Thursday, 1 February 2018

Mwalimu ahama nyumba kupisha Wanafunzi waitumie kama darasa



MWALIMU wa Shule ya Msingi Makazi Mapya, Kata ya Malangali Manispaa ya Sumbawanga, mkoani Rukwa, ameihama nyumba aliyokuwa akiishi ili kupisha wanafunzi waitumie kama darasa.

Mwalimu huyo, amelazimika kufanya hivyo kutokana na shule hiyo kutokuwa na vyumba vya madarasa vya kutosha.

Akizungumza na gazeti hili jana, Diwani wa Kata hiyo, Anthony Chomo, alisema  shule hiyo ilianzishwa mwaka 2003 lakini ina changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa.

Chomo alisema mwalimu huyo amehama katika nyumba ya shule aliyokuwa akiishi ili wanafunzi wa darasa la awali wapatao 51, waitumie kama darasa.

Alisema kutokana na uhaba huo wa vyumba vya madarasa, wanafunzi wa darasa la kwanza ambao idadi yao ni 101 pamoja na wengine 67 wa darasa la tatu,  wanalazimika kusoma kwa zamu katika chumba kimoja kwa zamu za asubuhi na mchana.

Diwani Choma alisema kutokana na changamoto hiyo, walimwomba Mbunge wa  Sumbawanga Mjini fedha na kuwapatia Sh. milioni tatu kutoka katika Mfuko wa Jimbo na wameanza ujenzi wa vyuumba vya madarasa ili kutatua tatizo hilo.

Choma alisema wamekwishafikisha suala hilo kwenye uongozi wa Halmashauri ya Manispaa na wanaendelea kusubiri licha ya kuwa imekuwa muda mrefu na mpaka sasa wanafunzi wanasoma kwa shida na walimu wanafundisha kwa shida pia.

Alisema iwapo jitihada hazitafanyika haraka  kujenga madarasa, wanafunzi hawatakuwa na uelewa mzuri kutokana na kusoma kwa shida na walimu pia ufundishaji wao utakuwa hauna kiwango kinachotakiwa, hivyo lengo la serikali la kila mwanafunzi kupata elimu bora litakuwa halijafikiwa.

Akizungumzia changamoto hiyo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Hamidu Njovu, alisema manispaa inasubiri wananchi waanze nguvu kazi ya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo ndipo wasaidie umaliziaji.

Njovu alisema iwapo wananchi watatekeleza wajibu huo, shule hiyo itapata madarasa upesi zaidi kwa kuwa halmashauri imepokea fedha kutoka mradi wa kuimarisha elimu ujulikanao Kama P4R, hivyo fedha hizo zitatumika katika kuboresha mazingira ya elimu ya shule hiyo.

Hata hivyo, Njovu alimwomba diwani huyo kuwahimiza wananchi ambao watoto wao wanasoma katika shule hiyo, kuhakikisha wanajituma katika kuboresha mazingira ya elimu ya watoto wao baada ya kukaa na kusubiri wahisani na serikali kwa kuwa yale yaliyo ndani ya uwezo wao, wanapaswa kuyafanya kwa maslahi ya elimu ya watoto wao na taifa kwa ujumla.

Shilole ampa onyo Dada wa kazi

STAA wa filamu na Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amesema kuwa tangu amekuwa mke halali wa Ashraf Uchebe, haruhusu dada wa kazi ampikie chakula mumewe huyo.

Akizungumza na gazeti hili, Shilole alisema kuwa mastaa wengi wakiingia kwenye ndoa wanajisahau sana kila kitu wanapenda kufanyiwa na mdada wa kazi na ndiyo maana ndoa zao hazidumu.

“Yaani mimi lazima mume wangu ale chakula cha mkono wangu sikubali mdada wa kazi ampikie, ni marufuku kabisa. Nimruhusu, je akinogewa na mapishi ya mkono wake inakuwaje? Chakula napika mwenyewe kuanzia chai mpaka cha jioni,” alisema Shilole. wanavyopakaza, huyo uliyepata picha zake ni kweli,” alisema Uwezo.

Nisha achoshwa na Wanaume wa Kitanzania

MSANII wa maigizo na vichekesho Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amesema kuwa, amekoma kutoa mapenzi yake kwa wanaume wa Kitanzania kwa kuwa wote wana mapenzi ya kuigiza ambayo yamempotezea muda mno.

Akizungumza na Ubuyu, Nisha alisema ameumizwa sana na mapenzi ya Kibongo, hivyo bora kama anataka kuwa na mpenzi ni afadhali atafute mwanaume wa nje na si Mbongo tena.

“Hivi sasa hivi naanzaje kutoka kimapenzi na mwanaume wa Bongo walivyo waongo na walaghai maana nimepoteza muda mwingi kwao lakini hakuna chochote nilichopata zaidi ya fedhea tu,” alisema Nisha ambaye amewahi kutoka na staa wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego.

Dar yakosekana katika mikoa 10 iliyofanya vizuri

    Dar es Salaam. Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetoa mpangilio wa ubora wa ufaulu kimikoa wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2017, huku Dar es Salaam ukikosekana katika mikoa 10 iliyofanya vizuri.

Hata hivyo, mkoa huo umepanda kutoka nafasi ya 18 mwaka juzi, hadi nafasi ya 16 mwaka jana. Katika orodha hiyo mkoa wa Kilimanjaro umepanda kutoka nafasi ya tano mwaka 2016 hadi nafasi ya kwanza mwaka jana.

