Sunday, 21 January 2018

Wizara ya Afya yatoa tahadhari juu ya homa ya CHIKUNGUNYA


Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imetoa tahadhari kwa umma kuhusu ugonjwa wa homa ya CHIKUNGUNYA ambao umeripotiwa na vyombo vya habari kutokea Mombasa nchini Kenya lakini bado Shirika la Afya Duniani (WHO) halijatoa taarifa rasmi.

Wizara ya Afya imetoa tahadhari ya ugonjwa wa CHIKUNGUNYA kutokana na muingiliano mkubwa uliopo kati ya nchi ya Kenya na Tanzania.

Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na homa kali na maumivu ya viungo, misuli, kichefuchefu na uchovu.

Ripoti za awali kabisa za kuwepo ugonjwa huo wa CHIKUNGUNYA zilipatikana katikati ya mwezi uliopita ambapo kilichofuatia kilikuwa ni kukusanya sampuli za damu na kuziwasilisha kwenye maabara kwa ajili ya uchunguzi.

Ugonjwa wa CHIKUNGUNYA unaweza kupunguzwa kwa kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kuhakikisha mazingira ni masafi ili kuepusha mazalia ya mbu.

ACT yaendeleza msimamo wake Siha, Kinondoni


Chama cha ACT-Wazalendo kimesema hakitashiriki uchaguzi katika majimbo ya Kinondoni na Siha kwa kuwa sababu zilizowafanya wasusie uchaguzi mdogo uliopita,  bado hazijafanyiwa kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 21, 2018 Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho-Bara, Msafiri Mtemelwa amesema changamoto walizozilalamikia katika uchaguzi wa Januari 13 katika majimbo ya Singida Kaskazini, Songea Mjini na Longido bado hazijafanyiwa kazi.

Amesema bado chama hicho kitaendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanya mageuzi katika mchakato wa uchaguzi.

Amesema malalamiko ya chama hicho kwa NEC ni matumizi ya nguvu ya vyombo vya dola dhidi ya vyama vya upinzani kwa lengo la kukisaidia chama tawala CCM.

Uchaguzi wa Siha na Kinondoni unafanyika baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kuhamia CCM Desemba mwaka jana.

Breaking News: ACT Wazalendo wametangaza kujitoa kwenye Marudio ya Uchaguzi

 Chama cha ACT Wazalendo kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu wake Bara Msafiri Mtemelwa kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi mdogo wa marudio katika Majimbo ya Kinondoni na Siha.

 Mtemelwa alisema wamefikia hatua hiyo baada ya kuona mazingira ya Uchaguzi ambayo waliyalalamikia kwa Tume ya Uchaguzi hayajafanyiwa marekebisho.

New VIDEO: Safi Madiba ft Rayvanny – Fine

New VIDEO: Safi Madiba ft Rayvanny – Fine

New VIDEO: Safi Madiba ft Rayvanny – Fine

Official Music Video by Safi Madiba from Rwanda featuring Rayvanny from Tanzania

The Video was Shot & directed by Extrafocus in Tanzania

Directed by: Eris Mzava




DOWNLOAD VIDEO

Audio | Safi Madiba ft Rayvanny – Fine | Mp3 Download

Audio | Safi Madiba ft Rayvanny – Fine | Mp3 Download

Audio | Safi Madiba ft Rayvanny – Fine | Mp3 Download
DOWNLOAD

New VIDEO: Isha Mashauzi – Nibembeleze

New VIDEO: Isha Mashauzi – Nibembeleze

New VIDEO: Isha Mashauzi – Nibembeleze

DOWNLOAD VIDEO


Hoteli ya Intercontinental Mjini Kabul yashambuliwa na Magaidi

Yamkini watu 20 wanahofiwa kuwawa baada ya hoteli maarufu ya Intercontinental mjini Kabul, Afghanistan kushambuliwa na magaidi.

Wanajeshi wa Afghanistan, wamekuwa wakipigana ghorofa baada ya ghorofa, ili kuchukua udhibiti wa hoteli moja ya kifahari katika mji mkuu Kabul, baada ya kuvamiwa na wapiganaji waliokuwa na silaha nzito nzito.

