Saturday, 20 January 2018

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

DOWNLOAD MP3

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya
DOWNLOAD VIDEO

DOWNLOAD MP3

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download
 
Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Wadaiwa kubakwa baada ya kujifungua hospitalini Kenya



Waziri wa afya nchini Kenya Dkt Cleopha Mailu ameamrisha uchunguzi kufanywa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta baada ya wanawake waliojifungua kudai kwamba wanadhalilishwa kingono.

Taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao zinadai kina mama waliojifungua wamekuwa wanashambuliwa na baadhi ya wafanyikazi wakati wakienda kwenye chumba cha watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao.

Chumba hicho cha watoto huwa ghorofa tofauti na wadi za wanawake waliojifungua.

Wasimamizi wa hospitali hiyo wamesema hawajapokea malalamiko yoyote.

Yote yalianza baada ya ujumbe kuandikwa aktika ukurasa wa Facebook kwa jina Buyer Beware ambao mara nyingi hutumiwa kuwatahadharisha wateja na wanunuzi wa bidhaa na huduma.

Ujumbe uliwatahadharisha kina mama wanaojifungulia katika hospitali hiyo kwamba wamo hatarini ya kudhalilishwa kingono na baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Wanawake wengine walichangia na kudai wamewahi kudhalilishwa au jaribio kufanywa, au jamaa na marafiki zao wakadhalilishwa.

Wengi wanadai kina mama waliojifungua waliviziwa wakiwa njiani kuelekea chumba hicho cha kunyonyeshea watoto au wakirudi chumba chao baada ya kunyonyesha.

Baadhi ya wanaodaiwa kunyanyaswa kingono, ujumbe unasema, walitendewa kitendo hicho siku chache baada yao kujifungua kupitia upasuaji.

Waziri Mailu ameagiza uchunguzi wa dharura kufanyika na ripoti kamili kuwasilishwa kwake kufikia Jumatatu.

Afisa mkuu mtendaji wa hospitali hiyo Lily Koros amesema hakuna mwanamke hata mmoja aliyewahi kulalamika kwamba alidhalilishwa kingono hospitalini humo.

Amesema hospitali hiyo huwa chini ya uangalizi wa kamera za usalama (CCTV) wakati wowote na hakuna kisa hata kimoja kilichogunduliwa.

Amewataka walio na habari kupiga ripoti kwa maafisa wa hospitali au polisi.

Hospitali ya taifa ya Kenyatta, Nairobi huwahudumia kina mama takriban 100 wanaojifungua kila siku.

Watoto waliozaliwa huwekwa chumbani ghorofa ya kwanza nao wanawake kwenye wodi za kujifungulia kwenye ghorofa ya chini.

Maswali sasa yameanza kuulizwa kuhusu muundo na mpangilio wa vyumba katika hospitali hiyo ambao huwalazimu kina mama waliojifungua kupanda ngazi au lifti kwenda kuwanyonyesha watoto wao, ikizingatiwa kwamba baadhi hujifungua kupitia upasuaji.

Diwani afariki dunia Kwimba



Diwani wa Kata ya Lyoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza, Julius Samamba (CUF), amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Taarifa kwa umma iliyotelewa leo Ijumaa (jana) na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Pendo Malebeja imeeleza kuwa diwani huyo alifariki dunia Januari 16 akiwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza alikolazwa kwa matibabu.

“Mazishi ya marehemu yanatarajiwa kufanyika leo Januari 19 katika kijiji cha Kimiza kata ya Lyoma,” anasema taarifa hiyo.

Pamoja na kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, madiwani na watumishi wa halmashauri hiyo, Malebeja amesema kifo cha diwani huyo kuwa pigo kwa halmashauri kutokana na umahiri na uwezo aliokuwa nao katika kujenga na kusimamia hoja kwenye mijadala ya masuala ya maendeleo.

Source: Mwananchi

Povu la kocha wa Simba kwa Mavugo


Laudit Mavugo.

