
Kuelekea mchezo wa leo wa ligi kuu soka Tanzania Bara kati ya Tanzania Prisons dhidi ya Azam FC, msemaji wa wa Azam FC Jafar Idd Maganga amesema watanzania wameanza kukubali falsafa ya timu hiyo ya kutumia vijana.
Jaffar amesema kocha mkuu wa timu hiyo Aristica Cioaba, amekuwa muumini wa kutumia vijana kitu ambacho awali kilionekana kupingwa na mashabiki wengi wa soka wakiamini kuwa timu hiyo haitafanya vizuri.
''Watanzania wengi wameshaanza kukubali na wanaunga mkono uongozi wa Azam FC kuwatumia vijana na kocha huyu (Cioaba) amekuwa akiwaamini zaidi vijana tofauti na makocha wetu waliopita'', amesema Jaffar.
Kuhusu mchezo wa leo jioni, Jaffar amesema benchi la ufundi limejipanga kuhakikisha linapanga wachezaji ambao wataendana na timu ya Tanzania Prisons pamoja na hali ya uwanja wa Sokoine ili kuhakikisha timu yao inapata matokeo mazuri.
Azam inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 27 huku vinara wa ligi Simba SC, wakiwa na alama 29. Mabingwa watetezi Yanga SC watakuwa dimbani pia kucheza na Ruvu Shooting.
Kocha msaidizi wa vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC Masoud Djuma, ameweka wazi kuwa pamoja na kumpatia nafasi ya kucheza hivi sasa nyota wa timu hiyo kutoka Ghana Nicholas Gyan, lakini aliwahi kumwambia hajui kucheza.




Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima leo Januari 21, 2018 amepata pigo kwa kuondokewa na mama yake mzazi Ruth Basondole Gwajima ambaye amefariki asubuhi ya leo.





Chama cha ACT Wazalendo kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake Bara Msafiri Mtemelwa kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Majimbo ya Kinondoni na Siha.