Msemaji wa Wizara ya usalama wa ndani nchini humo amesema kwamba, washambuliaji wawili kati ya wavamizi wanne, tayari wameuwawa.

Washambuliaji hao walivamia Hoteli ya Intercontinental jana Jumamosi jioni, na kuanza kuwamiminia risasi wageni na wafanyikazi pamoja na kurusha magruneti.


Marekani kuongeza askari Afghanistan


30 wafariki katika mlipuko Afghanistan


Taliban wawaua wanajeshi 26 wa Afghanistan


Msemaji wa Wizara ya usalama wa ndani nchini humo, Nasrat Rahimi, ameiambia BBC kuwa, walinda usalama wamechukua udhibiti wa ghorofa ya kwanza ya kifahari ya hoteli hiyo, lakini baadhi ya washambuliaji bado wangali katika orofa zingine hotelini.

Taarifa zingine zinasema kwamba, wakati wa uvamizi huo, hoteli hiyo ilikuwa inaandaa kongamano la Teknolojia ya mawasiliani (IT) iliyokuwa inahudhuriwa na maafisa wa mikoa.

Shahidi mmoja ameiambia shirika la habari la Reuters kuwa, washambuliaji hao wanawazuilia baadhi ya watu kama mateka.

Shambulio hilo linatokea siku kadhaa baada ya ubalozi wa Marekani mjini Kabul, kutoa tahadhari ya uwezekano wa kutokea shambulio la kigaidi lililolenga mahoteli kadhaa mjini Kabul.

Kufikia sasa haijabainika ni watu wangapi wameuwawa au kujeruhiwa, lakini taarifa ambazo bado hazijathibitishwa na BBC, zinaasema kuwa watu 15 wameuwawa.
Sehemu moja ya jumba la Hoteli hiyo inateketea, huku makabiliano makali ya risasi yakiendelea.

Jumba la Hoteli hiyo ya Intercontinental, linachukuliwa kama nembo ya mji mkuu Kabul.

Hoteli hiyo ilishambuliwa na kundi la wapiganaji wa Taliban, miaka 7 iliyopita.

Source; BBC

Waziri Mwakyembe amchangia Wastara

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe jana Januari 20, 2018 amemtembelea na kumjulia hali msanii wa filamu Wastara nyumbani kwake Tabata Sanene, Dar es Salaam.

Wastara kwa kipindi kirefu sasa amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mguu na yupo kwenye maandalizi ya safari kwenda India kwa matibabu zaidi.

Waziri Mwakyembe akiambatana na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu na Katibu Mtendaji wa BASATA alimtakia kheri Wastara na kumkabidhi mchango wa Shs. 1,000,000/= (milioni moja).

Aidha, Mwakyembe aliwasihi wasanii na Watanzania kwa ujumla kumchangia Wastara kwa hali na mali ili aweze kupata fedha za kumwezesha kwenda India kwa matibabu zaidi.

Yanga yamkingia kifua beki wake

Klabu ya soka ya Yanga imetoa sababu kwanini mlinzi wake mpya wa kimataifa Fiston 'Festo' Kayembe Kanku ameshindwa kujiunga na timu tangu asajiliwe Disemba 2017.

Akiongea leo Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Hussein Nyika amesema mchezaji huyo raia wa DR Congo hajajiunga na timu kwasababu anashughulikia matatizo ya kifamilia.

“Kanku ana matatizo makubwa ya kifamilia ndiyo maana tumempa ruhusa ya kwenda kuyashughulikia, akimaliza atakuja kuanza kazi, na atacheza tu ligi bado ina mechi nyingi sana,”amesema Nyika.

Kwa upande mwingine Nyika ameongelea suala la uhamisho wa kimataifa (ITC), amabapo ameeleza kuwa ulikuwa unasumbua ila kwasasa wapo kwenye hatua za mwisho kuupata japo kuwa tayari mchezaji huyo ni mali ya Yanga.

Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara wanashika nafasi ya 5 kwenye msimamo wakiwa na alama 22 kwenye mechi 13 walizocheza huku kesho wakishuka dimbani kucheza na Ruvu Shooting.

Johari afunguka siri ya kifo cha Mama yake

MREMBO wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ ameanika siri ya kifo cha mama yake kwa kueleza namna ambavyo alipigana kutetea kifo cha mama yake mzazi.

