Tuesday, 23 January 2018

AUDIO Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

AUDIO
Audio | Aslay & Nandy – Subalkheri Mpenzi | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)

Aslay X Nandy - Subalkheri Mpenzi (Official video)


VIDEO: Sakata la Nyoso Latua TFF


Sakata la Mchezaji wa Kagera Suger Juma Nyoso la kumpiga mshabiki na kuzimia leo limeibuka kwenye mkutano wa waandishi wa Shirikisho la Soka Nchini TFF na Kulitolea ufafanuzi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI .......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Kiwanja Cha Kujenga Nyumba Kinauzwa Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B


Kiwanja cha Kujenga Nyumba Kinauzwa , Kina Size ya 20 Kwa 20 Mita, Kipo Eneo la Mapinga Karibu na Bunju B, Kipo Karibu na Barabara ya Lami
Shilingi Mil 8. Maongezi yapo Kidogo

Piga simu 0714604974 Kwa Mawasiliano zaidi


Jeshi la Polisi lasema Nabii Tito anamatatizo ya akili


JESHI la Polisi mkoani Dodoma,  baada ya kumkamata na kumfanyia mahojiano Onesmo Machija (44) anayejiita ‘nabii’ Tito, kutokana na mahubiri ya kidini anayoyafanya, limesema mtu huyo ana  matatizo ya akili.

Akizungumza na wanahabari mjini Dodoma leo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Gillesi Muroto, amesema mnamo Juni 23, 2014, mtu huyo aliwahi kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu ya akili chini ya daktari aliyejulikana kwa jina moja la William ambapo aliporuhusiwa alitakiwa kurejea hospitalini hapo Julai 9 mwaka huohuo lakini hakurejea.

Kamanda Muroto aliendelea kusema kwamba baada ya hapo, Machija ambaye kanisa lake halijasajiliwa popote,  aliibukia mkoani Dodoma katika kijiji cha Nong’ona kilicho karibu na Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) akifanya  mahubiri ya kidini yaliyodaiwa kuwa hayakuwa na maadili ya kidini.

Kwa msingi huo, alisema jeshi la polisi limempeleka Hospitali ya Rufaa ya Mirembe iliyoko mkoani Dodoma  kwa ajili ya kumpima tena matatizo hayo ya akili na baada ya majibu kutolewa,  Dkt. Dixon Philipo aliyemshughulikia alithibitisha kwamba bado ana matatizo hayo.

Pamoja na hayo, Muroto alisema jeshi la polisi mkoani humo  bado linaendelea kumshikilia kutokana na matendo yake aliyoyafanya ili kufanya uchunguzi zaidi.

Source:Global Publishers

Wenger kumsajili Aubameyang




Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuendelea kwa mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa timu ya Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang.

Aubameyang mshambuliaji huyo wa kimataifa wsa Gabon amehusishwa kujiunga na the Gunners na Wenger amesema kila kitu kinaendelea.
Alipoulizwa na waandishi wa habari kama anauhakika wa kunasa saini ya Aubameyang, Wenger amesema “Kuwe na uhakika kusiwe na uhakika, mi sijui.”

Wenger ameongea “Huwezi jua ni kwa jinsi gani dirisha la usajili litakavyo kamilika.”

“Hivi ni vitu ambavyo uwezekano wa kukamili upo lakini pia tuna mambo mengine tunayofikiria mbali na usajili huo na nafasi tunayo na muda bado haujakwisha.”

“Kwa kipindi hiki bado hatujakamilisha dili lolote kuhusu Aubameyang au mtu mwingine yeyote.”

 Alipoulizwa kama mchezaji wake, Olivier Giroud atakuwa sehemu ya dili la kumnasa Aubameyang kwa yeye kuelekea Dortmund, Wenger amesema kuwa mazungumzo hayajafikia katika hatua hiyo.

Timu hiyo imekamilisha mpango wa Alexis Sanchez kutua Manchester United huku Arsenal ikinufaika kwa kumnasa Henrikh Mkhitaryan.


Onyo alilotoa Jaji Mkuu kwa viongozi wa serikali na wanasiasa


Jaji Mkuu wa Tananzania, Profesa Ibrahimu Juma amewataka viongozi wa serikali na vyama vya siasa kuacha mara moja vitendo vya kuingilia mhimili wa Mahakama na kuvunja amri zake.

Jaji Profesa Juma ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu wiki ya Sheria inayotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi ujao (Februari mosi), siku ambayo ndio itakayoashiria kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama kwa mwaka huu 2018 yatakayofanyika katika viwanja vya Mahakama vilivyopo mtaa wa Chimala jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais John Magufuli.

"Kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania mamlaka ya utoaji haki ni ya Mahakama tu, nawasihi viongozi wote wa serikali wenye mamlaka za kikatiba na kisheria wabaki ndani ya maeneo yao ya Kikatiba na wajiepushe kuingilia maeneo yaliyo ndani ya haki, hadhi na Mamlaka ya Kikatiba ya Mahakama", alisema Jaji Profesa Juma.

Kwa upande mwingine, Jaji Profesa Juma ametoa rai kwa wananchi na wadau wote wa sheria kutembelea Mnazi Mmoja kwa ajili ya kujifunza na kupata huduma mbalimbali za Kisheria kutoka kwa Majaji, Mahakimu, Wasajili, Watendaji, Mawakili wa serikali na Mawakili wanaojitegemea ambao watakuwa tayari kuwasikiliza na kuwahudumia ipasavyo.

Tanzia:Nguli wa muziki wa Jazz Afrika Kusini Hugh Masekela afariki dunia


Mwanamuziki maarufu nchini Afrika Kusini, Hugh Masekela anayefahamika kama baba wa muziki wa Jazz amefariki dunia baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya saratani ya tezi dume.

Hugh Masekela amefariki dunia baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na maradhi ya saratani ya tezi dume.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Afrika Kusini.  Masekela amabaye hadi kifo chake kinamkuta alikuwa na umri wa miaka 78.

Katika kipindi chake cha zaidi ya miongo mitano kwenye fani hiyo ya muziki alijijengea umaarufu kimataifa kutokana na utunzi wa nyimbo zake za muziki  wa Jazz ukiwemo wimbo  uliotumika katika harakati za kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo.

Hugh Masekela alitumbuiza katika hafla ya ufunguzi wa fainali za kombe la dunia za mwaka 2010 zilizofanyika nchini Afrika Kusini ikiwa ni mara ya kwanza fainali hizo kufanyika barani Afrika.

Rais Magufuli kuwa mgeni rasmi siku ya Sheria nchini



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria itakayofanyika Februari Mosi mwaka huu.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari, Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma kuhusu maonyesho ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini yenye maudhui ya ‘Matumizi ya TEHAMA katika utoaji haki kwa wakati na kwa kuzingatia maadili’.

“Kila mwaka Mahakama ya Tanzania huadhimisha Siku ya Sheria ambayo huashiria kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama, kwa mwaka huu maadhimisho hayo yatafunguliwa rasmi na Rais Magufuli katika viwanja vya Mahakama vilivyopo jijini Dar es Salaam,” amesema Jaji Mkuu Juma.

Jaji Mkuu amesema kuwa kabla ya kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria, Mahakama ya Tanzania pamoja na wadau muhimu katika Sekta ya Sheria watatumia siku tano kuanzia tarehe 27 hadi 31 Januari mwaka huu kwa ajili ya kufanya maonyesho yatakayotoa elimu kwa wananchi watakaopata nafasi ya kuhudhuria katika viwanja vya Mnazi Mmoja vilivyopo jijini humo.

Maonyesho hayo yatatanguliwa na matembezi maalum ya kuadhimisha Wiki ya Sheria yatakayofanyika Januari, 28 mwaka huu ambayo yataongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete yatakayoanzia katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mpaka viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo Rais Mstaafu Kikwete atazindua rasmi Wiki ya Sheria.

Aliongeza kuwa Wiki ya Sheria inatoa nafasi nzuri kwa wananchi kuzifahamu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mahakama pamoja na wadau wa sekta ya sheria ili kufanikisha maboresho endelevu ya Mahakama.

Wadau wengine watakaoshiriki katika wiki ya sharia pamoja na Tume ya Utumishi wa Mahakama, Mahakama ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, Taasisi ya Mafunzo ya Uanansheria kwa Vitendo Tanzania, Tume ya Kurekebisha Sheria, Chama cha Mawakili Tanganyika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Jeshi la Magereza, Jeshi la Polisi, na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Watumishi wa serikali wapewa masaa 72

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe limetoa masaa 72 kwa watendaji 37 kutoka katika kata 15 wawe wamewasilisha kiasi cha milioni 73 walichokusanya kama mapato vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Watendaji hao wanadaiwa kukusanya fedha hizo katika kipindi cha robo mwaka kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na kubaki nazo majumbani mwao bila kuwasilisha kwa mweka hazina wa halmashauri.



Akisoma azimio la kikao cha Baraza hilo ambalo limekutana mjini Vwawa, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Erick Ambakisye alisema uamuzi huo unafuatia kitendo cha watendaji hao kutowasilisha fedha za makusanyo katika kipindi kilichowekwa kisheria na kusababisha halmashauri kukosa mapato hayo ya Sh. 73,777,736.29 huku wakijua kufanya hivyo ni kosa.

