Wednesday, 20 December 2017

Diwani CHADEMA Ajiuzulu na Kujiunga CCM



KILIMANJARO: Diwani wa Donyomurwak kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Siha mkoani Kilimanjaro, Lwite Ndossi amejiuzulu nafasi yake na kujivua uanachama wake katika chama hicho na kijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amethibitisha hilo na kusema kuwa wamempokea diwani huyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kupoteza baadhi ya viongozi wake katika ngazi mbalimbali ambao wamekuwa wakijiuzulu nafasi zao na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kile wanachosema wanaunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuli na Serikali yake.

Kamati Ya Ushauri Wa Mazingira Yazindiliwa



Serikali imezindua kamati ya Taifa ya ushauri wa mazingira ambayo itakuwa ikijihusisha na uchunguzi wa masuala yanayohusu kulinda mazingira na kupendekeza hatua za kuchukua.
Akizungumza jana katika uzinduzi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba alisema kamati hiyo inayoundwa na wataalamu kutoka sekta mbalimbali ina mchango wa kutatua changamoto za mazingira bila kuwa na misigano. “Yote hayo ni kumjengea uwezo waziri mwenye dhamana ya mazingira ili katika kutekeleza majukumu yake awe na imput za kitaalamu,” alisema.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Joseph Malongo alisema kamati hiyo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria na kwamba wananchi wanapaswa kujua na kuzingatia umuhimu wa mazingira katika kila jambo.

Vyama Vya Upinzani Vyamkosoa Mzee Makamba



Baadhi ya vyama vya upinzani vimekosoa kauli iliyotolewa juzi na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba vikisema imelenga kudhoofisha upinzani nchini.
Juzi, akihutubia Mkutano wa Mkuu wa CCM, Makamba alisema Rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa ‘anabatiza’ kwa maji, lakini Rais John Magufuli anafanya hivyo kwa moto na mfano mzuri ni uchaguzi wa marudio wa kata 43 ambao CCM ilizoa viti 42.
“Huu si ubatizo wa moto? Kazi tunayoifanya leo ni kuchagua kocha ambaye ni wewe (Rais Magufuli), kocha msaidizi Mangula (Philip) na Dk Shein (Ali Mohamed). Kama haitoshi unatakiwa uchague dawati la ufundi Kamati Kuu, sasa wenzangu wajue nimlisikia rafiki mmoja alikwenda kwa jimbo la Mnyika (John) na kusema 2020 njia nyeupe,” alisema mwanasiasa huyo.
“Njia nyeupe kwa utaratibu huu, kwa matokeo haya na ubatizo huu wa moto 2020 mshindi ni CCM we’ lala. Naomba mniruhusu niwaambie kina Mrema (Lyatonga), ubatizo ni uleule na leo sitaki kutabiri.Natabiri 2020 mheshimiwa Lowassa (Edward), Mbowe (Freeman) na Mapesa (John Cheyo ), John Shibuda wajue njia si nyepesi.”
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema hakutarajia kama Makamba angetoa kauli hiyo kutokana na alichodai kuwa ni kuminywa kwa demokrasia nchini.
Alisema kinachofanyika sasa dhidi ya wapinzani ni sawa na refa anayechezesha mpira wa miguu kuwapa kadi nyekundu wachezaji wote wa timu husika, halafu timu nyingine inaendelea kucheza.
Naibu Katibu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema kauli hiyo haileti picha nzuri kwa siasa.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alisema Makamba yupo sahihi na upinzani unabidi kufanya kazi ya ziada kama wanataka kushinda 2020.
“Tulikosea na tulichelewa kuunda upinzani, mwaka 1995 tulikuwa na nafasi nzuri sana ya kuungana kwa sababu hakukuwa na rais kama Magufuli, lakini sasa hivi yupo na sisi wapinzani tusipobadilika na siasa zetu za kususa watatuchapa kweli 2020,” alisema Mrema.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen-Kijo Bisimba alisema Makamba alisema ukweli kutokana na hali na mazingira ya siasa nchini.