Mkoa wa Pwani nao umepanda kutoka nafasi ya saba mwaka juzi hadi nafasi ya pili mwaka jana. Katika orodha hiyo Tabora imeshika nafasi ya tatu kutoka nafasi ya 10 mwaka 2016.

Mikoa mingine iliyofuata na nafasi iliyoshika ni Shinyanga (nafasi ya nne kutoka nafasi ya tisa), Mwanza (nafasi ya tano kutoka nafasi ya sita).

Mkoa wa Njombe uliokuwa kwa kwanza mwaka 2016, mwaka jana umeporomoka hadi nafasi ya 15.

Mkoa wa Iringa ulishika nafasi ya pili mwaka 2016, lakini mwaka jana umeporomoka hadi nafasi ya 17 huku Kagera ulioshika nafasi ya tatu, ukishuka hadi nafasi ya tisa.

Mkoa ulioshika mkia katika mpangilio huo ni Kaskazini Unguja uliotoka nafasi ya 29 mwaka juzi hadi nafasi ya 31 mwaka jana, ukifuatiwa na Kusini Unguja ulioshika nafasi ya 30 ambayo pia uliishika mwaka juzi.

Mikoa mitano iliyoshika mkia ni Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba, Kusini Pemba na Lindi.   

Uzinduzi wa hati ya Kielektroniki yaibua mambo 10

 Dar es Salaam. Unaweza kusema uzinduzi wa hati ya kielektroniki ya kusafiria uliofanywa jana na Rais John Magufuli umeibua mambo 10.

Baadhi ya mambo hayo yalizungumzwa na kiongozi huyo mkuu wa nchi katika hotuba yake wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, mengine kuelezewa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk Anna Makakala na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida).

Ukiacha ulazima wa Mtanzania kuwa na Kitambulisho cha Taifa na Sh150,000 ili kupata hati hiyo mpya, kuna mambo mengine matano yaliibuka baada ya uzinduzi huo.

Mambo hayo ni sifa za hati hiyo zikiwamo za kuwa na alama nyingi za usalama, kuweza kuhifadhiwa katika programu ya simu ya mkononi “App”, hati za kusafiria za zamani kutumika hadi mwaka 2020, ikiwa mtu ana safari ya dharura na hana Kitambulisho cha Taifa, atapewa hati ya dharura na kuitumia si zaidi ya miaka miwili.

Mengine ni kutokuwapo uwezekano wa kughushi hati mpya, utaratibu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kutoa vitambulisho, hati mpya kuwa na kurasa nyingi kuliko ya zamani na hivyo kuweza kutumika muda mrefu zaidi na Mtanzania kupata huduma ya haraka katika balozi ikiwa ataipoteza.

Akitoa maelezo kabla ya uzinduzi huo uliofanyika Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini, Dk Makalala alisema mfumo wa uhamiaji mtandao ni muunganiko wa mifumo mbalimbali ambayo imesanifiwa kufanya kazi kwa pamoja, kutoa taarifa kwa watumiaji na wadau wa huduma za kiuhamiaji.

Alisema kupitia mfumo huo, Idara ya Uhamiaji imeanza kutoa hati za kusafiria, viza za kielektroniki, vibali vya ukaazi vya kielektroniki na udhibiti wa mipaka wa kielektroniki.

Alisema hati mpya ni ya kisasa ikiwa na alama nyingi zaidi za usalama, ni ngumu kughushi, “Ina kurasa nyingi zaidi ukilinganisha na ya zamani hivyo kumwezesha mtumiaji kuitumia zaidi na kwa muda mrefu.

“Pasipoti hii inamwezesha mtumiaji kuwa na nakala ya pasipoti ya kielektroniki kwenye simu yake ya kiganjani baada ya kupakua ‘app’ ya hati yake ya kusafiria katika simu.”

Alisema Mtanzania anapokuwa na nakala ya hati yake katika simu, itamuwezesha kupata huduma ya haraka katika Balozi za Tanzania nje ya nchi, ikiwa aitapoteza.

Kuhusu utaratibu wa kuipata, Dk Makakala alisema sharti kuu ni lazima mhusika awe na Kitambulisho cha Taifa.

“Nitoe wito kwa wanaoataka kuja kuomba pasipoti mpya waje na kitambulisho cha Taifa ndio sharti muhimu. Pasipoti za kawaida zinazotumika sasa zitaendelea kutumika hadi Januari 2020 kisha zitaondolewa kabisa,” alisema.

Alisema hati za kusafiria za Afrika Mashariki zilizokuwa zikitumika awali, hazitatolewa tena baada ya kuanza kutolewa hati za kusafiria za kimataifa.

Alipotakiwa na Mwananchi kutoa ufafanuzi kuhusu hati hizo mpya, Dk Makakala alisema “Tunaendelea kutoa hati za zamani katika kipindi cha miaka miwili hadi Januari 2020 tutakapositisha. Hatuwezi kusitisha moja kwa moja, tupo katika kipindi cha mpito.”

Alisema ikiwa mtu ana hati ya kusafiria ya zamani na anataka kubadili apate mpya, atalazimika kuambatanisha maombi yake na kitambulisho cha Taifa.

“Tunafanya hivyo kwa sababu kuna taarifa tunahitaji kuzichukua ingawa mhusika tayari tutakuwa na ukaribu naye kwamba tayari si mgeni kwetu,” alisisitiza.

Awali, alisema mradi huo ulianza mwaka 2013 na Septemba 2017 walisaini mkataba na kampuni ya HDI ya Marekani na kwamba hadi kufikia Desemba mwaka huu, mfumo mzima utakuwa umekamilika ikiwa ni pamoja na kuufunga katika balozi za Tanzania zilizo nje ya nchi.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Mwigulu Nchemba alisema gharama ya kupata hati mpya ni Sh150,000 na mhusika ataitumia kwa kipindi cha miaka 10.

