutoa taarifa kwa chama au Bunge ili wajue,” alisema Msekwa.

Alisema mbali na katiba ya CCM, hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema mtu aliyejivua uanachama wa chama cha siasa anapoteza sifa ya kuwa mbunge.

“Kuandika barua ni utaratibu tu... Chama pia kinaweza kumwandikia Spika ili ajue kwamba yule siyo mwanachama wake,” alisema.

Mbali na mazungumzo ya simu, baadaye Msekwa alituma ujumbe wa maandishi (sms) kupitia simu yake ya mkononi akisisitiza suala hilo.

“Nathibitisha tu maneno niliyoyasema kwenye simu kuhusu Nyalandu na mambo yake. Ni kwamba Nyalandu amepoteza uanachama wake wa CCM kutokana na ibara ya 13(1)(f) ya Katiba ya CCM. Na amepoteza ubunge wake kutokana na Ibara ya 71(1)(f) ya Katiba ya nchi. Hakuna haja ya yeye kuandika barua kwa chama au kwa Spika.

Aliongeza: “Kwa mfano, wakati mimi nikiwa Spika, Mhe. (Augustino) Mrema alikuwa Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi. Halafu akaamua ghafla kuhamia TLP. Hakuna barua niliyoandikiwa kuhusu jambo hilo. Lakini tamko lake lilitosha kuniwezesha kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwamba nafasi ya Mrema bungeni ilikuwa wazi kwa hiyo Tume ikachukua hatua za kuijaza. Hakuna utata wowote kuhusu Nyalandu,” alisema Msekwa.

Utata wa barua

Msekwa ametoa ufafanuzi huo wakati kukiwa na sintofahamu kuhusu barua ya Nyalandu kama imepokewa na Ofisi ya Bunge au la.

Wakati Ofisi ya Spika ikisema haijapokea barua hiyo, Nyalandu ameibuka na kuonyesha barua aliyoituma katika mhimili huo.

Nyalandu alimwandikia Spika Ndugai barua hiyo ambayo Mwananchi limeiona Oktoba 30, siku ambayo alitangaza kujiuzulu nafasi zote ndani ya chama hicho ukiwamo ubunge.

Lakini juzi, Ofisi ya Bunge katika taarifa yake ilisema haijapokea barua hiyo badala yake imepokea ile ya CCM Oktoba 30 ikieleza kuwa Nyalandu amepoteza sifa ya kuwa mwanachama wake.

Siku hiyo, Spika wa Bunge, Job Ndugai alihojiwa na Azam TV na kusema kuwa alikuwa hajapokea barua ya Nyalandu lakini hakusema kama alikuwa amepokea ile ya CCM. Alisema endapo angeipata (Barua ya Nyalandu) na kuthibitisha kujiuzulu kwake, angeshauriana na wasaidizi wake kabla ya kuchukua uamuzi.

Ikinukuu barua ya CCM, Taarifa ya Bunge inasema kuwa chama hicho kimekuwa kikifuatilia vitendo na kauli za Nyalandu zisizoridhisha kinyume cha misingi, falsafa na itikadi ya CCM.

“Hivyo, Chama cha Mapinduzi kuanzia tarehe ya barua yao kimemjulisha Mheshimiwa Spika kuwa Lazaro Nyalandu amepoteza sifa za uanachama wa Chama cha Mapinduzi na hivyo kupoteza nafasi zote za uongozi wa ndani wa chama hicho na ubunge kwa mujibu wa ibara ya 13 ya chama hicho,” inasema taarifa hiyo ya Bunge.

Taarifa hiyo inasema kutokana na barua hiyo, Nyalandu amekoma kuwa mbunge na hatua stahiki za kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi zinaendelea kuchukuliwa.

Hata hivyo, mara baada ya mbunge huyo kutangaza kujiuzulu, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole alikaririwa akisema Nyalandu ametumia haki yake ya kikatiba inayompa haki kila Mtanzania kuwa mwanachama wa chama chochote.

“Ibara ya 20 ya Katiba ya Jamhuri inaeleza kuwa kila Mtanzania ana haki ya kuwa na chama. Ninachoweza kusema ni kwamba kuna jambo la kawaida kabisa lililotokea na wala siyo kubwa kama linavyodhaniwa.”

Polepole alisema wameondoka wazito kwenye chama na kimebaki kimoja na kwamba Nyalandu si sehemu ya wazito, bali ni mwananchi wa kawaida mwenye haki na si mara ya kwanza jambo hili kutokea.

Barua ya Nyalandu

Katika barua yake kwa Spika Ndugai ambayo Mwananchi imeiona pamoja na mambo mengine, alimjulisha kuwa kama alivyotangaza kupitia mkutano wake wa wananabari ameamua kujiuzulu nafasi yake ya ubunge wa jimbo Singida Kaskazini kupitia CCM.

