Tuesday, 31 October 2017

Baada ya Uwoya kuonekana ameolewa, mume wake ajibu mapigo

Baada ya Uwoya kuonekana ameolewa, mume wake ajibu mapigoAliyekuwa mume halali wa muigizaji wa filamu bongo Irene Uwoya, mcheza soka kutoka nchini Burundi Hamad Ndikumana, ameonyesha kujibu mapigo baada ya mwenza wake kuonekana kuolewa, kwa kupost picha akiwa na mwanamke mwengine.


Kwenye ukurasa wake wa instagram Ndikumana amepost picha hizo, huku akiandika ujumbe kama ambao unaonekana ni kurusha vijembe kwa mwenza wake huyo, ambaye hivi karibuni alimuandikia waraka kuanika yale aliyokuwa akithubutu kuyafanya, na kusema yuko tayari kutoa talaka.

Wawili hao walitfunga ndoa takatifu katika kanisa la Mtakatifu Joseph la Jijini Dar es salaam, na kutengana baada ya muda mfupi wa ndoa yao, huku kukiwa na tetesi kuwa hakuna maelewano baina yao.

Tazama mapicha aliyopost Ndikumana

Mtandao wa WhatsApp Waruhusu Kufuta Ujumbe

Ilishawahi kukutokea kutuma ujumbe, picha au video au documenti yeyote kwa mtu usiyemkusudia kwa bahati mbaya kupitia programu ya WhatsApp? kama huwa unapatwa na matatizo hayo sahau kabisa kwani tayari programu hiyo imeshaongeza sehemu ya kufuta jumbe hizo.

WhatsApp is rolling out the Delete for Everyone (Recall) feature for all users! 🎉https://t.co/3bnbgxtPvU

— WABetaInfo (@WABetaInfo) October 26, 2017

WhatsApp tayari imezindua huduma hiyo ambayo imeongezwa kwenye programu kwa jina ‘Delete For Everyone’ ambapo mtumaji wa ujumbe, picha au video atachagua kufuta kwake au kwa mtu aliyemtumia kimakosa.



Kwa sasa huduma hiyo inapatikana kwa watumiaji wote wa iOS na Android kama bado basi cha kufanya update programu yako ya WhatsApp ili uanze kutumia.

Hii inakuwa hatua nyingine ya maboresho ya programu hiyo baada ya kutangaza kuongeza sehemu ya Live Chart  ndani ya mwaka huu.

Mwanzoni mwa mwezi Agosti mwaka huu WhatsApp Inc walitangaza kuwa wataleta mabadiliko makubwa manne ndani ya mwaka huu ambayo yataifanya programu ya WhatsApp kuwa ya kisasa zaidi.

Twambie wewe mtumiaji wa programu pendwa ya WhatsApp umeyapokeaji mabadiliko haya.

Majibu ya joti kwa Waliomsema Kafunga Ndoa na Kiduku

Jumamosi iliyopita ilikua harusi ya Mchekeshaji maarufu Tanzania Lucas Muhavile maarufu kama Joti ambapo gumzo lilikua pia nywele zake alizonyoa kwa staili ya kiduku na kuingia nacho Kanisani jambo ambalo lilifanya baadhi ya watu kuongea sana kwenye mitandao.

Joti kwenye Exclusive Interview ambapo amewajibu waliomsema kuhusu kiduku chake, >>> “Sidhani kama kuna sheria au kuna maandiko yameandika kwamba ukinyoa hivi hutakiwi kufunga ndoa, hii sanasana iko kwenye maadili tu“

“Nilimuomba Padri na akanielewa na kuniambia wewe ni Msanii tunajua cha kufanya usisuke tu, fumua hizo nywele ziwe tu kawaida zibanebane vizuri

Polepole: Nyalandu amejimaliza mwenyewe

Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amemponda aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu akisema walishamweka pembeni kwa kuwa hakuwa mtu wa muhimu kwao.

