Saturday, 23 December 2017

Watu 22 wahofiwa kufa maji na 115 kuokolewa Ziwa Tanganyika



Watu 22 wanahofiwa kufa maji katika Ziwa Tanganyika katika ajali ya boti iliyotokea iliotokea leo alfajiri.
Imeelezwa miili ya watu wanne imeopolewa na imetambuliwa na ndugu zao huku watu wengine 115 wameokolewa wakiwa hai baada ya boti kugonga mtumbwi.
Ofisa wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) Mkoa wa Kigoma, Amaniel Sekulu amesema ajali hiyo imetokea katika kitongoji cha Lubengela kijijini Msihezi, Kata ya Sunuka wilayani Uvinza.
Amesema mtumbwi uitwao Mv Pasaka uligongwa ubavuni na boti ya Atakalo Mola na kupasuka, hivyo kuzama ziwani.
Sekulu amesema mtumbwi ulikuwa umebeba abiria 137 waliokuwa wanakwenda kwenye mkutano wa injili katika Kijiji cha Sunuka.
Amesema boti ilikuwa ikitokea Kigoma kwenda Kalya ikiwa imebeba abiria 65.
Sekulu amesema boti na mitumbwi inayobeba abiria hairuhusu kufanya safari usiku.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Sweetbert Njewike akizungumzia ajali hiyo amesema wanaendelea kuwatafuta watu ambao hawajaonekana waliokuwa wakisafiri na vyombo hivyo.
Amesema shughuli za uokoaji zinafanywa kwa pamoja na vikosi vya Polisi, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Mwanamvua Mrindoko amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kulikuwa na dosari zilizosababisha ajali hiyo.
Amezitaja dosari hizo kuwa ni ukosefu wa vifaa vya uokoaji, vifaa vya kuzima moto na boti kufanya safari usiku.
Diwani wa Sunuka, Athumani Chuma amesema ajali hiyo imeacha simanzi kutokana na mazingira iliyotokea.
Amesema licha ya ajali kutokea saa tisa usiku, wanakijiji wameonyesha mshikamano katika kuokoa watu wakiwa hai na hatimaye kuopoa maiti nne.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Msihezi, George Gasper amesema ajali ilitokea umbali wa mita takriban 150 kutoka ufukweni, ikiwa ni muda mfupi baada ya boti la Atakalo Mola kushusha na kupakia abiria katika Kitongoji cha Lubengela.
Desemba 20, watu saba walikufa papohapo na wengine 12 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Saratoga kugongana uso kwa uso na gari ndogo la abiria.
Ajali hiyo imetokea saa 4:30 asubuhi katika Kijiji cha Kabeba katani Mwakizega wilayani Uvinza.

Hamisa Mobetto Na Zari Warushiana Vijembe



Usiku wa kuamkia leo kwenye jiji la Kampala Uganda kulifanyika Party mbili ambapo moja Hamisa Mobetto alihudhuria inaitwa Gal Power na nyingine ni ya Zari All White Party.
Sasa baada ya kumalizika kwa party hizo maneno ya Mashabiki yakaanza wengine wakiponda ya Zari na wengine wakiponda ya Hamisa kwamba ilikua na watu wachache.
Wao wenyewe wameandika vitu kwenye Snapchat zao na ikaonekana kama ni vijembe ambapo Zari ndio alianza kwa kuandika “Kuna tofauti kati ya Tembo na Mbu” ambapo Hamisa alijibu kwa kuandika “Tembo hana madhara sana kwa Binadamu ila mbu….. kila siku watu wanalazwa”

Haji Manara; kitendo cha Klabu yangu kufungwa kwa penanti ni aibu ya mwaka



Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara amefunguka na kusema kitendo cha klabu yake ya Simba jana kufungwa kwa njia ya penati na kuondolewa kwenye michuano ya Azam Sports Federation Cup ni aibu ya mwaka.
Haji Manara alisema hayo jana baada ya waliokuwa mabingwa watetezi wa (Azam Sports Federation Cup) Simba kupigwa na Green Warriors na kuondolewa katika michuano hiyo kwa penati 4-3
"Shame!! Aibu!!!Fedheha!!! Haivumiliki!!!Tumewakera fans wetu zaidi ya twenty millions... nimeumia kuliko siku zote toka nimeanza kazi Simba..Aibu ya mwaka" aliandika Haji Manara

