Friday, 26 January 2018

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download


  1. DOWNLOAD

MAGAZETI YA LEO 26/1/2018























Wema matatani kwa kudaiwa kuwafuga Mashoga




Mrembo wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu amejikuta akiingia matatani kwa kudaiwa ‘kuwafuga’ wanaume wanaodaiwa ‘si riziki’ (mashoga) nyumbani kwake, Salasala.

Kwa mujibu wa chanzo makini, mrembo huyo amekuwa akiishi na wanaume hao tata kwa muda mrefu jambo ambalo limekuwa likiwakera majirani wanaomzunguka na kuwafanya wamshitaki serikalini.

“Unajua hii tabia yake si ya leo, ameanza muda mrefu na amekuwa akiwakera majirani zake kwani wanahofia kuharibiwa watoto wao wa kiume kwa kufuata matendo yao,” kilidai chanzo.

Kikizidi kushusha madai hayo chanzo hicho kilienda mbali zaidi kwa kusema mrembo huyo ni sikio la kufa kwani alikuwa akiishi na mashoga hao tangu alipokuwa anaishi maeneo ya Ununio jijini Dar hadi kumsababishia matatizo pia. “Kule Ununio alikuwa nao hawa mashoga, sijui ni marafiki zake au ni watu wa aina gani kwake.

Watu wengi wanajiuliza kwanini anawakumbatia, wanakosa majibu. “Kama mnakumbuka vizuri hata mama yake aliwahi kwenda kuwatimua mashoga hao baada ya kuona wanamharibia lakini sijui Wema anawapendea nini, bado yuko nao tu,” kilizidi kumwaga ubuyu chanzo hicho. Baada ya kunasa ubuyu huo, wanahabari wetu walifika nyumbani kwa Wema alikohamia kwa sasa, Salasala jijini Dar ili kuweza kujionea mashoga hao lakini ilishindikana baada ya kugonga geti muda mrefu bila kufunguliwa.

Hata hivyo, Ijumaa lilifanikiwa kuzungumza na mjumbe wake wa nyumba kumi, Marko Mbaku ambaye alisema taarifa za uwepo wa mashoga amezisikia lakini ameshindwa kupata ushirikiano kutoka kwa Wema.

“Kwanza niseme tu simtambui Wema maana hajaja hata kujitambulisha kwangu tangu amehamia hapa, nimeletewa malalimiko mengi dhidi yake lakini kila nikimpelekea barua hajibu chochote wala haji,” alisema mjumbe huyo na kushauri waandishi waende ofisi za serikali ya mtaa kwani kuna taarifa zaidi.

Ijumaa lilifika Ofisi za Serikali ya Mtaa wa Salasala na kuzungumza na wajumbe wake ambao kwa pamoja walikiri kuwepo kwa mashoga nyumbani kwa Wema na kushauri waandishi wazungumze na mwenyekiti wao kwa  taarifa zaidi.

Alipotafutwa Mwenyekiti Hashim Bakari, alikiri uwepo wa malalamiko hayo ofisini kwake na kwamba wanajipanga kwenda kuzungumza na mrembo huyo ili kama atashindwa kuwatoa, basi wamhamishe mtaa.

“Ni kweli malalamiko hayo yapo, tunajipanga kwenda kumuona Wema Sepetu ili kama wapo hao mashoga awaondoe, akikaidi tutamhamisha hapa mtaani kwetu,” alisema mwenyekiti huyo

. Waandishi wetu katika jitihada za kumpata Wema ili kuzungumzia madai hayo, kwanza walifika nyumbani kwake tena ambapo safari hii walifunguliwa geti na mwanaume ambaye alisema staa huyo hayupo na kwa maelezo zaidi apigiwe simu. Wema alipopigiwa simu mara zote iliita bila kupokelewa. Jitihada za kumpata bado zinaendelea.

Barcelona watinga nusu fainali Kombe la Mfalme



Klabu ya Barcelona usiku wa kuamkia Leo imefanikiwa kutinga nusu fainali ya Kombe  la Mfalme maarufu kama Copa del Rey kwa ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Espanyol .

Magoli ya Barcelona yamefungwa na Lionel Messi na Luis Suarez ambapo kwa matokeo hayo Barca imefuzu kwa jumla ya tofauti ya goli 2-1 baada ya mechi ya kwanza Barcelona kufungwa goli 1-0.

Barcelona imeungana klabu ya Valencia, Sevilla na Leganes ambazo zote zimefuzu juzi

Trump kuinyima msaada Palestina?


Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kusitisha misaada kwa taifa la Palestina iwapo litakataa kushiriki katika mazungumzo ya amani.

