Sunday, 17 December 2017

Kilimo Cha Matikiti Maji,



Ili kulima matikiti maji, inakubidi uwe na sehemu ya kutosha, yenye jua la kutosha, maji mengi na ardhi yenye rutuba ya kutosha, matikiti maji hukua haraka kama mimea mimgine ya jamii yake itambaayo mfano Matango, maboga na maskwash.
Kwa mtu ambaye anaanza kilimo yatampa tabu kidogo tofauti na Yule ambaye ana ujuzi kidogo na mambo ya kilimo kwa sababu yanahitaji umakini kiasi.
HALI YA HEWA
Mimea hii haihimili hali ya joto kali sana, mvua nyingi na udongo unaotuamisha maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu, inastawi vizuri kwenye kuanda wa pwani na miinuko kidogo kama DSM,Tanga, Morogoro, Mtwara, lindi na Pwani ambapo kuna jua la kutosha. Muda mzuri wa kupanda ni kipindi cha kipupwe mwezi wa machi mpaka wa septemba .
UPANDAJI
Panda kwa kutumia Mbegu zinazouzwa madukani, ukitumia Mbegu kutoka kwenye tikiti ulilonunua linaweza likawa ni hybrid na matokeo yake matikiti yatakayozaliwa hayatakuwa bora kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2) Panda Mbegu yako moja kwa moja kwenye shamba, usinunue miche au kupanda Mbegu kwenyemifuko ya plastiki halafu ndi uhamishie shambani, panda Mbegu mbili sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 2 - 3 kutoka mstari hadi mstari, baada ya siku chache Mbegu zitaanza kuota, baada ya kama wiki 2 katika Mbegu mbili ulizopanda kata moja na uache ule mche wenye afya zaidi, angalizo using’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche uliobaki.
Unaweza kupandishia udongo kwenye mashina na hii itasaidia kupunguza maji yasituame kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba.
Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda yenye, na wakati wa kuanza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe mimea kwa kuielekezea kwenye waya na kufungia
MCHE ULIOCHIPUA
UANGALIZI
Miche ikiwa imetambaa kiasi unaweza kuweka matandazo kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu, unaweza kuweka samadi au mbolea za viwandani, mimea ikiwa midogo tumia zaidi mbolea zenye nitrojen na utumie zaidi mbolea za potasiam mara baada ya maua kutokeza hadi matunda kukomaa, matawi yakifikia urefu wa mita 2 kata mbele ilikuruhusu kutoa matawi na hivyo kupata maua mengi zaidi hatimaye mavuno zaidi
MAUA NA MATUNDA
Matikiti hutoa maua dume na jike kwenye tawi moja, maua dume ambayo ni madogo zadi hutoka kwanza yakifuatiwa na maua jike ambayo ni makubwa zaidi, usipoona maua dume na jike kuna tatizo mfano maji kidogo yalimwagiliwa, upungufu wa viritubisho kwenye udongo, hali ya hewa ni joto/baridi sana n.k
Uchavushaji kwenye matikiti hufanyika na wadudu, kama huwaoni wakifanya kazi yao unaweza kufanya mwenyewe, muda mzuri ni wa asubuhi, unakata maua dume kwa kisu na kufanya uchavushaji kwenye maua jike, maua jike ya mwanzo kwenye tawi ndiyo yenye ukuaji bora zaidi, unaweza kukata tawi lisiendelee kukua baada ya matunda kutokeza hii husababisha kuwa na matunda makubwa zaidi
UCHAVUSHAJI KWA MKONO
UVUNAJI MATIKITI
Ili kujua matikiti yamekomaa inahitaji ujuzi kidogo, upande wa chini wa tunda huanza kuwa na rangi ya njano, pia kikonyo juu ya tunda hukauka kabisa na kuwa kijivu, ila njia nzuri ni kuyapiga kwa kiganja na kusikiliza mlio wake kama tunavyofanya kwenye mafenesi, hii nayo ni shule nyingine. Tumia kisu wakati wa kuvuna matikiti, yabebwe na kuhifadhiwa vizuri kwenye makasha tayari kuuzwa au kwa matumizi binafsi
MAGONJWA NA WADUDU
Wadudu wa matikiti wako wanaoshambulia majani na maua, na wengine hushambulia matunda , pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea, ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kjupata dawa sahii, dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda na FUNGICIDE itasaidia kwa mashambulizi ya fangasi.