Wanaochakachua Pesa Za Tasaf waonywa



KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Tabora, Natalis Linuma, ameiomba serikali kusaidia vijiji ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika mkoa na vijiji.
Aliyasema hayo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tasaf III kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika.
Linuma alisema vijiji vingi ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini, watu wake wana hali duni na baadhi wameachwa na watoto yatima.
Aidha, alisema kutokana na kaya hizo kutoingizwa katika mpango huo, kumesababisha malalamiko.Linuma alimwambia Waziri Mkuchika kuwa kaya 953ziliondolewa wakati wa uhakiki wa kubaini kaya zisizokuwa nasifa.
Alisema, Mkoa wa Tabora una jumla ya wilaya saba na tarafa 19, kata 174 na vijiji 696, mitaa148 ambayo mpango huo unatekeleza uhawilishaji katika kaya zenye sifa.
Lengo lilikuwa ni utambuzi na uandikishwaji wa kaya 52,558 na kaya 47,805 ziliandikishwa, kuanzia mwezi Agosti 2017.
Aidha, jumla ya Sh. 20,038,121.000 zilihawilishwa kwa walengwa 39,293.
Katika halmashauri zote za mkoa wa Tabora, mpango wa kunusuru kaya maskini umesaidia kuwapatia elimu watoto wenye wazazi wasio na uwezo.
Waziri Mkuchika alisema amepokea taarifa hiyo, lakini alipata fununu kuwa kuna baadhi ya viongozi wasio waaminifu.
Mkuchika alisema kuwa taarifa alizozipata ni baadhi ya viongozi kuomba rushwa na kuwaonya wakiendelea na tabia hiyo watakiona cha mtemakuni.

Hamisa Mobeto Anasa kwenye mtego Wa Zari



Mwanamitindo Hamisa Mobeto.
Mwanamitindo Hamisa Mobeto anadaiwa kunasa mtegoni baada ya ‘kuuvaa mkenge’ ulioratibiwa na hasimu wake wa siku za hivi karibuni, Zarinah Hassan ‘Zari’.
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alimtumia mtu aitwaye William Bugeme ambaye pia ana ukaribu naye wa damu, ili aweze kumchukua mwanamitindo huyo, ambaye amezaa na baba wa watoto wake wawili.
Inadaiwa lengo la Zari ni kuona wawili hao wakiwa karibu, basi ni dhahiri kuwa ukaribu kati ya Hamisa na baba watoto wake utaisha, kwani uhusiano wa kimapenzi na William hauwezi kukubalika.
“Mnajua kuwa huyo Hamisa amenasa kwa Bugeme lakini hajui kuwa huo ni mpango wa Zari ili amtoe kwa baba mtoto wake, asipoangalia atatumika tu kisha atabwagwa kwani jamaa yupo kimaslahi zaidi kwa ajili ya kuokoa penzi la dada yake,” alisema Sosi huyo.
Kwa mujibu wa sosi huyo, picha za wawili hao wakiwa katika pozi tofauti zilinaswa hivi karibuni zikiwa zimerushwa mtandaoni.
Zarinah Hassan ‘Zari’
Sosi huyo alikwenda mbali zaidi na kuvujisha siri ya Zari kuwa ndiye anayemtuma ndugu yake huyo ili akifanikisha kuwa naye kimapenzi itakuwa rahisi kuachana na baba wa watoto wake.
Hata hivyo sosi huyo alidai fungu kubwa na zuri limeandaliwa kuhakikisha Hamisa hakwepi mtego huo.
“Mwanamke ni mjanja sana sana haongei ni pesa ndio inaongea, Bugeme toka zamani anafahamiana na Hamisa sasa ameamua kumtumia huyo huyo ili kuumaliza mchezo wake kabisa, unadhani mzazi mwenzake akiona ameingia kwenye penzi na Bugeme ataendelea naye, amecheza kwelikweli,” kilitiririka chanzo.
Risasi Jumatano lilimtafuta hewani Hamisa ili azungumzie sakata hilo kama ameshalifahamu au anajipanga vipi, lakini pia kuzungumzia picha zake zinazomuonesha akiwa na kaka huyo, lakini alipopokea simu yake alisikiliza madai yote kisha akakata simu.