Mtoto aliyefanyiwa upasuaji mara 10 aomba msaada kunusuru maisha yake




Uzinduzi wa kampeni ya Tuko Pamoja, Okoa Maisha ya Mariam imezinduliwa leo jijini Dar es salam huku ikilenga kuarifu Umma wakiwemo wadau kupitia vyombo mbalimbali vya habari kuhusu msichana mdogo Mariam (16) anayesumbuliwa na ugonjwa ujulikanao kama ”Intestinal Obstruction”.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi masoko wa DataVision International, ambaye pia ni Msemaji wa Dar24, Teddy Ntemi Qirtu katika ukumbi wa Serena amesema kuwa uzinduzi huo unalenga kuokoa maisha ya Mariamu na kuwaomba watanzania kwa ujumla kuhusika katika kampeni hiyo kwa kuchangia kwa namna moja au nyingine ili pamoja kuokoa maisha ya msichana huyo.
Aidha Qirtu amewaomba wananchi na wadau kwa ujumla kumchangia mtoto Mariam ili aweze kwenda nchini India kufanyiwa matibabu, mara baada ya jitihada za madaktari bingwa kutoka hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwemo Muhimbili kushindwa kutatua tatizo hilo na kupelekea kumfanyia oparesheni kumi bila mafanikio.
''Gharama za kuratibu shughuli nzima ya matibabu hayo akiwa nchini India ni kiasi cha shilingi milioni 44 za kitanzania'' alisema
Hivyo amewaomba wananchi kuungana na Dar24 kupigania maisha ya Mariam kwa kuchangia fedha kupitia M-lipa, tigo pesa, Airtell Money na Mpesa kwa kuandika namba ya kampuni 400700 na kumbukumbu namba 400700 au kupitia akaunti ya benki ya CRDB kwa akaunti namba 0150021209500 jina la akaunti ni Data Vision International – Tuko Pamoja.
Kupitia vyomba mbalimbali vya habari amewashukuru wale ambao tayari wamekwisha wasilisha michango yao kupitia mfumo maalumu wa M-lipa kama ambavyo imeelekezwa na kuwaomba wadau kuendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuokoa maisha ya Mariam ambae kwa sasa anashindwa kuendelea na masomo.