Tabia Hii Haifai Kwenye Biashara Na Uwekezaji Wowote,,



Kuonekana umefanya makosa mbele za watu ni kitu kinachotishia utambulisho wa mtu, ndiyo maana watu wengi wanachukulia kufanya makosa kama jambo la kurudi nyuma. Mtazamo wa waliowengi ni kwamba kwenda mbele ni pale tu wenzako wanapokuona uko sahihi kwa mtazamo wao binafsi. Kutaka kuonekana sahihi mbele ya macho ya wenzako ndiyo usababisha hali ya kupenda kila mara kujihami, kujilinda, kulaumu watu wengine au kusingizia kitu kingine, hasa pale inapotokea mambo yemekwenda ndivyo sivyo.
Watu walio na shauku ya kuonekana sahihi, mara nyingi ukazana sana kufanya kazi au shughuli zile zinazowathibitisha kwa watu wengine kuwa wao wana uwezo. Ukiwa mtu mwenye shauku ya kuonekana sahihi kila wakati, mara nyingi utapendelea kufanya kazi zako kwa kufuata maoni ya watu wengine.
Matokeo yake na bila kujua unajikuta unakuwa mtumwa wa watu wengine wanageuka kuwa mabosi wako. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kila jambo inabidi uwasikilize wao wanasemaje unapata ruhusa kutoka kwao.
Endapo ukifanya jambo la lenye manufaa kwako na kwa watu wengine lakini wale watu wako wa karibu wakasema siyo sahihi, basi wewe utaliacha “eti kwasababu watu wanasema siyo zuri”.
Unapokuwa mtu wa kuongozwa na maoni kutoka kwa watu wengine, ujue kuwa muda si mrefu utaanza kupoteza ubunifu wako. Kwa sababu, kila wakati unafanya kazi zako kwa tahadhari sana, ukilenga kutoonekana mbaya. Hofu ya kufanya kazi kwa kuogopa kuonekana mbaya ikizidi, kinachofuata ni kuziba kwa mfereji wa ubunifu kutoka kwenye akili yako.
Kuziba kwa mfereji maana yake ni kwamba, juhudi na akili zako hazijikiti tena kwenye kutafuta suluhisho kwa changamoto na matatizo yaliyopo, bali kwa kiwango kikubwa utatumia akili nyingi katika kufanya vitu ambavyo unadhani watu wako wa karibu watakupongeza au kukusifu.
Mtu anayependa kuonekana sahihi pia ni mtu asiyeamini kama kuna mtu mwingine anaweza kufanya vizuri zaidi ya yeye. Huyu ni mtu asiyeamini vipaji vya watu wengine. Siku zote anaamini asipofanya yeye hakutakuwepo na matokeo mazuri. Kila mara anakuwa ni mtu wa kujisemea rohoni ya kwamba“bila mimi kuwepo mambo hayawezi kwenda".
Ukweli ni kwamba bidhaa au huduma yoyote ile tunayoiona sokoni haiwezi kamwe kutolewa na mtu mmoja, kwa sababu hakuna binadamu anayeweza kuwa na vipaji vyote.
Tabia ya kupenda kuonekana sahihi kwa watu, kwenye biashara na uwekezaji haifai. Hii ni kwa sababu, kwenye biashara na uwekezaji tunaamini sana katika kuunganisha vipaji vya watu mbalimbali (timu) kwa lengo la kuzalisha suluhisho kwa changamoto na matatizo yaliyopo kwenye jamii. Tunafanya hivyo kwasababu, bidhaa na huduma unazotumia leo hii, ni matokeo ya vipaji mbalimbali vilivyounganishwa pamoja na mfanyabiashara au mwekezaji.
Katika nyanja nyingine za maisha, kuongezeka kwa watu ambao wanakupongeza na kukusifu hakuleti faida ya moja kwa moja kwako, kama ipo. Na mara nyingi ukifanikiwa kupata faida, inakuwa siyo ya kudumu. Wakati huohuo, hali ya nyanja za maisha ya biashara na uwekezaji ni tofauti kidogo na uko kwingine. Kwenye biashara, mpango mzima ni kuelekeza juhudi na akili kwenye kuzalisha, kuongeza, na kutoa thamani kubwa kwa watu wengine.
Kwenye biashara hasa kubwa, wateja ndio rafiki zetu wa karibu na ndio kipimo cha usahihi wa kile tukifanyacho. Jukumu kubwa ni pamoja na kuendelea kujituma na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa mpaka pale wateja wanaporidhika. Uzuri wa kufanya kazi kwa lengo la kuridhisha wateja wako ni kwamba, wale wateja wanaoridhika na kazi unayoifanya wanavyozidi kuongezeka, ndivyo kipato chako kinavyozidi kuongezeka pia.
Kama unataka kuwa mfanyabiashara na mjasiriamali mkubwa, anza leo kujiwekea mazingira ya kufuta tabia hii ya kupenda kila wakati kuwafurahisha watu. Kamwe usitake kuwa sahihi kwa ajili ya watu wengine, bali kuwa sahihi kwa ajili ya wewe mwenyewe binafsi, pia kufanya yale unayotakiwa kufanya. Usipoacha tabia hii ya kila wakati kutaka kufanya vitu vinavyokuthibitisha kwao kuwa wewe una uwezo mkubwa, nakuhakikishia kuwa haitatokea hata siku moja ukafanikiwa kwenye biasha