Alipoulizwa kuhusu idadi ya Watanzania waliopata Vitambulisho vya Taifa, msemaji wa Nida, Rose Mdami alisema wengi wamepata.

“Kwa asilimia kubwa Watanzania wengi wamepata vitambulisho na tunaendelea kutoa katika mikoa 20. Lengo letu ikifika Desemba mwaka huu Watanzania wenye sifa wawe wamepata.”

Katika hotuba yake ya uzinduzi, Rais Magufuli alitoa sababu za kumteua Dk Makakala, Februari 10 mwaka jana, kwamba ni kutokana na matatizo mengi yaliyokuwamo Uhamiaji.

Alisema miaka ya nyuma, Uhamiaji iligubikwa na matatizo mbalimbali ikiwamo utoaji ovyo wa vibali vya uraia hata kwa watu ambao hawakuwa na sifa za kupata uraia.

“Kuna raia wengi walipata uraia bila sifa na wapo waliopata uraia na vyeo vya juu kabisa serikalini. Hii ndiyo sababu niliamua kumteua mwanamama kuongoza idara hii muhimu na wanawake ni waaminifu sana, ameanza kutatua matatizo haya,” alisema Rais Magufuli.

Rais Magufuli alimwagiza kamishna huyo kuwachukulia hatua kali, ikiwamo kuwavua vyeo watumishi wa Uhamiaji ambao watashindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo, ikiwa ni pamoja na kudhibiti wahamiaji haramu.

“Haiwezekani wahamiaji haramu wanakamatwa Mbeya halafu wamepita Kilimanjaro, Manyara, wamepitaje kote huko hadi wakafika Mbeya? Au wamepita Chato (Geita), Buboka (Kagera) hadi Singida, huko walikopita hakuna watu?” alihoji.

Kuhusu mchakato wa mfumo huo wa utoaji hati mpya, Rais Magufuli alisema umegharimu Sh127.2 bilioni ikilinganishwa na makadirio yaliyowekwa awali ya Sh400 bilioni.

“Hapa tumeokoa fedha nyingi za Watanzania, kuna watu walikuwa wamejiandaa kutupiga na kuchukua hizo Sh400 bilioni, lakini tukatumia vyombo vyetu mbalimbali, tukafanya uchunguzi na tumefanikiwa kutekeleza mradi huu kwa gharama nafuu,” alisema.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa.

Wengine ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu, Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zubeir Ali Maulid, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson, Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume. 

Tanzia: Msanii Radio kutoka Uganda afariki Dunia

Muimbaji kutokea kwenye kundi la Good Lyfe Moses Sekibooga ambaye wengi wanamfahamu Radio kutokea Uganda imeripotiwa amefariki dunia asubuhi ya leo February 1,2018 baada ya kukaa ICU kwa siku kadhaa zilizopita, hii ni baada kuripotiwa kupata ajali ya gari  January 23,2018.

Muimbaji Radio ameacha pengo kubwa katika kundi la Good Lyfe ambalo liliundwa na yeye mwenyewe pamoja na Weasel ambaye ni mdogo wa muimbaji na legend wa muziki nchini Uganda Joseph Mayanja ambao wengi tunamfahamu kama Jose Chameleon.

Taarifa za kifo cha Radio zinakuja ikiwa ni siku moja imepita toka Rais wa Uganda Yoweri Museveni kuripotiwa kutoa milioni 30 kama mchango kwa ajili ya kuokoa maisha ya staa huyo kwa kugharamia matibabu.

Radio na Weasel wamefanya nyimbo nyingi ambazo zimewahi pia kupata Air time katika TV  na Radio Stations za Tanzania, Don’t Cry ft Wizkid, Zuena na wimbo wa Where You Are waliokuwa wameshirikishwa na Blu 3 na huu uliwafanya wajulikane zaidi Tanzania kutokana na wimbo huo kufanya vizuri.

Audio | Mbosso – Watakubali Cover by Gold Boy | Mp3 Download

Audio | Mbosso – Watakubali Cover by Gold Boy | Mp3 Download

Audio | Mbosso – Watakubali Cover by Gold Boy | Mp3 Download

DOWNLOAD AUDIO

Ugandan Musician Mowzey Radio Dies at 33

Singer Mowzey Radio has passed on. He was 33.

One of Uganda’s most popular artistes succumbed to the injuries he sustained a fortnight ago in a bar brawl in Entebbe.

Radio had been admitted at Case Hospital in Kampala where he was pronounced dead on Thursday morning.

One of his Managers, Balaam Barugahare, told New Vision at around 8:15am local time that Radio breathed his last at Case Hospital in Kampala.

“Yes, Radio is gone. He died at 6:00am this morning,” he said on phone.

“They are preparing to transfer his body to Mulago Hospital,” he added.

He was aged around 33.

Radio was a victim of an attack at a bar in Entebbe barely two weeks ago. The altercation left his with serious head injuries that necessitated a brain surgery at Case Hospital in Kampala.

Up until the time of his death Thursday morning, the Ugandan music star, who sang alongside Douglas Mayanja, aka Weasel, had remained in critical state at the health facility.

His death comes just days after his mother, Jane Kasubo, had told a press conference at Case Hospital that Radio’s condition was improving, as had been confirmed by doctors.

“My son has been breathing with the help of machines, but now he can breathe on his own,” she told reporters last Friday.

