Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Sunday, 4 February 2018
VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja
VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja

VIDEOS New VIDEO: Fally Ipupa ft. R. Kelly – Nidja
New VIDEO: Seyi Shay – Bia
New VIDEO: Seyi Shay – Bia

New VIDEO: Seyi Shay – Bia
Nigerian music star Seyi Shay has released the visuals for her current song BIA and it’s a must-see.
Shot by Clarence Peters, the Afro Pop jam with salsa elements is sure to capture minds from start to finish. It dropped officially on Thursday, February 1, 2018 and is a complete dose of freshness, energy and entertainment from the sexy singer. Seyi’s charm and creativity are infectious in this clip and fans can rest assured there’s more to come.

New VIDEO: Seyi Shay – Bia
Nigerian music star Seyi Shay has released the visuals for her current song BIA and it’s a must-see.
Shot by Clarence Peters, the Afro Pop jam with salsa elements is sure to capture minds from start to finish. It dropped officially on Thursday, February 1, 2018 and is a complete dose of freshness, energy and entertainment from the sexy singer. Seyi’s charm and creativity are infectious in this clip and fans can rest assured there’s more to come.
Shelisheli waanza mchecheto dhidi ya Yanga
St Louis ya Shelisheli
WAKATI wakiwa wanajiandaa kuvaana na Yanga kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, uongozi wa klabu ya St Louis ya Shelisheli umeanza mchecheto.
Timu hiyo inakuja nchini kucheza na Yanga Febrauri 11, mwaka huu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar. Meneja wa St Louis, Davis Khan aliidai kuwa; “Kucheza michuano hii wakati ligi yetu imeisha kunachangia sisi kufanya vibaya tena ukiangalia wapinzani wetu wao wanaendelea kucheza na wanashinda katika michezo yao migumu.”
Yanga wakiendelea na mazoezi yao.
“Pia katika wakati huu tunasaka kocha mwingine baada ya yule wa awali kujiuzulu, ambapo kocha huyo atakuwa na muda mdogo sana kabla ya kucheza kwa mchezo wetu huo na Yanga, ila tunajaribu kuwa na mtu haraka iwezekanavyo,” alisema Khan kupitia kwenye moja ya mitandao ya nchini kwao.
St Louis watacheza na Yanga kwenye michuano hiyo baada ya kuwa mabingwa wa Ligi ya Shelisheli ambayo ilimalizika mwezi Novemba mwaka jana.
Panya wawapa Wakulima wakati mgumu Morogoro

Wakulima wa Kata ya Kiberege Wilayani Kilombero mkoani Morogoro, wamejikuta katika wakati mgumu, baada ya mazao yao kuvamiwa na panya waharibifu, na kusababisha uharibifu mkubwa katika mazao ya mpunga na mahindi ambayo wameyapanda katika msimu huu.
Wakulima wa kata hiyo wamesema tatizo hilo limeanza kwa muda mrefu, na cha kushangaza licha ya mvua kunyesha bado panya hao wameendelea na uharibifu, hali ambayo inawapa mashaka juu ya hali ya chakula itakavyokuwa msimu huu.
Aidha wakulima hao kutoka katika vijiji vya Nyamwezi na Misufini, wamedai ndiyo mara ya kwanza kuwanaona panya hao wakiharibu mazao yao.
Naye Afisa Kilimo wa Kata ya Kiberege amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na ameeleza kuwa Serikali ya Wilaya hiyo imeanza kuchukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha inakabiliana na tatizo hilo.
Lulu Diva apokonywa kila kitu na Mpenziwe?

IMEVUJA! Ukiachana na habari ya kudaiwa kupangishiwa nyumba na kununuliwa gari mpya aina ya Jeep na kigogo, imebainika kuwa msanii huyo amepokonywa kila kitu alichokuwa amepewa na mpenzi wake wa zamani aitwaye Joho.