Njia 10 Za Kupunguza Magonjwa Ya Mlipuko Wa Kuku



Mlipuko wa magonjwa ni moja ya sababu za hasara kubwa kwa wafugaji na vifo vinavyotokea kwa wakati mmoja. Pindi mfugaji anapokumbwa na janga la vifo vya ndege, kabla ya kufikia mwisho wa mzunguko wa uzalishaji hivyo basi asitarajie kupata faida nzuri mara baada ya mauzo.
Hasara itokanayo na vifo inaweza kuepukika au kupunguzwa na kutokea kwa kiasi kidogo.
Hili linawezekana, ifuatayo ni namna ya kufanikisha hilo;-
1. Osha vyombo vya maji kila wakati na mwaga maji yaliyobaki.
Hakikisha unamwaga maji yaliyosalia mbali na kuosha chombo na sabuni kila siku, weka maji safi yasiyo na dawa na wala usitumie maji ya mto au yale usiyoyajua chanzo chake. Kama utaweka maji dawa basi tumia ‘vitamini’ muhimu kama ‘vitalyte’ ambazo zinasaidia kuua vijidudu.
2. Wape maji kabla ya chakula.
Ndege wapo tofauti na binadamu au wanyama wengine. Hakikisha unawapa maji kabla ya chakula hasa kama unatumia maranda, hii ni kuhakikisha hawakanyagani wanapogombania chakula sehemu moja.
3. Usiwape chakula chenye uvundo.
Ni hatari sana kuwapa ndege/kuku wako chakula chenye ukungu, ni kama kuwalisha sumu. Ukungu au uvundo huwafanya kuku waugue kirahisi sana au kuwasababishia madhara mengine kiafya.
4. Fuatilia kwa makini ratiba za chanjo na tiba.
Mfugaji unatakiwa kupata tiba na chanjo sahihi kwa ndege unaowafuga. Kuchanja ndege kutasaidia sana kuimarisha kinga yao dhidi ya magonjwa hatari kama kideri, ndui, gumboro na mareksi. Dawa kama vile za minyoo na antibayotiki ni muhimu sana kwenye afya ya kuku na ndege wengine.
5. Nunua na fuga vifaranga wenye afya njema.
Matatizo mengi ya afya ya ndege au kuku ni matokeo ya maisha duni ya awali ya kuku hao au huwa wanarithi. Itambulike hivi, baadhi ya ndege/kuku hurithi afya mbovu kutoka kwa wazazi wao. Hata hivyo baadhi ya watotoleshaji pia wanafuga kuku ambao wana afya mbovu na hivyo huuza vifaranga au mayai dhaifu na waathirika na hivyo mnunuzi anajikuta ananunua matatizo.
6. Zuia mkusanyiko wa hewa ya ammonia.
Maranda yakikaa muda mrefu bandani, hufanya hewa ya ammonia kuzalishwa kwa wingi, hewa hii hufanya ndege wapaliwe hadi kufa. Kila mara ondoa maranda mabichi au yaliyovunda na weka mengine haraka iwezekanavyo ili kuepuka vifo vitokanavyo na kupaliwa au magonjwa ya mfumo wa hewa.
7. Zuia panya na vicheche.
Banda la ndege linatakiwa lisiruhusu panya au wanyama wadogo jamii ya kicheche kuingia ndani, na ndege wa mwituni kwa kuweka nyavu au kupulizia dawa, ikiwa watapata upenyo wataua na kula ndege/kuku wako na kuacha vimelea vya magonjwa wanapokula vyakula au kunywa maji ya ndege wako.
8. Zingatia usafi na usalama.
Kipengele hiki cha usafi na usalama ni kipana ila unachotakiwa kufanya ni kuzingatia usafi nje na ndani ya banda. Unatakiwa ukamilishe usalama wa afya ya ndege/kuku wako kila wakati, jambo ambalo wafugaji wengi hutekeleza pindi wanapo shitukizwa na mlipuko wa magonjwa.
9. Wape chakula cha kutosha.
Ndege kama walivyo wanyama wengine, hawawezi kukua na kuzalisha vizuri endapo wanapewa chakula duni na kidogo. Chakula bora ni msingi imara na ni kinga kwani chakula duni hupelekea uzito kupungua na kinga kuwa chini na hivyo hufa mapema. Jitahidi wape kuku chakula cha kutosha ila usiwazidishie.
10. Wakinge dhidi ya baridi kali.
Baridi kali ni adui kwa afya ya wanyama, ndege na binadamu. Jaribu kila uwezavyo kuwakinga kuwakinga ndege wako na baridi kali kwani inaua haraka sana kama sumu. Wawekee chanzo cha joto wakati wa baridi au jenga banda ambalo halipitishi baridi kali.
Hizo ndizo njia muhimu ambazo ukiwa mfagaji unazoweza kuzitumia ili kukinga magonjwa yanatokanayo na kuku.