Wizara ya maswala ya kigeni imethibitisha kuwa alikuwa akizungumzia msaada wa kiuchumi na usaidizi wa kiusalama.

Bwana Trump aliishutumu Palestina kwa kuivunjia heshima Marekani akisema ''kwa nini tuwafanyie kitu na wao wenyewe hawatufanyii chochote''.

Palestina imeikataa Marekani kuwa mpatanishi asiyependelea upande wowote katika mazungumzo hayo ya amani.

Wamekasirishwa na hatua ya Washington kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.

Afisa aliyekuwa akiongoza ujumbe wa mazungumzo upande wa Palestina Saeb Erakat alijibu matamshi ya hivi karibuni ya rais Trump: Trump anaweza kununua vitu vingi na fedha lakini hawezi kununua heshima yetu.

Akizungumza katika kongamano la kiuchumi mjini Davos, Switzerland, bwana Trump alisema kuwa Marekani inawapatia Palestina mamia ya mamilioni ya madola kama msaada na usaidizi kila mwaka.

Alilalamikia hatua ya uongozi wa Palestina wa kukataa kukutana na makamu wa rais wa Marekani Mike Pence katika eneo hilo mapema wiki hii.

Amesema kuwa yeye ndio rais wa kwanza kwa kuhusisha msaada na mpango wa amani.

''Hizo pesa ziko katika meza lakini hazitawafikia hadi pale watakapokubali kuketi katika meza ya mazungumzo na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu''.

''Ninaweza kuthibitisha kwamba Israel inataka kuanza mazungumzo ya amani nao, na wao Palestina watalazimika kukubali kuanza mchakato huo ama la sivyo hatutashughulika tena''.


Kigwangala atoa siku saba kwa Kampuni za Uwindaji Nchini


WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangala, ametoa siku saba kwa kampuni sita za uwindaji nchini kufika katika ofisi za wizara hiyo Dodoma, kujieleza kutokana na tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ujangili.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Dk. Kigwangala alisema kampuni hizo zina leseni halali za uwindaji, lakini ndani yake wamekuwa wakifanya vitendo ambavyo vinaashiria uvunjifu wa sheria na uhalifu dhidi ya wanyama.

Alizitaja kampuni hizo kuwa ni Berlette Safari Corporation Ltd,  Game Frontiers of Tanzania Ltd, Mkwawa Hunting Safaris Ltd, Tanzania Game Trackers Safaris Ltd, Wengert Windrose Safari Ltd na Geenniles Safaris Ltd.

Alisema wakurugenzi wa kampuni hizo na washirika wao wanatakiwa kufika ofisi za Wizara Dodoma kuhojiwa na kikosi kazi maalum kuhusiana na tuhuma hizo.

“Waje hapa wazungumze na kikosi hiki wajieleze ni kwa nini tusichukue hatua za kisheria dhidi yao, lakini pia wajibu hoja mbalimbali zitakazohusisha makosa mbalimbali. Wakurugenzi wote na washirika wao wafike wao wenyewe bila kutuma uwakilishi na bila kutoa sababu zozote,” alisema.

Alisema baada ya kuwahoji watachukua hatua za kiutawala kulingana na sheria ya uwindaji na baada ya hapo kwa makosa yatakayojulikana ni ya jinai yatapelekwa vyombo vya dola vinavyohusika na makosa hayo ikiwamo ya ujangili kama itabainika kwenye kikosi hicho.

Dk. Kigwangala alitaja tuhuma zingine kuwa ni uwindaji haramu, uhawilishaji wa umiliki wa vitalu vya uwindaji bila kufuata sheria, ikiwamo makosa ya ujangili, kujaza fomu za udanganyifu, rushwa, uhalifu dhidi ya rasilimali za wanyamapori, uhujumu uchumi, ukiukwaji wa kanuni za uwindaji na kutolipa tozo mbalimbali.

Pamoja na kampuni hizo, alimwagiza mmoja wa watumishi wa wizara hiyo, Alex Aguma, afike pia kuhojiwa.

MTANDAO WA MAJANGILI

Waziri huyo alisema katika kipindi cha siku 100 ambazo amekuwa katika nafasi hiyo,  wizara hiyo imekamata watuhumiwa 74 na kubaini mitandao yao yote na hatimaye kubainisha mtandao mzima ambao una washirika 949 wa ujangili.

Alisema kati ya hao nusu wamechukuliwa hatua mbalimbali za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kwamba wanaendelea na ufuatiliaji wa watuhumiwa wengine ambao wametajwa na washiriki wao, lakini wengine wamekimbia maeneo mbalimbali.

“Lakini pia napenda kutambua kazi kubwa iliyofanywa tangu mwaka 2010 hadi 2013-2014 ambao ilikuwa  mwisho wa operesheni tokomeza ambayo ilikuwa inajibu mashambulizi kutokana na kukithiri kwa ujangili ambao ulikuwepo mwaka 2010-2015.