Akizungumza jana Jumatatu usiku katika kipindi cha Msemakweli kinachorushwa na Channel Ten, Polepole aliyekuwa akizungumzia mafanikio ya Rais John Magufuli kwa kipindi cha miaka miwili, alimtakia heri Nyalandu huku pia akisema amejimaliza mwenyewe.

“Ameondoka mwanachama mmoja wa CCM leo (jana) amekwenda upinzani. Katiba yetu hii ya Jamhuri ya Muungano inasema kila mtu ana uhuru wa kujiunga na chama chochote. Tunaheshimu uamuzi wake, tunamkatia heri katika chama anakokwenda,” alisema Polepole.

“Aliyeondoka leo ni ‘very insignificant’ yaani kwa Kiswahili hatujaona utofauti. Ndiyo maana sisi tumetoa maelekezo kwa Serikali kwamba, watu ambao hawakuweza kutukimbiza katika awamu ya tano kwenye maendeleo ya Taifa letu kwenye uongozi wa awamu ya tano wawekwe benchi kwanza. Sasa wamewekwa benchi,” alisema Polepole.

Hata hivyo alisema Nyalandu ana haki ya kikatiba kuamua kwenda chama chochote anachokitaka na kwa kuwa CCM ni chama cha kidemokrasia hakitamlazimisha kubaki.

“Chama chetu kina watu wengi wakongwe na wa muda mrefu na kitaendelea kuwepo na kinafanya kazi watu wanaona,” alisema.

Alisema kwa kuwa Nyalandu alishawekwa benchi alipaswa ajitafakari na kujipanga upya.

“Unajua unapowekwa benchi uelewe kwamba ama uongeze mazoezi au umeongezeka kilo mbio zako zimepungua, kwa hiyo tunakuweka benchi ujitafakari kwamba hauna msaada kwenye timu,” alisema na kuongeza:

“Sasa ukiwekwa benchi kwa muda mrefu ukapata timu ya mchangani, wanacheza chandimu, wewe unafahamu chandimu? Unatoka daraja la kwanza unakwenda daraja la nne na ndiyo chandimu na ndiyo umekwenda na maji.”
                                                                                                   
Aliendelea kujisifu akisema CCM haina wasiwasi kwa kuwa kiwango chake ni cha juu na wachezaji wake ni wa kimataifa na wametengenezwa vizuri kuwahudumia Watanzania.

Huku akipekua katiba ya CCM, Polepole alimsikitikia Nyalandu akisema anakwenda kwenye chama kisicho na itikadi akiacha CCM yenye itikadi ya ujamaa na kujitegemea.

“Unamtazama mtu amekwenda kutafuta itikadi pahala ambapo kuna itikadi isiyojulikana. CCM itikadi yetu ni nini? Ibara ya nne, ibara ndogo ya tatu, anakwambia itikadi ya CCM ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru,” alisema na kuongeza:

“Sisi ni wajamaa kwa maneno na kwa matendo. Uliza chama anachokwenda itikadi yao ni nini? Kuna malango ya mbinguni na malango ya jehanam. Sisi tunamtakia mafanikio mema

Muigizaji akiri kushiriki mapenzi ya jinsia moja



 Muigizaji mkongwe kutoka Uingereaza Kevin Spacey amefunguka kwa mara ya kwanza na kukiri kushiriki mapenzi ya jinsia moja.

Kevin ambaye ni maarufu pia katika tamthilia ya ‘House of Cards’ ameamua kutoa kauli yake baada ya muigizaji na msanii wa muziki Anthony Rapp kudai kuwa amekuwa akisumbuliwa na Spacey toka aliwa na umri wa miaka 14, wakati huo Kevin ana miaka 26.

Kauli ya Rapp(46) imetoka wakati akifanyiwa mahijiano na Buzzfeed, Hata hivyo Spacey(58) amefunguka na kuadai kuwa alimuomba radhi kijana huyo na kumtaka asionge ila anashangazwa na Rapp kuamua kusema sasa.