Jose Chameleone Posted in his Instagram “Let his light shine on eternally“

Audio | Wakazi – Hallelujah Refix | Mp3 Download

Audio | Wakazi – Hallelujah Refix | Mp3 Download


Audio | Wakazi – Hallelujah Refix | Mp3 Download


Soda ni SUMU


AFYA za mamilioni ya Watanzania wanaotumia vinywaji vya aina ya soda ipo hatarini, baada ya kugunduliwa uwepo wa chembechembe zenye kemikali za sumu ndani ya vinywaji hivyo, MTANZANIA Jumatano linaripoti.

Utafiti uliofanywa na Muungano wa Waandishi wa Habari za Uchunguzi Tanzania (Investigative Journalists Union of Tanzania- IJUTA) pamoja na tafiti zilizofanywa na wataalamu waliobobea katika afya ya umma duniani, umebaini kuwa vinywaji baridi aina ya soda ni hatari kuliko utumiaji wa sigara inayosababisha maradhi ya kansa katika mwili wa binadamu.

Kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi mbalimbali duniani, yapo madhara makubwa ya utumiaji wa vinywaji vya aina ya soda katika mwili wa binadamu.

Utafiti huo unaonyesha kuwa zipo sababu nane kuu zinazokiweka kinywaji aina ya soda kwenye kundi la vinywaji vyenye sumu ambavyo havifai kwa matumizi ya binadamu.

IJUTA imebaini kuwa makampuni makubwa yanayotengeneza vinywaji baridi aina ya soda yanatumia mabilioni ya dola kila mwaka kujitangaza na kutoa misaada ya kijamii kutokana na mauzo yake, bila kutaja madhara ya vinywaji hivyo kwa binadamu.

Kwamba matangazo hayo yanayogharimu mamilioni ya fedha ndiyo yanayokifanya kinywaji hicho kuwa maarufu zaidi duniani, licha ya kuwa na madhara makubwa katika mwili wa binadamu.

Aidha, utafiti huo unaonyesha kuwa umaarufu mwingine wa kinywaji aina ya soda ni utamu wa kupindukia ulio ndani ya soda.

Utafiti wa IJUTA unaonyesha kuwa utamu wa kupindukia iliomo ndani ya soda unawapumbaza wanywaji ili wasisikie ladha kali ya asidi iliyomo ndani ya soda.

IJUTA imegundua kuwa kiwango cha asidi kilicho ndani ya soda hakiwekwi wazi kwa walaji kwa sababu ya kuhofia kuwa wakibaini wataacha kikutumia kinywaji hicho.

Inaelezwa pia kuwa madini ya cola yaliyo ndani ya soda yana kilevi aina kafein kinachomteka mnywaji kuwa teja wa kinywaji hicho.

Tafiti za kitaalamu zimeonyesha kuwa soda inahusishwa na matatizo mengi ya kiafya kwa watoto na watu wazima, yakiwemo matatizo ya kuongezeka unene kupita kiasi, ugonjwa wa ini na mengineyo.

Utafiti uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa soda huwekewa ‘fructose’ (sukari) nyingi kupitia mfumo wa sirapu (fructose corn syrup) ambayo inaongoza kwa kusababisha magonjwa ya unene, kisukari, ugonjwa wa moyo na magonjwa mengine sugu yanayowakabili Wamarekani wengi hivi sasa na dunia kwa ujumla.

Dk. Mercola, ambaye ni mtaalamu wa masuala ya lishe asilia na tiba mbadala nchini Marekani, amekaririwa na tafiti mbalimbali zilizofanyika nchini humo akieleza kuwa kinywaji aina ya soda ni hatari kwa binadamu, sawa na mtu anayevuta sigara au zaidi, jambo alilosisitiza kuwa siyo la kutia chumvi, bali ukweli halisi.

Watumiaji wa vinywaji aina ya soda wanaelezwa kuwa wamekuwa wakinywa kiasi kikubwa cha kaboni, kafeini (dawa ya kulevya), sukari ya kupundukia na asidi kali ambayo huvuruga afya ya mtumiaji kwa kiwango cha juu.

Soda pia imebainika kutokuwa na lishe ya aina yoyote zaidi ya maji na sukari.

Uchunguzi wa IJUTA na utafiti ya wanasayansi mbalimbali duniani, umeonyesha kuwa watu wengi hawajui kuwa unywaji wa soda huwaongezea kiasi kikubwa cha madini joto.

Chupa moja ya soda yenye ujazo wa mililita 330 husababisha unene kwa kiwango cha paundi moja kwa mwezi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kisukari Tanzania (TDA), Ramadhan Mongi, amepata kukaririwa na vyombo vya habari hapa nchini akieleza kuwa ugonjwa wa kisukari Tanzania umeongezeka mara sita katika siku za hivi karibuni.

Alisema miaka kumi iliyopita, hali ya kisukari ilikuwa asilimia tatu (3), lakini katika miaka ya karibuni umeongezeka mara sita.

“Tunastahili kuongeza jitihada ya kupambana na gonjwa hili la kisukari kwa gharama zote kwa sababu kisukari ni moja ya magonjwa manne yanayomaliza Watanzania,” alisema.

Utafiti uliofanyika Mkoa wa Dar es Salaam ulibaini kwamba kati ya watu watano waathirika wa kisukari, mmoja tu ndiyo hupata matibabu ya serikali.

Unywaji kwa mpigo wa kabohaidrets iliyo na sukari nyingi kwenye soda hudhoofisha seli zinazozalisha vimeng’enya tofauti na vyakula vingine na pia imebainika kuwa sukari ikiingia kwa wepesi kwenye mzunguko wa damu husababisha kongosho kuzalisha vimeng’enya vingi mwilini.

