Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Wednesday, 3 January 2018
Sunday, 31 December 2017
Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download
Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download

Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download
DOWNLOAD

Audio | Magic Soldier Ft. Kolly The Magic – Vunja Goti | Mp3 Download
DOWNLOAD
Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download
Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download

Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download
DOWNLOAD

Audio | Msamaria Danielo – Yari Wewe | Mp3 Download
DOWNLOAD
Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download
Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download

Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download

Video | Mr 2Kay – Pray For Me | Mp4 Download
Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download
Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download

Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download
DOWNLOAD

Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download
DOWNLOAD
Manchester United yapata matokeo mabovu

Klabu ya Manchester United bado imeendelea kupata matokeo mabovu kwenye Ligi Kuu soka England baada ya jana kulazimishwa sare ya bila kufungana dhidi ya klabu ya Southampton.
Kwa matokeo hayo Manchester United ambayo ilikuwa nafasi ya pili kwa muda mrefu kwenye msimamo wa EPL imeshuka hadi nafasi ya tatu baada ya Chelsea jana kupata ushindi mnono.
Wakati hayo yakitokea Manchester United imepata janga lingine kubwa zaidi kwa kuumia mchezaji wao tegemezi, Paul Pogba jana kwenye mchezo huo.
Pia kupitia mtandao wa klabu hiyo umethibitisha kuwa mshambuliaji wao Zlatan Ibrahimović kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja kuanzia jana.
Matokeo hayo yanaifanya Manchester United kupata sare tatu mfululizo kwenye EPL na kupoteza mechi moja ya kombe la EFL.
Matokeo mengine ya ya mechi za jana za EPL ni kama ifuatavyo.

Countinho asaini Barcelona

Kampuni ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Nike imevujisha kuwa huenda usajili wa nyota wa Liverpool na Brazil Phillipe Coutinho kwenda Barcelona umekamilika tayari.
Nike kupitia tovuti yao jana waliweka picha ya jezi ya Barcelona ya msimu huu yenye jina la Coutinho, huku wakiambatanisha na ujumbe unaoonyesha kuwa nyota huyo anatua Cam Nou kabla ya msimu kumalizika.
"Philippe Coutinho yuko tayari kuipamba Camp Nou'', Waliandika Nike ujumbe huo kwenye picha ya jezi za FC Barcelona za msimu huu 2017-18 iliyoandikwa jina la Coutinho.
Baadae Nike walifuta ujumbe huo baada ya mashabiki wa Liverpool kuanza kuishambulia kampuni hiyo kuwa inashinikiza mchezaji wao ahamie Barcelona kwa kuwa Nike wanaidhamini klabu hiyo ya Hispania.
Coutinho mwenye umri wa miaka 25 amefunga mabao saba na kutoa msaada wa mabao sita kwenye Ligi Kuu soka nchini Englanda msimu huu.
BREAK NEWS; Askofu Kakobe azungumzia utajiri wake

Ikiwa yamebaki Masaa machache kabla ya mwaka 2017 kumalizika na kuukaribisha mwaka mpya wa 2018, Askofu Mkuu wa Makanisa ya Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe ameunguruma katika ibada aliyoiongoza Leo kanisani huku akijinasibu kuwa ni Tajiri kuliko Serikali zote duniani
Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe amesema kwamba yeye sio tu Tajiri kuliko Serikali ya Tanzania, Bali ni Tajiri kuliko Serikali zote duniani ikiwemo ya Marekani na Uingereza'.
" Wanaosema Kakobe amekimbia nchi nawashangaa sana sipo na wala siendi popote, kipindi Fulani walikuja kuchunguza uraia wangu lakini wakaambulia patupu, tutabanana hapa hapa" Askofu Kakobe
" Watu wanasema Niko kimya sana wala sipo kimya tatizo wanataka nizungumze wanayoyataka wao, sasa Mimi sio mtu wa namna hiyo, ukiniona nimesimama katika madhabau Hays basi ujue nina kibali cha Mungu, mtu ukitwa Mbwa kwani wewe ndio itakua Mbwa? Sasa nashangaa unaogopa nini kuitwa Mbwa wakati wewe sio Mbwa" Askofu Kakobe
Dkt. Shika atangaza nia ya kuoa