Ajibu ajazwa zawadi Jangwani



Mwigizaji na msanii wa filamu nchini Vicent Kigosi maarufu kama ‘Ray’, amewaongoza mashabiki wa Yanga SC kutoka kundi la ‘Yanga For Life’ kwenye mtandao wa WhatsApp kutoa zawadi kwa wachezaji wa timu hiyo.

Ray na wenzake wametoa zawadi ya fedha, viatu na ‘Shin Gard’, mchana wa leo kwa wachezaji watatu, waliofanya vizuri katika michezo ya Ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.

Miongoni mwa wachezaji waliopata zawadi hizo ni mshambuliaji Ibrahim Ajib ambaye amepewa kiasi cha Tsh Milioni moja, baada ya kuibuka nyota wa mchezo kwenye mechi mbili za Kagera Sugar na Stand United.

Kiungo kutoka DRC Papy Kabamba Tshishimbi, ambaye aliibuka nyota wa mchezo wa watani wa Jadi jumamosi iliyopita amepewa zawadi ya shilingi laki tano huku kipa Youthe Rostand, akipata shilingi laki mbili, viatu na ‘Shin Gard’. 

Baada ya kukabidhi zawadi hizo Ray amesema nia ya kundi lao ni kuwapa hamasa wachezaji wao ili waweze kutetea ubingwa wao wa ligi na kutwaa mara ya nne mfululizo

Rais Magufuli afunguka mazito kuhusu wanaohama CCM

Rais Magufuli afunguka mazito kuhusu wanaohama CCM




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa wapo watu ambao walikuwa ni wezi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema saizi watu hao wamekimbilia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Rais Magufuli amesema hayo leo Oktoba 31, 2017 akiwa ziarani mkoani Mwanza ambapo alikuwa akiongea na wananchi wa Mkuyuni na Butimba jijini Mwanza na kusema kuwa yeye anataka maendeleo kwa kuwa anaamini Tanzania inahitaji kujengwa na Watanzania wote na kudai ndani ya vyama vya siasa kuna wezi ambao hao ndiyo wamechelewesha maendeleo ya nchini.

"Tunataka Tanzania mpya hilo ndiyo lengo langu kwa sababu yapo yalikuwa ni majizi makubwa sana Chama Cha Mapinduzi (CCM) yakakimbilia CHADEMA ndiyo maana sijasema CUF oyeee kwa sababu wapo waliomo CUF wengine ni wabaya sana. Mimi nataka maendeleo kwa sababu maendeleo yanaletwa na Watanzania wote tushikamane ndugu zangu tutachelewa tushikamane sasa hivi tuipeleke Tanzania yetu mbele" alisisitiza Rais Magufuli

#Updates : Zitto Aachiwa, Polisi Wamkamata Tena

#Updates : Zitto Aachiwa, Polisi Wamkamata Tena



Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe, ameruhusiwa kwa kudhaminiwa na watu wawili hapa Kituo cha Polisi Chang'ombe, Temeke, Dar es salaam.

Polisi wamemkamata tena baada ya kudhaminiwa kwa amri ya DCI, na muda huu anapelekwa kuhojiwa katika Kituo cha Polisi Kamata.

Ado Shaibu
Katibu - Kamati ya Itikadi, Uenezi na Mawasiliano ya Umma
ACT Wazalendo
Oktoba 31, 2017

Miili 9 iliyokatwakatwa yapatikana kwenye nyumba Tokyo Japan

Miili 9 iliyokatwakatwa yapatikana kwenye nyumba Tokyo Japan




Polisi nchini Japan wamemkamata mwanamume mmoja baada ya kupata viungo vya miili tisa katika nyumba yake iliyo Zama huko Tokyo.

Polisi walipata vichwa viwili kwenye jokovu nje ya nyumba ya mshukiwa kwa jina Takahiro shiraishi, wakati wakichunguza kutoweka kwa mwanamke mmoja.

Pia walipata viungo vya watu saba kwenye majokovu yaliyo ndani ya nyumba yake.
Mtu huyo wa umri wa miaka 27 anashtakiwa kuwa ndiye alitupa miili hiyo.