Mwanasiasa huyo anasema licha ya kuondoka CCM na bungeni, bado anaamini kwamba Tanzania inahitaji kupata Katiba Mpya itakayoweka bayana ukomo wa mamlaka ya mihimili ya utawala (Bunge, Serikali na Mahakama) ili kuondoa mwingiliano unaonekana kufanyika kwa wazi sasa.

“Kwa sasa dola haionekani kuwa na mipaka katika dhana ya uongozi wa nchi na hivyo kufanya uwakilishi wetu wa wananchi bungeni kuwa legevu kuliko ilivyokusudiwa kikatiba.”

Nyalandu anawashukuru wabunge wenzake, Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani bungeni Freeman Mbowe, maspika wastaafu, Pius Msekwa, Samuel Sitta na Anne Makinda pamoja na Ndugai kwa ushirikiano waliomuonyesha katika vipindi vinne alivyokuwapo bungeni hapo ambako “Alifanya kazi kwa mapenzi makubwa, dhamira ya dhati na moyo mkunjufu.”

Katika barua yake hiyo, Nyalandu anadai kwamba dola imeingilia kwa kiasi kikubwa mfumo wa utendaji na uendeshaji wa CCM hadi kukosa uelekeo, jambo ambalo alisema linawaondolea au kuwapunguzia wabunge wake uwezo wa kufanya uamuzi binafsi wakati wa mijadala au katika kupiga kura kwa kadri ya dhamira zao zinavyowaongoza kama ilivyokuwa wakati wa mchakato wa Katiba Mpya.

Source: Mwananchi

Waziri Nchemba ameonekana mazoezi ya Singida Utd kulekea mechi vs Yanga




 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Mwigulu Nchemba ambaye ni mdau mkubwa timu ya Singida United leo Ijumaa asubuhi alikuwepo kwenye mazoezi ya mwisho ya timu hiyo kwenye uwanja wa Namfua Singida kuelekea mechi yao ya kesho dhidi ya Yanga.

Waziri Nchemba amekuwa karibu na Singida United tangu ikiwa ligi daraja la kwanza, baada ya timu hiyo kupanda kucheza VPL kwa mara nyingine baada ya muda mrefu bado amekuwa akionekana viwanjani kuisapoti kwa karibu.

Kumbuka kuwa, Waziri Nchemba ni Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi (Singida) mahali ambapo ni nyumbani kwa Singida United.

Waziri Nchemba pia alipiga penati kadhaa katika mazoezi hayo ya mwisho ambayo yalishuhudiwa na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo ambayo wataishuhudia kwenye uwanja wao wa nyumbani Namfua mjini Singida.

Uwanja wa Namfua utakuwa ukitumika kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa msimu huu, Singida United walikuwa wakiutumia uwanja wa Jamhuri Dodoma kupisha ukarabati wa uwanja wa Namfua.

Kwa mujibu wa Ibrahim Mohamed maneja wa Singida United, Nizar Khalfani ndio mchezaji pekee mwenye majeraha ambaye hajafanya mazoezi ya mwisho ya pamoja kwa hiyo ataukosa mchezo wa kesho.

“Nizar Khalfani ndio mchezaji pekee ambaye hata kuwa sehemu ya mechi ya kesho kwa sababu anasumbuliwa na majeraha, wachezaji wengine wote wako vizuri kabisa na wamefanya mazoezi ya pamoja.

TANGAZO: TUNZA GARI YAKO NA KICHOCHEO CHA NANO ( NANO ENERGIZER )

TANGAZO: TUNZA GARI YAKO NA KICHOCHEO CHA NANO ( NANO ENERGIZER )


Tunakitambulisha kichocheo madhubuti cha Nano  kilichothibitishwa ubora wake na shirika la 
viwango la kimataifa (ISO 9001:2015). Hii ni teknolojia ya kipekee na ya kimapinduzi kwenye tasnia ya magari na mitambo. kichocheo cha Nano kimetengenezwa na teknolojia ya kisasa duniani ya Nano (Nano technology) kwa ajili ya kuikarabati na kuipa ulinzi injini ya gari yako bila kuifungua. Kichocheo cha Nano huziba mikwaruzo yote ndani ya injini na kuirudisha nguvu ya injini kama ilivyokuwa mpya. Wasiliana nasi kupitia Namba 0715480174


Kichocheo cha Nano kinaipa injini ganda au tabaka gumu la ceramic na platinum. Tabaka hili linafanya muunganiko wa kudumu na chuma cha injini (cylinder wall) na kina uwezo madhubuti wa kuhimili uchakavu na michubuko itokanayo na msuguano. Inarudisha uwezo wa kusukuma wa injini (compression ratio) kwa kuweka ganda gumu kwenye ukuta wa cylinder.