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download



DOWNLOAD

Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download


Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download






Dalili Tano za Tezi Dume



Ugonjwa wa tezi tume imeelezwa ya kwamba ni miongoni mwa magonjwa ambayo yanasumbua jamii yetu kwa kiwango kikubwa sana na hata kupelekea kusababisha vifo.
Hata hivyo tafiti mbalimbali zinazidi kuonesha ya kwamba wanaume ambao wanatumia pombe kali kwa kiwango kikubwa wapo hatarini kupata ugonjwa huo. Licha ya wanywaji wa pombe kali lakini inasadikika ya kwamba wanaume ambao wanafanya kazi za viwandani, husasani viwanda vya rangi au wanaofanya kazi ya kupaka rangi wapo hatarini kupata ugonjwa huo.
Lakini pia wanaume ambao wapo hatarini kupata ugonjwa huo ni pamoja na wanaume wenye historia ya tatizo hili wenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zake (kaka au mdogo wa kiume) au baba kama amewahi ugua ugonjwa huu.
Lakini pia watalamu mbalimbali wa masuala ya afya, wanazidi kueleza ya kwamba wanaume wenye umri wa kati ya miaka 40-70 wapo hatarini kupata ugonjwa huu wa tezi dumi.
Lakini licha ya kuendelea kusambaa kwa kasi kwa ugonjwa huu watalamu wa afya wanaeleza ya kwamba endapo ugonjwa huu wa tezi tume utaweza kutambulika mapema unaweza kutibika.
Dalili za ugonjwa wa saratani dume.
Katika hatua zake za awali, dalili za saratani ya tezi dum hazitofautiani na zile za kuvimba kwa tezi dume (BPH). Dalili hizo ni pamoja na
1. Kukojoa mkojo uliochnanganyika na damu.
2. Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku.
3. Kukojoa mkojo wenye mtiririko mchafu.
4. Kutirirka kwa mkojo baada ya kumaliza kukojoa.
5. Kupata maamuvu wakati unapoanza kukojoa.

Faida zingine za Maji Mwilini



Moja kati ya kauli mbiu ambayo ipo katika matumizi ya maji wanasema ya kwamba, maji ni uhai. Huo ni ukweli usiopingika juu ya kauli hiyo ijapokua watu wengi huwa hawatumii maji hayo.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwa watu hao Makala haya yatakufaa kwani utakwenda kujua ukweli kuhusu faida za maji mwilini.
Faida za maji mwilini ni kama ifuatavyo;
1. Unywaji wa maji husaidia kuifanya ngozi yako kuwa nyororo na nadhifu.
2. Maji husaidia kwa kiwango kikubwa katika mfumo wa kuchanganya chakula katika mwili wa mwanadamu. Lakini pia maji husaidia kupunguza uwezekano wa kuapata saratani ya colonikwa asilimia 45.
3. Maji husaidia kupunguza calories mwilini, yaani badala ya kunywa vimininika vingine kama vile soda, juisi na bia ambavyo vina calories, hivyo unashauriwa utumie maji kwani yenyewe hayana calories. Lakini pia unashauriwa ya kwamba kila wakati uendelee kutumia maji kwani yenyewe hayana mafuta, sukari ambavyo husababisha athari mbaya katika mwili wa binadamu.
4. Kwa wale ambao hushambuliwa na maumivu ya kichwa, tunaambiwa ya kwamba maji husaidia kutibu maamivu ya kichwa, kwani inasdikia ya kwamba upungufu wa maji mwilini husababisha kichwa kuuma, hivyo kila wakati ni vyema ukatumia maji ili ujitibu.
5. Utumiaji wa maji kwa kiwango kikubwa kila wakati humsaidia mtu kuweza kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo, hivyo unashauriwa kwa siku tunywe zaidi walau bilau nane kwa siku

Tuesday, 19 December 2017

Mwenyekiti Sau Kuzikwa Disember 22



Mwenyekiti wa Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Dk Paul Kyara aliyefariki dunia jana anatarajiwa kuzikwa Desemba 22,2017 kijijini Legho, Kilema mkoani Kilimanjaro.
Dk Kyara alifariki dunia jana asubuhi Jumatatu Desemba 18,2017 akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam.
Katibu wa chama hicho, Johnson Mwangosi amesema Desemba 21,2017 saa tano asubuhi wanatarajia kuwa na ibada na kuaga mwili wa marehemu nyumbani kwake Madale.
Mwangosi amesema baada ya shughuli hiyo mwili wa Kyara utasafirishwa kwenda kijijini Legho.
Majaliwa, mtoto wa marehemu Kyara amesema baba yake alikuwa akisumbuliwa na figo tangu mwaka 2012.
Amesema Ijumaa Desemba 15,2017 alipata tatizo la shinikizo la damu na sukari ilipanda.
Majaliwa amesema alipelekwa hospitali alikopatiwa matibabu na aliruhusiwa kurejea nyumbani.
Amesema Jumamosi Desemba 16,2017 alizidiwa na saa tatu usiku walimpeleka katika Hospitali ya Regency kwa matibabu.
Amesema madaktari walijitahidi kuokoa maisha yake lakini shinikizo la damu na kisukari hakikushuka hivyo kusababisha kifo chake.
“Nitamkumbuka baba, wakati amelazwa neno alilokuwa akisisitiza ni upendo na umoja," amesema Majaliwa.

