Saturday, 20 January 2018

Waziri arudi CCM atwae jimbo 2020

Mwanasiasa  wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.

 Ole Medeye juzi alisema kilichomkimbiza CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chadema ni vitendo vya rushwa katika mchakato wa kupata wagombea wa chama hicho tawala.

Alisema anafurahi kuona sasa vitendo hivyo havipo ndani ya CCM baada ya kudhibitiwa na Rais Magufuli.Ole Medeye alikuwa mmoja wa wabunge watano wa CCM waliojiunga na Chadema Agosti 12, 2015 wakiongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (Monduli).

Ole Medeye aliteuliwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwania nafasi ya Uspika wa Bunge baada ya Uchaguzi Mkuu.

Wengine waliohama pamoja na Lowassa ni Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli (Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya ambaye sasa ni mwakilishi wa wananchi wa Bunda Mjini (Chadema).

Hata hivyo, Ole Medeye alihama Chadema kabla ya mwaka kumalizika na kujiunga na UDP kinachoongozwa na John Cheyo Juni 12, 2016.

Medeye alisema alihamia UDP kwa kuwa inasimamia haki na demokrasia na kwamba yeye alikuwa akitaka demokrasia ya kweli na jukwaa la haki katika kuleta haki na maendeleo kwa Watanzania.

Alisema  kuwa alikaa chama hicho cha 'Bwana Mapesa' kwa miezi mitatu tu hata hivyo, kwa kuwa "nilikwenda kufanya kazi maalum."

Na sasa, Ole Medeye amesema ameamua kurejea CCM kwa kuwa kila mwanachama anayo fursa kushiriki uchaguzi, ikiwamo kugombea nafasi yoyote bila kutoa rushwa na akashinda.

"Mimi sijawahi kuwahonga watu ili wanichague," alisema Ole Mideye na "wakati huo CCM kulikuwa na rushwa sana; ndiyo maana nikaamua kukimbia.

"Lakini kwa sasa hakuna tena kitu kama hicho, hivyo nimeamua kurejea CCM."

Ole Medeye alisema katika Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2020, anataka kurudi na kuwatumikia wananchi kupitia nafasi ya ubunge.

Maseneta wakwamisha serikali ya Trump

Bunge la Seneti nchini Marekani limeshindwa kuidhinisha mswada ambao ungeongeza ufadhili wa serikali ya kitaifa kwa mwezi mmoja.

Kufuatia hatua hiyo huduma nyingi za serikali zitakwama, hata hivyo athari kamili itaanza kuonekana siku ya Jumatatu, wakati wafanyakazi wa serikali watarejea kazini.

Mara ya mwisho shughuli za serikali zilikwama nchini Marekani ni mwaka wa elfu mbili na kumi na tatu, na ilidumu kwa muda wa siku kumi na sita wakati ambapo wafanyakazi wengi wa serikali walishurutishwa kwenda likizo ya lazima.

Ni mara ya kwanza kwa huduma za serikali kukwama huku chama cha Republican kudhibiti mabunge yote na ikulu ya White house.

Ikulu ya whitehouse imewalaumu wabunge wa Democrats kwa kuweka siasa juu ya maswala ya kiusalama , familia za wanajeshi, watoto walio katika mazingira magumu, na uwezo wa taifa hilo kuwahudumia raia wa Marekani.

Lakini kiongozi wa wabunge wa Democrats Chuch Schumer, alisema kuwa rais Trump alikataa makubaliano yasiopendelea upande wowote na hakukishinikza chama chake katika bunge la Congress.

Mkwamo wa huduma za serikali nchini Marekani ulifanyika mara ya mwisho 2013 na ukachukua muda wa siku 16.

Republicans waliutaja muswada huo kwa jina la ''Schumer Shutdown' na hawakukosea.

Chuck Schumer na wabunge wenzake wa Democrats kupitia usaidizi wa wabunge wachache wa Republican walizuia muswada ambao ungesaidia serikali kuendelea na shughuli zake, hata ijapokuwa kwa muda.

Hatahivyo kuchukua jukumu na kutoa lawama ni vitu viwili tofauti.