Vigezo anavyotumia mwanamke kupenda



Watu wengu hujisikia vizuri wanapowavutia wenzao wa jinsia nyingine. Je, unafikiri ni kitu gani kinachomfanya mwanamke aonekane wa kuvutia?
Kuna vitu vingi vinavyojulikana vizuri zaidi kwa upande wa mwanamke kama vile; mwili mzuri, sauti yenye mvuto, nywele, mikono mizuri na mengineyo mengi. Lakini, kuna vingine ambavyo siyo vya kawaida vinavyohusu mwanaume kumvutia mwanamke.
Je, ni vitu au mambo gani ya kipekee ambayo, humfanya mwanamke aguswe na mwanaume fulani na huku mwanamke mwingine akishangaa ni kwa nini mwanamke mwenzake ameguswa sana na huyo jamaa?
Inawezekana yapo mengi ambayo, huyajui. Kwa mfano, mwanamke anaweza akavutiwa na jina la kwanza au la ukoo la mwananume fulani. Hapa mwanamke hufikiri kwamba, huyo mwenye hilo jina hawezi kuwa mtu wa kawaida, na kila kitu anachofanya ni lazima kiwe cha ajabu.
Labda ni kutokana na jina hilo kuwa ni la kigeni au anatoka kwenye ukoo ambao ni bora au wa kipekee au anafikiri labda huyo mwanaume atamwezesha kile ambacho, mara nyingi amekuwa hakipati.
Lakini, inawezekana kabisa kwamba, mwanamume huyo si mzuri sana wa kuvutia au ni mbaya sana kuliko wengine. Hakuna anayejua, labda anachotaka mwanamke huyo ni kujaribu bahati yake ili aone kitakachotokea kwa uhakika ziadi.
Inawezekana pia kuwa, mwanamke anaweza kuchanganyikiwa zaidi baada ya kuona umbo la mwanamume huyo au gari lake. Pengine mambo hayo ndiyo ambayo, amekuwa akiyapenda zaidi. Inawezekana ikawa ni dalili ya bahati kwake kwamba, ametokea katika maisha yake mtu ambae, kwa muda mrefu amekuwa akitamani kumpata.
Upo uwezekano pia kwamba, mwanamke akavutiwa na mwandiko au sahihi ya mwanamume fulani. Wakati mwingine mwanamke hutokea kuwa na uhakika zaidi na kuamini yale anayoambiwa kuhusu tabia ya mwanaume huyo, bila hata kufanya uchunguzi wa kina. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, upo uwezekano wa kuisoma tabia ya mwanaume huyo kwenye sahihi au mwandiko wake.
Mwanamke pia huvutiwa na lafudhi ya mwanamume, fani yake, hobi, na kitu kingine kisicho cha kawaida ambacho mwanamume huyo anakipenda na kukifanya. Hata hivyo, mwanamke anatakiwa awe mwangalifu mno na upande wa pili wa mtu huyo ambao, yeye haujui. Hapa ikiwa na maana kuwa , pamoja na sifa zote hizo alizozibaini kutoka kwake, anapaswa kujua kwamba, mwanamume huyo kama binadamu asiyekamilika pia ana mapungufu na udhaifu mwingi.
Kuufahamu ukweli huu, kutamsaidia katika kuimarisha zaidi na kumfanya awe makini anapotafuta mwanaume wa kuishi naye. Na akumbuke kuwa, wapo wanaume ambao huficha makucha yao au kasoro zao kwa wapenzi wao.
Kuna mwanamke mwingine hupenda mwanaume mwenye vituko, kilema au mwenye kasoro nyingine za kimwili. Yote hayo hutokana na asili ya mwanamke. Na ni mambo yanayoongea ndani mwake kwamba, anataka kumjali na kumhurumia mwanaume huyo.
Kwa kawaida, mwanamke huvutiwa zaidi na kwa urahisi, pale mwanaume anapoonyesha tabia ya usikivu na utulivu. Hata hivyo, mtazamo huu kwa upande wa mwanamke, huhesabika kuwa ni ushindi kwake.
Hali kadhalika, mwanamke huvutiwa na tabia fulani ya kipekee ambayo, mwanaume anayo. Kwa mfano, jinsi mwanaume huo anavyoutumia mkono wake wa kushoto, kwani watu wengi wanatumia mkono wa kulia. Ukweli ni kwamba, labda huyo ndiye mwanaume ambae mwanamke huyo anamtaka, kwani pia wanawake wengine hawawezi kujizuia kuwapenda wanaume wenye macho ya bluu. Hilo pia ni jambo la kawaida.
Mwanamke anaweza kumpenda mwanaume kutokana na jinsi anavyofanya kazi za nguvu au kutokana na mwili wake kuwa na misuli. Ni jambo la kawaida kwa wanawake kufurahia wanaume waliojazia, na inavyoonekana wanawake huwaona wanaume ambao ni lainilaini kuwa wana haiba ya kike au ni mashoga.
Hapo ndipo mwanamke anapolazimika kufikiria kwa makini, kuhusu mwanaume anayetumia muda mwingi kujipodoa na fedha nyingi kwa mambo ya urembo na vipodozi kuliko hata mwanamke, kama kweli anamvutia na anamfaa.
Na kitu kingine ni kwamba, mwanamke humpenda mwanaume anayesaidia kufanya kazi za nyumbani. Kwa kufanya hivyo, mwanamke huamini kwamba, mwanaume huo anamjali na kumthamni.
Kwa kumalizia ni kwamba, mambo mengi yanayomchanganya mwanamke kuhusiana na mwanaume anayemtaka, kwa kweli ni ya kipekee sana na wakati mwingine huonekana kuwa ni kituko, ingawa wakati mwingine yanaweza yakaeleweka vizuri. Mara nyingi vigezo hivyo huonekana kuwa sahihi, iwapo tu mwanamke huyo atajisikia vizuri na kupata ridhiko la nafsi yake.

Friday, 22 December 2017

Tanzania yapolomoka katika viwango vya FIFA



TANZANIA imezidi kuporomoka katika viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ambapo hivi sasa inashika nafasi ya 147 kutoka 142 ya mwezi Oktoba.
Jana Alhamisi, Fifa ilitoa viwango hivyo ambapo inaonyesha ndani ya miezi mitano kuanzia Julai, mwaka huu, Tanzania imeshuka kwa jumla ya nafasi 33.
Ikumbukwe kuwa, kwa siku za hivi karibuni, Tanzania ilifanya vizuri kwenye viwango vya Juni baada ya kushika nafasi ya 114 kutoka nafasi ya 139 ya mwezi Mei. Baada ya hapo, Julai ikashika nafasi ya 120, Agosti 125, Septemba 136, Oktoba 142 na sasa Novemba ni 147.
Kushuka huko kwa Tanzania kunatokana na Novemba, mwaka huu, Taifa Stars kutoka sare ya bao 1-1 na Benin katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye Uwanja wa l’Amitie, Benin.
Katika 10 Bora ya duniani, Ujerumani inaongoza ikifuatiwa na Brazil, Ureno, Argentina, Ubelgiji, Hispania, Poland, Uswisi, Ufaransa na Chile.

