Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Tuesday, 30 January 2018
Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download
Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download

Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download

Audio | Mo music ft Roma – BAJAJI | Mp3 Download
CSEE – FORM FOUR EXAMINATION RESULTS (Matokeo Kidato cha Nne) 2016/2017

CSEE – FORM FOUR EXAMINATION RESULTS (Matokeo Kidato cha Nne) 2016/2017
CSEE 2017 CLICK HERE
(QT) 2017 CLICK HERE
Monday, 29 January 2018
New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are
New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are

New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are
DOWNLOAD VIDEO

New VIDEO: Di’Ja Ft. Tiwa Savage – The Way You Are
DOWNLOAD VIDEO
Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download
Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download

Audio | Gigy Money – Mimina | Mp3 Download
Bunge kuunguruma kesho, wabunge watatu kuapishwa

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajiwa kuanza kunguruma kesho (Jumanne) na Mkoani Dodoma kwa kuanza kuapisha Wabunge wapya watatu pamoja na kupitisha miswada miwili ya sheria ambayo ilisomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano wa tisa.
Hayo yamewekwa wazi na taarifa rasmi iliyotolewa na ofisi za Bunge kupitia Kitengo cha Habari na Mawasiliano na kusema kuwataja wabunge hao ambao watakula kiapo cha uaminifu kuwa ni Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kutokea Songea Mjini, Mhe. Monko Justine Joseph wa Singida Kaskazini na kumaliziwa na Mhe. Dkt. Stephano Lemomo Kiruswa wa Longido.
Aidha, katika mkutano huo wa 10 kutakuwa na wastani wa maswali 125 ya kawaida yanayotarajiwa kuulizwa na Wabunge huku wastani wa maswali 16 ya kiwa ya papo kwa hapo kuenda kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu ambayo yanatarajiwa kuulizwa siku ya Alhamisi mnamo februari mosi.
Kwa upande mwingine, Kamati 16 za Bunge za kudumu zitawasilisha taarifa zake Bungeni hapo.
Lita 85 za Gongo zakamatwa Manyara

Jeshi la Polisi mkoani Manyara limesema limekamata mitambo ya kutengenezea pombe haramu ya gongo pamoja na lita 85 za pombe hiyo, ambayo ni kinyume na sheria za nchi.
Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara Agustino Senga, amesema vifaa hivyo pamoja na pombe imekamatwa kutokana na operesheni maalum inayoendeshwa na jeshi hilo.
“Mkoa wetu wa Manyara umeendelea na misako mbali mbali ambapo tumekamata mitambo ya gongo pamoja na gongo huko mbulu, kijiji cha hydom Manyara, walimkata mtu mmoja Moshi Bula mwenye miaka 55, akiwa na mitambo minne ya kutengenezea mitambo ya gongo, hivi sasa yupo mahabusu na taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani,”, amesema Kamanda Senga.
Kamanda Senga ameendelea kuelezea kwamba...Sambamba na hilo tumekamata lita 65 za pombe haramu ya moshi pamoja na watu watatu wanaohusika na pombe hiyo, ambao ni Neema Doto Matayo, mwenye miaka 21, Lawawa Sakara na Patrima Bula na wote watafikishwa mahakani”.
Licha ya hayo Kamanda wa Senga amesema pia wamemkatama mwanamke mmoja akiwa na lita 20 za gongo, na kufanya idadi ya lita 85 za pombe hiyo haramu.
Tani 3.5 za meno ya Kiboko zapata mnunuzi