Uchunguzi wa kitabibu katika Hospitali ya wanawake ya Boston nchini Marekani na katika Chuo cha Kitabibu cha Harvard umeonyesha wanawake 51,000 hawakuwa na kisukari mwanzoni mwaka wa 1991, lakini miezi minane baadaye wanawake 741 waligundulika na kisukari.

Ripoti ya utafiti huo ilionyesha kuwa wanawake waliokuwa wakitumia kinywaji aina ya soda moja ama mbili kwa siku waliongezeka uzito maradufu na walikuwa hatarini kupata ugonjwa wa kisukari.

Pia ilionyesha kuwa soda hudhoofisha mifupa na husababisha hali ya mifupa kupuputika, hali inayomuweka mtumiaji kuwa katika hatari ya kuvunjika mifupa kirahisi.

Madhara mengine yaliyobainika kusababishwa na unywaji soda ni kupukutika kwa meno na ama kuoza. Pia soda husababisha matatizo ya figo.

Soda yenye chembe ya cola husababisha figo kuwa na mawe kwa sababu ya asidi na kemikali mbalimbali zinazofichwa vipimo vyake kwa walaji.

Madaktari bingwa wa wanamichezo wanaeleza madhara yanayosababishwa na soda mwilini kuwa ni pamoja na shinikizo la damu, uharibifu wa ini, huvurugu mfumo wa kumeng’enya chakula tumboni kutokana asidi ya kiwango cha juu iliyo kwenye soda.

Wanashauri kuwa soda haistahili kutumika kama kishawishi kwenye mchezo, kwa sababu ina madhara makubwa kwa wanamichezo kwa sababu hunyonya maji kwenye mwili na kudhoofisha mwili.

Wakati utafiti huo ukidhihirisha hayo, Taasisi ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imeshindwa kutoa tamko lolote kuhusu utafiti huo, hata baada ya kupelekewa maswali kwa maandishi yanayoomba ufafanuzi wa ubora wa vinywaji vya soda katika mwili wa binadamu.

Soda yapigwa marufuku Ughaibuni
Jumatano, Mei 15, 2013 05:22 Na Fred Okoth

Yakatazwa shuleni, watoto chini ya miaka 12
Sasa yabainika kuwa ina sumu inayoua taratibu
Yagundulika kupumbaza na kusababisha uteja


SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda, katika utafiti wake gazeti hili limebaini mengine mapya.

Kwa mujibu wa utafiti huo, imebainika kuwa soda imepigwa marufuku kutumiwa na watoto walio na umri chini ya miaka 12 na walio shuleni katika baadhi ya mataifa ya Ulaya na Marekani, kutokana na madhara ya kiafya yanayosababishwa na kinywaji hicho.

Taarifa zilizotolewa na Shirika la Habari la The Press Television Technology Advertising and Branding (Adweek) zinazonukuu taarifa ya kampuni moja kubwa duniani inayozalisha kinywaji aina ya soda, imeamua kupambana na unene (obesity), unaosababishwa na unywaji wa soda kwa kuondoa matangazo ya vinywaji vyake kwenye vyombo vya habari.

Kampuni hiyo kupitia taarifa yake hiyo iliyotolewa katika moja ya sherehe zake, ilieleza kuwa lengo la kuondoa matangazo hayo ni kuwanusuru watoto wadogo na matumizi ya vinywaji aina ya soda vilivyobainika kuwa na madhara katika mwili wa binadamu.

Nchini Marekani, tayari imekwishapitishwa sheria inayokataza watoto walio na umri wa chini ya miaka 12, kunywa kinywaji aina ya soda.

Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, alieleza kuwa mipango ya mbeleni ya kampuni yake ni kutengeneza kinywaji hicho kikiwa na kiwango kidogo cha Kalori na kubuni kinywaji cha aina hiyo ambacho kitakuwa hakina Kalori.

Alisema mipango hiyo itatekelezwa duniani kote ambako kinywaji cha aina ya soda kinatengenezwa na nchini Marekani tayari imekwishaanza kutekelezwa.

Aidha, Kampuni hiyo imeahidi kuweka wazi virutubisho vyote vinavyotumika kutengeneza bidhaa zake na kuahidi kutoa misaada ya hali na mali kwa nchi zote 200 duniani ambako kinywaji cha soda kinauzwa.

Mbali na Marekani, kinywaji cha aina ya Soda kimekwishapigwa marufuku shuleni katika nchi za Uingereza, Ufaransa na katika majimbo ya Los Angeles, Philadelphia na Miami nchini Marekani na kwa watu wazima matumizi yake yanaelekezwa kuwa ya kiwango kidogo sana.

Vyombo vya habari vya nchini New Zealand, mwezi Machi mwaka huu viliripoti kuwa mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Natasha Harris (31), alifariki kutokana na unywaji wa soda nyingi.

Shirika la habari la AFP la Ufaransa, liliripoti tukio hilo kwa kueleza kuwa Natasha alikuwa akinywa soda nyingi kila siku, jambo ambalo liligeuka kuwa sehemu ya maisha yake kwa kipindi cha miaka mingi.

Kwamba familia ilikuwa ikimuita teja wa soda, baada ya meno yake kuoza kwa sababu ya kunywa soda, alijifungua mtoto ambaye hakuwa na fizi jambo ambalo liligundulika baadaye kuwa lilisababishwa na matumizi makubwa ya kinywaji hicho.