Airtel yaja na ofa kabambe msimu huu Wa sikukuu



Kampuni ya Simu za Mkononi nchini Airtel imezidi kuonesha ukomavu wake katika kuwaletea wateja wake huduma bomba baada ya sasa kuja na kifurushi cha Smatika ambacho kinaanzia Sh 2,00 hadi Laki moja.
Vifurushi hivyo vimekuja mahususi kwa lengo la kukata kiu ya bando la intaneti kwa watumiaji wa Airtel huku wakiboresha vifurushi hivyo katika msimu huu wa Sikukuu ambapo kifurushi cha MB 50 kwa Sh 250 sasa kitakujia kwa Sh 2,00 ili kwenda sawa na vocha za 2,00 zilizopo lakini kikikupatia bando la MB 40 kwa siku.
Airtel pia imekuja na bando jipya kabisa la Sh 2,000 ambalo litakua na kifurushi chenye ujazo wa GB 3 kwa siku tatu kulinganisha na awali ambapo Sh 2,000 mteja alikuwa akipata kifurushi cha GB 1.3 kwa siku.
Akizungumzia lawama ambazo zimekuwa zikitolewa na wateja wa mtandao huo kuhusu kupunguzwa kwa vifurushi vya mtandao huo, Meneja Masoko Airtel, Aneth Muga alisema wateja wengi wamekuwa wakilalamika kuhusu kuondolewa kwa vifurushi vya UNI lakini wamesahau kuwa vifurushi hivyo vilikuwa maalumu kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo.
“ Ndugu zangu wanahabari Airtel imeendelea kukata kiu ya watumiaji wa mtandao wetu, watu wengi wanalalamika kuwa tumepunguza vifurushi vyetu bila kuangalia kwa undani, mathalani kifurushi cha 250 kilikuwa kikimpatia mteja MB 50 lakini sasa tunatoa MB 40 kwa Sh 200.
“ Ukiangalia hapo huoni utofauti wowote lakini pia kuwa na kifurushi cha Sh 200 kunampa unafuu mteja ambaye ananunua vocha za Sh 200,” alisema Aneth.

Rais Magufuli amwaga Neema Ruvuma



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia wizara ya Nishati, ametoa kiasi cha shilingi bilioni 210 kwaajili ya ujenzi wa mradi mkubwa wa Umeme unaojengwa mkoani Ruvuma.
Akiongea katika ziara yake ya siku tatu mkoani Ruvuma Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amesema Rais Magufuli ametoa fedha hizo kwa kushirikiana na wahisani wengine.
“Mheshimiwa Rais ndio ametoa fedha hizi bilioni 210 kwa kushirikiana na wahisani ambapo bilioni 104 ni kwaajili ya kusambaza umeme katika wilaya zote za mikoa ya Ruvuma na Songea”, amesema Waziri Kalemani.
Mradi huo wa umeme unatarajiwa kuwafikia wananchi zaidi ya 32,000 katika vijiji 120 vya mikoa hiyo. Waziri ameongeza kuwa mradi huo utawawezesha wananchi kuingiza fedha nyingi kutokana na fursa zitakazojitokeza baada ya kukamilika.
Kalemani amewataka Wakandarasi kumaliza kwa wakati mradi huo kwani tayari wameshapewa fedha zao bila kucheleweshewa. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2018.

Mtulia Kurudi tena Kinondoni



Aliyekuwa Mbunge Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia ambaye amehamia CCM ametangaza nia ya kugombea tena ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Desemba 2 Mtulia amejiuzulu nafasi ya ubunge, huku akisema amefikia uamuzi huo bila kushawishiwa mtu yeyote na amebaini Serikali ya CCM inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo upinzani iliahidi kuyatekeleza.
Baada ya hatua hiyo, chama cha CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba ametangaza kuwaomba radhi wapiga kura wa Kinondoni kwa Mtulia kujiuzulu uanachama kisha ubunge.
Lakini leo Jumanne Desemba 19, 2017 kupitia andiko lake alilolituma kwa vyombo vya habari, Mtulia amesema atachukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa ndani ya CCM ili agombee tena nafasi hiyo.
“Chama changu kikiridhia nitakwenda mbele ya Wanakinondoni kuomba ridhaa ya kuwatumikia katika nafasi ya ubunge kupitia CCM. Pia nawapa pole sana kwa maumivu mliyoyapata kutokana na uamuzi wangu wa kujiuzulu ubunge wa Kinondoni,” amesema Mtulia.
Hata hivyo, Mtulia amewahakikishia wakazi wa Kinondoni kuwa bado anawapenda na yupo tayari kutumikia tena kwa lengo la kuleta maendeleo ya jimbo hilo ambalo awali lilikuwa likishirikiliwa na CCM kwa kipindi cha muda mrefu.