“Operesheni tokomeza serikali iliweza kubainisha watuhumiwa mbalimbali takribani 2130 ambao walituhumiwa kwa uhujumu uchumi, lakini kukutwa kwa silaha 3715 zilizokamatwa, meno ya tembo ghafi 3789 yenye uzito wa kilo 12,194, vipande 695 vya meno yaliyochakatwa,”alisema.

Jangili adakwa Loliondo

Aidha Dk.Kigwangala alisema usiku wa kuamkia jana amekamatwa muuaji Loliondo ambaye yeye kazi yake ni kulenga shabaha na silaha anachukua kwa mtu mwingine.

“Tumetengeneza utaratibu wa kuwafuatilia katika ngazi tofauti tofauti hadi tuvunje mtandao mzima wa ujangili hapa nchini, na sasa tunawatambua kwa ngazi tano za ujangili na biashara haramu na tunawabainisha majangili kwa madaraja yao, daraja la anayeenda kuua, kulenga shabaha, kusafirisha, wakala, anayefadhili, anayevuka mipaka kwenda nchi nyingine, mitandao ya kuuza nyara nje ya nchi,” alisema.

Hizi ndizo sababu za Kagera Sugar kutomuadhibu Nyoso



JUMA NYOSO.

SIKU chache baada ya kuachiwa kwa dhamana beki wa kati wa Kagera Sugar, uongozi wa timu hiyo umetoa sababu kwa nini hawatamchukulia hatua mchezaji huyo anayetuhumiwa na madai ya kumpiga shabiki wa soka.

Nyoso, alikamatwa na Jeshi la Polisi mara baada ya mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Simba uliofanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba na wenyeji kulala kwa mabao 2-0.

Akizungumza jana na kituo kimoja cha redio, Mratibu wa Kagera Sugar, Mohamed Hussein, alisema kuwa klabu hiyo haitamchukulia hatua yoyote Nyoso kutokana na kitendo hicho kwa sababu jambo hilo lilifanyika nje ya uwanja na pia shabiki huyo Shabaan Hussein alimfanyia vitendo vya ‘kumpandisha hasira’ Nyoso.

“Nyoso kwa sasa yupo nje kwa dhamana na amejiunga na kambi ya timu, lakini niweke wazi hatotumchukulia hatua yoyote sisi kama klabu,” alisema Hussein.

Alisema kuwa Nyoso ni binadamu na kitendo cha shabiki yule kumpulizia Vuvuzela sikioni na kumtukana kilimtia hasira.

“Hatukubaliani na kitendo cha kupiga shabiki, lakini kama ni adhabu basi vyombo vya dola au Shirikisho (TFF),” aliongeza kusema.

Nyoso aliwekwa mahabusu kuanzia Jumatatu mpaka juzi baada ya hali ya shabiki huyo kuwa mbaya katika kipindi hicho.

Simba kujichimbia tena Morogoro

KIKOSI cha Simba kinatarajia kwenda tena Morogoro au Zanzibar kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kuwavaa wapinzani wao katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika, klabu ya Gendarmarie Nationale kutoka Djibouti, imefahamika.

Vinara hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ambao wanadhaminiwa na Kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ya SportPesa wanatarajia kuwakaribisha Gendarmarie katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Februari 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah "Try Again" alisema jana kuwa uamuzi kamili utafanywa katika kikao cha pamoja na benchi la ufundi baada ya kumaliza mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Majimaji itakayofanyika Jumapili.

Salim alisema uongozi wa klabu hiyo unaamini kuwa kambi hiyo watakayokaa itasaidia kuwaweka wachezaji tayari kupambana kusaka matokeo mazuri katika mchezo wao wa kwanza wa kimataifa ambao utakuwa ni mtihani wa kwanza wa kimataifa kwa kocha mpya Mfaransa, Pierre Lechantre.

"Jumatatu wachezaji watapumzika lakini tutakuwa na kikao na benchi la ufundi kwa ajili ya kuamua kambi itakuwa wapi, kama ni Zanzibar au Morogoro, ila mazoezi wataanza Jumanne na baadaye ndiyo wataingia kambini," alisema kiongozi huyo.

Aliongeza kuwa mbali na kuandaa timu yao, vile vile wameunda "kikosi kazi" ambacho kazi yake maalumu kuwapeleleza wapinzani kabla hawajafika nchini na hatimaye kujipanga kuwakabili.

Baada ya wiki mbili, Simba itasafiri kuelekea Djibouti kuwafuata wenyeji wao ambao wanatumia uwanja wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 40,000.