Johari alipata pigo hilo usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita katika Hospitali ya Hindu Mandali, jijini Dar es Salaam baada ya mama yake kulazwa kwa ugonjwa wa kisukari kwa saa chache tangu afikishwe hospitalini hapo.

Kabla ya kupatwa na umauti huo, Johari alikuwa akiishi na mama yake mzazi, maeneo ya Gereji, Mabibo jijini Dar ambapo kwa zaidi ya miaka mitatu, msanii huyo alihangaika kutetea uhai wa mama yake, kwa nyakati tofauti.

Katika kipindi chote hicho, Johari alikuwa mzito sana kuelezea mateso aliyokuwa anayapitia mama yake, zaidi alikuwa akiwaelezea watu wake wa karibu sana. Akizungumza na Risasi Jumamosi, akiwa kwenye nyumba ya familia, Mburahati jijini Dar, Johari alisema kifo cha mama yake kimekuwa pigo kubwa kwake na kueleza namna alivyopambana kumpigania.

“Nimehangaika jamani. Nilikuwa silali, mchana na usiku nilikuwa nikipambana kuhakikisha naokoa maisha ya mama yangu. “Unajua alikuwa kuna wakati anakuwa na hali nzuri, kuna wakati ndio hivyo kikipanda, hali inakuwa mbaya sana. Kwa miaka zaidi ya mitatu nimekuwa nikipambana na afya ya mama yangu,” alisema Johari huku akilengwalengwa machozi.

Akizungumza kuhusu ratiba ya mazishi Jumatano iliyopita, muigizaji Salum Mchoma ‘Chiki’, ambaye alichaguliwa kuwa msemaji wa familia, alisema siku ya Alhamisi (juzi), mwili wa mama yake Johari ungefikishwa nyumbani hapo kisha ungepelekwa Msikitini wa Mbukusi, Mburahati baadaye kuzikwa katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar. Msiba huo ulihudhuriwa na waigizaji wengi akiwemo, Vincent Kigosi ‘Ray’, Ndambangwe Misayo ‘Thea’, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Nuru Nassor ‘Nora’ na wengine wengi.


Waziri Mpina awasilisha majina ya Viongozi waliokaidi agizo la Serikali

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewasilisha majina ya viongozi wa halmashauri ambazo hazijaanza kutekeleza upigaji chapa mifugo na zile ambazo ziko chini ya asilimia 10 ya utekelezaji,

Kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo ili zichukuliwe hatua.

Mpina alibainisha hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa upigaji chapa mifugo nchini, mjini Dodoma.

Alisema kwa tathmini iliyofanyika hadi sasa jumla ya ng’ombe 10,306,359 sawa na asilimia 59.3 wamepigwa chapa huku asilimia 40.7 wakiwa hawajapigwa chapa na zoezi hilo linatarajiwa kukamilishwa Januari 31, mwaka huu.

“Halmashauri 100 zimepiga chapa zaidi ya asilimia 50, halmashauri 54 zimepiga kati ya asilimia 10 hadi 50, halmashauri 14 zimepiga chini ya asilimia 10 na Halmashauri 9 hazijaanza kupiga chapa,” alisema Mpina.

Alizitaja halmashauri ambazo hazijaanza kabisa ni Tandahimba, Nanyumbu, Mafia, Newala, miji ya Newala, Nanyamba na Masasi na manispaa za Kigamboni na Ilemela.

Kwa upande wa punda, Mpina alisema jumla ya punda ni 572,353 na watapigwa chapa.

Alibainisha kuwa sababu za kutokamilika kwa zoezi ni uwapo wa changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wafugaji kukataliwa kupigiwa chapa mifugo yao kwa kisingizio kuwa ni wavamizi au wahamiaji haramu.

“Mfano katika wilaya za Kibiti, morogoro, Rufiji, Sumbawanga, Tanganyika na Kibondo wamekumbana na changamoto hii,”alisema Mpina

Aidha alitaja changamoto nyingine kuwa ni wafugaji kuhamisha ng’ombe katika kipindi hichi cha kilimo na hivyo kutoshiriki, baadhi ya ng’ombe kuendelea kuwa katika maeneo ya hifadhi na Mapori Tengefu mfano kwa mkoa wa Kigoma na Ruvuma.

