Monday, 18 December 2017

Pori la Grumenti lafanikiwa kudhibiti majangili



Kaimu Mkuu wa pori la Akiba la Ikorongo Grumeti lililopo katika wilaya za Bunda na Serengeti Erdwin Njimbi amesema wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti tishio la ujangili wa kutumia silaha za moto za jadi na mitego ya kienyeji ya kutumia nyanya ngumu kwa wanyama wadogo na wakubwa kama tembo na faru baada ya kuanzisha kitengo cha iinterejensia na kutumia mbwa wenye uwezo wa kugundua walipo wahalifu hata kama tukio limefanyika kwa siku kadhaa zilizopita na kwamba kufanikiwa kukamata zaidi ya majangili mia moja na sitini katika kipindi cha mwaka 2016/17.
Kaimu mkuu huyo wa pori la akiba la Ikorongo Grumeti amesema palikuwa na tishio kubwa la ujangili hasa wa kutumia mitego ya nyaya ambazo unasa wanyama wa aina zote bila kuchagua lakini baada ya serikali kuanza kutumia mbinu hizo ujangili umepungua kwa kiasa kikubwa na kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama wakiwemo simba pamoja na tembo.
Afisa kutoka Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori TAWA makao makuu Seleman Kirario anasema kuimarika kwa ulinzi kwenye maeneo hayo pia kunachangiwa na uelewa wa wananchi baada ya kuona manufaa yanayo patikana kutokana na uhifadhi pamoja na uanzishwaji wa jumuiya za hifadhi za jamii kwenye maeneo hayo.
Mkuu wa ya Serengeti Nurdin Babu anasema baada ya mafaniko katika uhifadhi halmashauri ya Serengeti imeanza kunufaika ambapo inapata zaidi shilingi milioni miambili tofauti na awali na wawekezaji nao wakataja miradi waliianzisha kwa manufaa ya wananc

Utalii Mpya Wapatikana Ngarongoro



Simba wanaopanda juu ya miti wamekuwa kivutio cha watalii katika eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwa kuwa ni kitu kipya.
Tabia ya simba imeanza kushangaza watalii na maofisa wanyamapori kwa kuwa si kawaida ya wanyama hao kupanda juu ya miti na kukaa.
Ofisa wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (Tawa), Suleiman Keraryo amesema simba wanaopanda miti walizoeleka katika Hifadhi ya Manyara pekee sasa inaonekana inasambaa hivyo kuhitajika utafiti zaidi.
"Hili si jambo la kawaida linaweza kusababishwa na vitu vingi lakini ni geni na kivutio kizuri kwa watalii," amesema leo Jumapili Desemba 17,2017.
Ofisa wanyamapori mkuu na ushirikishwaji jamii kwenye uhifadhi wa Tawa, Seth Ayo amesema hali hiyo si ya kawaida.
Hata hivyo, amesema jambo hilo linaweza kuwa linasababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa na ongezeko la joto ardhini.
"Hili ni jambo jipya na linasambaa tumeona simba juu ya miti Grumeti na leo hapa Ngorongoro," amesema.
Idadi kubwa ya watalii walikuwa wakitazama simba katika eneo la Kingo creta ya Ngorongoro ambaye alikuwa amepumzika juu ya mti.

Rayvanny aeleza lini kolabo ya Derulo itatoka



Msanii wa muziki Bongo, Rayvanny amefunguka kinachokwamisha kolabo yake na mkali wa R&B kutoka ardhi ya Trump.
Muimbaji huyo wa WCB ambaye June 26 mwaka huu alionekana studio na Jason Derulo amesema kuwa kazi hiyo ilishafanyika ila anasubiri Derulo aimalizie mixing kisha amtumie.
“Nilifanya ngoma kwenye studio yake lakini ratiba yake inakuwa imebana sana anakuwa anazunguka kwenye miji mingi tofauti, so akaniambia siwezi nikakutumia kitu ambacho hakijakaa proper subiri mpaka tuimix vizuri” amesema Rayvanny.
Hata hivyo Rayvanny ameeleza kuwa katika safari yake ya sasa ya Marekani ambapo ameenda kwa ajili ya ku-shoot video atafuatilia na hilo pia.