Mwenyekiti huyo alisema sambamba na hilo baraza limechukua hatua ya kuwaonya kwa barua kwa mara ya pili watendaji wa kata 15 za Wasa, Magamba, Ipunga, Nyimbili, Myovizi, Itaka, Mlangali, Halungu, Isansa, Kilimampimbi, Nambinzo, Bara, Ruanda, Iyula na Shiwinga huku wengine 16 wakiwa wakishindwa kutumia mashine za kielektroniki katika kukusanya mapato ya halmashauri na kutakiwa kujieleza na kuwasilisha fedha walizokusanya ifikapo tarehe hiyo saa 4.00 asubuhi.

Aidha mwenyekiti huyo alisema ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji mapato halmashauri yake iliweka mkataba na watendaji hao wenye lengo kukusanya asilimia 50 ya lengo la makusanyo katika kipindi cha kila robo na kutoa zawadi ya Sh. 500000 kwa kata ya kwanza itakayokusanya vizuri, Sh. 300000 (kata ya pili) na Sh.200000 (kwa kata ya tatu) na kutoa ngao ya kufanya vibaya kwa kata tatu zilizofanya vibaya.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo akizungumza wakati akitoa salamu za serikali alisema wilaya ina fursa ya vyanzo vingi vya mapato lakini watendaji wamekuwa hawakusanyi ipasavyo kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.

Kwa upande mwingine Mbozi alisema hatua kali lazima zichukuliwe kwa watendaji wanaoshindwa kukusanya mapato na kwamba ofisi yake itasimama imara kusaidia katika kuhakikisha halmashauri inakusanya mapato inayostahili.

Atiwa mbaroni kwa kuiba jeneza


Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Boniface mkazi wa Mwananyamala kwa Msisiri anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa kuiba masanduku ya kuzikia (majeneza) mawili na kuyaficha nyuma ya choo cha mkazi mwengine wa mtaa huo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, amesema tukio hilo limetokea kati ya ofisi mbili za kuuza masanduku hayo ambapo moja ndiyo iliyoibiwa majeneza hayo, ambayo moja ni la mtu mzima na moja likiwa la mtoto mdogo

“Kuna work shop mbili ambazo zinajishusisha na kutengeneza masanduku, zipo kwenye sehemu moja, asubuhi mtu kaingia kwenye work shop yake akakuta masanduku mawili hayapo akaanza kufuatilia, baada ya muda akajua yapo kwenye workshop nyingine, kwa hiyo kilichofanyika ni ufuatiliaji na askari wakafanikiwa kuyapata, ni suala ambalo linachunguzwa kujua kama wanadaiana au ni wizi umefanyika, ndipo sheria ifuate”, amesema Kamanda Muliro.

Mmiliki wa masanduku hayo Bi. Judith Carlos amesema masanduku hayo aligundua yapo kwa jirani yake baada ya kumuahidi mtu atampa elfu 50 iwapo atamsaidia kujua nani kayachukua, na ndipo baadaye akaambiwa mahali yalipo.

ANC yaendelea kumjadili Jacob Zuma


 Chama tawala cha African National Congress kimethibitisha kwamba mazungumzo yanaendelea kuona namna Rais Jacob Zuma atakavyoondoka ofisini bila shaka ikiashiria mwanzo wa mwisho wa kashfa zilizodumu miaka tisa ya utawala wake.

Zuma amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu tangu alipoachia uaongozi wa ANC kwa makamu wake Cyril Ramaphosa.

 Kashfa

Halmashauri kuu “ilijadili suala hili...kutakuwa na majadiliano kati ya maofisa, Rais Zuma na kwa chama Ramaphosa," alisema Katibu Mkuu Ace Magashule.

"Hakuna muda uliowekwa...Hatufanyi kazi kwa mtindo huo, tunashikiana, tunajadili,” aliongeza Magashule kwamba hakuna uamuzi wa mwisho uliowekwa kuhusu kuondoka kwa Zuma.

Urais wa Zuma ulikumbwa na kashfa za rushwa na ulichafuliwa na kudorora kwa uchumi hali iliyochangia chama kukosa kuungwa mkono kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2019.

Wafuasi wa Ramaphosa wanafanya kampeni atawazwe sasa kama rais na ajaribu kufufua uchumi kabla ya uchaguzi mkuu ambao ANC inaweza kupoteza udhibiti wake kwa mara ya kwanza tangu ulipokomeshwa utawala wa ubaguzi wa rangi.

Audio | Nutty Neithan X Wyre X J’bryte X Ketchup X Gabiro – AYAWA Remix | Mp3 Download

Audio | Nutty Neithan X Wyre X J’bryte X Ketchup X Gabiro – AYAWA Remix | Mp3 Download

Audio | Nutty Neithan X Wyre X J’bryte X Ketchup X Gabiro – AYAWA Remix | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3