"Tanzania imeshaonekana kuwa ni kichaka cha fedha za kigeni" - JPM
Tanzania\'s leading online News Edition (The National Newspaper). Get access to the most current and latest authoritative news on local issues, politics, events, celebrations, editorial, columnists, features, people and business.
Wednesday, 13 December 2017
Audio | S Kide – 900 Itapendeza | Mp3 Download
Audio | S Kide – 900 Itapendeza | Mp3 Download

Audio | S Kide – 900 Itapendeza | Mp3 Download
DOWNLOAD

Audio | S Kide – 900 Itapendeza | Mp3 Download
DOWNLOAD
Alichoandika Zari kwenye Birthday ya Marehemu Ivan
Alichoandika Zari kwenye Birthday ya Marehemu Ivan
Spidi ileile kuileta Treni ya Umeme Tanzania, Prof. Mbarawa kagoma kulala
Spidi ileile kuileta Treni ya Umeme Tanzania, Prof. Mbarawa kagoma kulala
LIVE: "Tanzania imeshaonekana kuwa ni kichaka cha fedha za kigeni"
LIVE: "Tanzania imeshaonekana kuwa ni kichaka cha fedha za kigeni"
Mazoezi ya Yanga Yashusha Majembe Mawili ya Kimataifa
Mazoezi ya Yanga Yashusha Majembe Mawili ya Kimataifa
Afanya sherehe ya kuagwa kabla hajafariki

Satoru Anzaki akiwa kwenye karamu hiyo
Mfanyabiashara mmoja nchini Japan ambaye anaugua saratani na anatarajiwa kufariki karibuni aliwashangaza watu baada ya kuandaa karamu kubwa ya kuaga.
Satoru Anzaki aliwaalika wageni karibu 1,000 wakiwemo marafiki zake, watu waliosoma naye, washirika wake wa kibiashara na wafanyakazi wake.
Satoru, 80, ambaye ni mkuu wa zamani wa kampuni ya kuunda mashine ya Komatsu alipatikana na saratani ya kibofu cha nyongo Oktoba.
"Nimeridhika kwamba niliweza ksuema 'asante' kwa watu niliokutana nao maishani," aliwaambia wanahabari baada ya sherehe hiyo.
"Kwa kuwa nilitaka kufurahia kabisa sehemu ndogo ya maisha niliyobaki nayo, nimeamua nisipokee matibabu baada ya kuzingatia madhara ya tiba," alisema.
Alitangaza mpango wake wa kufanya sherehe hiyo kupitia tangazo gazetini, taarifa ambazo zilisambazwa sana mtandaoni watu wakitaniana kuhusu ingelikuwa wao wangewaalika nani.
Satoru alikodisha chumba katika hoteli moja Tokyo na akaipamba kwa picha za kumbukumbu ya maisha yake.
Marekani iko tayari kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini

Rex Tillerson
Marekani iko tayari kwa mazungumzo wakati wowote na Korea Kaskazini bila ya masharti yoyote, waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tillerson amesema.
Taaarifa yake ilionekana kuwa tofauti na msimamo wa awali wa Marekani kuwa Korea Kaskazini ni lazima iharibu zana zake kabala ya mazungummzo yoyote kufanyika
Lakini saa chache baadaye Ikulu wa White House ilisema msimamo wake Trump kwa Korea Kaskazini haujabadilika.
Hatua ya Korea Kaskazini ya kuunda zana za nyuklia imesababisha Marekani kuongoza vikwazo vikubwa dhidi ya nchi hiyo.
Jordan yaitaka Marekani isiutambue Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel
Kando na hilo mkuu wa masuala ya siasa wa Umoja wa Mataifa ambaye hivi karibu alizuru Korea Kaskazini aliwaambia waandishi wa habari kuwa maafisa wa Korean Kaskazini wanaamini kuwa ni muhimu kuzuia vita.
Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Marekani na Korea Kaskazini umeharibika kufuatia majaribio ya hivi karibuni ya mabomu ya nyuklia na makombora na kuwepo vita vya Maneno kati ya rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Akizungumza kwenye mkutano wa baraza la nchi za Atlantic siku ya Jumanne, Bw Tillerson alisema kuwa Marekani haiwezi kukubali Korea Kaskazini kujihami kwa silaha za nyuklia.
Viongozi wa ACT Wazalendo Singida watimkia CCM

Mwenyekiti na katibu wa Chama cha ACT Wazalendo mkoani Singida, wamejivua uanachana na vyeo vyao na kuhamia CCM.
Viongozi hao ni aliyekuwa mwenyeketi Wilfred Noel Kitundu na katibu wa mkoa wa chama hicho, Loth Robert Thomas.
Viongozi hao wamechukua uamuzi huo mbele ya mkutano mkuu wa uchaguzi CCM mkoa wa Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhazili mjini hapa juzi.
Kwa nyakati tofauti walisema changamoto ambazo upinzani walikuwa wakizipigia kelele, Rais John Magufuli ameendelea kuzitatua kwa ufanisi.
Viongozi hao walikabidhi kadi za vyama vyao vya zamani, kwa mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Hadija Abood na kupewa kadi za CCM.
Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Jimson Mhagama alisema kwamba wataendelea kuwapokea wanachama wanaorejea kutoka upinzani lakini ni lazima wafuate taratibu za chama.
Baada ya Askofu kuhojiwa Uraia wake, Bashe afunguka