Hatua 10 za kuchukua wakati wakutafuta mchumba



Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.
Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.
Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.
Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.
Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.
Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.
Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Suzzy aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.
Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.
Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.
Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.
Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.
KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.
Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.
PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.
TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.
NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, dini, viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.
Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.
TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.
Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.
Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.
SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.
Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.
SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana
NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.
TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.
KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.
Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.

Mambo yanayoweza kukuvunjia heshima



HAKUNA kitu kibaya maishani kama kuonekana upo katika daraja la chini na mtu wa kudharaulika kwenye jamii unayoishi. Kisaikolojia kuna madhara makubwa.
Ni imani yangu kuwa kila mwanadamu timamu anapenda kuheshimiwa lakini wengi wetu tunashindwa kupata heshima tunayoitaka kwa sababu hatufahamu jinsi ya kuishi mbele ya wenzetu.
Kitaalamu, hakuna jambo ambalo hutokea maishani bila sababu maalumu hivyo hata kudharauliwa kwako au kwetu ndani ya jamii tunayoishi kunatokana na jinsi tunavyoenenda.
Mwalimu wangu wa somo la maisha na saikolojia, Eric Shigongo, aliwahi kuniambia ‘Nothing happens in the sky, but the elements should be there,’ akimaanisha kuwa hakuna kitokeacho angani pasipo kuwa na dalili au sababu zake.
Naomba nianze kutoa njia za kukusaidia kurejesha heshima yako kwa kuperuzi na wewe baadhi ya dokezo muhimu zinazoweza kukusaidia kujitambua na kuweza kuyaepuka maisha ya kudharauliwa.
MUONEKANO
Kwanza kabisa ni jinsi unavyoonekana. Muonekano ninaouzungumzia hapa ni usafi wa mavazi na mwili kwa ujumla. Hata siku moja hakuna mchafu anayeheshimika katika jamii anayoishi hata kama ana kipaji kikubwa kiasi gani.
Kwa hiyo uchafu wa mavazi na mwili huchangia mtu kudharauliwa katika jamii anayoishi. Linaweza kuwa jambo dogo sana lakini ni moja kati ya sababu kubwa inayochangia kuporomoka kwa thamani yako mbele ya wenzako.
Mazungumzo
Hapa naomba nieleweke kuwa unachokizungumza kinaweza kukujengea heshima au kukubomolea heshima. Kauli zisizo na busara zitakufanya udharaulike kwa kila mtu. Uropokaji usiokuwa na mantiki huchangia kuporomosha heshima yako hasa kama utakuwa muongeaji zaidi. Biblia inasema penye wingi wa maneno hapakosi uovu.
UTENDAKAZI WAKO
Ndugu zangu, siku zote heshima ya mtu ni kazi. Watu wengi hawapendi kufanya kazi kwa bidii huku wengine wakijiendekeza kwa tabia ya kuombaomba, jambo hilo halifai kwa vile huchangia kubomoa heshima yako mbele ya jamii. Fanya kazi usiishi bila kujishughulisha.
KUTOTIMIZA AHADI
Kama una tabia za kuahidi mambo halafu unashindwa kuyatekeleza, basi unajiweka katika nafasi mbaya ya kutunza heshima yako katika jamii unayoishi. Bora ukwepe kutoa ahadi kuliko kuahidi na kutotimiza.
SIFA ZISIZO NA MAANA
Nakumbuka msemo mmoja kutoka kwa mwandishi mwandamizi aliyekuwa mtaalamu wa falsafa za maisha, marehemu Adolf Balingilaki, ambao unasema kwamba:
“Ukitafuta heshima kwa gharama ya juu, basi utalipwa dharau kwa bei nafuu.”
Msemo huu unamaanisha nini? Siku zote ukiwa unafanya mambo yako kwa ajili ya kusifiwa au mazungumzo yako kuwa ya kujiinua, watu watakudharau.
KUTOKUWA MWAMINIFU
Suala la uaminifu ni pana, kuna uaminifu wa fedha, siri, dhamana na mambo kama hayo, hivyo ni vema kila unachoaminiwa lazima ukitunze kwani ukiwa mtu wa kuvunja uaminifu fahamu kuwa utashusha heshima yako.