Dkt. Louis Shika ambaye amejipatia umaarufu baada ya kutangaza dau la kununua nyumba za Lugumi, amefunguka na kutangaza nia ya kutaka kuoa endapo atapata mwanamke ambaye anamuhitaji.
Dkt. Shika amesema kuwa kwa sasa hana mpango wowote wa kurudiana na wanawake ambao amezaa nao watoto nchini Tanzania bali anatafuta mwanamke mwingine mpya ambaye atamuoa
"Nikimpata anayenihitaji na mimi nikamuhitaji nitaoa , saizi nipo tu kwanza nasubiri ila siyo kama sina mpenzi kwani wapenzi huwa hawakosekani mnakutana, mnapendana lakini mjue kuwa mpenzi na mke ni watu wawili tofauti. Siwezi kabisaa kurudiana na wazazi wenzangu kwani hicho kipindi kimepitwa na wakati saizi nataka mpya" alisema Dkt. Shika
Mbali na hilo Dkt. Shika amesema kuwa hawezi kuhama katika nyumba ambayo anaishi kwa kuwa anaishi bure kwenye nyumba hiyo hivyo ataondoka endapo atapata nyumba yake ila kuondoka na kwenda kupanga ni jambo ambalo hataliweza na kuwa hata huyo rafiki aliyempa nyumba hiyo atamshangaa.
Serikali yatoa maagizo kuhusu matumizi ya Fedha za kigeni

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ametoa maagizo kuhusu matumizi ya fedha za kigeni katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusisitiza kuwa utekelezaji wake uanze tarehe 1 Januari, 2018.
Maagizo hayo ni kama ifuatavyo: –
i. Bei zote hapa nchini zitangazwe kwa shilingi ya Tanzania. Bei hizi zinajumuisha kodi ya nyumba za kuishi na maofisi, bei ya ardhi, gharama za elimu na afya, bei za vyombo vya usafiri na vifaa vya kielektroniki.
ii. Bei ambazo walengwa wake wakuu ni watalii au wateja wasio wakazi zinaweza kutangazwa kwa fedha za kigeni na malipo yake yanaweza kufanyika kwa fedha za kigeni. Bei hizi zinajumuisha gharama za usafirishaji kwenda nchi za nje kupitia Tanzania, gharama za mizigo bandarini kwenda nchi za nje, gharama za viwanja vya ndege na viza kwa wageni, na gharama za hoteli kwa watalii kutoka nje ya nchi. Walipaji wanaotumia fedha za kigeni watambuliwe kwa vitambulisho vyao kama pasi za kusafiria na nyaraka za usajili kwa makampuni.
iii. Viwango vya kubadilishana fedha vitakavyotumika katika kuweka hizo bei katika sarafu mbili viwekwe wazi na visizidi vile vya soko. Ifahamike wazi kuwa ni mabenki na maduka ya fedha za kigeni tu yanayoruhusiwa kupanga viwango vya kubadilisha fedha kutokana na ushindani katika soko la fedha za kigeni.
iv. Mkazi yeyote wa Tanzania asilazimishwe kulipia bidhaa au huduma yeyote hapa nchini kwa fedha za kigeni.
Aidha Dkt. Mpango ameviagiza vyombo vya dola viwachukulie hatua za kisheria wale wote watakaobainika kukiuka maagizo haya ya Serikali.

PPF wazungumzia kukamatwa kwa mfanyakazi wao na mirungi

MFUKO wa Pensheni wa PPF umesema mfanyakazi wake, Anitha Oswald, wa ofisi ndogo ya Moshi aliyekamatwa wiki hii akiwa na madawa ya kulevya aina ya mirungi huko Moshi, Kilimanjaro, alikuwa kwenye likizo ya dharura na kwamba alikamatwa akiwa kwenye gari lake binafsi na nje ya eneo la kazi.
Kwamujibu wa taarifa iliyotolewa na PPF vyombo vya habari na Meneja Uhusiano leo, shirika hilo limesema tuhuma hizo zinamkabili mfanyakazi huyo yeye binafsi na si PPF. Vilevile limelaani vitendo vya aina hiyo na linaunga mkono juhudi za serikali za kupiga vita madawa hayo.
Shirika pia limemchukulia hatua mfanyakazi huyo kwa kuzingatia sera za wafanyakazi wake.
Subscribe to:
Comments (Atom)
 

 