KOCHA Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma amesema kuwa ushindi ambao timu yake iliyoupata juzi Alhamisi katika mchezo dhidi ya Singida United ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya wachezaji wake huku akimtolea ‘povu’ straika wale Laudit Mavugo.

Simba ilipata ushindi wa mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya wababe hao wa Singida ambapo mabao yake yalifungwa na Shiza Kichuya, Asante Kwasi na Emmanuel Okwi aliyefunga mawili. Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Djuma alisema nafasi ya Okwi kucheza ilitakiwa ichukuliwe na Mavugo lakini kwa kuwa

Mavugo hakuonyesha kiwango kizuri mazoezini ilimbidi afanye mabadiliko hayo. “Okwi amefanya mazoezi na sisi siku mbili tu kama mnavyojua hakuwepo kambini, nilipanga kumtumia Mavugo lakini nimemwambia kuwa hakuonyesha uwezo mzuri, ndiyo maana nikaamua kumpa nafasi Okwi na kweli ameitumia vizuri. “Nimeshamueleza Mavugo kuwa yeye ni ndugu yangu lakini katika hili suala la kazi anatakiwa kuonyesha uwezo na kufanya kweli, siwezi kumpa nafasi kama haonyeshi uwezo,” alisema kocha huyo.

KUHUSU KOCHA MPYA

Kuhusu kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyekuwepo jukwaani akifuatilia mchezo huo, Djuma alisema yeye hana tatizo na ujio wa kocha huyo, anamkaribisha na yupo tayari ku- fanya naye kazi. “Nipo tayari wala sina tatizo, namkaribisha na tutakuwa pamoja, kuhusu mfumo na maendeleo mengine nitampatia ripoti kisha yeye ndiye atakayeamua juu ya kutumia au la,” alisema. Upande wa Kocha wa Singida United, Hans van Pluijm alisema matokeo ya mchezo huo yametokana na walinzi wake kufanya makosa na Simba wakayatumia vizuri.

Mapenzi yamtesa Kajala kisa mwanaye



STAA wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa hivi sasa anaumizwa na mapenzi ya kufichaficha kwa sababu ya kulinda heshima yake kwa mtoto wake wa kike, Paula kwa kuwa sasa amekuwa msichana mkubwa.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Kajala alisema amekuwa kwenye wakati mgumu sana wa kuwa na uhusiano wa kificho lengo likiwa ni kutomharibu mwanaye huyo ambaye ana uelewa mkubwa na anatambua kila kitu.

“Sipendi Paula anijue kiundani kuhusiana na mahusiano kwa sababu kwa umri aliofikia na darasa alilopo (Kidato cha nne) kama sitakuwa na usiri ataelewa kila kitu, sio Kajala yule tena wa zamani wa kuweka mpenzi wazi ingawa inaniumiza kwani sikuzoea, na mapenzi ya siri yanaumiza asikwambie mtu,” alisema Kajala.



Chuchu Hans afunguka kuachana na Ray


MSANII wa filamu za Kibongo, Chuchu Hans ameibuka na kusema kuwa tetesi zilizozagaa akidaiwa kuachana na mzazi mwenziye Vincent Kigosi ‘Ray’ na kwamba ndiyo sababu ya kubadili jina lake kwenye ukurasa wake wa Instagram siyo za kweli.

Awali kwenye ukurasa wa Insta Chuchu alikuwa akijiita Chuchu Hans the Great na sasa anajiita Chuhans Kichuna, jambo lililowafanya wengi waamini safari ya mapenzi yao imefika mwisho.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu alisema kuwa yeye ameamua tu kubadili jina na wala hajaachana na Ray na kama wapo wanaosubiri penzi livunjike, watasubiri sana.

“Waniache jamani kila siku nimeachana na Ray… nimeachana na Ray…, nina sababu zangu za kubadilisha jina, haina maana kwamba tumeachana, hata hivyo sitaki kuongelea sana suala hilo kama tumeachana au la, majibu mtayapata subirini tu,”alisema Chuchu.