Democrats watasema kuwa walikuwa wamekubaliana na rais kupitisha muswada usiopendelea upande wowote kuhusu mabadiliko ya sheria ya uhamiaji, kabla ya kukiuka makubaliano hayo wakati wa mkutano katika afisi ya Oval wiki iliopita.

Swala la kurushiana lawama lilianza saa sita usiku na mshindi bado hajatangazwa.

Hatahivyo atakayeshindwa katika mkwamo huu ni chama kitakachoingia katika vita na idadi ndogo ya wabunge ikiwa ni habari mbaya kwa rais Trump na chama cha Republicans.

Habari njema ni kwamba , pande zote mbili na ngome zao za kisiasa zitafurahishwa kwa kufanya mambo kuwa magumu.

Kwa nini pande hizo mbili zisikubaliane?

Swala linalogombaniwa ni lile la Democrats kutaka zaidi ya wahamiaji wasio na vibali walioingia nchini Marekani kutofurushwa.

Wahamiaji hao walipatiwa vibali vya kuwa nchini humo kwa muda chini ya mradi ulioanzishwa na rais wa zamani Barrack Obama.

Mnamo mwezi Septemba, bwana Trump alitangaza alikuwa anasitisha mpango huo huku akilipatia bunge la Congress hadi mwezi Machi kuwa na mpango mbadala.

Waziri Ndalichako awapa wiki moja TBA

Waziri wa elimu,sayansi,na teknolojia na ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewapa wiki moja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuonyesha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa, hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzil

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo leo alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea mradi huo na kutoridhishwa nao, baada ya kukuta hauna maendeleo yoyote huku serikali ikiwa imeshalipa gharama za ujenzi.

“Ninawapa wiki moja, nataka hapa nione vifaa vyote vya ujenzi viwe vimemwagwa vywa kutosha, nataka nione mafundi wa kutosha, haiwezekani site kubwa kama hii mafundi hawafiki hata 40, kweli kazi itaenda!? Niliwaambia muongeze mafundi mwezi wa 11 lakini kwa sababu mlizozijua wenyewe hamjaongeza, sasa ndani ya wiki moja wasipoongeza mafundi, hatuwezi kuwa na mkandarasi ambaye haendani na matakwa ya mteja, nimekwisha wapatia bilioni 3 na milioni 900,  nikiangalia fedha nimezitoa tangu mwezi wa 8 sioni kazi ambayo inafanana na kiwango cha fedha ambayo nimewapatia, ndani ya wiki moja wasipotimiza angalieni namna ya kuvunja huo mkataba.”, amesema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako ameendelea kwa kulalamika kuwa wakandarasi hao wamekuwa wakiaminiwa na serikali na kuwapa miradi mingi, lakini wamekuwa wakisua kukamilisha miradi kwa muda.

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

DOWNLOAD VIDEO

Nafasi za kazi leo Jan 20

Kocha Mpya wa Simba apagawishwa na Okwi

KIKOSI cha Simba,  Alhamisi kilijitanua kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ambao Simba ilikuwa ikihitaji zaidi matokeo ya ushindi ili ijihakikishie nafasi yake ya kukaa kileleni, ilifanikiwa kupata bao la mapema dakika ya tatu lililofungwa na Shiza Kichuya. Beki wa kati wa timu hiyo,

Asante Kwasi, aliongeza bao la pili dakika ya 24 baada ya kukwepa mtego wa kuotea aliowekewa na mabeki wa Singida United.

Mara baada ya Kwasi kufunga bao hilo, kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa, alinyanyuka kwenye kiti chake akiwa jukwaani na kuanza kushangilia pamoja na ofisa habari wa timu hiyo, Haji Manara huku akiwapungia mkono mashabiki wa timu hiyo.

Dakika ya 65 wakati Emmanuel Okwi wa Simba anajiandaa kuingia kuchukua nafasi Mzamiru Yasin, mashabiki wa timu hiyo walikuwa wakimshangilia kwa nguvu jambo ambalo lilimhamasisha straika huyo na kuipatia Simba bao la tatu dakika ya 75.