Hatua 5 Za Kuzungumza na mpenzi wako aliekasirika



Kwenye mapenzi kuna nyakati za kutofautiana, kukasirishana. Katika hali ya kawada kipindi hiki huwa ni za hatari kwa sababu husababisha nyufa kubwa za uhusiano na kulifanya penzi kukosa ladha.
Sote tunajua, watu hupigana, huachana, hujeruhiana, hutukanana, hudhalilishana wakiwa na hasira. Hata hivyo si wote wanaojua wafanye nini wanapojikuta wameingia kwenye hatua hiyo mbaya.
Msomaji wangu, hebu jaribu kukumbuka ugomvi mmoja uliotokea kati yako na mpenzi wako na ikiwezekana jikumbushe mlivyoanza! Utabaini kuwa mlianza kama utani na mkajikuta mmefura kwa hasira, mkatwangana makonde, mkatamkiana maneno makali ya kuudhi na pengine mkaamua kuachana.
Yote hii ni kwa sababu mlikosa elimu ya mazungumzo. Ingekuwa mmoja wenu hasa yule aliyekuwa wa pili kukasirika anafahamu hatua za kuzungumza na mtu aliyekasirika angechukua jukumu la kutuliza machafuko na kuleta amani kwenye mapenzi. Tazama hatua tano za kuzungumza na mpenzi aliyekasirika.
MPUNGUZE MHEMKO
Hasira hujaza kifua, huathiri mzunguko wa damu na ufahamu. Mtu aliyekasirika huwa vigumu kwake kusikiliza au kutazama mambo kwa jicho la tatu. Mwenye hasira huwa hafikirii matokea yajayo badala yake hutazama zaidi tukio na jinsi ya kupata ushindi iwe kwa maneno au kwa mapambano.
Katika hali ya namna hiyo, mtu mwingine akija na busara za kutaka kumgeuza haraka haraka hawezi kumuelewa. Muhimu hapo ni kuacha kumwadama, kujibizana naye, kumshawishi asikilize badala yake mpe nafasi ya kusema atakavyo, abwate ajuavyo huku wewe ukimuitikia na kumkubalia lawama zake. “Basi mpenzi mwenye makosa ni mimi.” Kauli za aina hii zitampunguza hasira kwani atajiona msindi.
MSOME SAIKOLOJIA YAKE
Kwa kuwa unamfahamu mpenzi wako kwa kina itakuwa rahisi kwako kumtambua kuwa amepunguza hasira na kurudi katika hali yake ya kawaida. Ukisha fahamu hilo chukua jukumu la kumsoma kisaikojia ili kujua kama yuko kwenye hali nzuri ya kusikiliza yale uliyotaka kumwambia wakati alipokuwa na hasira.
Zoezi hili linaweza kuchukua saa kadhaa na wakati mwingine hata siku mbili. Lengo ni nini? Ni kupata matokeo sahihi ya kuondoa chuki za mwenza wako na kumfundisha madhara ya kukasirika kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi. “J, nakupenda sana, lakini juzi uliniumiza, uliniambia mimi malaya kwa kosa ambalo sikufanya?” Bila shaka muda huo atakusikiliza zaidi kuliko ungebishana naye alipokuwa na hasira.
MRUHUSU AKUJIBU
Pamoja na kumsoma kisaikojia na kumwambia kinagaubaga makosa yake, usimzuie kujitetea, mpe nafasi ya kuzungumzia kilichomkasirisha. “Unaona bado unanitukana, sasa naamini siku ile ulikuwa umedhamilia.” Usisiseme hivyo, mwache ajibu hoja hata kama atakuwa anakukandamiza na kuzidi kujijengea ushindi. Mvumilie aoshe ubongo wake.
EPUKA MARUMBANO
Kama nilivyosema kwenye hapo juu, wapenzi wengine huwa wagumu kuelewa, ni watu wa kuficha udhaifu wao na kutopenda kuonekana wamekosea. Watu wa namna hii unapowarejeshea mazungumzo wanaweza kujikuta wanahamaki tena.
“Kwa hiyo ulikuwa unasemaje…nilifanya ndiyo,… wewe unaamuaje?” Mkifika kwenye alama hiyo usikubali kurumabana naye mwache aseme halafu wewe ingia kwenye hatua ya tano.
MUOMBE MSAMAHA
Hata kama atakuwa yeye ndiye mwenye makosa na amekataa kukiri, usijali, chukua jukumu la kumuomba msamaha na kueleza tena nia yako ya kumazungumzo ilikuwa ni kuelewana si kugombana. Kumbuka hata kama amekiri kosa, bado unatakiwa kumuomba radhi kwa kurejea yaliyopita. “Mpenzi inawezekana nikawa nimekuudhi kwa niliyosema, nakuomba sana tusameheane.”
Bila shaka kwa haya machache msomaji wangu utakuwa umejifunza na kuchukua hatua za kuzuia migogoro mikubwa inayotokana na hasira za mpenzi wako. Leo niishie hapa, nikushukuu kwa kunisoma. Kaa mkao wa kura, kile kitabu bora cha mapenzi nchini TITANIC, TOLEO LA NNE, kitakuwa mtaani hivi karibuni. Usikose nakala yako.