FAIDA ZA KICHOCHEO CHA NANO.

  1. Hupunguza matumizi ya mafuta kwa 8% - 21%.
  2. Huongeza nguvu ya injini hadi kufikia 100%.
  3. Hupunguza mlio na makelele ya injini na mtetemo hadi Mara 5 zaidi.
  4. Inatoa ulinzi wa injini hadi kufikia 40000 km.
  5. Husaidia Kuboresha uhai wa injini na vifaa vingine.
  6. Hulinda injini na kuirudisha kwenye ubora wake kama ilivyokuwa mpya.
  7. Huongeza msukumo wa injini na kuboresha uunguaji wa mafuta.
  8. Hulainisha usukani na gear box.
  9. Hupatikana kwa magari ya aina zote, generator, compressor, pikipiki, bajaji na kila aina ya mtambo.
  10. Hupunguza utoaji wa moshi kati ya mara 3 hadi 9.
  11. Ina garantii ya utendaji kazi kwa 100%.
  12. Haiharibiki kwa nanma yoyote ile.
  13. Bidhaa bora kabisa iliyothibitishwa kimataifa na kitaifa.
  14. Inakupa faida ya kutoifungua injini hivyo kuongeza thamani ya gari hata ukitaka kuiuza.
  15. Inakupa faida ya kupata mafuta bure kila unapoweka kwa mara ya 9.
  16. Faida isiyolinganishwa ya ulinzi wa gari lako hadi kufikia km 40000 kwa sh 60000 tu ukilinganisha na gharama za  mafuta na services kwa kipindi hicho.


MATUMIZI

  1. Injini inatakiwa iwe imetumika kwa km 3000.
  2. Kichocheo cha Nano kinatumika kwa injini za aina yoyote inayotumia oili ya aina yoyote (mineral or synthetic oils).
  3. Ili kupata matokeo bora zaidi weka unapofanya service.
  4. Ipashe injini yako.
  5. Tikisa kichocheo cha Nano kabla ya kuweka kwenye injini.
  6. Fungua kifuniko cha injini oili halafu mimina kichocheo cha Nano.
  7. Funga kifuniko. Hongera, umefanikiwa.
  8. Baada ya kumimina kichocheo cha Nano usibadili oili ya injini mpaka kipindi cha matumizi yafuatayo (kilomita 400 kwa pikipiki na bajaji, kilomita 1200 - 1500 kwa magari madogo na kilomita 3000 kwa malori na mabasi).


MAPENDEKEZO.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio na kukubaliwa na taasisi zifuatazo.

  • Chuo kikuu cha Taifa cha Kyungpook - Korea.
  • Chuo Kikuu cha Taifa cha Seoul - Korea.
  • Taasisi ya Korea ya Mashine na Vifaa.
  • Chuo Kikuu cha Yeungnam - Korea.
  • Taasisi ya Korea ya Teknolojia ya magari.
  • Jeshi la ulinzi wa Taifa la Korea.
  • Kituo cha Jeshi la Anga la India.


UTHIBITISHO WA UBORA.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio maabara, kuthibitishwa, kukubalika na kutunukiwa vyeti vya ubora na taasisi zifuatazo.


  1. Shirika la Ubora la Kimataifa ISO 9001:2015.
  2. Shirika la viwango la Tanzania - TBS.
  3. Mkemia mkuu wa serikali ya Tanzania - GCLA.
  4. Maabara ya kimataifa ya SGS.
  5. Maabara ya kimataifa ya TUV SUD Industrie Service GmbH.


USHUHUDA / MAPENDEKEZO.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio na makampuni ya kutengeneza magari, kimethibitishwa na kupendekezwa kutumika na makampuni yafuatayo.
  • MERCEDES BENZ
  • TOYOTA
  • GM DAEWOO
  • VOLVO
  • HONDA
  • HYUNDAI
  • AUDI
kichocheo cha Nano sasa kinapatikana Tanzania na kusambazwa na POWER ENERGY ENGINEERING COMPANY LTD. Tunakaribisha mawakala kutoka wilaya zote za Tanzania. Wasiliana nasi kupitia Namba 0715480174.

Kwa wafanyabiashara: usiikose fursa hii ya kibiashara.
Kwa wamiliki wa vyombo vya moto (Magari, pikipiki, bajaji nk): Tumia Kichocheo cha Nano kwa ulinzi madhubuti wa chombo chako.