Kampuni ya Ontour Tanzania Limited imenunua kwa Sh30.9 milioni meno ya viboko tani 3.5 yaliyokuwa yakipigwa mnada na Serikali baada ya kukusanywa kwa miaka 14.
Mnada huo umefanyika leo Januari 29, mwaka 2018 jijini Dar es Salaam na kuongozwa na kamati maalumu ya mnada inayoundwa na maofisa wa Wizara ya Fedha na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (Tawa), kuongozwa na Karerema Kwareh kutoka wizara hiyo.
Awali, Kwareh alieleza masharti ya mnada huo, huku sharti namba tano linalimtaka mnunuzi kununua mzigo wote likiibua mjadala kwa baadhi ya wanunuzi wakitaka liondolewe.
Licha ya kupingwa na wanunuzi, Kwareh amesema wazo hilo limechukuliwa na litafanyiwa kazi katika mnada ujao, si mnada wa leo.
Mfanyabiashara wa kwanza alitaka kununua meno hayo kwa Sh25.2 milioni lakini alizidiwa kete na mkurugenzi wa Ontour, Crey Kilasi aliyetoa Sh30.9 milioni.
Kaimu Mkurugenzi wa Tawa, Mabula Misungwi amesema meno hayo yameuzwa ili thamani yake isiendelee kushuka na hatua hiyo haiwezi kuwa chachu ya kuongezeka kwa ujangili.
"Nyara hizi huwa zina thamani yake na zinavyozidi kukaa huwa thamani inashuka. Meno haya ni yale yanayopatikana kutokana na vifo vya kawaida vya viboko na yale yanayokamatwa kwa majangili," amesema Misungwi.
Amesema meno ya kiboko yana soko kubwa ulaya ambako hutumika kutengenezea urembo na bidhaa nyingine za mapambo.
Akizungumza baada ya kufanikiwa kununua meno hayo, Kilasi amesema atatumia wastani wa miezi sita kutafuta soko.
"Soko lake kubwa ni Japan na China ambapo huyatumia kama mbadala wa meno ya tembo, bei yake inaweza ikafikia Dola 25 za Marekani," amesema Kilasi.
Amesema asilimia 60 ya meno hayo ndio inaweza kuuzika vyema sokoni, huku asilimia 40 yakiwa hayapo katika hali nzuri.
VIDEO: Mbowe - Asema Mtulia Ni Gunia La Misumari
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA leo kimeendelea na kampeni zake za ubunge wa jimbo la Kinondoni ambapo Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe aliwahutubia wanachama na wafuasi wao huku akimnadi mgombea wao, Salumu Mwalimu.
"Fursa aliyoitoa Mwenyezi mungu ya kuwapa nafasi ya kuchagua mbunge makini ambae atawatetea, inapaswa muitumie vizuri kuliko kuwa na Mbunge mzigo ambae ni gunia la misumali'' amesema Mbowe
TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KU SUBSCRIBE
"Fursa aliyoitoa Mwenyezi mungu ya kuwapa nafasi ya kuchagua mbunge makini ambae atawatetea, inapaswa muitumie vizuri kuliko kuwa na Mbunge mzigo ambae ni gunia la misumali'' amesema Mbowe
TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KU SUBSCRIBE
Waziri Jaffo atoa agizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jafo amewaagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri (DED) kutunza siri za Serikali.
Jafo ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Januari 29,2018 mjini Dodoma alipofungua mafunzo ya uongozi kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa mikoa sita.
Mafunzo hayo ni mwendelezo wa ambayo yanatolewa kwa viongozi wa kada hiyo.
Waziri Jafo amesema ujenzi wa Serikali utakuwa mzuri iwapo viongozi hao watakuwa makini na kutunza siri.
"Hivi unakuwaje wewe mkurugenzi au mkuu wa wilaya unapeleka siri za Serikali kwenye mitandao ya kijamii na nyingi unaziona kwenye WhatsApp, inatia aibu sana," amesema Jafo.
Amewataka wakurugenzi kujipambanua na kusimamia miradi ya maendeleo katika kukusanya mapato na kuyatumia vyema na hasa ya ndani.
Jafo amesema tatizo kubwa kwa wakurugenzi ni kutofanya uamuzi kwa haraka.
Ndoa zilizofungishwa bila leseni kubatilishwa

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini RITA, imesema, ndoa zote zilizofungwa bila kuzingatia sheria ya ndoa ikiwemo viongozi wa dini waliofungisha ndoa hizo kutokuwa na Leseni ya kufungisha ndoa huenda zikabatilishwa.
Afisa Usajili Msaidizi wa RITA Jane Barongo, amefafanua kuwa ndoa hizo zitabatilishwa tu endapo itabainika viongozi waliofungisha ndoa hizo hawakuwa na Leseni ya kufungisha ndoa kutoka serikalini.
Barongo ameongeza kuwa kiongozi wa dini atakayebainika kufungisha ndoa bila kuwa na Leseni ya serikali anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya ndoa ambayo imeipa Rita mamlaka ya kisheria, kusajili ndoa zote zilizofungwa kihalali.
Kwa upande mwingine amesema tayari serikali imewakumbusha viongozi wote wa dini kuhakikisha wanakamilisha taratibu za kukata Leseni ya kufungisha ndoa kabla ya kufungisha ndoa yoyote nchini.
Subscribe to:
Posts (Atom)