Katika kuimarisha kikosi chake, Simba iliamua kuimarisha benchi lake la ufundi na vile vile kuboresha safu ya ulinzi kwa kumsajili beki wa kati kutoka Lipuli, Asante Kwasi, ambaye ni raia wa Ghana.


Man U dimbani Leo, Sanchez Kazini


MANCHESTER Unit­ed inatarajiwa kuwa uwanjani leo Ijumaa kuivaa Yeo­vil Town katika raundi ya nne ya Kombe la FA.

United itakuwa ugenini kuivaa timu hiyo ya dara­ja la pili ambapo kuna mambo kadhaa yatakuwa gumzo juu ya mchezo huo.

Alexis Sanchez kuanza kazi

Kocha Jose Mourinho wa United anatarajiwa kuan­za kumtumia staa wake mpya kikosini hapo kwa mara ya kwanza. Hiyo ni kiu ya mashabiki wengi ku­muona mchezaji huyo ka­tika kikosi hicho.

Mourinho mechi 100

Leo ni siku ya ku­zaliwa ya Mourinho ambaye anatimiza umri wa miaka 55 pia atakuwa akifikisha mchezo wake wa 100 akiwa na Man Unit­ed. Ameshinda 61, sare 23 na kupoteza 15, mabao ya ku­funga ni 176, mabao ya kufungwa 70 na ana mataji matatu.

Mabadiliko kikosini

Mourinho anaweza kufanya mabadiliko ya kikosi ikiwemo kumpa nafasi kipa Sergio Romero na kumpumz­i ­s h a David De Gea.

A n d e r H e r r e r a mechi 150

Kiungo h u y u ame s h ­a c h e z a m e c h i 149 aki­wa United k a m a atache­za basi atafiki­sha mechi 150.

Walimu wapewa onyo Sumbawanga



HALMASHAURI ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa imewaonya walimu kutochangisha michango kwa wanafunzi na atakayebainika atachukuliwa hatua za kinidhamu kwani kufanya hivyo ni kukiuka agizo la serikali.

Onyo hilo lilitolewa na Meya wa Manispaa hiyo, Justine Malisawa wakati akifunga baraza maalumu la madiwani lililoketi kwa ajili ya kupitisha bajeti ya Sh. bilioni 47.2 ya mwaka wa fedha 2018/2019, katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Alisema kuwa halmashauri hiyo kamwe haitakuwa tayari kumvumilia mwalimu yeyote ambaye atachangisha fedha wanafunzi kwa ajili yoyore, ikiwamo masomo ya ziada kwani serikali imekwisha piga marufuku suala hilo kupitia Rais John Magufuli.

Malisawa alisema kuwa serikali imeshatangaza elimu bila malipo ni vizuri walimu katika halmashauri hiyo wakatekeleza nia hiyo ili kila mtoto aweze kupata elimu kwa usawa kwa kuwa baadhi ya wazazi hawana uwezo wa kugharamia elimu.

Chuchu afunguka zawadi anayotaka kwa Ray


BAADA ya kumzalia mtoto wa kiume na kuwa gumzo mitandaoni, muigizaji mkongwe wa filamu Bongo, Chuchu Hans amefungukia zawadi aitakayo kutoka kwa mzazi mwenziye ambaye naye ni msanii, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuwa ni busu tu.

Akizungumza na Star Mix, Chuchu alisema kuwa baada ya kumzalia Ray hahitaji kupewa zawadi kubwa kwani hata busu litamtosha.

“Unajua mimi nachojua zawadi ni zawadi tu hata kama Ray akiamua kunipa busu kwangu mimi linatosha kabisa wala asiwaze sana zawadi ya kunipa,” alisema Chuchu.



Watu zaidi ya 30 wafariki katika ajali ya moto Korea Kusini


Hospitali yaungua moto Korea Kusini

Zaidi ya watu 30 wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali ya moto uliyotokea katika Hospitali moja nchini Korea Kusini. Hata hivyo maofisa wanasema idadi ya waliokufa huenda ikaongezeka kutoka katika ya majeruhi hao.

Imefahamika kuwa moto huo ulianzia katika chumba cha dharura cha Hospitali ya Sejong, kusini mashariki mwa nchi hiyo.

Zaidi ya majeruhi 100 wanasemakana wamo katika jengo la hospitali hiyo.

Picha za mitandao ya jamii, zinaonyesha vikosi vya zima moto wakijaribu kukabiliana na moto huo huku kukiwa na moshi mkubwa.

Mwaka jana watu 29 walikufa katika mji wa Echeon, Korea Kusini, na wengine kujeruhiwa baada ya moto kuzuka katika sehemu ya mazoezi ya wazi.

Thursday, 25 January 2018