Friday, 26 January 2018

Wanaume watatu waliokunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume walazwa hospitali



Wanaume watatu waliokunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume huko nchini Zambia  wamejikuta wakilazwa hospitali baada ya kuanza kutapika nakuharisha mfululizo baada ya kutumia dawa hizo.

Vyombo vya habari nchini Zambia vimeeleza kuwa wanaume hao walilazwa kwa makosa kwenye vituo vya zahanati za kuhudumia wagonjwa wa kipindu pindu wakidhaniwa kuwa wanaugua kipindu pindu hadi baadaye walipokuja kukiri kuwa walikunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume na ndio zimepelekea waharishe na kutapika.

Kwa mujibu wa mtandao wa The Mast Online wa nchini humo umeeleza kuwa wanaume hao walikuja kubainika kuwa hawaugui kipindupindu wakati Kiongozi Mkuu wa Jimbo la Mashariki nchini Zambia, Chanda Kasolo alipotembelea kujua idadi ya wagonjwa juzi (Jumatano) katika Hospitali ya Katete jimboni humo..

“Mpaka kufikia jana kulikuwa na kesi mbili za wagojwa waliolazwa kutoka Lusaka, hivyo idadi ya wagonjwa imeongeka kutoka 24 hadi 26 jambo ambalo limeongeza hofu kwenye jamii yetu. Na kingine cha kushangaza jana tumepata wagonjwa wengine watatu kutoka Katete eneo ambalo halijawahi kupatwa kabisa na kipindu pindu lakini baada ya  uchunguzi wa madaktari tumebaini kuwa Wagonjwa hao hawakuwa wanaugua Kipindu Pindu,“amesema Kasolo na kuelezea kilichowakumba.

“Baada ya majibu ya vipimo kupatikana , inaonekana kuwa wanaume hao walikutwa na mchanganyiko wa pombe, vyakula na dawa za kienyeji ambazo zilisababisha mchafuko wa mfumo wa chakula na hivyo ikahusishwa na kipindupindu lakini baada ya kuwauliza maswali, baadaye walikiri kuwa walikunywa dawa ya kuongeza nguvu,”amesema Kasolo.

Hata hivyo tayari wanaume hao wamehamishwa kwenye hospitali hiyo inayolaza wagongonjwa wa kipindu pindu na kulazwa kwenye hospitali ya kawaida.

Mpaka sasa vifo vya watu wapatao 70 vimeripotiwa kutokea tangu mwaka jana kwa kesi za ugonjwa wa kipindu pindu .

Mwishoni mwa mwaka jana Rais wa Zambia, Edgar Lungu alitangaza kuwa ugonjwa huo ni janga la taifa huku akitaka kila mwananchi kuwajibika kwa usafi.

Nabii Tito ajikata na wembe tumboni


Nabii Tito ameibua mengine baada ya kujijeruhi kwa kujikata na wembe tumboni ambapo kumepelekea ashonwe nyuzi 25 katika zahanati ya polisi Dodoma.

Daktari wa hospitali hiyo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na ameeleza kuwa Tito alifikishwa hospitali saa 9 mchana akiwa anavuja damu eneo la tumbo.

”Ni kweli Tito alifikishwa hapa majira ya saa 9 mchana, tulimfanyia matibabu kwa kumshona nyuzi 25 kutokana na ukubwa wa majeraha hayo” amesema Daktari.

Hata hivyo kamanda wa polisi Dodoma, Gilles Muroto hana taarifa kutokea kwa tukio hilo.

Nabii Tito sasa anashikiliwa na polisi kutokana na kauli zake zinazopingana na dini, amekuwa akihamasisha watu kunywa pombe, na wanaume kulala na wadada wa kazi akidai kuwa kufanya hivyo sio dhambi.

Hivyo baada ya matibabu hayo nabii Tito alirudishwa polisi kwa mahojianao zaidi.