Okwi aliongeza bao la nne dakika ya 82 ambapo kwa mara nyingine, Mfaransa, Lechantre aliinuka kwenye kiti na kushangilia kwa nguvu. Katika mchezo huo, Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji wawili ambapo ilianza kumtoa Mwinyi Kazimoto dakika ya 22 na nafasi yake kuchukuliwa na Said Ndemla kabla ya dakika ya 65 kutoka Mzamiru na kuingia Okwi.

Kwa upande wa Singida United, dakika ya 59 ilimtoa Kiggy Makasi na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Chuku. Kwa matokeo hayo, Simba inaendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 29 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27. Mtibwa Sugar ni ya tatu ina pointi 24, Singida inakamata nafasi ya nne na pointi 23, huku Yanga ikiwa ya tano na pointi 22.

Wafanyabiashara waifungukia Serikali

Waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango

Wafanyabiashara nchini wameiomba Serikali kuacha kufanyakazi kwa kukurupuka ikiwamo kuwaadhibu kwa makosa ya wengine badala yake iwe kitu kimoja na sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa Taifa.

Wito huo ulitolewa jana na makamu mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte kwenye mkutano baina yao na Serikali ulifanyika katika ukumbi wa Hazina mjini hapa na kuhudhuriwa na wabunge na baadhi ya mawaziri.

Shamte alisema katika baadhi ya maeneo, Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka na kujikuta ikiwaumiza wafanyabiashara ikiwamo masuala ya kodi.

Makamu mwenyekiti huyo alisema sekta binafsi inaumizwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa kukurupuka hasa wa kuwaadhibu watu wasiohusika kwa kosa la mtu mmoja.

“Wakati mwingine watu wanaumizwa sana kwa ajili ya maamuzi haya, kodi na kufunga biashara za watu ilhali kosa linakuwa la mtu mmoja. Kwa nini hamuondoi kasoro hiyo?” alihoji Shamte wazo ambalo liliungwa mkono na mkurugenzi mtendaji wake, Godfrey Simbeye.

Akijibu hoja hiyo, waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango alikiri kuwapo kwa uamuzi wa kushtukiza serikalini na kusema wakati mwingine inalazimika kufanya hivyo.

Dk Mpango alisema wakati mwingine kuna madhara kwa watu kukurupuka na kufanya vitu visivyokuwepo na kusema ndani ya Serikali, kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wanafanya vitu ama kwa kukurupuka au kutokujua.

“Nakiri kweli ndani ya Serikali kuna watu ambao wanafanya mambo ya ovyo na kuisababishia Serikali hasara kubwa, lakini kuna wakati tunafanya hivyo kwa sababu inabidi tufanye hivyo kwa masilahi ya nchi,” alisema Dk Mpango.

Hata hivyo, aliwatupia lawama baadhi ya wafanyabiashara akisema wamekuwa na tabia ya kukwepa kodi jambo ambalo ni kinyume na Serikali.

Sababu ya Engine kumchukua Wolper

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Engine ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kumng'oa Jackline Wolper na kumuweka ndani, ameweka wazi sababu za kuamua kumtumia msanii huyo kwenye kazi yake.

Akizungumza kwenye Friday Night Live Engine amesema Wolper ni miongoni mwa wanawake wachache Tanzania wanaojitambua, na ndio sababu iliyomfanya asifikirie mara mbili kumfuata.

“Wolper ni mwanamke jasiri, mwanamke anayejitambua , anajituma yuko fit kila idara, na ndio maana nikamfuata”, amesema Engine.

Msanii huyo ambaye ameachia kazi yake mpya, amewaomba watanzania kufuatilia kazi zake kwani alishafanya kazi nyingi siku za nyuma lakini hazikuwahi kufanya vizuri.

Waziri Mkuu aagiza kiongozi huyu akamatwe

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said.

Agizo la Waziri Mkuu limekuja kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Wilayani Bunda mkoani Mara zinazomkabili Mkuregenzi huyo. Waziri Mkuu yupo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Mhandisi Gantala Said ameshindwa kueleza sababu zilizosababisha mradi wa maji mjini Bunda kutokamilika pamoja na Serikali kutoa fedha nyingi kwaajili ya kutekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.