Polisi walikuwa wamepata miili ya wanawake 8 na mwanamume mmoja, mingine tayari ikiwa imeanza kuoza.

"Niliwaua na nikaifanyia kazi miili yao ili kuficha ushahidi," shirika la habari la NHK lilimnukuu akisema.

Jirani wake alisema kuwa alikuwa ameanza kuhisi harufu mbaya kutoka kwa nyumba yake tangu Bw. Shiraishi ahamie nyumba hiyo mwezi Agosti.

Polisi walifanya ugunduzi huo walipokuwa wakimtafuta mwanamke wa umri wa miaka 23 ambaye amekuwa hajulikani aliko tangu tare 21 mwezi Oktoba.

Wachunguzi waligundua kuwa Bw. Shiraishi amekuwa akiwasiliana na mwanamke huyo baada ya kuandika kwenye mitandao ya kijamii kuwa alikuwa anataka kujiua


Profesa Jay atupa jiwe gizani

Profesa Jay atupa jiwe gizani

Mbunge wa Jimbo la Mikumi Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay ametoa ujumbe unaoonekana kama ushauri kwa vyama vya siasa huku ukilenga matukio ya hivi karibuni ya wanasiasa kuhama kutoka chama kimoja kwenda kingine.

Katika Ukurasa wake wa mtandao wa Twitter Profesa Jay ameandika “Mkimaliza hiyo HOJA yenu Mfu ya UFISADI, leteni tuhuma za wote waliobaki huko na Muwatimue mapema msisubiri waondoke wenyewe... TUMEELEWANA”?

Ujumbe huu wa Profesa Jay umekuja ikiwa ni chini ya saa 24 toka Mbunge wa Singida Kaskazini kupitia CCM, Lazaro Nyalandu ajiuzulu Ubunge pamoja na nyadhifa zingine ndani ya chama ikiwemo kujivua uanachama.

Kwa upande mwingine ujumbe huo umechukuliwa kama jibu kwa Chama cha Mapinduzi ambacho kupitia kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole kilijibu suala la Nyalandu kuhama kwa hoja ya kuwa ni miongoni mwa wanachama wengi wasio waadilifu ambao wameamua kuondoka kabla ya Panga kuwafikia.

Hata hivyo Profesa Jay amegoma kufafanua undani wa ujumbe huo iwapo umelenga kupuuza hoja hiyo ya Ufisadi. Awali Profesa Jay aliandika ujumbe wa kumpongeza Nyalandu kwa uamzi wake na kumkaribisha Chadema. “Hongera sana my brother Lazaro Nyalandu kwa Ujasiri na kusimamia kile unachokiamini!! KARIBU SANA KIUMENI SPEAK YOUR MIND”, aliandika Profesa Jay.

Kiongozi wa Catalonia aliyefutwa "aenda Ubelgiji"



Rais wa Catalonia aliyefutwa Carles Puigdemont ameenda nchini Ubelgiji, wakili wake aliye chini humo anasema.

Wakili huyo Paul Bekaert, hakuzungumzia ripoti kuwa Bw. Puigdemont anajiandaa kuomba kupewa hifadhi.

Mwendesha mashtaka nchini Uhispania ametaka mashataka ya uasi kufunguliwa dhidi yake na viongozi wengine ya kura ya maoni iliyopogwa marufuku.

Serikali ya Uhispania ilichukua udhibiti kamili wa Catalonia siku ya Jumatatu, kuchukua mahala pa viongozi waliofutwa.

Ilifuta utawala wa eneo hilo na kuitisha uchaguguzi mpya baada ya Bw Puigdemont na serikali yake kujitangazia uhuru wiki iliyopita.

Wakili huyo wa Ubelgiji Paul Bekaert alisema kuwa Bw. Puigdemont kwa sasa yuko mji mkuu wa Ubelgiji Brussels.