Hivi karibuni, Lulu Diva aliripotiwa kuwa amepangiwa nyumba na kupewa gari jipya ambapo aliibuka sosi mwingine na kudai kuwa Lulu si mkweli, aliyenunua gari hilo ni mpenzi wake Joho ambaye alikuwa akiishi naye kinyumba kwa takriban miaka mitatu kiasi cha kufikia hatua ya kutolewa mahari ambayo ilirudishwa hivi karibuni na hata hivyo gari hilo amepokonywa hayuko nalo tena.
Akipiga stori na Risasi Jumamosi kwa sharti la kutotajwa jina sosi huyo alisema kuwa anawajua vilivyo Lulu na Joho kwa sababu Joho ni rafiki yake hivyo anachokisema yeye ana uhakika nacho kwamba Lulu hajanunuliwa gari bali ni lile lile alilopewa na Joho.
“Hivi mnajua kuwa huyo Lulu ni muongo mbona gari analosema amepewa na kigogo ni la rafiki yangu Joho alimnunulia na walikuwa wakiishi pamoja ila kwa sasa ameachana naye na ninavyojua amechukua vitu vyake.
“Hii yote ilikuja baada ya jamaa kumshtukia kuwa Lulu anatembea na msanii mwenzake, Rich Mavoko,” alisema sosi huyo.
Sababu ya Ndege kuanguka yajulikana Z'bar
Hitilafu ya mfumo wa umeme imetajwa kuwa chanzo kikuu cha ajali ya ndege ambayo ilisababisha vifo vya watu wawili juzi visiwani Zanzibar.
Ajali hiyo ilitokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume majira ya saa 7:00 mchana, wakati ndege hiyo ikijaribu kuruka.
Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji (NIT) cha Dar es Salaam, Dk. Bwire Rufunjo, alisema jana kuwa uchunguzi zaidi wa chanzo cha ajali hiyo unaendelea hata hivyo.
Dk. Rufunjo alisema katika hatua za awali wamebaini chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu katika mfumo wa umeme wa ndege kusabisha moto uliozaa mlipuko kutokana na ndege kuwa na mafuta mengi.
Alisema ndege hiyo yenye usajili wa 5H-TDF yenye uwezo wa kubeba abiria wanne ni mali ya NIT na ilikuwa Zanzibar kwa ajili ya matengenezo.
“Wakati ikiwa katika matengenezo, marubani wetu walikuwa wakiifanyia majaribio ili kuweza kufanya kazi yake ambayo ilikuwa kwa ajili ya ufundishaji wa wanafunzi wetu wanaochukua mafunzo ya urubani,”alisema mkuu huyo wa chuo.
Alisema waliofariki katika ajali hiyo ni Injinia Edger Mcha (26) na rubani Dominic Bomani (64) ambao ni wafanyakazi wa NIT.
Daktari bingwa wa uchunguzi katika Hospital Kuu ya Mnazi Mmoja, Dk. Msafiri Marijani, alisema vifo vya watu hao vilisababishwa na kukosa hewa safi wakati ajali ilipotokea.
“Marubani hao walikosa msaada kwa muda mrefu tangu ndege hiyo ianguke na kulipuka,” alisema.
Serikali ya Zanzibar imesema kuwa imepokea kwa mshtuko mkubwa vifo vya marubani hao kutokana na ajali hiyo na uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea.
Mama Mobeto amfungukia Diamond
KUFUATIA skendo nzito inayofukuta ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kudaiwa kutoka kimapenzi na warembo, Wema Isaac Sepetu na Tunda Sebastian, mama mzazi wa mwanamitindo Hamisa Mobeto, Shufaa Lutigunga ‘amemtapika’ jamaa huyo kuwa vitu vyote vinavyoendelea kwenye mitandao ya kijamii havihusiani na mwanaye.
Akizungumza na gazeti hili, mama Mobeto alisema kuwa, kwa sasa, kwa upande wao, yeye na mwanaye Mobeto hawataki malumbano na kuwekana kwenye mitandao wa kijamii ndiyo maana hawataki kusikia habari zinazomhusu Diamond.