Majaliwa amesema Mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi wa mradi huo ameshalipwa zaidi ya Sh. bilioni saba na mradi haujakamilika huku wananchi wakiendelea kutumia maji ambayo siyo salama.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw. Adam Malima ameagiza kufungwa kwa ofisi za MUWASA na kuwataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchungi utakapokamilika.

Wastara: "Sitozikwa na wasanii pekee"



Msanii Wastara Juma

Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amesema hatokuja kumladhimisha mtu yeyote katika tasnia ya 'bongo movie' kuwa yeye hana pesa ya kujitibia ugonjwa wake unaomsumbua kwa madai hata siku ikitokea akifa hawezi kuzikwa na hao pekee yao.

Wastara ametoa kauli hiyo kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) kinachorushwa na EATV tinga namba moja kwa vijana, baaada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kutomuamini kwa kile kinachomsumbua huku wengine wakidiriki hata kujaribu kumwambia anatafuta kiki kupitia tatizo hilo linalomsumbua la mguu wake.

"Yani hapa mtu anaweza akaniumiza kwa maneno au vitendo kwa sababu yeye anaamini kwa mawazo yake na kichwa chake kwamba, mimi nimekaa kitandani siumwi au pengine nimejiona nimepotea katika ulimwengu hivyo natafuta kiki yaani nijifunue nguo niupige picha mguu wangu uliyochanika kisha niuweke kwenye gazeti ama kwenye runinga (Tv) ?", alihoji Wastara.

Hata hivyo Wastara amesema hawezi kubadilisha fikra za watu wanavyofikilia kwa kuwa hayo ndiyo maisha yao ya kutoamini jambo lolote lile.

"Na kama kuna wasanii ambao wanaamini mimi siumwi siwezi kumladhimisha hata siku moja na ambaye atasema hatokuja kumtembelea Wastara kwa sababu haumwi au hana shida pesa, mimi siwezi kumfanya aniamini kwamba sina pesa. Sitoweza kufanya hicho kitu kwa sababu maelezo ninayoyaeleza katika runinga ndiyo yaleyale hayotokuja kubadilika. Kwa hiyo ninachoongea hapa ni ukweli hautokuja kubadilika miaka yote hata nikifa", alisisitiza Wastara.

Pamoja na hayo Wastara aliendelea kwa kusema "wapo watu wa kweli wanaoamini na wengine wasioamini ambao huwezi kuwafanya waniamini. Watanzania wanaoniamini mimi wanatosha kwa sababu mwisho wa siku sitokuja kujizika mwenyewe au kuzikwa na wasanii pekee yake", alisema Wastara.


Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Yawaandikiia Barua Wabunge Kutaka Miamala Yao

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewaandikia barua baadhi ya wabunge, ikiwataka kuwasilisha taarifa za miamala ya benki za kuanzia Januari hadi Desemba 2017.

Sekretarieti hiyo imetaka taarifa hizo ziwe zimeifikia ndani ya siku 30 kuanzia Januari 15, 2018.

Barua hiyo  inawataka wabunge hao  kutekeleza agizo hilo ili kuthibitisha taarifa zilizomo kwenye tamko lake  alilowasilisha.

Ofisa mmoja wa taasisi hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, alithibitisha kuwepo kwa barua hizo, akisema si wote walioandikiwa barua za kutakiwa kutoa taarifa hizo.

Hata hivyo, alisema wabunge walioandikiwa ni wale ambao fomu zao zinaonyesha haja ya uhakiki zaidi wa taarifa zao.

Rais wa John Pombe Magufuli ndiye alikuwa wa kwanza kuwasilisha fomu yake ya tamko kuhusu rasilimali na madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo Mtaa wa Ohio, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam Desemba 28, 2017.

Baada ya kuwasilisha fomu hiyo, Rais aliipongeza sekretarieti hiyo kwa kazi inazofanya na kumtaka Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu, Harold Nsekela kutopokea fomu ya kiongozi yeyote ambaye angeshindwa kuwasilisha tamko la kabla ya Desemba31, 2017.

Kauli hiyo ya Rais iliwaamsha viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge na viongozi wengine wa Serikali kufurika kwenye ofisi hiyo kuwasilisha matamko yao ya mali walizonazo.