Aina 10 za wanawake wanaopendwa na wanaume


WENYE MSIMAMO
Wanawake daraja la kwanza wanaopendwa zaidi na wanaume ni wale wenye msimamo, uelewa mkubwa wa mambo na maamuzi sahihi, wako makini kwenye matendo yao na siku zote hufanya vitu kwa ajili ya kupata mafanikio.
WAPENDA USAWA
Aina ya pili inayohitajika katika katika ulimwengu wa kimapenzi ni wanawake wanaoheshimu usawa wa jinsia, walio tayari kubeba majukumu ya kifamilia kwa ulinganifu sawa na wanaume, wenye uwezo wa kuongoza jamii kwa asilimia 50 kwa 50.
WANAOJUA MAPENZI
Wanawake wajuzi wa mambo ya faragha wanapendwa sana. Sifa yao kubwa ni uwezo wa kutosheleza katika tendo la ndoa. Tafiti zinaonyesha kuwa wanaume hupenda sana wanawake watundu katika mchezo wa sita kwa sita. Mara nyingi wanatajwa kuwa na uwezo wa kuteka akili za wanaume bila kujali sifa zao za nje au za ndani.
MARAFIKI
Wanawake wenye sifa sawa na rafiki ni aina ya nne inayowavutia wanaume. Wao hutegemea zaidi nguvu ya kushawishi inayotokana na namna wanavyojali na kujitolea kuhakikisha wanakuwa marafiki wa kweli kwenye shida na raha kwa wapenzi wao. Si wakorofi, waungwana na wapenda amani.
WA WAZI
Aina nyingine ya wanawake inayowavutia wanaume ni wenye msimamo na uwazi. Si wepesi wa kuburuzwa katika maamuzi ya msingi kwa kisingizio cha wao ni wanawake. Utafiti unaonesha wanawake wa aina hii wamekuwa muhimu hasa kwa wanaume wenye tabia za ubabe na udhaifu katika uelewa wa mambo.
WANAOJITEGEMEA
Wanawake wanaojitegemea wana soko kubwa kwa wanaume tofauti na akina naomba vocha kila siku. Uchunguzi unaonyesha kuwa wanaume wa leo hawapendi wanawake tegemezi, wasiokuwa na kazi na wanaoendekeza starehe za upande mmoja.
WASIO NA PRESHA
Nikisema wanawake wasiokuwa na presha namaanisha wasiolazimisha vitu vitokee haraka haraka. Wao siku zote huacha mambo yatokee yenyewe na kazi yao kuwa ni kutenda sehemu ya majukumu yao kama wapenzi.
MARIDADI
Kundi lingine la wanawake wanaopendwa na wanaume ni wanaozingatia usafi na kujiremba. Wanaokwenda na wakati katika mavazi na mvuto wa nje. Lakini pia ni welewa wa mazingira, si wasamba. Wanapendeza kwa muonekano.
WANAORIDHIKA
Wanawake ambao hulidhika na hali walizonazo ni kivutio kikubwa kwa wanaume, hili ni kundi linalohitajika sana katika ulimwengu wa mapenzi kwa upande wa wanaume ambao maisha ya sasa yamekuwa yakiwageuza kutoka juu kwenda chini au chini juu. Kukubali hali zote bila kubadili tabia ni sifa njema ya mwanamke.
WA MMOJA
Wanawake wanaochagua mara moja na kutosheka na kuwa tayari kukwepa kila aina ya vishawishi toka kwa wanaume ambao kimtazamo wana vitu vya ziada zaidi ya waliowachagua mwanzo wanahitajika sana. “Niliye naye ananitosheleza kwa kila kitu sitaki mtu mwingine.” Kundi la wanawake wa aina hii ni adimu na muhimu sana.