Mambo 5 Ya Kuzingatia, Kama Wewe Ni Mjasiriamali Unayetaka Mafanikio Makubwa.



Mafanikio ni kitu cha lazima sana katika safari ya mjasiriamali. Uwe mjasiriamali mdogo, wa kati au mkubwa kwa vyovyote vile unahitaji mafanikio. Lakini ili kufanikiwa na kufikia mafanikio hayo, yapo mambo ya msingi ambayo unatakiwa kuyazingatia.
Mambo hayo ni kama haya yafuatayo:-
1. Kujiwekea malengo.
Ukiwa kama mjasiriamali unayetakiwa kufikia mafanikio makubwa, suala la kujiwekea malengo ni lazima kwako. Unapokuwa na malengo yanakuwa yanakupa mwelekeo sahihi wa kupata kile unachokitaka. Hiki ni kitu ambacho unahitaji kukizingatia sana kwani ni nguzo kubwa ya kufikia mafanikio makubwa.
2. Kujitoa Mhanga(Take Risks)
Hakuna mafanikio makubwa utakayoyapata bila kujitoa mhanga. Wajasirimali wote wakubwa ni watu wa kujitoa mhanga sana. Wanakuwa wako tayari kutoa kitu chochote ilimradi wafikie malengo yao. Kitu cha kuzingatia hata kwako wewe unalazimika kujitoa mhanga na kulipia gharama ili kufikia mafanikio makubwa.
3. Kutokuogopa Kushindwa.
Wengi wetu tumefundiswa sana kuwa kushindwa ni vibaya. Hali ambayo hupelekea tunakuwa tunaogopa kujaribu karibu kila kitu kwa sababu ya hofu ya kushindwa. Ikiwa wewe ni mjariamali unatakiwa kuwa jasiri na kujua kwamba mafanikio yanataka roho ya ujasiri na kutokuogopa kushindwa. Hiyo ndiyo siri itakayokifikisha kwenye kilele cha mafanikio na sio uoga unaouendekeza.
4. Acha kuridhika mapema.
Ni kosa kubwa sana kujikuta unaridhika mapema eti tu kwa sababu ya faida unayoitengeneza sasa. Ni vizri kujua, safari ya mafanikio bado ni ndefu kwako, hivyo hutakiwi kuridhika kwa namna yoyote ile. Kama kuna jambo umelifanikisha, endelea kwenye jambo lingine hadi kujenga mafanikio makubwa kabisa.
5. Tafuta ‘Mentor’
Acha kujidanganyai kuingia kwenye safari ya mafanikio huku ukiwa peke yako. Ikitokea umekwama kwa sababu huna mtu wa kukuelekeza au kukushauri, huo ndiyo unakuwa mwisho wako. Hivyo ni muhimu kuwa na kiongozi wako ‘mentor’ ambaye atakuongoza kwenye kufikia mafanikio yako.
Kwa kuyajua mambo hayo yatakusaidia wewe mjasiriamali kuweza kuendelea mbele zaidi na kufanikiwa katika safari yako yamafanikio.