Nafasi za kazi leo Jan 26

Bill Gates ampa onyo Trump kuhusu Afrika



Tajiri na Mfanyabiashara mkubwa duniani, Bill Gates amemuonya rais wa Marekani Donald Trump kwa misimamo ya sera yake ya “Marekani Kwanza” kuwa inaweza kuharibu uhusiano wa nchi hiyo na bara la Afrika.

Ameyasema hayo katika mkutano wa dunia wa uchumi World Economic Forum (WEF) unaofanyika huko Davos nchini Switzerland ambapo amesema kuwa kunatakiwa kuwepo kwa uwiano wa wenye nguvu kubwa na nguvu kidogo.

Amesema kuwa Marekani inaweza kupoteza ushawishi wake barani Afrika huku nchi kama China zinazidi kuimarisha uhusiano na bara hilo kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Bill Gates anamfuko wake barani Afrika unaoitwa Bill & Melinda Gates Foundation, ambao umekuwa ukijihusisha kwa kiasi kikubwa kutoa huduma za afya katika nchi kadhaa.

Hata hivyo, Rais Trump amesema kuwa atakata msaada wa bajeti ya afya kwa takribani dola bilioni 2.2 katika mfuko wa dunia, huku akiwakasirisha viongozi wa Afrika bada ya kuyaita mataifa ya Afrika machafu kupindukia.

Gwajima azuia watu kulia kwenye msiba wa Mama yake


ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dk. Josephat Gwajima ameacha gumzo na mshangao baada ya kuzuia watu kulia kwenye ibada ya kuaga mama yake mzazi, Bi. Ruth Paulo Gwajima iliyofanyika nyumbani kwa mchungaji huyo na kisha mwili wa marehemu kuzikwa kwenye shamba la familia, nje kidogo na nyumbani hapo, Salasala jijini Dar.

Shaka amvaa Maalim Seif


Wakati wananchi wa Jimbo la Kinondoni wakijiandaa na kampeni za ubunge wa jimbo hilo, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umemtaka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad akijiandaa kushiriki kampeni hizo kwanza awathibitishie wanachama wake ni lini ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar kama alivyowaahidi.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka amesema hayo jijini Dar es Salaam jana, mara baada ya kikao na watendaji wa sekretarieti za Wilaya za Dar es Saalam.

Shaka amesema Maalim Seif ni miongoni mwa wanasiasa ambao hawapaswi kusikilizwa na wananchi kutokana na kufanya siasa ionekane ni sehemu ya uongo kwani haaminiki.

“Maalim Seif kwanza awaambie wale aliowadanganya lini ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar, amewaongopea sana wanachama wake na sasa amechusha, kelele za kulilia urais wa Zanzibar kwa njia ya uongo zimezimika, tunamsubiri kwa hamu aje Kinondoani vijana tumejipanga kushughulika naye,” amesema.

Waziri Lukuvi atangaza uamuzi mzito Mwanza


WANANCHI wanaomiliki nyumba 664 katika mitaa ya Kigoto na Kabuhoro katika Kata ya Kirumba Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikitafuta ufumbuzi wa mgogoro uliopo kati yao na Jeshi la Polisi.

Pia wamezuiwa kujenga nyumba zingine mpya kwenye maeneo ya mitaa yao na badala yake wawe walinzi na kuonya watakaothubutu kujenga hawatalipwa fidia ambapo awali walitakiwa kuondoka na kupisha eneo hilo baada ya kuandikiwa ilani ya siku saba na jeshi la polisi.

Akizungumza na wananchi hao Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema serikali imesikia kilio chao na hivyo amekuja chunguza mgogoro huo ili ifanye uamuzi wa kuutatua.

 Alisema serikali inataka kufahamu mahitaji ya wananchi na polisi na kuonya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo wasithubutu kujenga (kuongeza) majengo mengine zaidi ya yaliyopo sasa na watakaokaidi hawatalipwa fidia.