“Pia baadhi ya wafugaji kuendelea kugoma kupiga chapa mifugo yao kutokana na imani potofu na wengine kuficha idadi ya mifugo kwa mfano mkoa wa Manyara,”alisema

Mpina alisema kuwakatalia wafugaji kupiga chapa kwa kisingizio cha uhamiaji haramu haikubaliki kwa kuwa wilaya zote zilipewa jukumu la kuhakiki mifugo yao na kuwasilisha taarifa Wizarani.

“Hakuna halmashauri hata moja iliyoleta taarifa za wahamiaji haramu, pia zoezi lisihusishwe na migogoro ya muda mrefu ya matumizi ya ardhi, mifugo yote ipigwe chapa isipokuwa ile ya kutoka nchi jirani,”alisema

Kadhalika, Mpina alisema wafugaji watakaoshindwa kufanya hivyo ndani ya muda uliowekwa hatua kali zitachukuliwa kwa mujibu wa sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji namba 12 ya mwaka 2010 ibara ya 4 kifungu cha 26.

Rais wa Z'bar atembelea eneo ambalo kutahifadhiwa Mafuta

RAIS wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein, ametembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya mradi wa kuhifadhi mafuta na gesi asilia pamoja na ujenzi wa bandari itakayotumika kusafirishia na kuingiza maliasili hizo.

Akiwa katika eneo hilo lililoko Mangapwani na Bumbwini lenye ukubwa wa hekta 399.25 juzi, Dk. Shein alipata maelezo kuhusu hatua zinazoendelea katika mradi huo.

Katibu wa Wizara ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Ali Halil Mirza, alisema hatua inayoendelea hivi sasa ni upembuzi yakinifu unaotekelezwa na Benki ya Dunia ambao utakamilika miezi sita ijayo.

Mirza alisema kukamilika kwa upembuzi huo yakinifu ndiko kutaleta mapendekezo ya kulisanifu eneo hilo kwa ajili ya bandari na majengo mengine ya utawala na shughuli nyingine zinazoenda sambamba na mradi huo.

Alisema miongoni mwa sababu ya kutengwa eneo hilo kwa shughuli hizo ni kutokana na kuwa na kina kirefu cha maji ya bahari ambacho kitarahisisha kujengwa kwa bandari hiyo muhimu ambayo itatumika kwa ajili ya kusafirishia gesi asilia na mafuta ndani na nje ya nchi.

Alisema miongoni mwa faida kubwa za mradi huo baada ya kukamilika kwake ni pamoja na kuondoa kabisa uhaba wa mafuta nchini na kuipatia Serikali pato kubwa.

Wakati huo huo, Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein, akiwa na ujumbe wake alipata fursa ya  kulikagua eneo la Kampuni ya Salama International linalojengwa maalum kwa ajili ya kusafisha mafuta na kupata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Abdallah Said Abdallah.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa eneo hilo ambalo ni kwa ajili ya kusafisha mafuta limefikia asilimia 65 za ujenzi.Mkurugenzi huyo alieleza kuwa matenki ya uwezo wa kuhifadhi lita milioni 24 kwa wakati mmoja yanajengwa kwa ajili ya kuhifadhia diseli, petroli, mafuta ya taa pamoja na mafuta ya kulainisha mitambo.

Alieleza kuwa kuanzia mwezi ujao wataendelea na shughuli za ujenzi zilizobaki, shughuli ambazo zilianza mwaka 2015.

Alisema hadi walipofikia wameshatumia dola za Marekani milioni tano (sawa na zaidi ya Sh. bilioni 10) ikiwa ni awamu ya kwanza.

Alisema watakuwa wakisafisha tani 600 ambazo zitatumika Zanzibar kwa asilimia 70 na kiasi kilichobaki kitauzwa nje ya nchi.

Akiwa katika eneo hilo, Rais Dk. Shein alisisitiza haja ya uhifadhi wa mazingira katika mchakato wa usafishaji wa mafuta mara mradi huo utakapokamilika.

MAGAZETI YA LEO 21/1/2018