Kama unaogopa kufanya kitu hiki, sahau kuhusu Mafanikio katika Maisha yako yote


Fikiria kila unachokijua na kukikumbuka kuhusu mabadiliko unayotaka yawe katika maisha yako, halafu uone ukweli huu kama kweli nawe ni mmoja kati ya watu wanaotaka mafanikio au uko nje ya mstari wa mafanikio na pengine tu wewe hujijui. Kama kweli unataka mafanikio, ni kwanini mara kwa mara umekuwa ukisita au kuogopa kufanya jambo ambalo lingeweza kubadili maisha yako na kukuletea mafanikio mkubwa? Hili ndilo tatizo walilonalo watu wengi wanahofia sana kufanya mabadiliko kwa namna moja au nyingine hata kwenye yale malengo waliojiwekea wao wenyewe kuna wakati huwa wanaogopa pia.
Kimaumbile, kila binadamiu anahofia mabadiliko, lakini hofu ya mabadiliko inapozidi kuwa kubwa na kukuzuia kufanya mambo ya maana kwako, hofu hii sasa hugeuka kuwa ni maradhi yanayokuzuia wewe kufanikiwa. Hebu fikiria tena, ni mara ngapi umekuwa ukitaka kufanya mabadiliko Fulani katika maisha yako, lakini umekuwa ukijikuta ukishindwa kufanya hivyo kutokana na kuogopa kufanya vitu Fulani? Ni mara ngapi umekuwa ukitaka kuingia kwenye biashara lakini umekuwa na hofu nyingi zinakuzuia? Hivi ndivyo ilivyo mabadiliko huogopwa, wakati mwingine bila sababu ya msingi.
Wengi wetu kutokana na kuogopa mabadiliko, hujikuta ni watu wa kutoa sababu ambazo hata hazina mashiko zinazosababisha wao washindwe kutekeleza malengo na mipango waliojiwekea. Utakuta mtu anakwambia hawezi kufanya biashara ni kwa sababu hana mtaji, ukija kuchunguza kidogo utagundua kuwa hiyo ni sababu ambayo amekuwa akiitoa kwa muda mrefu, iweje kila siku mtu huyohuyo awe hana mtaji tu. Kama uko hivi una hofu tu hata kwa vitu vidogo ambavyo ungeweza kuvifanyana , tambua kuwa kuanzia sasa unaye adui mkubwa ndani mwako anayekuzuia kufanikiwa. Na unapoogopa kufanya mabadiliko ambayo unaahitaji sasa ili ufanikiwe, sahau kuhusu mafanikio katika maisha yako yote.
Tatizo kubwa utakalokuwa nalo linalosababishwa na hofu hii ya kuogopa kufanya mabadiliko ni lazima utakuwa mtu wa kutaka mafanikio ya harakaharaka. Watu wengi wenye mawazo ya kutaka kufanikiwa leoleo hata kama wameanza biashara leo, wengi wao huwa wana hofu hii kubwa ya mabadiliko ndani mwao, unaweza kufanya utafiti mdogo utagundua ukweli huu ulio wazi. Hawa ni watu ambao kiuhalisia hawaijui wala kuiamini subira ndani mwao, bali ni watu wakutaka mfumo wa maisha uwe ambao unaanza leo biashara na wiki ijayo uwe tajiri ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa.
Hivi ndivyo walivyo watanzania wengi wanaogopa mabadiliko na kuamini katika miujiza, sio katika wao wenyewe kutenda na kuona matokeo. Hebu jaribu kukagua maisha ya walio wengi utakuja kugundua ukweli huu ni watu wanaofikiria sana leo, sasa hivi, siyo baadaye. Hata malengo yao ni ya karibu sana na hawataki shida, wanataka wafanye leo, wamudu leo na kila kitu kimalizike leo. Sijui kesho watafanya kitu gani? Ukimwambia mtanzania aanzishe mradi ili aje faidi baada ya miaka 10 kutoka sasa kwanza atakushangaa, kisha atakucheka we hadi mbavu zimuume. Anataka leo hata kama ni kwa miujiza.
Ndiyo maana wengi kati ya Watanzania hawana malengo, wanaishi tu na kutawaliwa na hofu za mabadiliko. Kuweka malengo siyo sehemu ya maisha yao, kwani malengo yanataka mtu mwenye subira, mtu anayeamini kwamba maisha ni kuanguka na kusimama. Wanachojua kikubwa ni kulalamika na kulaumu, kuponda na kukejeli, kwa sababu wao wamekata tamaa bila kujijua. Ndiyo maana ni watanzania wanne tu kati ya kumi ambao wanafanya kazi, wanatoka jasho na wanaweza kusubiri bila kukata tamaa, wengine waliobaki wanasubiri ujanja ujanja tu ilimradi wafanikiwe hata kama ni kwa kufanya uhalifu wa aina yoyote.
Ni watu ambao wanataka kuishi kihadithi, wawe na pete ambayo wanaweza kuiamuru iwape wakitakacho na wakipate. Maisha ni ya kibunuasi- abunuasi tu, watu hawa kwao mabadiliko ni kitu kigumu sana kwao na kinaogopwa kweli. Kama unataka mafanikio ya kweli yawe kwako, unatakiwa kubadilisha fikra za zako na kuamua kukubali kuwa mafanikio yanahitaji mabadiliko makubwa sana ambayo wewe mwenyewe unatakiwa uyafanye kwa kujitoa hasa. Acha kuwa na hofu zisizo na maana zinazokuzuia wewe usifanikiwe, chukua hatua katika maisha yako, kuyafikia maisha unayoyataka.