Alisema kuwa, muda huo wa malumbano hawana kwa sababu mwanaye anaendelea na maisha yake mengine kabisa ya kutafuta maendeleo na jinsi gani ya kuwalea watoto wake na si kumtegemea mwanaume huyo.
“Jamani sisi mambo hayo ya kwenye mitandao muda huo hatuna tena. Hata mtoto wangu (Mobeto) ameshayasahau mambo hayo na badala yake yupo bize na mambo yake mengine kabisa,” alisema mama Mobeto.
Mama Mobeto aliendelea kueleza kuwa, mtoto wake yuko kwenye mchakato mkubwa wa kufungua biashara yake ya lipstiki hivyo muda wa kufuatilia chochote kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii hana.
“Michakato yetu sisi zaidi ni kutafuta pesa na si vingine. Muda wa kuchokonoana kwenye mitandao hatuna kwa sababu tukifanya hivyo hatuwezi kupiga hatua hata siku moja, lakini kama kuna watu wanaweza kufanya hivyo, wafanye kwani sisi tulishajivua siku nyingi sana na wala hatutaki kumsikia huyo Diamond na mambo yake,” alisema mama Mobeto.
Saturday, 3 February 2018
Nchemba awataka wanaotoa vitambulisho wawe makini
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wanaosimamia usajili wa wananchi kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho wa Taifa kuwa makini.
Akizungumza leo Februari 3, 2018 katika uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho hivyo kwa wakazi wa Tabora, Mwigulu amesema umakini huo utasaidia vitambulisho hivyo kutotolewa kwa watu wasiostahili.
Amesema miaka ya nyuma wakati utaratibu wa kutoa vitambulisho hivyo haujaanza, baadhi ya raia wa kigeni walikuwa wakitumia mwanya huo kunufaika na huduma za jamii kama elimu.
“Watu hao walipomaliza masomo walirejea katika nchi zao na kuzinufaisha kwa namna moja au nyingine wakati wametumia pesa za watanzania. Mnapaswa kuwa makini ili kubaini wageni,” amesema Mwigulu.
Amesema kila mwananchi anatakiwa kuwa mlinzi wa mwenzake ili kuhakikisha hakuna mgeni anayepenya na kupata kitambulisho hicho.
“Uandikishaji na utoaji wa vitambulisho hivi ni bure. Wananchi hawapaswi kutozwa fedha yoyote,” amesema.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Andrew Massawe amesema lengo ni kuhakikisha mpaka Desemba, 2018 utoaji wa vitambulisho hivyo uwe umefanyika nchi nzima.
Ametaja faida za vitambulisho hivyo kuwa ni kusaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi na wananchi kutambulika haraka wanapokwenda kupata huduma mbalimbali, zikiwemo afya na elimu
Wanaofanya udanganyifu kwenye asasi za kiraia waonywa
Asasi za kiraia zimetakiwa kufuata taratibu kabla ya kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi ili kukwepa udanganyifu, ikiwa ni pamoja na kuwachangisha fedha na kutokomea kusikujulikana.
Kauli hiyo imetolewa leo Februari 3, 2018 na ofisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Temeke, John Bwana wakati akizindua mradi wa kuwajengea wanawake uwezo kuhusu ujasiriamali ili kujiinua kiuchumi ulioandaliwa na asasi ya Iwapoa.
Amesema kuna lundo la asasi za kiraia zinazotoa mafunzo kiholela na kuwatapeli wanawake kwa kuwachangisha michango na kutokomea na fedha zao.
“Iwapoa mmefanya jambo la maana kufuata taratibu za kuonana na mamlaka husika na kupata wataalamu kutoka katika kata mtakazofanya kampeni hii ya kupunguza umasikini kwa kuwajengea wanawake uwezo,|” amesema na kuongeza,
“Nawaunga mkono na ninatoa rai kwa asasi nyingine zisizofuata utaratibu zifanye hivyo mara moja kwa sababu tunazifuatilia na tukizibaini tutazizuia kufanya kazi zake katika maeneo yetu.”