Serikali Yakataza Kulima Pamba kwa Mkataba


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imekataza kilimo cha pamba cha mkataba kwa sababu kinawanyonya wakulima.

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 19, 2018) wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua zahanati ya Hunyari wilayani Bunda, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mara.

“Ni marufuku kwa wanunuzi wa pamba kulima pamoja na wakulima kwa sababu wakulima wanakosa uamuzi wa kupanga bei. Kuanzia sasa zao hilo litauzwa kwa njia ya mnada.”

Alisema Serikali imeweka mkakati wa kuimarisha mazao makuu ya biashara ambayo uzalishaji wake umeanza kupungua likiwemo na zao la pamba.

Waziri Mkuu alisema Serikali imeamua kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa kilimo cha zao la pamba kuanzia hatua za maandalizi ya shamba, pembejeo hadi masoko.

Pia Waziri Mkuu amewaagiza Maofisa Kilimo katika wilaya hiyo wawafuate wakulima vijijini kwa ajili ya kutoa elimu itakayowawezesha wakulima kulima kwa kufuata njia bora za kisasa.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wafugaji kuhakikisha wanakuwa na idadi ya mifugo kulingana na uwezo wa eneo lao.“Marufuku kulisha mifugo katika mashamba ya watu.”

Amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa mfugaji yeyote atakayelisha mifugo yake katika mashamba ya wakulima kwani tabia hiyo huchangia migogo baina yao.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Steve Nyerere: “Nimekaa Ndani Wiki 3, Nimeona Waliosema Nina Ukimwi”


January 19, 2018 Muigizaji maarufu wa Bongomovie Steve Nyerere amezungumza baada ya kuugua kwa wiki tatu Steve ameeleza kuwa alichokuwa anaumwa kuwa ni miguu na siyo VVU kama ilivyokuwa inasemwa kwenye mitandao japo hashangai watu kumsema.

Steve amesema hakuna mtu wake wa karibu aliyezusha suala la ugonjwa wake bali ni mitandao tu ndo imevujisha, alipoulizwa kama Wema Sepetu alikuwa miongoni mwa watu walioenda kumtembelea alijibu kuwa Utu haulazimishwi na kumuona mgonjwa hakulazimishwi pia.


Jenerali wa Jeshi ampa Rais Kabila siku 45 aachie Urais



Haijapita hata miezi mitatu toka tushuhudie Jeshi likiingilia kati na kumuondoa madarakani Rais aliekaa muda mrefu madarakani, Robert Mugabe wa Zimbabwe….. leo tena tunasikia huko Congo DRC Mwanajeshi mmoja ampa Rais Kabila siku 45 awe ameachia madaraka.

Tunafahamu kwamba Rais Kabila alimaliza muhula wake wa pili na wa mwisho kikatiba kuwa Rais mwezi December 2016 lakini hajaachia madaraka, mengi yamesemwa na Serikali ikiwemo “hatuna pesa za kutosha kufanya Uchaguzi Mkuu”

January 19 2018 Mwandishi wa habari Byobe Malenga alieko Congo DRC ameiambia millardayo.com kwamba Jenerali mmoja wa Jeshi aitwae John Tshibangu ameasi na kutangaza vita na Rais Kabila, amempa siku 45 aachie madaraka.

Asubuhi ya Ijumaa January 19 2018 Wanajeshi walionekana kuizingira kwa wingi IKULU ya Kinshasa huku video iliyorekodiwa na Jenerali Tshibangu ikiendelea kusambaa ambapo ndani yake ameonekana kazingirwa na Wanajeshi wenye silaha.