Saturday, 16 December 2017

Zaidi Ya kaya 100 zakosa makazi Songea



Zaidi ya Familia 100 hazina mahali pa kuishi kufuatia nyumba zao kubomoka na kuezuliwa kwa upepo uliuoambatana na mvua kali iliyonyesha usiku wa kuamkia leo ambapo nyumba zaidi ya 60 na vyumba vitano vya madarasa ya shule ya msingi Chandamali kata ya Bombambili manispaa ya Songea vimeezuliwa.
Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Songea chini ya mwenyekiti wake mkuu wa wilaya Pololeti Mgema wamewatembelea wananchi waliokumbwa na kadhia hiyo kwa lengo la kutoa pole kwa wahanga.
Serikali imewataka wananchi kuzingatia kanuni bora za ujenzi kwani nyumba nyingi zilizoezuka zimejengwa bila kuzingatia kanuni za ujenzi, aidha serikali itaelekeza nguvu zake kukarabati vyumba vitano vya shule ya msingi Chandamali hivyo wananchi waanze kukarabati nyumba zao bila kusubiri msaada.
Wakati huo miundo mbinu ya Tanesco nguzo zimedondoka na nyaya za umeme kusambaa hovyo, aidha huko Matimila halmashauri ya wilaya ya Songea nyuma 15 zimeezuka na jengo la utawala la sekondari ya Matimila gharama za hasara iliyotokana na maafa hayo bado haijafahamika serikali inaendelea kukusanya taarifa sahihi.