“Tumegundua kwamba, kwa kuzingatia ushahidi uliopo, kama sio unywaji wa soda uliopitiliza, Natasha Harris asingekufa katika muda ule na katika hali alivyokufa

“Ripoti ya Daktari aliyechunguza maiti yake (Pathologia), iligundua kwamba ini lake lilipanuka sana, likawa na mrundiko mkubwa wa mafuta kutokana na kula sukari kwa wingi. Kuwepo kwa madini aina ya ‘potasiam’ kwa kiwango kidogo sana kwenye damu yake, pia kulitokana na unywaji wa soda.” Taarifa ya kitabibu katika Hospitali aliyofia nchini New Zealand ilieleza.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za kisayansi zilizo kwenye mitandao ya wanasayansi waliobobea duniani, unywaji wa soda humpumbaza mtumiaji na kumsahaulisha kula vyakula vyenye madini muhimu mwilini.

Moja ya andishi linalotahadharisha utumiaji wa kinywaji cha soda na kukitaja kuwa cha hatari kwa matumuzi ya binadamu, ni Jack Winkler, Profesa wa sera za lishe katika Chuo Kikuu cha Metropolitan nchini London, linaloeleza kuwa Soda ni bidhaa ya kishetani inayoua binadamu taratibu baada ya kinywaji hicho kumzalishia magonjwa mengi mwilini yanayomfanya kuwa tegemezi wa dawa.

Wakati msomi huyo akieleza hayo katika utafiti wake, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Dk. Raymond Wigenge, amelieleza gazeti hili soda siyo kinywaji hatari kwa matumizi ya binadamu kwa sababu kinatumiwa na mamilioni ya watu duniani kote.

Akizungumza na MTANZANIA Jumatano ofisini kwake wiki iliyopita baada ya kutoa ufafanuzi kuhusu madhara yanayosababishwa na kinywaji aina ya soda katika mwili wa binadamu, Dk. Wigenge alisema pamoja na changamoto zilizopo katika kinywaji hicho, taasisi yake haipingi uwepo wa kinywaji hicho sokoni.

“Soda haina shida kwa binadamu na hata mkiendelea kuandika suala hili, sisi tutaendelea kuueleza umma kwamba waendelee kupata kinywaji, hivyo kama ambavyo tumekuwa tukifanya,” alisema.

Alipoulizwa kama anakubaliana na tafiti za wanasayansi bingwa wa magonjwa ya binadamu walioeleza katika tafiti zao kuwa unywaji wa soda una madhara katika mwili wa binadamu, alisema hizo ni changamoto za kawaida, kwa sababu madhara yaliyomo kwenye soda hayamuathiri mtu mara moja bali huchukua muda mrefu.

Wakati Dk. Wigenge akieleza msimamo wake kuhusu kinywaji aina ya soda, nchini Mexico, taasisi ya El Poder del Consumidor inayojihusisha na kutetea walaji, inashinikiza Serikali ya nchi hiyo kuzilazimisha kampuni za soda kuorodhesha madini na chembechembe zote za kemikali zinazotumika kutengeneza kinywaji hicho.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Alejandro Calvillo, amekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo akieleza kuwa unywaji wa soda ni hatari na hilo limethibitishwa na wataalamu wa afya duniani kuwa soda ni sumu mbaya, inauwa taratibu.

Tafiti mbalimbali za wanasayansi zinaeleza kuwa soda ina asidi aina ya ‘phosphoric’ yenye uwezo wa kuvuruga madini ya ‘calcium’ yaliyoko mwilini na kusababisha mifupa na meno kudhoofika.

Aidha, asidi aina ya ‘phosphoric’ huvuruga asidi aina ya ‘hydrochloric’ iliyo tumboni mwa binadamu na hivyo kuharibu mfumo wa kusaga chakula.

Viwanda vya soda ndio watumiaji wakubwa wa sukari na wanasayansi wanasema sukari hupandisha kiwango cha ‘insulin’ ambayo husababisha kasi ya mzunguko wa damu, ugonjwa wa moyo, kupanda kwa ‘Cholesterol, kisukari, kuzeeka mapema, ongezeko la uzito na maradhi mengine.

Aidha inadaiwa kuwa viwanda vya soda pia hutumia dawa ya kulevya aina ya kafeini. Wataalamu wanasema vinywaji vyenye kafeini, husababisha kupanda kwa mapigo ya moyo, kasi ya mzunguko wa damu na matatizo ya kizazi.

Faida za Kiafya za Kitunguu Swaumu (Garlic)


Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum. Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba.

Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen'genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu.

Historia inaonesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika China mwaka 510 K.K na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Roma. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana.

Mwaka 1858, mtafiti na mwanasayansi wa nyakati hizo, Louis Pasteur aligundua uwezo wa kitunguu swaumu katika kuua vimelea mbalimbali vinavyosababisha magonjwa, na hivyo vikaanza kutumika kama dawa ya kusafishia vidonda na kuzuia kidonda ndugu hasa zama za vita ya kwanza na pili ya dunia. Isitoshe, mpaka sasa zipo dawa kadhaa zilizotengenewa kwa kutumia jamii hii ya vitunguu swaumu ikiwemo dawa ya kusafisha mdomo (mouth wash) ingawa watumaiji wake wengi huilalamikia dawa hiyo kwa sababu ya harufu mbaya ya dawa hiyo inayowasababishia kunuka kwa mdomo.