Kwenye video hiyo Tshibangu amenukuliwa akisema “Nafahamu siri ya Rais Kabila, sasa ni muda wa kuondoa Serikali ya Mabeberu na Udikteta, na ni lazima Rais Kabila aombe msamaha kwa Wakongo kuanzia Makanisani, Shuleni na hata Raia wa kawaida kwa kosa la kushindwa kuiongoza Nchi”

“Mimi kama Mwananchi mwenye msimamo na huruma kwa mateso yenu, niliamua kujitokeza ili kumfukuza Joseph Kabila kwa nguvu za vita na kijeshi, nawahakikishia kwamba tutamuwinda na atakimbia. ” – John Tshibangu.

Tshibangu amelitaja kundi lake la Waasi kwamba linaitwa Forces Nouvel du Congo ikimaanisha NGUVU MPYA KWA AJILI YA CONGO ambapo Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa kumekuwa na majaribio ya mapinduzi katika Serekali ya Congo ambapo IKULU ya Taifa imezungukwa na Wanajeshi wengi wanaoonekana kama Wageni, yaani sio Wanajeshi wa congo.

Raisi Kabila amekabiliwa na upinzani mkali kutokana na nia yake ya kutaka kugombea Urais kwa muhula wa tatu baada ya muhula wake wapili kumalizika mwezi December 2016.

John Tshibangu

Source: Millardayo

Friday, 19 January 2018

Ndege yatetemeka angani



Ndege moja ya Malaysia ililazimika kutua katika eneo la Australia ya kati baada ya tatizo la kiufundi kuifanya kuanza kutetemeka ikiwa angani, wamesema abiria.

Ndege hiyo aina ya MH122 ilikuwa inasafiri kuelekea Kuala Lumpur kutoka Sidney siku ya Alhamisi wakati iliporudi katika eneo ambalo haliko mbali na Broome, kaskazini Magharibi mwa Australia.

Ndege hiyo iliokuwa ikiwabeba watu 224 ilitua salama katika uwanja wa ndege wa Alice Springs Airport.

Abiria wanasema kuwa ndege hiyo ilikuwa ikitetemeka na kutoa sauti kubwa.

Katika taarifa yake, kampuni ya ndege ya Malaysia Airline ilisema kuwa ndege hiyo ilibadilsha safari kutokana na tatizo la kiufundi.

Hatahivyo haikusema ni matataizo gani. Abiria Sanjeev Pandev alisema kuwa ndege hiyo ilionekana kuwa na tatizo hilo saa nne kabla ya safari kuanza.

''Ilikuwa ikitetemeka na kelele zilikuwa kubwa '', aliambia BBC.

''Watu walikuwa wakiomba na wengine walikuwa wakitokwa na machozi'', aliambia BBC.

Alisema kuwa abiria walionyeshwa njia za kubaliana na dharura na wafanyikazi wengi wao wakionekana kuogopa na kushtuka.

Simba kukutana na waliokwamisha mipango




Vinara wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC leo alfajiri wameondoka kwa ndege kuelekea mjini Bukoba mkoani Kagera kwaajili ya mchezo wao wa raundi ya 14.

Simba ambayo jana ilishinda mchezo wake wa raundi ya 13 kwa mabao 4-0 dhidi ya Singida United kwenye uwanja wa Uhuru, inakwenda kukutana na Kagera Sugar ambayo ilikwamisha mipango yake ya ubingwa msimu uliopita.

Kagera Sugar ilitibua mipango hiyo April 2 mwaka jana baada ya kuifunga Simba mabao 2-1 kwenye mechi iliyopigwa uwanja wa Kaitaba hivyo kuinyima nafasi ya kurejea kileleni ikibaki na alama 55 katika nafasi ya pili na kuwaacha Yanga wakiwa na alama 56 kileleni.

Endapo Simba ingeshinda mchezo huo ingefikisha alama 58 hivyo huenda ingetwaa ubingwa kutokana na bingwa wa msimu uliopita kupatikana kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa, baada ya timu hizo mbili za Kariakoo kufungana pointi.

Simba ambayo kwasasa inaongoza ligi kwa alama 29 mbele ya Azam FC yenye alama 27, itashuka dimbani Kaitaba siku ya Jumapili.