Simba yafanya Maamuzi Magumu



SIMBA SC imesajili wachezaji watatu wapya wa kigeni, beki Mghana Asante Kwasi, kiungo mshambuliaji Mzambia Jonas Sakuwaha na mshambuliaji Antonio Dayo Domingues kutoka Msumbiji.
Wakati dirisha dogo la usajili linakaribia kufungwa jana, viongozi wa Simba walikuwa wanahaha kukamilisha usajili huo, hususan wa mchezaji Kwasi, ambaye bado ana mkataba na klabu yake ya sasa, Lipuli ya Iringa.
Lakini kwa Sakuwaha na Domingues hakukuwa na tatizo na habari zinasema wachezaji hao watachukua nafasi za beki Mzimbabwe, Method Mwanjali na washambuliaji, Mghana Nicholas Gyan na Mrundi Laudit Mavugo.
Wapinzani wao, Yanga wamesajili wachezaji wawili tu wapya, beki Fiston 'Festo' Kayembe Kanku kutoka Balende FC ya kwao, DRC na mshambuliaji kinda, Yohanna Nkomola ambaye ni mchezaji huru, aliyekuwamo kwenye kikosi cha timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys.
Azam FC imeingiza mmoja tu mpya, mshambuliaji Bernard Arthur kutoa Liberty Professional ya Ghana, baada ya kumuacha Mghana mwenzake, Yahya Mohammed na Singida United imesajili saba wapya; Lubinda Mundia kwa mkopo kutoka Res Arrows ya Zambia, Daniel Lyanga kutoka Fanja ya Oman, Kambale Salita 'Papy Kambale' kutoka Etincelles ya Rwanda, Issa Makamba, Assad Juma, Ally Ng’azi na Mohamed Abdallah wote huru waliokuwa Sereneti Boys.
Singida imewaacha wawili, Atupele Green na Pastory Athanas waliovunjiwa mikataba wakati Mohamed Titi na Frank Zakaria wametolewa kwa mkopo Stand United na Mbeya City imewasajili George Mpole kutoka Maji Maji na Abubakar Shaaban huru, baada ya kuwaacha Emmanuel Kakuti na mkongwe Mrisho Ngassa anayehamia Ndanda FC.

Ronaldo Atimiza ndoto yake



Nyota wa klabu ya soka ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo,
amesema anajisikia vyema kutimiza malengo yake kwenye ulimwengu wa soka na anafuraha kushindana na Lionel Messi kwa muda mrefu.
Akifanya mahojiano na tovuti rasmi ya FIFA, Ronaldo amesema ndoto yake ilikuwa kuweka historia na kuacha kumbukumbu kwenye ramani ya soka na hicho kitu kimetimia akiwa ametwaa mataji mengi pamoja na mafanikio binafsi ikiwemo tuzo tano za Ballon d’Or.
“Najisikia vizuri kutimiza malengo yangu, nilitamani sana kuweka historia kuacha jina langu kwenye vitabu vya soka, nimepata mafanikio mengi sana ngazi ya klabu na taifa, nafurahia kuwa mmoja wa wachezaji waliofanikiwa zaidi kama kuchukua tuzo tano sawa na Messi”, amesema Ronaldo.
Ronaldo ameongeza kuwa katika maisha yake amefanya kitu anachokipenda zaidi ambacho ni kucheza soka na amefanikiwa sana na hiyo inamuhamisha kuendelea kufanya vizuri akiwa bado anapenda soka kwasababu utafika wakati hawezi tena kufanya hivyo.
Ronaldo ameshinda taji la Ligi Kuu ya England EPL mara tatu akiwa na Manchester United kabla ya kutua Real Madrid na kushinda ubingwa wa La Liga mara mbili. Pia ameshinda taji la ligi ya mabingwa barani Ulaya UEFA mara nne.

BREAKING NEWS : Mkurugenzi Mkuu NHC Asimamishwwa kazi



Zitto Kabwe ahoji kuhama kwa makada Wa ACT



Kiongozi wa chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe ametumia hotuba yake ya ufunguzi wa kikao cha Kamati Kuu kuzungumzia wimbi la kuhama kwa makada wa chama hicho, akihoji iwapo kimeanza kupoteza mwelekeo.
Katika hotuba yake leo Jumamosi Desemba 16,2017, Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma Mjini amewataka wajumbe wa kamati hiyo kujiuliza maswali magumu, likiwemo la kwa nini hali hiyo inakikumba chama chao.
Makada wa chama hicho waliojiunga na CCM ni Profesa Kitila Mkumbo aliyeachia nafasi ya ushauri wa ACT –Wazalendo baada ya kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho; wakili Albert Msando, Samson Mwigamba na Edna Sunga.
Katika hotuba hiyo, Zitto amesema hamahama hiyo imezua taharuki kwenye chama hicho na kuacha maswali juu ya kinachoendelea katika siasa za Tanzania.
“Ni lazima tujiulize maswali magumu sisi wenyewe na kuzungumza tukitazamana machoni, je hakuna sababu za ndani sisi wenyewe zinazokimbiza wanachama wetu? Kama zipo ni zipi? Je ni sababu ambazo tunaweza kurekebisha na kukiimarisha chama," amehoji Zitto.
Amesema, "Kama ni sababu zilizo nje ya uwezo wetu tunafanya nini ili kuzikabili, je bado sisi tunaamini katika misingi ya chama kwa mujibu wa Azimio la Tabora? Tulikuwa kundi tu tulioumizwa na vyama tulivyokuwamo na tukaamua kuunda chama kupoza hasira zetu tu na sasa hasira zimeisha hakuna sababu ya chama kuwapo."
Amesema kati ya waanzilishi watatu wa ACT, wawili wamekikimbia na kujiunga na CCM na kwamba, jambo hilo huenda likarutubisha hoja kuwa chama hicho kilikuwa mradi wa chama tawala, kwamba sasa hauna maana tena.