Sunday, 17 December 2017

Kigogo anaswa na TAKUKURU

Kigogo anaswa na TAKUKURU

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU inamshikilia Rais mstaafu wa Chama Cha walimu Tanzania (CWT) Gracian Mkoba kwa tuhuma za rushwa.

Hilo limethibitishwa na Afisa Uhusiano wa TAKUKURU Makao Makuu, Mussa Misalaba, ambaye amesema wanamshikilia Mkoba kwa tuhuma za kugawa fedha kwa baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho ili kuwashawishi wamchague mgombea anayemtaka.

"Mukoba ameshastaafu, lakini kuna mgombea mmoja alikuwa anataka achaguliwe, tumemkamata leo asubuhi akigawa rushwa kuwashawishi wapiga kura kwenye ukumbi wa Chimwaga wamchague huyo mgombea wake," amesema Misalaba.

Misalaba ameongeza kuwa TAKUKURU inaendelea kufanya uchunguzi zaidi dhidi ya Mukoba kabla ya kumfikisha mahakamani.

Mukoba anakuwa mtu wa tatu kukamatwa na TAKUKURU kwa tuhuma za rushwa kwenye uchaguzi ndani ya wiki moja, wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Juma Khamis na mfanyabiashara Haider Gulamali.

Klopp Aeleza Alivyotaka Kuacha Kumsajili Salah Hadi Alipolazimishwa



Kocha Jurgen Klopp wa Liverpool amefunguka kwamba aliingia hofu kumsajili Mohamed Salah hadi alipigwa presha.

Klopp amesema kitengo cha kusaka wachezaji cha Liverpool kilimpa presha kutaka Salah asajiliwe jambo ambalo alikuwa hakubaliani halo kwa hofu ya jumbo dogo la Salah.

Kocha huyo Mjerumani amesema, aliamini kwa jumbo la Salah kulikuwa na hofu ya kufanya vizuri Ligi Kuu England.

Wakati huo, wachezaji wake watatu ambao ni Philippe Coutinho, Sadio Mane na Roberto Firmino, aliamini wangebadilika na kumbeba.

Baadaye alikubali na Liverpool iliilipa AS Roma kitita cha pauni million 34 hali ambayo pia ilizua mjadala.

Lakini tayari Salah ametupia mabao 19 katika michuano tote akiwa na Liverpool na sasa winga huyo anaonekana ni tegemeo.

Salah ambaye ni mchezaji bora wa Afrika kupitia BBC ndiye anayeongoza kwa upachikaji wa mabao katika Ligi Kuu England akiwa na mabao13.