Bashe.
MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ameelezwa kusikitishwa kwake baada ya Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge, Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera, Severine Niwemugizi (61), kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Bashe ameandika;
I know how it feels unapo ambiwa AMA kuanza kujazishwa Fomu na kuhojiwa juu ya Uraia Wako its like kujazishwa fomu kuambiwa huyu sio Mama yako or Baba yako Pole Askofu Severine Niwemugizi wanaofanya haya hawana hata Khofu ya Mungu.
Askofu Niwemugizi aliehojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake kwa mara ya kwanza Novemba 28 mwaka huu na mara ya pili alihojiwa Desemba 4, mwaka huu.
Askofu Niwemuzi aliingia kwenye headlines baada ya kueleza kuwa serikali itoe kipaumbele kwa katiba mpya ya nchi ili iweze kukamilika.


Askofu Niwemugizi
Mama Mjamzito ajifungulia kichakani

MKAZI wa Kijiji cha Ibondo, Kata ya Ludete, wilayani Geita, Ester Balele, amelazimika kujifungulia kwenye kichaka hatua chache kutoka kwenye nyumba anayoishi mkunga wa zahanati ya Ibondo, baada ya kukosa huduma kwa wakati.
Akizungumza na gazeti hili kijijini hapo, Balele alisema alikutwa na hali hiyo Novemba 29, majira ya saa 12.30 alfajiri alipo kwenda katika zahanati hiyo kujifungua na mkunga kugoma kufungua mlango.
Alisema kuwa siku hiyo majira ya saa tisa usiku akiwa amelala nyumbani kwake alipata dalili ya uchungu na kuamua kwenda kumuamsha mama mkwe na shemeji yake ili wampeleke zahanati akajifungue, lakini baada ya kufika kwenye zahanati hiyo mkunga huyo aligoma kufungua licha ya kugongewa mlango mara kadhaa.
Alisema waliamua kumgongea mkunga huyo kwenye nyumba anayolala baada ya kukuta zahanati imefungwa.
Alisema ilipofika majira ya saa 12.30 alfajiri wakati wanaendelea kumgongea, hali ya uchungu ilizidi akalazimika kusogea kwenye kichaka ili ajifungue na alipomaliza mkunga huyo alitoka nje na kuwahoji kwa nini wanamsumbua usiku na kudai wanataka kumvamia.
Mkunga wa zahana hiyo, Aloyce Emmauel katika mahojiano na gazeti hili, amekiri kugoma kufungua mlango akihofia usalama wake huku akionyesha waandishi wa habari eneo la kichaka alipojifungulia mwanamke huyo .“Ni kweli nilisikia watu wanagonga mlango sikuweza kufungua kwa wakati huo, ilipofika majira ya saa 12.30 nilifungua mlango nikawakuta watu watatu nje wakiwa na mwanamkemmoja akihangaika kujifungua wakati narudi ndani kuchukua vifaa ghafla akawa amejifungua mtoto wa kiume,” alisema mkunga huyo.
Hata hivyo, zahanati hiyo kwa muda mrefu imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kwa lugha chafu kwa wagonjwa, kufanya kazi kwa mazoea na huku wakidaiwa kujihusisha na rushwa.
Wakati mkunga akikiri kutokea kwa tukio hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Geita, Solomon Shati, amekanusha kuwapo kwa mwanamke aliyejifungulia nje.
“Sijafika eneo la tukio, lakini nimewasiliana na mkuu wa zahanati ya Ibondo, Asteria Chekanabo, amesema hakuna mwanamke mjamzito aliyejifungulia kichakani,” alisema.
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mwalimu Hermani Kapufi, alipotafutwa kuelezea tukio hilo, ofisi yake imedai kuwa yuko safarini kikazi.
Source: Nipashe
Wanandoa wauawa kwa kupigwa mapanga na watu wasiojulikana

Mume na mke wakazi wa kitongoji cha Kidogue wilayani Mkalama wamefariki dunia kwa madai ya kukatwa mapanga shingoni na kichwani na watu wasiojulikana.
Mauaji ya wanandoa hao, Kija Kitundu (53) na mkewe Mwajuma Ramadhan (59) yalitokea Desemba 10 saa sita usiku nyumbani kwao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba alisema watoto wa wanandoa hao, Ramadhani (14) na Namagalu (12), wamepelekwa hospitali kwa matibabu baada ya kujeruhiwa katika tukio hilo.
Magiligimba alisema siku ya tukio wauaji hao walitumia ngazi kupanda juu ya paa la nyumba ya Kija kisha kuingia chumbani kwa wanandoa hao na kuwacharanga mapanga.
Alifafanua kuwa kabla ya tukio hilo, kuna mtu alikwenda nyumbani kwa Kija kuomba pampu lakini aliponyimbwa ndipo ugomvi ukaanza baina yao.
Subscribe to:
Posts (Atom)