Faida za vitunguu swaumu
Katika tafiti mbalimbali vitunguu swaumu vimeonekana kuwa na uwezo wa kutibu maambukizi ya bakteria, fangasi na virusi vya aina mbalimbali. Aidha husaidia kuzuia magonjwa ya moyo ikiwemo kuondoa lijamu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kurekebisha shinikizo la damu. Faida nyingine za vitunguu swaumu ni pamoja na
Kutibu saratani ikiwemo saratani ya tumbo na utumbo mkubwa. Tafiti zinaonesha idadi ndogo ya wagonjwa wa saratani katika nchi ambazo wakazi wake wana utamaduni wa kutumia vitunguu swaumu kwa wingi.
Vitunguu swaumu husaidia kudhibiti kiwango cha sukari katika damu. Hata hivyo inashauriwa kwamba wagonjwa wa kisukari wanaotumia sindano za insulin wasitumie kitunguu swaumu kwa wingi mpaka watakaposhauriwa na daktari.
Huzuia kusanyiko la chembe sahani zinazosaidia kuganda kwa damu (platelet aggregation)
Husaidia ufyozwaji wa thiamin, hivyo kusaidia kuepusha mwili na ugonjwa wa beriberi
Ina kiasi kikubwa cha vitamini C ambayo husaidia kuzuia ugonjwa wa kiseyeye
Hutumika kutibu magonjwa nyemelezi kama toxoplasmosis, hasa kwa watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

Ushahidi wa Kitafiti
Katika utafiti uliofanyika nchini Czech ilionekana kuwa matumizi ya vitunguu swaumu yalisaidia sana katika kupunguza kusanyiko la lijamu (cholesterol) pamoja na mafuta yasiyofaa mwilini (low density lipoproteins) katika mishipa ya damu. Aidha, mwaka 2007 BBC iliripoti matumizi ya vitunguu swaumu katika kusaidia kumkinga mtumiaji dhidi ya aina fulani ya mafua iliyosababishwa na virusi.

Mwaka 2010, ulifanyika utafiti mwingine ambao ulijumuisha wagonjwa 50 wenye shinikizo la damu sugu ambalo lilikuwa ni vigumu kudhibitiwa hata kwa matibabu yaliyozoeleka ya dawa na njia nyingine. Kama njia ya kuchunguza ufanisi wa vitunguu swaumu katika kutibu shinikizo la damu, baadhi ya wagonjwa hao walipewa vitunguu swaumu wakati wengine walipewa dawa isiyohusika na matibabu ya shinikizo la damu (au placebo).

Ilionekana kuwa wale waliopewa vitunguu swaumu kama dawa ya shinikizo la damu walionesha maendeleo mazuri kwa vitunguu swaumu kuweza kushusha vizuri kiwango cha shinikizo la damu, hususani systolic pressure, tofauti na wale waliopewa placebo.

Nini siri ya kitunguu swaumu?
Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida zilizoainishwa hapo juu ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa (ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na mambo yafuatayo;

Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu (vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu.
Husaidia uthibiti wa kiwango cha sukari mwilini kwa kushusha kiwango cha kemikali ya homocystine na kupunguza madhara ya kisukari.
Iwapo vitapondwa pondwa vizuri, vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo Allicin ambayo ni dawa dhidi ya bateria, na phytoncide ambayo huua fangasi wa aina mbalimbali.
Harufu mbaya ya kitunguuu swaumu hutokana na gesi aina ya hydrogen sulfide ambayo inayotolewa baada ya kuvila.


Nini Madhara ya vitunguu swaumu?
Ukiacha faida zake, vitunguu swaumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;

Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.
Aidha, vinaelezwa pia kuwa na madhara kwa wanyama jamii ya paka na mbwa.

Madhara Ya Kufanya Mapenzi Kupita Kiasi


Katika hali ya kawaida kufanya mapenzi kuna faida nyingi, lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi tunapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara kwa watu wanaoendekeza sana ngono.

Kuna watu ambao hawezi kulala bila kufanya mapenzi na huku wengine wakikosa uwezo wa kuvumilia hata kwa siku mbili au tatu.

Mtu anaweza kuwa na mke na kujikuta kila siku anatumia ‘chakula cha usiku’ kwa sababu tu hakuna wa kumkataza na kwamba ana haki ya kufanya hivyo kwa sababu amelipa mahari, hapa nimeweka chumvi kidogo lakini huo ndio ukweli halisi.

Hilo linaweza kuwa jambo jema kwa upande mwingine, lakini uchunguzi unaonyesha kuwa watu wengi kati ya watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka katika kundi la watu wapenda ngono.

Pamoja na tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema tukajifunza ili tusiwe watu wa kuendekeza miili kiasi cha kulazimika kufanya mapenzi kila tunapokutana.

Twende pamoja katika kutazama madhara hayo kwa kina.

1.    Kupoteza hamu ya tendo la ndoa.
Watu wenye pupa za kufanya mapenzi hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa ufanyaji wa tendo la ndoa mara kwa mara.

Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu.

Aidha kukinai haraka staili za kimapenzi kunatajwa kujitokeza kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake na hivyo kupoteza hamu naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

2.   Kuujaza mwili tamaa kubwa.
Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani?

Watu wanaojiendekeza katika kufanya mapenzi mara kwa mara ndiyo wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake.

Hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa watumishi wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi.

Unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy ili akukate kiu ya penzi.

3.   Kupoteza raha kamili ya tendo.
Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyokuzwa kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako.

 Kama ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo!

4.   Kupoteza nguvu ya mwili.
Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili.

Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke. Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha.

Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

5.   Kupatwa na magonjwa.
Kama tulivyojifunza kuwa watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa na tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi, lakini ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwakinga na michubuko wakati wa kujamiiana na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

Kama Unaogopa Kufanya Kitu Hiki, Sahau Kuhusu Mafanikio Katika Maisha Yako Yote


Fikiria kila unachokijua na kukikumbuka kuhusu mabadiliko unayotaka yawe katika maisha yako, halafu  uone ukweli huu  kama kweli nawe ni mmoja kati ya watu wanaotaka mafanikio au uko nje ya mstari wa mafanikio na pengine tu wewe hujijui. Kama kweli unataka mafanikio, ni kwanini  mara kwa mara umekuwa ukisita au kuogopa kufanya jambo ambalo lingeweza kubadili maisha yako na kukuletea mafanikio mkubwa? Hili ndilo tatizo walilonalo watu wengi wanahofia sana kufanya mabadiliko kwa namna moja au nyingine hata kwenye yale malengo waliojiwekea wao wenyewe kuna wakati huwa wanaogopa pia.

Kimaumbile, kila binadamiu anahofia mabadiliko, lakini hofu ya mabadiliko inapozidi kuwa kubwa na kukuzuia kufanya mambo ya maana kwako, hofu hii  sasa hugeuka kuwa ni maradhi yanayokuzuia wewe kufanikiwa. Hebu fikiria tena, ni mara ngapi umekuwa ukitaka kufanya mabadiliko Fulani  katika maisha yako, lakini umekuwa ukijikuta ukishindwa kufanya hivyo kutokana na kuogopa kufanya vitu Fulani? Ni mara ngapi umekuwa ukitaka kuingia kwenye biashara lakini umekuwa na hofu nyingi zinakuzuia? Hivi ndivyo ilivyo mabadiliko huogopwa, wakati mwingine bila sababu ya msingi.

Wengi wetu kutokana na kuogopa mabadiliko, hujikuta ni watu wa kutoa sababu ambazo hata hazina mashiko zinazosababisha wao washindwe kutekeleza malengo na mipango waliojiwekea. Utakuta mtu anakwambia  hawezi kufanya biashara ni kwa sababu hana mtaji, ukija kuchunguza kidogo utagundua kuwa hiyo ni sababu ambayo amekuwa akiitoa kwa muda mrefu, iweje kila siku mtu huyohuyo awe hana mtaji tu. Kama uko hivi una hofu tu hata kwa vitu vidogo ambavyo ungeweza kuvifanyana , tambua kuwa kuanzia sasa unaye adui mkubwa ndani mwako anayekuzuia kufanikiwa. Na unapoogopa kufanya mabadiliko ambayo unaahitaji sasa ili ufanikiwe, sahau kuhusu mafanikio katika maisha yako yote.

Tatizo kubwa utakalokuwa nalo linalosababishwa na hofu hii ya kuogopa kufanya mabadiliko ni lazima utakuwa mtu wa kutaka mafanikio ya harakaharaka. Watu wengi wenye mawazo ya kutaka kufanikiwa leoleo hata kama wameanza biashara leo, wengi wao huwa wana hofu hii kubwa ya mabadiliko ndani mwao, unaweza  kufanya utafiti mdogo utagundua ukweli huu ulio wazi. Hawa ni watu ambao kiuhalisia hawaijui wala kuiamini subira ndani mwao, bali ni watu wakutaka mfumo wa maisha uwe ambao unaanza leo biashara na wiki ijayo uwe tajiri ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa.

Hivi ndivyo walivyo watanzania wengi wanaogopa mabadiliko na kuamini katika miujiza, sio katika wao wenyewe kutenda na kuona matokeo.  Hebu jaribu kukagua maisha ya walio wengi utakuja kugundua ukweli huu ni watu wanaofikiria sana leo, sasa hivi, siyo baadaye. Hata malengo yao ni ya karibu sana na hawataki shida, wanataka wafanye leo, wamudu leo na kila kitu kimalizike leo. Sijui kesho watafanya kitu gani? Ukimwambia mtanzania aanzishe mradi ili aje faidi baada ya miaka 10 kutoka sasa kwanza atakushangaa, kisha atakucheka we hadi mbavu zimuume. Anataka leo hata kama ni kwa miujiza.

Ndiyo maana wengi kati ya Watanzania hawana malengo, wanaishi tu na kutawaliwa na hofu za mabadiliko. Kuweka malengo siyo sehemu ya maisha yao, kwani malengo yanataka mtu mwenye subira, mtu anayeamini kwamba maisha ni kuanguka na kusimama. Wanachojua kikubwa ni kulalamika na kulaumu, kuponda na kukejeli, kwa sababu wao wamekata tamaa bila kujijua. Ndiyo maana ni watanzania wanne tu kati ya kumi ambao wanafanya kazi, wanatoka jasho na wanaweza kusubiri bila kukata tamaa, wengine waliobaki wanasubiri ujanja ujanja tu ilimradi wafanikiwe hata kama ni kwa kufanya uhalifu wa aina yoyote.

Ni watu ambao wanataka kuishi kihadithi, wawe na pete ambayo wanaweza kuiamuru iwape wakitakacho na wakipate. Maisha ni ya kibunuasi- abunuasi tu, watu hawa kwao mabadiliko ni kitu kigumu sana kwao na kinaogopwa kweli. Kama unataka mafanikio ya kweli yawe kwako, unatakiwa kubadilisha fikra za zako na kuamua kukubali kuwa mafanikio yanahitaji mabadiliko makubwa sana ambayo wewe mwenyewe unatakiwa uyafanye kwa kujitoa hasa. Acha kuwa na hofu zisizo na maana zinazokuzuia wewe usifanikiwe, chukua hatua katika maisha yako, kuyafikia maisha unayoyataka.