Chadema kugombea Kinondoni na Siha

 Wakati naibu katibu mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu akichukua fomu ya kuwania ubunge wa Kinondoni, mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ameeleza sababu zilizowafanya kurejea katika uchaguzi wa Februari 17.

Mwalimu na mwenzake wa Siha, Elvis Mosi walipitishwa na Kamati Kuu ya Chadema jana kugombea ubunge wa majimbo hayo huku Mbowe akisema, “hiki ni chama cha siasa si zege inayoendeshwa na matamanio na ushawishi wa wananchi.”

Chadema na vyama vinavyounda Ukawa- NLD, CUF, NCCR Mageuzi- pamoja na Chaumma na ACT Wazalendo vilisusia uchaguzi mdogo wa ubunge wa Longido, Songea Mjini na Singida Kaskazini uliofanyika Januari 13 kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutoridhishwa na mazingira ya uchaguzi wa udiwani katika kata 43 uliofanyika Novemba 26.

Vyama hivyo viliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kusitisha uchaguzi huo ili kutoka fursa ya kukutana na kufanya tathmini ya mazingira ya uchaguzi huo jambo ambalo tume hiyo ililipinga ikisema inasimamia sheria.

Jana, Mbowe alisema walipotangaza kutoshiriki uchaguzi wa Januari 13 walitoa sababu za kutoridhishwa na uchaguzi wa madiwani wa kata 43. “Hatukusema kwamba hatutashiriki kabisa uchaguzi hapana, tulitoa sababu kuwa hatukuridhishwa na uchaguzi wa zile kata 43. Bila shaka mmeona wenyewe hata uchaguzi ulivyokuwa, kama haukuwepo na hata vyama vingine vilivyoshiriki kama havikuwepo vile,” alisema mbunge huyo wa Hai.

“Kilio chetu kimesikika ndani na nje ya nchi, kimesikika kwa wananchi na kwa hatua hiyohiyo tumeona hatutawatendea haki wananchi wa Kinondoni na Siha ambao wamewekewa wagombea ambao hawawataki na hilo kila mtu analijua.”

Mgombea wa CCM aliyepitishwa kugombea Jimbo la Kinondoni ni Maulid Mtulia, ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CUF kabla ya kuhamia chama tawala kwa madai ya kuunga mkono utendaji kazi wa Rais John Magufuli. Katika Jimbo la Siha, chama tawala kimemuweka Dk Mollel aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chadema, lakini akakihama chama hicho na kujiunga CCM kwa madai ya kuunga mkono utendaji kazi wa Rais Magufuli.

Mbowe alisema, “Tunarudi katika uchaguzi, vyombo vinavyopaswa kusimamia haki vifanye hivyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vingine vyote, hatutaidai tena haki kwa kupiga magoti hivyo watekeleze majukumu yao ipasavyo.”

Alipoulizwa ilikuwaje wakampitisha Mwalimu ambaye hakushiriki kura za maoni, Mbowe alisema utaratibu wa kura ya maoni ndani ya Chadema haupo kikatiba, wanaamini maridhiano ndiyo njia sahihi ya kutokukigawa chama.

“...Unajua unapofanya kura za maoni unaweza kuwa na makundi mawili na adui yako akayatumia makundi hayo kufanikisha kumpata mtu ambaye ni dhaifu, kwa hiyo Kamati Kuu imeyaona hayo na ililiona hilo Kinondoni ndiyo maana ikamteua Mwalimu,” alisema Mbowe

Vuguvugu laisukuma

Wakati Mbowe akitoa sababu hizo, baadhi ya watu waliojitokeza kuomba kuteuliwa kugombea ubunge wa Kinondoni walisema vuguvugu la kuanzisha mchakato wa kuchukua fomu limesaidia chama hicho kushiriki uchaguzi huo mdogo.

Vuguvugu hilo lilitokana na Chadema Wilaya ya Kinondoni kutoa ruhusa kwa wanachama wao kutangaza nia ya kugombea jimbo hilo kisha mchakato wa kuchukua na kurudisha fomu kwa ajili ya kuomba kuteuliwa uliofanyika Januari 16.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki, mkurugenzi wa mambo ya nje na itifaki wa Chadema, John Mrema alinukuliwa akisema msimamo wa Ukawa wa kutoshiriki uchaguzi wa majimbo ya Siha na Kinondoni haujabadilika na kwamba wameunda kamati ndogo inayofanya utafiti kuhusu mchakato huo.