Dk Mwakyembe Awapongeza Sportpesa Kudhamini Tusa, Ataka Wengine Wawaige



Waziri wa Michezo Dk Harrison Mwakyembe amewapongeza Sportpesa lianza kwa kushukuru SportPesa kwa kudhamini mashindano hayo ya Vyuo Vikuu (TUSA) yanayoendelea mjini Dodoma na kuomba kampuni mengi kuiga mfano wa kampuni hiyo.
Dk Mwakyembe amesema udhamini wa makampuni umekuwa msaada mkubwa katika kusaidia kuendeleza michezo katika nchi mbalimbali.
“Kuna wachezaji au makocha wengi wametokana na michezo ya vyuoni sote tunajua, sasa anayedhamini michezo vyuoni anajua faida yake kuwa ni ya baadaye lakini kubwa kwa taifa, hivyo niwapongeze hawa SportPesa kwa kazi nzuri,” alisema.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo Ofisa Uhusiano wa SportPesa Tanzania, Sabrina Msuya alisema yafuatayo:
"Sisi kama SportPesa, tukiwa wadau wa maendeleo ya michezo nchini, hatukuwa na kigugumizi tulipoombwa kuyadhamini mashindano haya ya vyuo vikuu kwa maana moja kubwa,
Hakuna asiyejua jinsi vipaji vingi vya michezo na Sanaa vinavyopatikana kutoka kwa wanafunzi wa sekondari wa nyuo vikuu, nah ii ni duniani kote.
Ni kwasababu hiyo, nchi kama Marekani inajivunia kuwa na ligi ya mpira wa kikapu ya NBA iliyosheheni nyota wakubwa kama vile Kevin Durant na Stephen Curry ambao wametoka vyuoni na kuingia kwenye ligi moja kwa moja.
Kupitia mfano huo, imefika kipindi tunatakiwa kujua kuwa wasomi wetu si tu kwamba wamejaliwa uwezo wa kupambana na madesa, lakini pia wana vipaji vikubwa katika sanaa na michezo na ndio maana sitashangaa kusikia mtu kama Didier Drogba ni mhasibu wa ngazi ya Chuo Kikuu bila kumsahau mzee Arsene Wenger mwenye degree ya uchumi.
Nimalize kwa kuwapongeza nyote mliopo hapa hususani wachezaji kwani tunajua mmeacha madesa vyuoni na mkirudi mtakuta assignment za kutosha bila kusahau test one ambazo ndio msimu wake huu.
Tunaamini sio tu kwamba mtakuja kulitumikia taifa kama wasomi wa taaluma mbalimbali, lakini pia katika tasnia ya michezo kwani hapa hamkuja kwasababu ya GPA zenu bali ni vipaji vyenu.

Uhakiki Matokeo Wazazi Yafyeka Matokeo



Dar es Salaam. Uongozi wa Jumuia ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) umesema umekamilisha kuhakiki matokeo ya kura zilizopigwa katika uchaguzi uliofanyika Desemba 13,2017.
Taarifa iliyotolewa jana Jumamosi Desemba 16,2017 na Idara ya Itikadi na Uenezi ya CCM imesema uhakiki umefanyika baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wajumbe wa jumuia hiyo walioshiriki uchaguzi.
Mwenyekiti wa Wazazi, Dk Edmund Mndolwa leo Desemba 16,2017 amesema matokeo yaliyotangazwa na kumpa ushindi Nuru Bainaga kwa nafasi ya Wazazi kwenda Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) yanatenguliwa.
Dk Mndolwa amemtangaza Zainab Sige kuwa mjumbe halali wa Wazazi kwenda UWT badala ya Nuru.
“Huu ni mwendelezo wa kuhakikisha kuwa haki inatendekea katika chaguzi za chama na jumuia zake,” imesema taarifa hiyo.
Dk Mndolwa Desemba 13, 2017 alitengua ushindi wa Ngingite Mohamed aliyechaguliwa kuwa mjumbe wa NEC kutokana na kasoro wakati wa uchaguzi.
Mwenyekiti huyo wa Wazazi, alimtangaza Kitwala Komanya kuwa mjumbe wa NEC kupitia Wazazi (Bara) kuchukua nafasi ya Mohamed.
Mwananchi:

Historia inaibeba Z'bar Fainali Challenge Cup



Leo Jumapili December 17, 2017 wadau wengi wa soka wanasubiri kuona Zanzibar Heroes watafanya nini nchini Kenya kwenye mchezo wa fainali ya CECAFA Senior Challenge Cup mwaka 2017 ambapo watacheza dhidi ya wenyeji Kenya.
Rekodi zinaonesha kwamba, Zanzibar wameshinda ubingwa wa Challenge mara moja tu, ilikuwa mwaka 1995 walipowafunga wenyeji wa michuano hiyo mwaka huo timu ya taifa ya Uganda kwa bao 1-0. Miaka 22 baadaye, Zanzibar wamefika hatua ya fainali jambo zuri na la kuvutia wanacheza dhidi ya mwenyeji wa mashindano (Kenya) Je watarudia walichofanya mwaka 1995 dhidi ya timu mwenyeji?
Historia inaendelea kutukumbusha kwamba, Zanzibar inatafuta ubingwa wake wa pili kwenye mashindano hayo wakati Kenya wakitaka kuweka rekodi ya kutwaa kombe hilo kwa mara ya saba. Mra ya kwanza Zanzibar kushinda taji hilo ilikuwa ni 1995 wakati Kenya wameshatwaa kombe hilo mara sita (nafasi ya pili nyuma ya Uganda ambao wameshinda ubingwa huo mara 14)
Makundi CECAFA 2017
Group A: Kenya (wenyeji), Rwanda (Guest), Libya, Tanzania bara, Zanzibar (mechi zilichezwa Machakos) Group B: Uganda, Burundi, Ethiopia, Sudan Kusini (mechi zilichezwa Kakamega)
Kumbuka timu ambazo zimefuzu kucheza fainali (Kenya vs Zanzibar) zote zimetoka Group A, ambapo Kenya waliongoza kundi wakifuatiwa na Zanzibar waliomaliza katika nafasi ya pili.
Road to final
Kenya
Kenya 2-0 Rwanda
Kenya 0-0 Libya
Kenya 0-0 Zanzibar
Kenya 1-0 Tanzani
Zanzibar
Zanzibar 3-2 Rwanda
Tanzania 1-2 Zanzibar
Kenya 0-0 Zanzibar
Libya 1-0 Zanzibar
Nusu Fainali
Kenya 1-0 Burundi
Uganda 1-2 Zanzibar
Failani
Kenya ?? Zanzibar
Kocha wa Zanzibar Heroes Hemes Suleiman ‘Morocco’ amesema, timu yake ipo tayari kwa mchezo wa fainali huku akiamini watapata matokeo bora.
“Karibu wachezaji wote wako vizuri isipokuwa mchezaji mmoja tu (Kassim) na tuliweza kucheza mechi ya nusu fainali bila yeye, tuko vizuri na tayari kwa ajili ya mchezo wa fainali dhidi ya Kenya.”
“Watu waendelee kutupa support kama ambavyo walifanya kwenye mechi nyingine na sisi tutajitahidi kuhakikisha tunapata matokeo bora.”

Rais Wa Zimbabwe Awaonya Wananchi wake



Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa ametaka wanachama wa Chama cha Zanu-PF kuachana na nyimbo za kumsifu na kuwataka watilie mkazo wimbo wa Taifa na nyingine zinazozungumzia ukombozi.
Mnangagwa amesema hayo katika mkutano wa chama hicho ambapo amewataka wanachama kutambua kuwa yeye ni Rais wa watu wote na wala si wa kikundi fulani.
Mkutano huo umemwidhinisha Mnangagwa kuwa Mkuu Mpya wa chama na mgombea urais katika uchaguzi wa mwaka 2018. na kumvua rasmi uongozi aliyekuwa kiongozi mkongwe wa chama na Serikali ya Zimbabwe, Rais Robert Mugabe.
Rais Mnangagwa amesema wanachama wanapaswa kurekebisha uchumi ikiwa wanataka wawe na nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani.
“Huu si wakati wa kutambiana kuwa kundi gani limeshinda bali kila mwanachama anapaswa kuzingatia mahitaji ya wananchi ambao wanataka maendeleo” amesema