WASAMBAZAJI WA NANO MIKOANI- TANZANIA

DAR ES SALAAM
UBUNGO OIL COM Jengo la oil com juu kwenye bango la Bima 0715 480 174   
RealMaps Mtaa wa sikukuu/mkunguni kariakoo 0755 366 658 0713 360 040                  
Dubai traders Livingston/mafia Kariakoo 0716 302 626   
Luesha central Mtaa wa msimbazi/ mvita jingo la kisangani 0768 820 344   
Japan auto spare parts Mwenge( karibu na Maryland bar) 0714 363 637   
Bk japani auto spare parts Segerea stand karibu na Fantasy park 0653 519 653  0758 519 653   
Darajani Geraji Darajani ubungo karibu na Land Mark Hotel 0765 447 803  0686 615 298   


MOSHI KILIMANJARO
Mshiu 0714 229 079
  
MOROGORO
Jumbo Lubnzants Morogoro eneo la Fine Mazimbo Road 0715 003 738   
Nuba auto Auto Accessories Mtaa wa Fine morogoro 0653 129 307
  
DODOMA
Temu auto parts Mtaa wa mji mpya chenja Dodoma 0754 265 211  0715 265 211   
Nuba auto Accessories Eneo la CBE Dodoma 0653 746 907
  
MWANZA
GT. Sahara general supplies Pamba Road mwanza0754 560 284   0754 560284   
Libety mkabala na Coconut Hotel mwanza 0626 450 450   

GEITA  
Kashakara auto spare parts Nyerere Road Geita
  
SHINYANGA
Green Star Expresses Stendi ya mikoani 0766 876 057     0759 933 290   
Phanuel  jeremia  Machinjioni eneo la viwanda shinyanga 0755 042 505  0787 592 871   

SINGIDA
Bingo spare Centre Standi ya zamani C Bomba la maji mkabala na Asma Hotel Singida  0755 961 679 0712 504 579
   
ZANZIBAR
Bengkok Accessories Kwa Biziredi mkabala na Bin Rashid Madawa 0779 959 850   0788 106 469   

Kwa maelezo zaidi na kutaka uwakala katika wilaya na mikoa ya Tanzania piga simu No: 0715 480 174


Republican wabuni mbinu za marekebisho ya kodi

Wanachama wa Republican nchini Marekani wamebaini mpango wa marekebisho ya kodi kubwa kwa kipindi cha miaka 30 ijayo.

Marekebisho hayo ya kodi, yamekuwa kipaumbele cha ajenda za Rais Donald Trump.
Mapendekezo yaliyotolewa ni pamoja na kupunguza kodi katika biashara kutoka asilimia 35 hadi asilimia 20 na kupandisha posho binafsi ya kodi.

Marekebisho mengine yaliyopendekezwa ni kuondoa viwango vya kodi katika magari ya umeme, hali itakayo waathiri watengenezaji wa magari kama vile kampuni ya general Motors,Tesla na Nissan.

Mpango huu wa Republican ambao unapaswa kuidhinishwa na bunge Congress, unatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa deni la taifa

Mawaziri wawekwa kizuizini Catalonia



Raia wa jimbo la Catalonia wanaotaka kujitenga wameandamana nje jengo la bunge la jimbo hilo mjini Barcelona baada ya jaji mjini Madrid kuwaweka kizuizini mawaziri nane wa serikali ya jimbo la Catalonia.

Taarifa zinasema kuwa hadi sasa kuna jumla ya wanasiasa kumi wa Catalonia waliowekwa kizuizini nchini Hispania wakiwemo pia viongozi wa kitamaduni wawili ambao nao wanashikiliwa.

Jaji Carmen Lamela amesema kuwa aliamua kuwaweka kizuizini viongozi hao nane kwa kuhofia kwamba wanaweza kutorokea nje ya nchini ama kuharibu ushahidi.

Waendesha mashitaka wanawatuhumu wanasiasa hao kwa makosa mawili ambayo ni mapinduzi na uchochezi katika jaribio la kutaka kujitenga na Hispania.

Hata hivyo jaji bado hajatoa kibali cha kukamatwa nje y nchi kwa kiongozi wa watu wa jimbo la Catalonia Carles Puigdemont na wenzake wane ambao wote wapo nchini Ubelgiji.



MAGAZETI YA LEO 3/11/2017


MAGAZETI YA LEO 3/11/2017




Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download

Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download


Enock Bella - Sauda

Audio | Enock Bella – Sauda | Mp3 Download

                                       
https://my.notjustok.com/track/download/id/287696/by/eM_J1W76fP

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download

Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees - Double Double

Audio | Nyandu Tozzy Ft. Young Dee , Chin Bees – Double Double | Mp3 Download


https://my.notjustok.com/track/download/id/287534/by/6NAtshXQUW