Mratibu wa mradi huo kutoka Iwapoa, Yusuph Kutegwa amesema mradi huo utatekelezwa katika kata sita za Manispaa ya Temeke.
Amezitaja kata hizo kuwa ni Buza, Keko, Chamazi, Vituka, Azimio na Charambe.
Amesema utawafikia wanawake 150 kutoka katika maeneo hayo waliyoyachagua kutokana na kuwa na wingi wa watu, wakiwamo wanawake wasiokuwa na shughuli za kudumu.
“Ili kuwapatia masoko na mitaji tutawaunganisha katika vikundi vya watu watano watano, ili iwe rahisi kuwapa ujuzi kwa pamoja, ”amesema Kutegwa.
Nduda, Mbonde njiani kurejea dimbani
Mlinda mlango namba mbili wa Simba, Said Mohammed 'Nduda' wiki ijayo anatarajia kujiunga na wenzake tayari kuanza mazoezi baada ya kuwa nje kwa miezi mitano, kufuatia kufanyiwa upasuaji wa goti Oktoba mwaka jana nchini India.
Nduda aliyesajiliwa na klabu ya Simba Julai mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro, hajacheza mechi yoyote msimu huu kutokana na maumivu ya goti aliyoyapata Agosti mwaka jana mazoezini akiwa visiwani Zanzibar wakati Simba inajiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wa jadi, Yanga Agosti 23, mwaka jana Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Kwa sasa mlinda mlango huyo ameanza programu za mazoezi yake binafsi tangu mwanzoni mwa mwaka huu, akijifua ufukweni kwa mazoezi.
Wakati huo huo, beki wa kati wa Simba, Salim Mbonde anaendelea na mazoezi ya gym baada ya kuwa nje kwa zaidi ya miezi mitatu kufuatia kuumia Oktoba 15, mwaka jana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya timu yake ya zamani, Mtibwa Sugar uliomalizika kwa sare ya 1-1 mjini Dar es Salaam.
Kiongozi mwengine wa Upinzani akamatwa Kenya
Mbunge mwingine nchini Kenya, amekamatwa kuhusiana na mzozo unaozunguka kujiapisha kwa aliyekuwa waziri mkuu Raia Odinga kwa kile anachokitaja kama rais wa watu wa Kenya.
Mbunge wa Makadara jijini Nairobi George Aladwa alikamatwa asubuhi ya Jumamosi nyumbani kwake na maafisa wa idara ya upelelezi na kupelekwa hadi makao makuu ya idara hiyo kwa mahojiano zaidi.
Aladwa ambaye amewahi kuwa meya wa jiji la Nairobi, alikuwa katika mstari wa mbele katika mipango ya sherehe hizo ambayo haikuwa na idhini ya serikali.
Aladwa sasa ni mbunge wa pili kukamatwa kuhusiana na hafla hiyo ambayo pia imeshutumiwa na jamii ya kimataifa.
Mbunge mwingine wa Nairobi Tom Kajwang alikamatwa na kufikishwa mahakamani na hatimaye kuachiliwa kwa dhamana.
Mwanaharakati mwingine wa upinzani wakili Miguna miguna pia alikamatwa siku ya Ijumaa na angali anazuliwa na polisi licha ya mahakama kuruhusu kuachiliwa kwake kwa dhamana.
Bwana Aladwa alikamatwa siku ya Ijumaa usiku katika nyumba yake iliopo Buruburu kulingana na kiranja wa walio wachache bungeni Junet Mohamed.
Bwana Mohammed ambaye pia mbunge wa Suna Mashariki alisema kuwa bwana Aladwa kwa sasa anazuiliwa katika makao makuu ya ujasusi.
Polisi hawajatoa tamko lolote kuhusiana na kukamatwa kwa Aladwa
Subscribe to:
Posts (Atom)