“Nimekuja kuangalia mgogoro huu na kuchungumza jambo hili ili serikali ifanye uamuzi. Msidhani nina majibu, majibu yatatolewa ndani ya mwaka mmoja lakini msituhubutu kuongeza nyumba zingine zaidi, kuweni walinzi wa maeneo haya na tunataka muwe maeneo mzuri ili tuwarasimishie,”alisema Lukuvi.

Waziri huyo wa ardhi alisisitiza baada ya uchunguzi atamshauri vizuri Rais John Magufuli namna ya kumaliza mgogoro huo baina ya wananchi na taasisi hiyo ya serikali.

Lukuvi alieleza eneo la Kigoto ambalo Polisi inadai inataka kujenga Chuo cha Polisi wanamaji, nyumba za askari na  gati la boti na meli za doria zinaweza kujengwa popote lakini eneo hilo lazima lipangwe upya hata kama matumizi yakibadilishwa kwa kuwa haiwezekani watu waishi kwenye nyumba za ovyo ovyo.

“Miaka 70 hadi leo kwa nini ujenzi haukuzuiwa,hakuna viongozi hapa na kama mngewashirikisha wangewasaidia kuzuia.Je, upembuzi yakinifu ulifanyika kwenye eneo mnalotaka kujenga mdomo huo wa gati la boti za polisi?

Aidha akizungumza kwa niaba ya wenzao ,Ferdinand Mtundubalo alimweleza Waziri kuwa hawana tatizo na ujenzi wa gati la boti za polisi isipokuwa warasimishiwe makazi yao ili waondokanane na mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi aliwataka wataalamu wa wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waainishe eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha Ihale ili kila mmoja alinde eneo lake.

Pia alishauri eneo la Nyamwilolelwa litakalobaki baada ya kutengwa la uwanja wa ndege na JWTZ lipimwe wapewe wananchi wa eneo wapatao 1,961 na kuhusu barabara ya Mwanza –Igombe uamuzi wa Rais Magufuli ubaki ulivyo na uheshimiwe.

Kampeni za Ubunge Jimbo la Ubungo kuzinduliwa na Lowassa, Mbowe


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edward Lowassa pamoja na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe kesho Januari 27, 2018 watakuwepo katika uzinduzi wa kampeni za Ubunge jimbo la Kinondoni.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na CHADEMA leo inasema kuwa viongozi hao watakuwepo katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa marudio katika jimbo la Kinondoni kumtambulisha Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA, Salum Mwalimu.

Uzinduzi wa kampeni hizo utafanyika katika viwanja vya Mapilau kuanzia saa nane mchana mpaka saaa kumi na mbili jioni ambapo wageni rasmi watakuwepo Lowassa pamoja na Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA.

Tarehe 17 Februari mwaka huu unatarajiwa kufanyika uchaguzi wa marudio katika majimbo ya Siha na Kinondoni kutokana na wabunge wa majimbo hayo kujiuzulu nafasi zao za Ubunge wakiwa katika vyama vya upinzani na kuingia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sasa wanagombea nafasi hizo wakiwa chini ya CCM.

New VIDEO: Maleek Berry – Pon My Mind

New VIDEO: Maleek Berry – Pon My Mind

New VIDEO: Maleek Berry – Pon My Mind


Audio | King James – Uri mwiza | Mp3 Download

Audio | King James – Uri mwiza | Mp3 Download

Audio | King James – Uri mwiza | Mp3 Download

New Audio | AKA – Sweet Fire

New Audio | AKA – Sweet Fire
New Audio | AKA – Sweet Fire

New Audio | Professor ft Cassper Nyovest & Mono T – Can’t Get Away

New Audio | Professor ft Cassper Nyovest & Mono T – Can’t Get Away

New Audio | Professor ft Cassper Nyovest & Mono T – Can’t Get Away

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download

Audio | Man Fongo ft Badria – Kimya Kimya |Mp3 Download


  1. DOWNLOAD