Waziri Kigwangalla kuwakutanisha Joketi Na Wema Sepetu





Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla jana Desemba 21, 2017 aliteua majina mengine ya Kamati ya Kitaifa ya kuandaa mwezi maalum wa maadhimisho ya Urithi wa Tanzania. Miongoni mwa wajumbe walioteuliwa ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jokate Mwegelo na Wema Sepetu ambao wataungana na wajumbe 23 aliowateua awali kuunda Kamati ya Kitaifa ya Kuandaa Mwezi Maalumu wa Maadhimisho ya Urithi wa Tanzania.

Mashindano Ya Miss Tanzania kutokuwepo 2017



WAANDAAJI wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, Kampuni ya Lino International Agency Limited, wamesema kwamba hakutakuwa na Fainali za Taifa za shindano la Miss Tanzania kwa mwaka 2017.
Katika taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo imeeleza kuwa sababu kubwa ya kuahirishwa kwa shindano hilo ni ukosefu wa Wadhamini ambao kwa njia moja au nyingine huwezesha kufanyika kwa mashindano hayo kwa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo zawadi za washiriki.
Aidha waandaaji hao pia wamesema kuwa kuchelewa kupata kibali cha kuanza mchakato wa Miss Tanzania 2017, ambacho kilitolewa na BASATA mwezi Septemba mwaka huu pia kimechangia kukosa kwasababu muda ulikuwa umeshaenda.
Mashindano ya kutafuta warembo wa Miss Tanzania yamekuwa yakifanyika kila mwaka na baadae kuibua mastaa mbalimbali kama Wema Sepetu, Lulu Diva, Jokate Mwegelo na wengine 

Thursday, 21 December 2017

Orodha ya mastaa BONGO waliopata watoto mwaka huu 2017




Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto
MWAKA 2017 ndiyo huo unayoyoma na zimebaki siku kumi tu kuingia mwaka 2018. Mwaka 2007, mengi yametokea kwa kila mtu katika maisha yake ya kawaida.
Wapo waliofanikiwa, waliofeli na wapendwa wetu wengine walitutoka kabisa. Kama ilivyo kwenye maisha ya kawaida kuwa na mengi yaliyotokea, vivyo hivyo kwenye ulimwengu wa burudani. Ukiachana na kiki zilizotikisa, matukio ya kuvutia na mengine mengi mazuri na mabaya tumeyashuhudia kwa staa mmojammoja.Miongoni mwa hayo mazuri ni kwa baadhi ya mastaa wa kike ambao walihabatika kuitwa mama kama ifuatavyo;
Muigizaji Faiza Ally akiwa na mtoto wake Lil Junior
MAMA KAIRO (HAPPINESS MILLEN MAGESE):
Mwishoni mwa Julai, mwaka huu, baada ya kutafuta mtoto kwa muda mrefu, mwanamitindo maarufu wa kimataifa, Happiness Millen Magese ‘Ladiva Millen’ alijibiwa kilio chake na Mungu wake.
Millen alijaliwa mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Kairo Michael Magese. Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram, Millen alionesha furaha yake kwa kuandika ujumbe matata ambapo pia alifafanua jina la mtoto wake huyo la Kairo kwamba, linamaanisha ‘utukufu kwa Mungu.’
MAMA JADEN (CHUCHU HANS):
Uhusiano wake na muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ ulianza kama siri. Ghafla, muigizaji Chuchu Hans ni mjamzito. Baadaye mambo yalikuwa wazi hasa Mwezi Januari, Chuchu alipojifungua mtoto wa kiume ambaye yeye na mpenzi wake, Ray walimpa jina la Jaden.
MAMA GOLD (AIKA):
Baada ya kudumu kwenye uhusiano kwa zaidi ya miaka nane, Aika na mpenzi wake, Nahreel, mwanzoni mwa Mwezi Desemba walibahatika kupata mtoto wa kiume ambaye
walimpa jina la Gold.
MAMA PRINCE ABDUL (HAMISA MOBETO);
Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto naye anaingia kwenye orodha hii baada ya Mwezi Agosti, mwaka huu kupata mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Abdul. Kwa Hamisa, huyu ni mtoto wa pili kufuatia awali kupata mtoto wa kike aitwaye Fantas.
MAMA CLARIBELL (ESHA BUHETI);
Wakati ikiwa imepita siku moja tu baada ya mwanamitindo Hamisa Mobeto kupata mtoto wa kiume, muigizaji Esha Buheti naye alibahatika kupata mtoto
wa kike ambaye alimpa jina la Claribell. Kama ilivyo kwa Hamisa, kwa Esha pia huyo naye ni mtoto wake wa pili. Mtoto wa kwanza anaitwa Clarisa.
MAMA LIL JUNIOR (FAIZA ALLY);
Muigizaji Faiza Ally naye yumo kwenye orodha hii. Mwaka 2017, kwake umekuwa na mafanikio mengi ikiwemo kupata mtoto wa kiume ambaye amemuita Lil Junior. Naye ni mtoto wake wa pili baada ya Sasha aliyezaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Wengine waliopata watoto kwa mwaka 2017 ni pamoja na staa wa Bongo Fleva, Estarlina Sanga ‘Linah’ Khadija Nito na muigizaji Welu Sengo.