Alisema hata mchakato wa kuchukua fomu uliokuwa unafanywa na ngazi hiyo ya wilaya haukuwa na baraka za ngazi za juu.

Pamoja na hayo, mchakato wa kura za maoni Kinondoni uliendelea kwa wanachama saba ambao ni David Assey, Nicholus Agrey, Rose Moshi, Mustafa Muro, Ray Kimbitor, Juma Uloleulole na Mozah Ally kupigiwa kura.

Katika mchakato huo wa kura za maoni, Kimbitor aliibuka kidedea kwa kuwabwaga wenzake na baada ya kumalizika viongozi wa wilaya walisema wanayapeleka majina hayo yote saba katika kikao cha dharura cha Kamati Kuu kilichoketi jana ili kupata baraka na kusubiri uteuzi wa mgombea mmoja kutoka katika chombo hicho cha uamuzi.

Akizungumzia uamuzi huo wa Kamati Kuu, Kimbitor ambaye pia ni Diwani wa Hananasif alisema shida yao ni kuona Chadema inashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na kuna dalili za chama hicho kuibuka mshindi kutokana na misingi bora iliyojiwekea.

“Kila mtu anajua kulikuwa na sintofahamu Chadema kushiriki au kutoshiriki. Ndiyo maana sisi tulianzisha lile vuguvugu la kuchukua fomu ndani ya chama na hatimaye limezaa matunda kwa chama kuingia katika uchaguzi huu,” alisema Kimbitor.

Katibu wa Chadema Mkoa Dar es Salaam, Henry Kilewo alisema Kamati Kuu ilipelekewa majina tisa na jina la Mwalimu lilirudi baada ya kupendekezwa na alisisitiza mchakato uliofanywa na ngazi ya wilaya haukuwa na baraka ya juu.

“Kesho (leo) tutatoa ratiba za kampeni baada ya mchakato huu kukamilika. Nawaomba wana-Chadema na Ukawa wawe watulivu kila kitu kitakwenda sawa na mgombea wao yupo makini,” alisema Kilewo.

Kwa upande wake, Mwalimu ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 aligombea Jimbo la Kikwajuni na kushindwa na mgombea wa CCM, Hamad Yussuf Masauni aliishukuru Chadema kwa imani naye na kumpa nafasi hiyo.

“Naingia katika kinyang’anyiro cha kuomba ridhaa ya wakazi wa Kinondoni kuwa mbunge wa Kinondoni. Siendi kuwa mbunge wa Chadema au Ukawa, nitakuwa mbunge wa watu wa Kinondoni,” alisema Mwalimu na kuongeza.

“...Naomba wakazi wa Kinondoni watupime, watuchuje na watutathmini wagombea na baadaye waamue nani anakidhi vigezo na anatosha kuwatumikia katika kipindi cha miaka mitatu iliyobakia.”

Alisema Kinondoni ni taswira na sura ya nchi na imebeba vitu vingi kuliko kawaida na ana imani ya wakazi wa jimbo hilo watawapima vizuri kabla ya kufanya uamuzi wa kuwachagua na atahakikisha anasimamia vyema masilahi ya Taifa.

Amber Lulu afunguka historia ya kusikitisha ya maisha yake

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alipata umaarufu kwa kupiga picha za utupu na kuweka mitandaoni, Amber Lulu, amesimulia historia ya maisha yake ambayo imemfanya abadilike na kuwa alivyo sasa.

Akizungumza kwenye Backstage ya Bongo Fleva Top 20 ya East Africa Radio, Amber Lulu amesema maisha yake ya nyuma yalikuwa yenye mahangaiko ya maisha akiwa na umri mdogo, huku akilazimika kujitafutia hadi pesa ya shule.

Amber Lulu amesema wakati yupo mdogo akisoma mama yake alikuwa na tatizo na lililomfanya ashindwe kutimiza majukumu mengi ya kifamilia, hivyo akaamua kujiingiza kwenye masuala mbali mbali ya kujitafutia riziki ili aweze gharama za kumudu maisha.