Mbona Puigdemont akaenda Ubelgiji?
Uhispania ilikuwa imekumbwa na mzozo wa kikatiba tangu kura ya maoni iliyopangwa na serikali ya Bw. Puigdemont, ilipoandaliwa tarehe mosi Oktoba kinyume na amri ya mahakama iliyoamua kuwa kura hiyo ilikuwa kinyume na katiba.

Serikali ya Ctalonia ilisema kuwa asilimia 43 ya wapiga kura walishiriki huku asilimia 90 ya wapiga kura hao wakiunga mkono uhuru

Siku ya Ijumaa bunge la Catalonia likatangaza uhuru, Kisha waziri mku wa Uhispania akatangaza kuvunjwa kwa bunge la eneo hilo na kuondole kwa Bw. Puigdemont kama kiongozi wa Catalonia.

Sababu za kukamatwa Zitto hizi hapa



JESHI la Polisi linaendelea kumshikiria Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kwa mahojiano kwa kosa ya kutoa kauli za uchochezi katika mkutano wa hadhara alioufanya Kata ya Kijichi, Temeke,

Zitto alikamatwa mapema leo asubuhi nyumbani kwake na kupelekwa katika kituo cha polisi cha Chang’ombe kwa mahojiano kwa makosa hayo ambayo anadaiwa kufanya katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za udiwani wa kata ya Kijichi.

Kwa mujibu wa viongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto anahojiwa kwa kutoa maneno yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani kwa wananchi na kujenga chuki kwa serikali yao.

Maneno hayo yaliyopelekea Zitto kushikiliwa na kuhojiwa ni pamoja na kusema: “Wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kufanya uchunguzi na kuwakamata watu waliompiga risasi Mbunge Tundu Lissu mpaka siku hiyo.”

Zitto pia anadaiwa kusema: “Wananchi wasiichague CCM kwa sababu Serikali yake imeshindwa kueleza chanzo cha miili ya watu wanaookotwa kwenye fukwe za bahari kama Coco Beach. Hivyo kuichagua CCM ni sawa na kuwaunga mkono waliofanya vitendo vya kumshambulia Tundu Lissu na wanaoua watu wanaookotwa kwenye fukwe.”

Timu ya mawakili wa chama cha ACT-Wazalendo na ndugu na jamaa wa Zitto wapo pamoja naye katika mahojiano hayo na wataendelea kutoa taarifa kila kinachoendelea

900 wasimamishwa shule, kisa binti mmoja

900 wasimamishwa shule, kisa binti mmoja


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, karibu wanafunzi 900 wa Shule ya Sekondari Kabale katika Manispaa ya Kabala nchini Uganda wamesimamishwa masomo kutokana na vurugu kubwa zilizoibuka shuleni hapo, chanzo kikielezwa ni kumgombea kimapenzi binti mmoja ambaye pia ni mwanafunzi shuleni hapo.

Wanafunzi hao waliibua vurugu kubwa na kuanza kupigana mchana wa Ijumaa iliyopita shuleni hapo. Inaelezwa kuwa, mwanafunzi wa kidato cha sita aliomba kuwa na uhusiano na binti ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi mwingine wa kidato cha nne.

Kutokana na kuvuja kwa taarifa hizo, makundi mawili ya wavulana hao yaliibua uhasama ulioishia kupigana. Ugomvi huo haukuishia kwa wanafunzi tu, waliharibu pia mali za shule na hata za majirani wanaoishi karibu na shule hiyo.

Kutokana na hali hiyo, jeshi la Polisi lililazimika kuingilia kati kutuliza ghasia kwa kutumia mabomu ya machozi na silaha nyingine kutawanya wanafunzi hao. Kaimu Ofisa anayeshughulikia usalama wilayani Kabale, Kenneth Birungi amethibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kuongeza kuwa, timu ya wanausalama baadaye ilikutana na uongozi wa shule na kukubaliana kuwasimamisha masomo wanafunzi hao, huku Bodi ya Shule ikitarajiwa kutoa uamuzi juu ya hatima yao.