Shilole afunguka kuhusu ndoa yake



STAA wa miondoko ya mduara, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amefunguka kuwa, watu wasimfikirie ameamua kuingia kwenye ndoa kama maonyesho bali amedhamiria kwenda kuwa mke anayestahili kuwa mfano wa kuigwa.
Mrembo huyo anayesumbua na wimbo wa Hatutoi Kiki, alisema kuwa anajua wazi watu wengi wanamuhesabia siku za uhusiano wao kuvunjika kama ilivyo kwa mastaa wengine, lakini kwa jinsi alivyodhamiria kutulia kwenye ndoa atawashangaza walimwengu.
“Najua wazi watu watakuwa wananihesabia siku ndani ya ndoa yangu lakini ukweli ni kwamba nitawashangaza watu wengi na sina sababu ya kuacha kuwa mke bora na mwenye heshima kwa
mume,” alisema

Ben Pol awataka wasanii Wa bongo kuacha uvivu



Msanii wa kiume wa bongo fleva Ben Pol, amewataka wasanii wenzake kuacha uvivu na kufanya kazi kwa bidii, kwani licha ya sanaa kuwahitaji, pia wana majukumu ya kutimiza.
Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Ben Pol amesema wao kama wasanii wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii, kwani kuna watu wanawategemea, ikiwemo familia zao na mashabiki wao.
“Niwaambie wasanii wenzangu tuache uvivu hii ni kazi yetu, familia zinatutegemea, tuna-teams ambazo zinaishi kupitia sisi, tuna mashabiki wanatuangalia, turudi studio turudi studio tutoe albam, kama kuna changamoto tutakabiliana nazo mbele kwa mbele”, amesema Ben Pol.
Ben Pol hakuishia hapo aliendelea kwa kuitaka serikali kuhakikisha wanasimamia ipasavyo kazi zao za sanaa, kwani na wao tayari wameshaanza kuchangia pato la serikali kwa kukatwa kodi.
“Tushaanza kulipwa kodi, kwenye shows tunakatwa, mtu anakuja pale mlangoni na mashine, kwa hiyo na wao serikali watusaidie kwenye biashara yetu”, amesema Ben Pol.
Ifahamike kwamba Ben Pol ni miongoni mwa wasanii wachache ambao mwaka huu wameachia albam, kitendo ambacho wasanii wengi wanakiogopa.

Wednesday, 20 December 2017

Diwani CHADEMA Ajiuzulu na Kujiunga CCM



KILIMANJARO: Diwani wa Donyomurwak kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Siha mkoani Kilimanjaro, Lwite Ndossi amejiuzulu nafasi yake na kujivua uanachama wake katika chama hicho na kijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amethibitisha hilo na kusema kuwa wamempokea diwani huyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kupoteza baadhi ya viongozi wake katika ngazi mbalimbali ambao wamekuwa wakijiuzulu nafasi zao na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kile wanachosema wanaunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuli na Serikali yake.

Kamati Ya Ushauri Wa Mazingira Yazindiliwa



Serikali imezindua kamati ya Taifa ya ushauri wa mazingira ambayo itakuwa ikijihusisha na uchunguzi wa masuala yanayohusu kulinda mazingira na kupendekeza hatua za kuchukua.
Akizungumza jana katika uzinduzi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba alisema kamati hiyo inayoundwa na wataalamu kutoka sekta mbalimbali ina mchango wa kutatua changamoto za mazingira bila kuwa na misigano. “Yote hayo ni kumjengea uwezo waziri mwenye dhamana ya mazingira ili katika kutekeleza majukumu yake awe na imput za kitaalamu,” alisema.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Joseph Malongo alisema kamati hiyo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria na kwamba wananchi wanapaswa kujua na kuzingatia umuhimu wa mazingira katika kila jambo.