Wabakaji Watoto Kuuwawa India



Wabakaji wa watoto wanapaswa kuuawa katika muda wa miezi sita tangu watekeleza uovu huo, mteteaji mkuu wa haki za wanawake India amependekeza.
Swati Maliwal ametoa ombi hilo katika barua aliyomuandikia waziri mkuu Narendra Modi.
Iliandikwa kuendana na kumbukumbu ya mwaka wa tano tangu mwanafunzi Jyoti Singh mwenye umri wa miaka 23 alipobakwa na gengi la wanaume, kifo chake kilichozusha maandamano ya kitaifa.
"Hakuna kilichobadilika kaika miaka mitano iliyopita," Bi Maliwal, ameiambia BBC.
"Delhi bado ndio mji mkuu wa ubakaji. Mwezi uliopita, mtoto wa kike wa mwaka mmoja na nusu alibakwa na gengi la wanaume, na ubakaji wa mtoto wa miaka saba,na mwingine wa kike wa mwaka mmoja na nusu alibakwa."
Kwa wastani, alisema, watoto watatu wa kike na wanawake wasita wanabakwa katika mji mkuu huo kila siku.
India ilifanyia mageuzi sheria zake kuhusu ubakaji kutokana na shutuma miaka mitano iliopita, na ilichukua hatua kuharakisha kusikilizwa kesi na kuwashinikiza maafisa wa polisi kutilia uzito tuhuma za ubakaji na unyanyasaji wa kingono.

Rais Mstaafu CWT anaswa na TAKUKURU



Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU inamshikilia Rais mstaafu wa Chama Cha walimu Tanzania (CWT) Gracian Mkoba kwa tuhuma za rushwa.
Hilo limethibitishwa na Afisa Uhusiano wa TAKUKURU Makao Makuu, Mussa Misalaba, ambaye amesema wanamshikilia Mkoba kwa tuhuma za kugawa fedha kwa baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho ili kuwashawishi wamchague mgombea anayemtaka.
"Mukoba ameshastaafu, lakini kuna mgombea mmoja alikuwa anataka achaguliwe, tumemkamata leo asubuhi akigawa rushwa kuwashawishi wapiga kura kwenye ukumbi wa Chimwaga wamchague huyo mgombea wake," amesema Misalaba.
Misalaba ameongeza kuwa TAKUKURU inaendelea kufanya uchunguzi zaidi dhidi ya Mukoba kabla ya kumfikisha mahakamani.
Mukoba anakuwa mtu wa tatu kukamatwa na TAKUKURU kwa tuhuma za rushwa kwenye uchaguzi ndani ya wiki moja, wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Juma Khamis na mfanyabiashara Haider Gulamali.

Waziri azindua mfumo Wa kieletroniki utambuzi wanamuziki



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe leo December 16, 2017 amezindua mfumo mpya wa Kieletroniki wa Utambuzi wa Wanamuziki ambao utaanza kutumika nchini kwa ajili ya kulinda maslahi ya wasanii.
Moja ya vitu ambavyo Dr. Mwakyembe amevizungumza ni kuhusu kuibiwa na kutumiwa kwa kazi za wasanii na watu wachache bila ridhaa yao “tulipotoka ni kubaya, mimi nilikuwa DRC nilichoshangaa sana nilipita sehemu nikakuta picha kubwa ya Kanumba kule ni Star, ukija hapa mi nlifikiri kaacha mali za ajabu sana,”
“Vijana wetu wana majina makubwa, mifukoni hawana kitu, mambo mengi yanaudhi ni kwenye sanaa, tutakwenda Mahakamani haiwezekani huu unyonyaji, ngoja tuondoe hii njaa ya mwanzo afu nianze kupambania mambo mengine,” – Dr. Mwakyembe